Inauma!......mpaka lini? mpaka lini?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Inauma!......mpaka lini? mpaka lini?
Hata maovu yanazidi kuongezeka duniani, so what does that tell you?
Mwanakijiji! mzee wetu Mohamed Said ameianza nakala yake kwa kuturudisha nyuma kidogo na habari ya yule Sheikh aliyerudishwa "kwao" Zanzibar halafu akaendelea kutupeleka mwaka 1964 wakati masheikh wengi waliwekwa kizuizini, hakutuacha hapo bali alitukumbusha mwaka 1993 ambapo kulizuka tafrani kati ya askari na Waislamu akamalizia tukio la Sheikh Kishki juzijuzi na Mufti wa Yemen halafu akaunganisha na lilomkuta yeye.Yeah naUlimboka alitekwa na kuteswa kwa sababu ni mkristu!!!
NI maaskofu wangapi waliorudishwa makwao au kuwekwa kizuizini wakati wa Nyerere?Wee jamaa unaonekana ni mtu mzima na msomi lakini hoja zako ni za kitoto ile mbaya! Hivi wakati wa kipindi cha Nyerere ni watu wangapi waliokuwa detained kutokana na sababu mbalimbali? Au walioondoshwa na kurudishwa kwao; wazungu kwa waafrica? Tukianza kuwa na akili na mawazo mgando kama haya, basi hata wakinga watakuja na kichwa cha habari kinachosema udhalilishaji dhidi ya wakinga kwa kuwa tu Tuntemeke Sanga alinyanyaswa na Nyerere. Au wale watu wa Ukerewe watakuja na hoja kama hizo hizo kwa kuwa wengi wa walioko kule walipelekwa kama adhabu. Ni ufinyu wa fikra, kutolea mfano wa shehe aliyerudishwa Zanzibar kama mfano wa unyanyasaji dhidi ya uislamu.
labda walikuwa hawana kiherehere kama hao masheikh ...NI maaskofu wangapi waliorudishwa makwao au kuwekwa kizuizini wakati wa Nyerere?
Anazungumzia kilichotokea BAADA ya uchomwaji wa mabucha ikimaanisha waliingizwa hata wasiohusika!S.Liondo said:katika kuusoma uzi wako nimegundua kwamba una udini wa hali ya juu, maana chuki uliyonayo dhidi ya watu wa imani nyingine na hasa wakristo inajidhihirisha wazi kabisa katika maneno yako hilo huwezi kukana. Ina maana wewe uliona ni halali kabisa waislamu kwenda kubomoa mabucha ya nguruwe kwenye nchi kama hii ya watu wa imani zote? Hii maana yake nini hasa?
Hapa inabidi ututhibitishie kwanza kuwa ni Waarabu Waislamu ndio walioleta utumwa Tanganyika.S.Liondo said:Halafu umetuambia waislamu walipigania uhuru dhidi ya wajerumani na waingereza, mbona hukusema kama wapigania kuondolewa kwa utumwa ulioletwa na Waarabu ambao ni waislamu wenzako? Au kwa kuwa unyama huo uliofanywa dhidi ya waafrika wenzetu ulifanywa na mwarabu mwislamu basi unakuwa ni halali? Kwahiyo ubaya ukitendwa na mtu wa imani nyingine ni dhambi lakini ubaya ule ule ukitendwa na mwisilamu unakuwa ni safi na halali. Umeona jinsi ulivyo na chuki za kidini?.
Hawa "wanaolialia" na kupanda majukwaani na kuelezea hisia zao au wanaoandamana ni watu wazuri Mkuu, ogopa wale wasio lialia!S.Liondo said:Halafu, msipende kuwa watu wa kulia lia kila wakati
Why encouraging the enlargement of the circle of concerns instead of enlarging the circle of influence? Kila siku ni kulia lia tu na kutafuta mtu wa kuwaonea huruma watu wachache wasio na agenda nyingine yoyote zaidi ya Nyerere. Nyerere is gone and we cant change that fact. Kizazi hiki kianze kushughulika na mambo yasiyotuhusu ili iweje? Tukumbuke wa mbili havai moja! Tupigane kutoka hapa tulipokwamba.
"Hans Roger Dibagula, utafiti wako ni dhaifu, kwa sababu umeangalia maeneo machache tu na wala haujaainisha hizo nyadhifa. naomba uainishe, na ulete tafiti kamili, sababu hapo sijaona idara nyingine muhimu. ainisha pia ugawaji wa madaraka kwa ngazi tofauti. otherwise siwezi kuiamini tafiti yako, huenda ulikaa tu, kwa vile una MS Word kwenye desktop yako, basi ukawashwa washa mpaka kuja na pumba hizi.
Hili nalo linahitaji uthibitisho? Ina maana wewe historia ya darasa la tano hukusoma? Mbona liko wazi kwamba walioendesha biashara ya utumwa Tanganyika ni waarabu, na kama ni waarabu, definitely ni Waislamu, sasa unataka ushahidi gani tena?Hapa inabidi ututhibitishie kwanza kuwa ni Waarabu Waislamu ndio walioleta utumwa Tanganyika.
Anazungumzia kilichotokea BAADA ya uchomwaji wa mabucha ikimaanisha waliingizwa hata wasiohusika!
Mimi binafsi siwaoni na hatia waliochoma mabucha (lakini hilo ni suala jingine unaweza kulifungulia thread ukitaka, nitakuja huko)Hapa inabidi ututhibitishie kwanza kuwa ni Waarabu Waislamu ndio walioleta utumwa Tanganyika.Hawa "wanaolialia" na kupanda majukwaani na kuelezea hisia zao au wanaoandamana ni watu wazuri Mkuu, ogopa wale wasio lialia!