Udhaifu wa taarifa ya askari aliyejinyonga Mtwara

Udhaifu wa taarifa ya askari aliyejinyonga Mtwara

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Aliyeandaa ile taarifa kama hakukurupuka basi ana agenda ya siri ama hakuwa timamu kiakili, tangu kuiandaa mpaka kuisoma na pengine sasa anajutia makosa ya wazi yanayoacha shaka kubwa!

Jamii, wazazi na ndugu wa marehemu wana hamu ya kujua ni nini hasa kilimaliza uhai wake! Baadhi wanatuhumu kwamba aliuawa akiwa mahabusu na wengine wanahoji daktari polisi imekuwaje awe sehemu ya watuhumiwa?

Pengine jeshi la polisi litakuja na ufafanuzi utakaoondoa ukakasi na lawama kwenye tukio zima lililoondoka na uhai wa mmoja wa watuhumiwa. Kuna maswali 10 common itabidi yapate majibu

1. PGO ya polisi inasemaje inapokutana na tukio la mtu kujinyonga?

2. Je, kuna picha zozote za ushahidi zilichukuliwa? Ili kuja kuondoa shaka baadae?

3. Je, selo ya mtumiwa ilikuwa salama kiasi gani kuweza kumhifadhi mtuhumiwa muhimu kama yeye?

4. Je, ni nani aliweka tambara la deki ndani ya selo? Na kwanini halikuondolewa?

5. Je, tambara la deki lililotumika kama kitanzi lilifungwa eneo gani la selo? Darini? Dirishani? Kuna ushahidi wowote wa picha?

6. Report ya PM haijawekwa wazi lakini ni wazi kwamba shingo itakuwa na michubuko ama alama ya kitanzi

7. Je, kama picha zilisahaulika kupigwa ni nani mashuhuda wa tukio? Wa kwanza kuona na waliohusika kuushusha mwili?

8. Kwa kawaida mtu akijinyonga lazima ama atoke haja ndogo au kubwa. Je, nguo za marehemu alizovaa wakati anajinyonga zimehifadhiwa kwa ushahidi?

9. Je, tambara la dekio alilotumia kujinyongea limetunzwa vema kama kielelezo?

10. Je, ni nani alithibitisha kuwa marehemu kajinyonga na hakunyongwa?

Mpaka sasa taarifa rasmi ya ufafanuzi iliyotoka ni namna ya kuzikwa kwa askari aliyekufa ambayo hata hivyo imezua mjadala na kuzidisha utata kuwa kwanini itoke kipindi hiki.

Maswali 10 husika hayajatolewa taarifa wala ufafanuzi wowote mpaka sasa.

Pengine hili litafanyika kabla tetesi hazijawa habari kamili na kuzidi kulichafua jeshi letu la polisi
 
Haya mapolisi ndo yanatumika kiiweka ccm madarakani kwahiyo ccm nayo inayatetea kwakuwa bado wanahitaji Polisi kuendelea kukaa madarakani. Kwao kubali madarakani ni muhimu kuliko raia kuuawa na policcm
Hapo ndipo hitaji la katiba mpya linapoonekana
 
Halafu Sirro yupo Kilindi ameenda kusikitikia tukio la jana amesahau kusikitika tukio la juzi Mtwara linalowahusu watu wake, hata kama ni kukosa fikra mbona hili ni common sense tu!!
#aibukwamama
 
Afu Sirro yupo Kilindi ameenda kusikitikia tukio la jana amesahau kusikitika tukio la juzi linalowahusu watu wake....jamani, hata kama ni kukosa fikra mbona hili ni common sense tu!!
#aibukwamama
Sense of guilty
 
Kwani ushahidi wa picha unatosha kukuaminisha siyo? Je kama alitundikwa?

Kesi ya watu kujinyonga selo zmeshatokea sana wengine wamejinyonga na suruali zao inabidi sahiv mtu akiingia selo aingie na boksa tu
 
Ndio maana tunahitaji KATIBA mpya ambayo itatuletea IPID,hawa watakua wanachunguza kesi zote zilizohusisha member's of police,maana tukio kama hili police now ni suspects na huwezi kujichunguza mwenyewe,why police wanakua wazito kuweka ukweli hadharani kama wapo innocent?
 
Hili tukio lina utata mwingi. Msemaji wa polisi alishindwa hata kutuambia uchunguzi wa kifo cha marehemu umefanywa na Madaktari kutoka hospitali gani?

Na je, ndugu wa marehemu walishirikishwa katika hatua zote za huo uchunguzi? Kinyume na hapo, basi polisi wakiri tu hadharani wamemuu mwenzao ili kuficha ushahidi.
 
Kwani ushahidi wa picha unatosha kukuaminisha siyo? Je kama alitundikwa?

Kesi ya watu kujinyonga selo zmeshatokea sana wengine wamejinyonga na suruali zao inabidi sahiv mtu akiingia selo aingie na boksa tu
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kunyongwa na kujinyonga , picha ni ushahidi wa kwanza sio wa mwisho
 
Kwani ushahidi wa picha unatosha kukuaminisha siyo? Je kama alitundikwa?

Kesi ya watu kujinyonga selo zmeshatokea sana wengine wamejinyonga na suruali zao inabidi sahiv mtu akiingia selo aingie na boksa tu
Bila shaka hujawahi kuingia mahabusu. Mahabusu hazijengwi kama nyumba ya kuishi.

Hiyo suruali utaitundikaje katika chumba chenye kadirisha kadogo kalikowekwa juu kwa lengo la kupitisha mwanga na hewa pekee? Utapanda kwa kutumia kifaa gani?
 
Back
Top Bottom