Udhalilishwaji wa waislam na vyombo vya dola

Mzee Mohamed Said naona kama umeamua kurudi kivingine kuleta ile historia yako yawapigania uhuru.

Nimeisoma vizuri hadithi yako ambayo imechukua kama 92% ya mada yako na nimeshangazwa katika matukio hayo ya kusikitisha yaliyokutokea mwaka 2006 hukuwahi kutaja raisi aliyekuwa madarakani kipindi hicho. Vivyo hivyo hukuwahi kutaja nani alikuwa madarakani mwaka 1993 wakati ndugu zetu waislam wanapigwa na mabomu ya machozi lakini hukusita kumtaja Nyerere mara mbili katika paragraph ya kwanza. Unawea kutueleza kinagaubaga kwanini hukuwataja?
 


Majibu na kejeli zako zinaonyesha unakijua kilichomkuta huyo Shekh. Hakuna marefu yasiyo na ncha.
 
Ni kweli kabisa unachosema vijiwe vya kahawa ndio maskani yangu, mie ni mtu wa kujichanganya sana sina matabaka ndio watu wangu.
Siyo kujichanganya huko mkuu vijiwe vya kahawa vina watu wa aina moja
 
Pole sana Mohamed Said, haya yana mwisho
 
Ha, ha, haaa! mbavu zangu...hadithi njoo, uwongo njoo, utamu kolea!
 
Mengi na mtoto wake walinusulika kubambikiwa madawa ya kulevya hapohapo uwanja wa ndege kisa eti ni wakristo!
 
Mzee Said,
Awali ya yote nieleze neno linalotumika katika medani ya vita. Neno hilo ni 'shoot any moving object'.
Kauli hii inatumika majeshi yanapokuwa katika wakati mgumu, ya kwamba mbinu zote zimeisha na hakuna mkakati. Nitafafanua wakati nahitimisha maelezo yangu.

Kwa mtu asiyeielewa Tanzania na utangamano wa wananchi wake wenye imani, makabila na itikadi mbali mbali za kisiasa,pindi anaposikia mihadhara yako ima anatishika sana au anajawa na hasira kama ulivyowajaza WaNigeria.

Kwa mantiki hiyo utaangaliwa kwa jicho toafauti na lile la Kapuku Nguruvi3.
Umaarufu unagharama zake na katika dunia ya sasa gharama yake ni hiyo ya wewe kuangaliwa kwa jicho mujarabu si kwasababu ya jina lako au imani yako, bali kwa facts na spinning zako katika habari.

Kwa kuanzia hili la vyombo vya dola, mtu anayesoma vizuri 'between the lines' atagundua mambo kadha.
1. Umeeleza kisa cha Sheikh Amir kufukuzwa akiwa na khanga kana kwamba huyo alikuwa malaika.
Umesahau kuwa ukombozi unaosema ulifanywa na Waislam ulikuwa si bahati mbaya bali mikakati.
Sijui utawezaje kumsafisha Sheikh Amir kwa hilo ili serikali ya Nyerere ionekane imemuonea. Hata hivyo, hivi Mohamed, Sheikh huyo angefanya alichokusudia leo ungeandika kama kaonewa au shujaa?

2. Katika kueleza kisa cha Sheikh Amir,umemtaja Nyerere na Siyo serikali ya Nyerere 'iliyomdhalilisha'.
Ilijuzu uwe 'consistently' katika kuelezea visa vilivyofuata.
Sijui kwanini mabucha ya Nguruwe yalipovunjwa husemi serikali ya Mwinyi unasema 'mapambano ya waislam na vyombo vya dola'? Sijui kwanini unapoeleza masheikh waliogaragazwa Bagamoyo usiseme Kikwete unasema vyombo vya dola? Je hii siyo double standard na kwamba inaharibu mtirirko mzima wa maoni, mada au tuhuma zako!

3. Viongozi wa dini hasa wageni wanatakiwa watoe taarifa ili kuwalinda na kulinda hadhi zao. Mara nyingi kiongozi wa Ismailia au Shia anapokuja nchini hupewa waongozi tena wakiwa na vimuli muli. Je, huyo Mufti wa Yameni alijulikana yupo nchini na alitolewa taarifa za uwepo wake? Hivi askari watawezaje kuwatambua wageni maarufu kwa mavazi tu bila taarifa?

4. Mohamed, unaweza kuuthibitishia umma kuwa ni viongozi wa kiislam tu ndio 'wanaodhalilishwa' na hakuna wa imani, au wapagani wanaofanyiwa hivyo? Je, wazee wa iliyokuwa EAC nao walipobebwa na Landrover walichaguliwa kwa misingi ya dini au majina yao? Je, yule Padri aliyeondolewa miaka 70 kwa amri ya 24hrs naye alikuwa Mwislamu?

5. Tunapoongelea bunge kukubali sheria ya kigaidi umesema ni shinikizo la Wakristo na wala si shinikizo la Bunge.
Sasa, kwanini masheikh wakidhalilishwa isiwe ni shinikizo la Said Mwema liwe la vyombo vya dola?
Je, mzee Said, mumewahi kumona IGP kuhusiana na sakata hili? Je IGP angekuwa John William Joseph hadithi hii ingebeba kichwa cha hapo juu au ingegeuka kuwa hadithi ya kanisa? Je, ilikuwaje Rais Kikwete anayejua hadhi ya Mufti aachilie vitendo vya namna hiyo, achilia mbali Urais wake?

Mohamed, wengi tunasafiri duniani na tunakutana na vituko vya ubaguzi. Siku moja nilikuwa Dubai nikaona Raia wenye rangi nyeusi wakiwekwa pembeni na passport zao kuingizwa kwa uchunguzi zaidi. Raia wengine hasa wa kihindi wenye passport za nchi hiyo hiyo waliachiwa kuingia ndani ya ndege bila kikwazo. Sasa hapa tusemeje, waliobaguliwa kwa rangi na Waarabu wale wale unaodhani ni wema sana kuliko Wamarekani ilikuwa ni halali yao au iliuma kama inavyokuuma leo hii

Lakini pia lazima ujiulize, iweje London, New York, Sidney, Bon n.k. kuna miskiti na lisiwepo kanisa Saudia au Bahrain kama yalivyo kwa wenzetu. Hapa kuna nini kama si ubaguzi.

Lazima ujiulize,kwanini mtu aombe ukimbizi Australia na siyo Malysia, Uingereza na siyo Saudia, New York na siyo Qatar?
Je, hapo hakuna ubaguzi? Huko wanakofikia Ulaya na Marekani kwanini wasibaguliwe katika 'social security' ambazo wao ni wafaidika wakubwa kwa takwimu za Uingereza, Australia, Canada na Marekani.
Kwanini majina yao yasiwahukumu kama linavyokuhukumu lako.

Na mwisho, kuhusu kubaguliwa kwa tuhuma za Ugaidi ni makosa kuwalaumu wanaojilinda. Imefika mahali mtu kama Abdumutwalab alivaa chupi ya bomu kwenda kuua watu wasio na hatia ili tu amtie chuki mmarekani.

Majuzi wapo waliokuwa wanataka kulipua majengo tu hata kama majengo hayo wamo watoto. Mohamed Ghailan kutoka ZNZ amelipua ubalozi wetu na kuua watu wasioweza hata kutamka Marekani. Wote hawa wanafanya uharamia na uhuni na ujahilia huo kwa jina la Uislam. Ni nani anayeweza kutenganisha Muislam Gaidi na Muislam Muumini.

Yale ya Nigeria ndiyo ya UAMSHO. Kupinga muungano kwa kuua watu.
Ninachotaka kusema hapa ni kuwa hao wanaojinasibu kuupigania usilam hawafanyi hivyo kwa misingi ya dini.
Hapo ndipo jeshi la wajahidini linapokuwa na kauli yangu ya awali 'shoot any moving object', kwamba hawana mkakati na hawajui wanapigania nini.

Kama unaushahidi kuwa ukiuaa wanadamu 300 wasio na hatia kwasababu tu unataka kuua Mmarekani mmoja utakwenda peponi, basi weka ushahidi huo kwa aya, hadithi na suna na kama huna basi jitenge na utetezi wa kisichodhahiri na kilicho na shaka! Hivyo ndivyo vinakutia matatani. Msome Mkuu Chama hapo juu.

Watu wanaokusikiliza usidhani ni wajinga! wanafanya tafiti na huenda wanakubaliana nawe au la.
Kitu kiomja nachopenda kukuasa ni kuwa una maneno ya uchochezi sana tena ukipindisha hadithi ili zilete kile ulichokusudia. Una ajenda ya kisiasa nyuma ya mgongo wa dini. Kwa vile unazunguka duniani nitaishangaa serikali yoyote itakayokuangalia kama inavyomwangalia Kibwengo na kapuku Nguruvi3. You deserve thorough scrutiny the least to say.

When there are no rules of engagement, anything is fair!
 

aCHA UDAKU WEWE! nYerere aliwalea vizuri sana waislamu kupita uwezo wako wa kufikiri. aliwanyang'anya wamisonari shule na kuhakikisha waislamu watasoma bila kubaguliwa kidini. Pugu, minaki, tosanaganga, chidya na kigonsera ziliwasomesha waislamu wengi sana bila kubaguliwa kwa sababu ya mapendo ya nyerer kwa wailsamu. leo hii mu Irani nakupatia schoraship ya kuchochea dini TZ unamuona ni bora kuliko JKN?
 
NI maaskofu wangapi waliorudishwa makwao au kuwekwa kizuizini wakati wa Nyerere?
kwa nini wapelekwe?wewe umesikia wapi maaskofu wa Nigeria wamefanya revenge kwa mauaji ya kinyama ya kinyama ya boko haram kwa wakristo?
 
Kweli nimeamini jinsi elim ya mwarabu ilivyoamuathiri mwafrika, yani personal issue inazichanganya na dini? Huyu mleta thread nashindwa kuelewa hata elimu yake ni jinsi gani imemkomboa? Tuseme basi Na Godbless lema alivyotesa ARUSHA ni kwa sababu ya dini yake? Ulimboka je? Alafu dunian kote na hata historia inajidhirisha kuwa materrorist wengi ni waarabu maana hata kwenye dini yenu mnafundishwa kujilipua eti mtaenda ahera, sasa Rasi na viongozi wengi wa juu ni dini yenu sasa mnataka nini? Tatizo nyie mnataka nchi yote tuwe waislamu na tuongozwe na sharia kama jinsi historia inavyojionehsa west Afirica kwenye jihad war!

Mungu wangu wa Israel awahurumie nyie na hizo inferiority complexity zenu.
 


Nitakuwa sijibu posts ambazo hazikuandikwa vyema.
 
Sasa hapo ikaja kejeli. "Ala wewe mtu wa Kariakoo lakini umefika hadi Chuo Kikuu!" .... Ndipo ikatengenezwa hadithi ya kuku jike na ng'ombe dume (cock and bull story)
Sikujua kwamba kumbe cock ni kuku jike. Nashukuru kwa kuchangia elimu yako ya "nimefika Chuo Kikuu japo natokea Kariakoo."

Lakini yule mchezaji wa Simba ni Muislam na yeye ndiye aliekuwa mkubwa pale akiongoza ile shughuli yote tena kwa kujidai na kujifaharisha sana.
Sasa kama afisa mkubwa aliyekumata airport ni Muislam, unasema mwenyewe kiongozi wa wanausalama waliokukamata pale ulimtambua alichezea Sunderland na Simba na ni Muislam, itakuwaje useme ulikamatwa kwa ajili ya uislamu wako na ni kazi ya Kanisa? Huyu afisa Muislam alitumwa na Kanisa? Muamedi unaona jinsi usivyokuwa na intellectual honesty? Halafu unatuambia kama ulivyowaambia maafande eti nimesoma chuo kikuu japo natokea Kariakoo, bila kuulizwa. Umesoma nini huko chuo kikuu ukitokea Kariakoo?

Ujerumani niliambiwa mzigo wangu umepotea lakini hata kabla sijatoka uwanjani nikatafutwa na kukabidhiwa mzigo wangu na kwa hili sikuwa peke yangu ... New York kadi yangu ya benki ilikataa kutoa fedha kwa siku nzima hadi siku ya pili.
Sasa kama mzigo wako ulikuwa misplaced kwa dakika chache na "kwa hili sikuwa peke yangu" kwa nini ujifanye kwamba wewe ndio ulikuwa targeted wakati ushasema mwenyewe "kwa hili sikuwa peke yangu"? Such mindless, contradictory arguments.

Kadi ya benki imekataa kutoka fedha, kisa Muislam! Incredibly ridiculous! Unawapa waislamu jina baya. Wewe ndio unafanya Waislamu watukanwe na kudharauliwa kwamba hawaishi ku whine and pine kila uchwao. Kikadi chako sijui cha Tembo sijui cha nini kimekwama New York, kisa Muislam! How preposterous is that?


Kumbe sababu ya kukamatwa ni "Wamarekani kuleta taarifa Dar es Salaam kutaka taarifa zangu za ugaidi..."

Wamarekani! Sasa hapo Kanisa linaingiaje hapo Muamedi? Unajiona hoja zako zilivyojaa matundu? Kaka, usitangulize kutangaza kwamba "nimefika chuo kikuu," fanya vitu na andika vitu ambavyo mtu akiviona atasema hata bila kuambiwa kwamba huyu Muhamed kweli ameelimika, uwe umefika au hujafika chuo kikuu. Ukijenga hoja za kimadudu madudu halafu unasema umefika chuo kikuu unakuwa kituko! Kwa hiyo Wamarekani wametumwa na Kanisa la Tanzania watume taarifa serikalini ili Muamedi akamatwe Airport! hahahahahaha... that is the height of absurdity.

Muamedi ukiongea utadhani mtu mwenye uadilifu na mtu wa maaana kumbe mnafiki mkubwa, Mwenye Enzi Mungu Subhanahu Wa taala amesema wanafiki "unapowaona, miili yao inakupendeza, na wakisema, unasikiliza usemi wao. Lakini wao ni kama magogo yaliyo egemezwa. Wao hudhania kila ukelele unao pigwa ni kwa ajili yao."

That verse is typical of you Muamedi, unajishtukia na ku play victim kumbe huna jema, kazi kutukana imani za wengine na kutupandia mbegu ya chuki za kidini tu. Hampati msamaha nyinyi ujue, Maandiko yanasema "sawaon aalayhim astaghfarta lahum amlam tastaghfir lahum lan yaghfira Alalhu lahum inna..." Hupati msamaha wewe almnafiqoona mkubwa!
 
Karibu tena Brother MS............
 
Karibu tena ... Kaka yetu .. mwalimu wetu.. Mohammed said.. darasa lako huru sikuzote linaeleweka pamoja na mashambulizi uyapatayo
 
GREAT THINKERS

badala ya kujibu hoja na kuzivunja hoja za MSAID mmeishia kumshambulia binafsi

watu wa ajabu sana nyie mnaojiita ma great thinkers
 

Umenikuna sana. Hoja zote ni za msingi. Unajua kuna waislam wazuri tu na wanaishi kwa kufuata imani yao na hutaona hata siku moja wakilalamika lalamika kama watoto wadogo. Wanachofanya ni kuendelea na shughuli zao za kuendeleza maisha yao huku wakitumia fursa za kiuchumi. Waislam wa aina hii, hata familia zao utaona zimejaa wasomi na zinathamini elimu.

Waislam wa aina ya mtoa uzi, kazi yao ni kukaa vijiweni na kuwajadili wakristo. Wanapoteza muda wao kwenye vijiwe vya kahawa huku wakijadili mambo yasiyo na maana zaidi ya kujenga chuki zisizo na msingi. Mleta uzi anachohitaji ni huruma ya waislam wenzie kwa jambo ambalo ilikuwa ni halali yake kufanyiwa. Upuuzi gani huuu, ptuuuu!!
 

Mnajitungia uongo na mnaufanya ukweli. Kwa nini shule za taasisi za kidini zilitaifishwa? Taasisi zipi ziliathirika zaidi kwa shule zake kutaifishwa? Kulikuwa na mgao shule za sekondari (mwanafunzi aliepata C Mtwara alichaguliwa kwenda sekondari huku aliepata B Moshi akikosa kutokana na nafasi walizotengewa) lengo lilikuwa nini kama sio kuwapa upendeleo watu wa mikoa uliyoitaja?
Mnang'ang'ana "oh Marekani adui wa uislamu", mbona waislamu hawaachi kuhamia huko? Ukweli ni kuwa muislamu alieko USA anaishi maisha ya amani zaidi kuliko alie Iran! Mtasema machafuko yanayotokea Mali leo hii chanzo chake ni Marekani? Hamna mnachokipenda zaidi ya vurugu nyie watu! Dini gani isiyohubiri uponyaji bali kuua kuua na kuua? Sidhani uislamu ndivyo unavyofundisha, labda uislamu wako na mleta maada!
Give us a break!
 
Yeah naUlimboka alitekwa na kuteswa kwa sababu ni mkristu!!!

Afande msangi ni dini gani vile, aliyemtuma ni dinio gani vile? mbona wakristo hawajalalamika kuwa serikali au waislamu walitaka kumuua Ulimboka? hakuna taasisi yoyote ya kikristo, wala padre wala mchungaji, je ni wajinga au wanyonge? Muuaji ni muuaji tu bila kujali dini yake. Kati ya waliotaka kumuua unaweza kuona wana dini,jinsia, na makabaila, mikoa, wilaya et etc....kwanini tusianze kuangialia mengine tunaangalia dini.


Mwanakijiji i get your point, these people are ****** and uneducated fools. I think we should start to respond to them rigorously and show how stupid they are. Kiongozi ni kiongozi kutokana na uwezo wake na si kutokana na dini yake, muuaji huwa hachagui mwislamu au mkristo. I am sure serikali imeua wakristo na waislamu, that makes us the same. Huo ujinga wanaouleta hao wapuuzi unatakiwa kupigwa vita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…