Lie,lie ,lie .angalia syria ,iraq ,yemen ,afghanistan,lebanoon .somalia. Wanauwana kilasiku ,sijui mungu gani huyo unae mzungumzia . Njoo huku tukubatize kwa jina la yesu
Bwana Chama,
Ikiwa kwa hakika uanpenda kujua historia ya Bakwata kwa undani wake nakuomba tafadhali soma kitabu changu. Kisa kizima nimekieleza humo.
Hapa nafasi itakuwa ndogo na nitawachosha wanaukumbi.
Asante sana kwa uchambuzi wako makini. Barubaru amekosa kabisa uungwana, anatumia uislam kama mwamvuli kueneza chuki zake dhidi ya Nyerere! Ama kweli dunia haitaisha maajabu.Gwalihenzi;
Barubaru asikuumize kichwa ni mmoja kati ya wanafiki wakubwa hao ndio wanaodai mfumo kristo cha ajabu yeye watoto wake wanaishi na kusoma Marekani kwenye mamilioni ya wakristo; Barubaru huyu huyu amesoma chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa sera za Mwalimu Nyerere; Barubaru amesoma Canada kwa pesa za walipa kodi wakristo wa Canada; hana jipya; kama si sera za Mwalimu Nyerere Barubaru angekuwa mvuvi Pemba au anauza Ice Cream kwa Bakhresa
Chama
Gongo la mboto DSM
Mkuu jaribu kumjibu nguruvi kwa hoja...kuna hoja hapo zinahitaji majibu siyo kuishia kusema ushahidi upo...Hoja nzuri na zinahitaji majibu ambayo yatamfahamisha msomaji ukweli wa mambo.
Waislam wamegundua mengi katika mfumo wa serikali yetu na wameitahadharisha kuwa kuna upendeleo kwa Wakristo na hujuma dhidi ya Waislam.
Ushahidi upo.
Rejea tu matatizo ya hivi karibuni yaliyogunduliwa NECTA achilia mbali utafiti wa Warsha wa mwaka 1991 na aliyoyagundua marehemu Prof. Malima ndani ya Wizara ya Elimu.
Ingependeza kama serikali yenyewe ikatoa majibu.
Serikali iko kimya majibu yanatolewa na watu wengine kabisa kama hivi humu JF.
Somo hili mimi nimeliandikia kitabu kizima.
Itakuwa vigumu kukupa jibu humu JF.
Hata hivyo ukiwa una wasaa soma kitabu changu "Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...." sehemu ya tatu ya kitabu inaitwa, "Njama Dhidi ya Uislam."
Hapo utasoma nilichosema kinachofanyika kwa miaka mingi dhidi ya Waislam kuanzia ukoloni wa Wajerumani hadi hivi sasa.
Kitabu hiki ndicho kilichonifanya nikajulikana kwingi.
Maudhui yaliyo ndani ya kitabu hiki yamegusa fikra za wasomi wengi duniani.
Haijafanyika utafiti wowote kuhusu siasa za Tanzania sharti mtafiti apitie kitabu hiki.
Hapa jamvini kitabu hiki ni mashuhuri.
Mimi niko tayari kusimama na yeyote na mahali popote kuhusu mada hii.
Kwa Mzee Mohamed, chochote kinachomilikiwa, kuongozwa au kuhusishwa na BAKWATA, hicho si cha WAISLAMU ikiwemo BAKWATA yenyewe!Kinondoni Muslim School sio shule ya waislamu??? Nimewahi kufundisha kwa muda mfupi kabla waalimu "wagalatia" kufukuzwa kwa kuwa tu ni "wagalatia" leo hii imekuwa si shule ya waislamu!! Makubwa haya!
Mkuu wangu Mohamed Said, tatizo lako ni kuwa unapenda sana kujisifu halafu unasahau ulichokwisha kisema. Kule kwetu kunausemi kuwa ukiwa muongo usiwe msahaulifu, kwakuwa umesahau bora nikukumbushe maneno yako wewe mwenyewe ya kujisifu kuhusu usomi wako;Majisifu si uungwana.
Ikiwa umeona hapo nimejisifu ukweli ni kuwa sijafanya hivyo.
Aliyetoa sifa za usomi si mie mimi nimejibu tu kuwa sijasimama katika mada ya usomi.
Kasifiwa mtu kwa "nondo" na "usomi" kuwa nimeshindwa kumjibu huyo msomi.
Ndipo nakasema sijasimama katika usomi.
Hayo unayoita "majisifu" ni maelezo yangu nifahamike kwa wasionijua.
Bwana Gwalihenzi,
Ingekuwa mie nataka kushindana humu kwa usomi nadhani ni wachache sana wangekuwa na ujasiri wa kusimama na mimi uso kwa uso.
Mimi sishindani na usomi wa Nguruvi3 na nadhani yeye binafsi hilo alishalitambua kwangu siku nyingi sana.
Duuh! we mzee kiboko....hii inaitwa counter attack a.k.a za uso.Wanajamvi,
Nimefuatilia mjadala huu nikidhani kuwa tunaijadili mada kama ilivyoletwa. Tofauti, naona takwimu za elimu na mengine yasiyo na uhusiano na mada. Ukifutailia utagundua kuwa MS anakwepa kujibu hoja na kutumbukiza mengine au zile mada zake zimewaingia vema baadhi yetu na kila mara wanazifikiri bila tafakuri.
Wanakosa tafakuri kwasababu makala za MS zinachanganya na zinahitaji utulivu na fikra kuzielewa na kuzinyumbulisha ili upate hitimisho alilokusudia. MS anauwezo sana wa kufanya majumuisho yanayoeleweka kiurahisi sana kwa wale aliokusudia (Conclusion) hata kama hawaielewi mada...
Hana hoja za kupambana na Nguruvi3 wala Chama eti anadai akifunguka kwa mahoja ataijaza JF yote na wanaukumbiwMkuu jaribu kumjibu nguruvi kwa hoja...kuna hoja hapo zinahitaji majibu siyo kuishia kusema ushahidi upo...
Pole sana kwa yaliyo kukuta...walikushuku umebeba madawa na si kwa sababu za kidini la hasha...hii inatokana na nchi unazotembelea mara kwa mara hivyo walikuwa na haki ya kukukagua..hata polisi wakimshuku mtu wana haki ya kumpekua kwa mujibu wa sheria.Wangeamua kukumaliza wangekuwekea dawa za kulevya.hivyo walikushuku tu na si vinginevyo..
mzee said,
awali ya yote nieleze neno linalotumika katika medani ya vita. Neno hilo ni 'shoot any moving object'.
Kauli hii inatumika majeshi yanapokuwa katika wakati mgumu, ya kwamba mbinu zote zimeisha na hakuna mkakati. Nitafafanua wakati nahitimisha maelezo yangu.
Kwa mtu asiyeielewa tanzania na utangamano wa wananchi wake wenye imani, makabila na itikadi mbali mbali za kisiasa,pindi anaposikia mihadhara yako ima anatishika sana au anajawa na hasira kama ulivyowajaza wanigeria.
........"!
Matatizo ya waislamu yameanza siku nyingi,lakini mimi kwa umri wangu mkubwa nilio nao sijawahi kusikia au kuona muislamu akionewa,akinyanyaswa na mkristo kuanzia shule ya msingi hadi chuo nilichosoma eti kwa kuwa tu ni muislamu,kwa maoni yangu ni kwamba waislamu hawajiamini na dini yao kwamba ni ya kweli.kama dini ya uislamu imetoka kwa Mungu wao wana wasiwasi gani juu ya wengine? wafuate dini yao inavyosema,wawapeleke watoto shule na sio kubaki kusema tu Wakristo wanapendelewa.Siku zilizopita waislamu walichoma makanisa Zanzibar kisa muungano,lakini wakristo hawakusema lolote kwa sababu wanamtegemea Mungu atawapigania,jiulize ingekuwa msikiti umechomwa moto sijui ingekuwaje.
Sijaelewa, huyu Mohamed alikatamwa kwa sababu ya dini yake? Na kwenye ndege ni yeye pekee alikuwa muislam?
Ndio nini tena!! wamissionary walipokuja Africa pamoja na dini walitoa elimu kwa watu wao kwa sharti la kubadilisha dini ili uwe mkristo,lakini,waarabu wao wakaleta quoran tu na matokeo yake waislam wengi hawajasoma.Sasa unalalamika niniMen lie, women lie numbers don't lie
Mzee Mohamed,Bwana Erick kwa kuwa umesema una umri mkubwa ni wazi mie nawe tutakuwa tunalingana umri.
Kwa jili hii hata mijadala baina yetu itakuwa ya kiungwana zaidi.
Bahati mbaya inaelekea hujui nchi yetu inatawaliwa vipi na nani kashika madaraka na hayo madaraka yamepatikanaje.
Lakini nina hakika ulishuhudia harakati za kudai uhuru kama ulikuwa Dar es Salaam itakuwa umewaona wazee wangu walivyokuwa bega kwa bega na Nyerere kupambana na Gavana Edward Twining.
Nimeandika kitabu "Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes..." ni kitabu maarufu unaweza kukipata Tanzania Publishing House, Samora Avenue.
Kitabu hicho kimeeleza mambo mengi kuanzia jinsi TANU ilivoundwa, harakati za uhuru, wafadhili wa harakati, nini kilitokea baada ya uhuru, ugomvi katika ya Nyerere na Waislam kuanzia 1963, kuwekwa kwa masheikh kizuizini mwaka 1964, Kuhujumiwa ujenzi wa chuo kikuu cha Waislam mwaka 1968 na Nyerere na mwishowe kuivunja East African Muslim Society (EAMWS) taasisi iliyokuwa ikitaka kujenga chuo hicho Bakwata ilvyoundwa nk. nk. harakati za Waislam chini kwa chini kudai haki zaokuanzia miaka ya 1970 hadi kufika hapa tulipo leo.
Yaliyomo humo yamebadilisha historia yote ya Tanzania.
Ndiyo unaona humu JF tunajadili mambo ambayo miaka labda kumi iliyopita hakuna aliyekuwa anayajua.
Binafsi nimezunguka kwingi, Afrika, Ulaya, Marekani nikifanya mihadhara katika vyuo na kuhudhuria makongamano.
Somo hili la matatizo ya nchi yetu yanafahamika na baada ya yaliyotokea Rwanda wapenzi na marafiki zetu wanaiomba serikali yetu isipuuze malalamiko ya Waislam.
Wanashauri yazungumzwe matatizo yote bayana na kasoro zirekebishwe.
Nadhani hadi hapa umepata picha kidogo.
Kilichobaki ni wewe kufanya bidii kujua zaidi.
Kulikoni?
Ninakuhakikishia ndugu yangu hakuna Muislam anaeweza kuthubutu kunyanyua mkono wake kuchoma kanisa. Allah (SW) ametukutaza hayo. Makanisa yamechomwa na maadui wasioitakia Zanzibar kheri. Kanisa la Mkunazini lipo Zanzibar zaidi ya miaka 100 mbona Waislam hawajalitia kibiriti?
Tafakari ndugu yangu tusichonganishwe tukajagombana bila sababu na mwisho sote tukajuta tukajiuliza.
Ilikuwaje?
Majuto siku zote ni mjukuu.
Huo ndiyo ukweli.
Bw.mohamed said,usicheze na mwisrael yeye ni hatari,kwani hao marekani wanafanya mambo ambayo israel inayataka.Mwakijila,
Baada ya mkasa ule nikajaelezwa kisa cha kukamatwa kwangu.
Nimeeleza katika makala.
Kile ambacho sikupenda kueleza ni kuwa wakati naandika pp ile nilikuwa naingia katika web ambazo nilionywa nisifanye hivyo.
Mimi nilikaidi.
Ahsante kwa mchango wako.