Udhalimu wa Utumwa Zanzibar na Pemba: Mababu zetu waliteswa, walihasiwa, walibakwa, na kuuawa kinyama

Udhalimu wa Utumwa Zanzibar na Pemba: Mababu zetu waliteswa, walihasiwa, walibakwa, na kuuawa kinyama

Hauna hoja yoyote ni ubaguzi tu,mbona watanzania wingi wanauwa,wanafungwa na kufanyiwa madhira mengi ya kutisha chini ya utawala wa CCM? Na bado mnachukua nchi,udharimu hauna rangi wala dini wala kabila,udharimu ni udharimu tuu,kwani aliyeua wazanzibar 2000 ni Sultan???acha unafki
Umepanic sana, pole.
 
Mkuu naomba nikurekebishe kwenye modern slavery wahabeshi,wasomali na sudan wenye light skini hawakupelekwa utumwani naomba kutoa hoja
Historia inasema Nchi zote zilizoko ktk Fukwe za Bahari ya Hindi zilihusishwa ktk biashara ya Utumwa.
Hatq BIBLIA book of Leviticus INAELEZEA UTUMWA uliokuwa Huko ETHIOPIA Wakati huo hata Somalia ilikuwa ndani ya ABYSSINIA. Na kabla ya hapo ikiitwa THE Kingdom of Kush(1070 BC–AD 350)

Sasa unaposema Wasomali na Wahabesh hawakuwemo Ungeambatanisha na Ushahidi wa HISTORIA Inaokubalika ili tukufahamu Vizuri vinginevyo utakuwa Unaleta vitu kutokana na Fikra zako binafsi. NA Hili ni kosa Kubwa sana Ktk Kuandika Historia.
 
Ni heshima ya mkwe kufunika uso kwa vidole huku ukichungulia! Lugha yangu ni fasaha na ya kizanzibari ijapokuwa imechafuka kidogo kutokana maisha yangu niliyoyaapotezea Tanganyika kwa muda mrefu.

Mimi sijali nani anashika dola, lakini awe na mapenzi na Zanzibar na watu wake. Aheshimu silka, Imani na desturi na Mamlaka ya Zanzibar.

Uundwaji wa tume ya maridhiano ilikuwa moja ya ahadi ya chama cha CUF kama ikiingia madarakani.Wazanzibari wakaitikia wito na kuichagua CUF. Lakini Uamuzi wao ulizikwa pale majeshi ya JWTZ ilipozima demokrasia na azimio hilo limegeuka ndoto.

Mtawala Tanganyika hapendi kuiona Zanzibar kuwa kitu kimoja. Wanaendeleza siasa za DIVIDE & RULE ili kuzidi kututawala pamoja na rasilmali zetu
Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika iliyomegeka miaka mingi nyuma, yule Mwinyi Mkuu aliyemkaribisha Mwarabu, ni Mtanganyika, walipomchoka Mwarabu, wakamtimua na kuitawala Zanzibar wenyewe. Kati ya Tanganyika na Zanzibar, nani anatumia rasilimali za mwenzake?!.

Mali ni yako mwenyewe unakuwa huru kuitumia utakavyo!, ila kuna mtu alikaibishwa, akazoea na kujiona mali za makaribisho ni zake, aliporudi mwenyewe mwenye mali zake, mgeni mkaribishwa kaambiwa akae kando, anaona kama anaonewa!.

Pasco
 
Uzi wa mauaji upo na tumeichangia kule, huu ni uzi wa madhila ya Utumwa na mababu zetu walichofanyiwa na Waarabu!.

Nyuzi zipo, tena kipindi hicho mimi nilikuwa newsoom, ni mimi niliyeripoti yale ya Mwembechai, ni mimi niliyeripoti yale ya Zanzibar, na Mwembe Madema nimelala, tena niliwa na Ali Saleh wa BBC, kumbe mwenzangu ana chama!, saa hizi yuko bungeni!. Mimi sina chama niko mtaani!.

Pasco
Pasco,
Ally Saleh ni ''level'' nyingine.

Yeyote mwenye uwezo wake ana haki ya kuwa Mbunge
na zaidi ya Mbunge.

Namfahamu vyema Ally Saleh.

YzLoxEtF2KigvnfEfYg76jWBGcfnFqIZ_C1srjbkSI3IwiFw8a3vALz4biWl_d5MbMgX3s0c2bL2PxR2jyLdPCr7UgtdYzNFeKuuerGcDFp6p2CswLCSTO8nkk6ZfyPBt4YY5SMJRgRs93zdPNpIJxr95hi5coMEsAv50q7OKjpqYVJVoooC3lz16uyi-Rv-0eGl76aRdTx9XQboQu_Bd0JVPJgdjl-JGlRIXCeAx2X0TSlcFl8tL7NbWdiCxDb9_o2oicCHDrVNq23uDl1QTI5wAlvcbsMHkGhFQyDJblZY31HT-B4B1iav1kYovEabHqlMWABP1CjonZQNt4fNP_nzpLkAjUq-pOTPD-wfRjd3tgWkcGUMQl_oGZHJzw1K2bOC0K9uudSxzqTkYRzeBkV5mWLoNwJADlsPIWzlHlo_NkxWLooOEJU6oR2zYNXNR98s7LjCHgRsPsya9e07bMl0ZzJiM1YkOC85SGe0UvWVQ0mbvmiZf025F47xsL7iZubXYnsRE-KkV_mHemGepiJXNy6c0_c8n4BzKrQgYanP2wlChgSx8MtZ2bsBZTNCm6Oz=w858-h643-no
 
Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika iliyomegeka miaka mingi nyuma, yule Mwinyi Mkuu aliyemkaribisha Mwarabu, ni Mtanganyika, walipomchoka Mwarabu, wakamtimua na kuitawala Zanzibar wenyewe. Kati ya Tanganyika na Zanzibar, nani anatumia rasilimali za mwenzake?!.

Mali ni yako mwenyewe unakuwa huru kuitumia utakavyo!, ila kuna mtu alikaibishwa, akazoea na kujiona mali za makaribisho ni zake, aliporudi mwenyewe mwenye mali zake, mgeni mkaribishwa kaambiwa akae kando, anaona kama anaonewa!.

Pasco
Hii ni hatari, nilidhani una makengeza pekee lakini natongo pia. Hiyo historia iliosema Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika iliomeguka umeisoma Kisonge au Lumumba. Basi na mie nakwambia Tanganyika ni sehemu ya Zanzibar kwa kuitawala kwa karne mpaka akaja mjerumani kukomboeni

Waliomkaribisha mwarabu kuja kuuondoa utawala dhalimu wa kireno ni jopo la maulamaa ( masheikh) kutoka Zanzibar( Mafia, Kilwa,Mombasa, Pemba) waliosafiri kwenda Oman kuwaomba ndugu zao katika imaan, kuja kuwasaidia kuondoa dhulma na fitina ya wareno ambayo ilishanza kuota mizizi.


Nakumbuka mwaka 1974 wakati wa utawala wa Alhaj Jumbem kwenye uwanja wa Amani, Mwl. Nyerere katika hotuba zake za " kisungura" alipoitaka Zanzibar kuchangia shughuli za Muungano si kwa ukubwa la eneo lake lakini kwa mujibu wa ustawi wa Uchumi wake.Huko nyuma Karume alikuwa kagoma kutoa senti kuipa Tanganyika, akilipiza kisasi kuwa Benki ya Tanzania kuilazimisha Zanzibar kununua pesa za madafu za Tanzania kwa fedha za kigeni.

Tanganyika uliuporomosha uchumi wa Zanzibar kutoka kisiwa tajiri kuwa ombaomba. Mafuta yetu mnayakodolea macho. Watu 1.5 Million na rasilmali tuliokuwa nazo ni rahisi kuifanya Zanzibar kuwa Singapore ya Afrika. Lakini hili linawezekana tu tukiwa na Mamlaka kamili ya nchi yetu.
 
Akili za kawaida zishatolewa na kuwekewa kinyesi kichwani. Dini zimeshawafanya mataahira hamjitambui wala hamtaki kuifagamu historia yenu. Baya la Mwarabu linahalalishwa na baya la Mzungu....pumbavuuuuuuuu
 
Kwa mujibu wa nilivyohadithiwa, ilikuwa ni zaidi ya hivyo, lakini kwa vile umenishauri nifute nimefuta ila mambo ya jf, hata vitu visivyo na maana huwa tunaacha tuu. Hicho kisa kizuri kifungulie uzi wake!.

Pasco
Pasco,
Fungua wewe uzi huo mimi In Sha Allah nitakuja kutoa darsa.
 
1) Waraabu hawakuwatesa babu zetu.

2) Waraabu na Wazanzibari weusi (Waislamu) ndio walioteswa na John Okello (kutoka Uganda) na wafuasi wake walipo ipindua Serekali ya halali ya Zanzibar (John Okello na wafuasi wake walifanya mauwaji ya kinyama kabisa, waliuwa maelfu ya Waislamu bila ya hatia yeyote ile).

3) Kwenye uzi huu wa bieshara ya watumwa, kwanini huyu Pasco hakuwataja Wazungu waliowatesa sana Waafrika? na kuwauza Waafrika huko South American na Europe? na wanaendelea kuwatesa Waafrika mpaka hivi leo kwa siasa zao za ubaguzi.

4) Pasco Acha chuki dhidi ya Waislamu
Mkuu pasco ame base zanzibar labda uzi anzisha maeneo mengine .vp au ww mwarabu?
 
Wengi wetu hatufahamu uhusiano kati ya Oman na Zanzibar/Mombasa/Kilwa Na Pwani hii ya Mashariki..wengi tunafundishwa kuwa Wa Oman walikuja kutawala Znz Na pwani yake....Tukumbuke Wa Oman walifika Znz kitambo kwa biashara na Makaazi ya kawaida. Zile Pepo za bahari ziitwazo Moonson zilianza hata kabla ya Yesu...visiwa hivyi na pwani hii ilikua tayari imeshavuka na kufikia dunia nyengine.
Tusome Makala hii ambayo ni nadra kwa vijana wa leo kusomeshwa mashuleni na tumekua wavivu wa kusoma na kufanya tafiti za maana . Tumekua tukiamini kama Pasco anavo amini propaganda za kisonge kuhusu kufagia kwa matiti...
tuone vipi wa Oman walifika mashariki na kuhamia Znz nz Mombasa..namna gani walisaidia kuondoa ukoloni wa kireno walotawala Znz kwa miaka 200. Wareno walifanya ushenzi na hujuma kubwa na mateso lakini haya husomeshwi shule ..kwani tume chaguliwa ya kufundishwa ..
Lakini moja walo liacha Pemba ni Mchezo kufukuzana Na Ngombe !


Uvamizi Zanzibar Msumbiji na kilwa mombasa na Mogadishu na Wareno
Wareno waliivamia Oman na Zanzibar katika karne ya kumi na sita 16.
lakini baadaye wa Omani walifanikiwa kujikomboa kutoka kwa wareno Ukombozi wa Omani ndio ulioleta tija ya kukombolewa kwa zanzibar, kwani ni wa Oman hawa hawa ndio walioikomboa zanzibar Oman ilivamiwa mwaka 1508.
Chini ya Aifonso Albuqueque ambaye aliishambulia Sohar, Maskat, na karyat na kuziweka chini ya Himaya yake wakati Zanzibar Unguja ,ilivamiwa mwaka 1503. chini ya Lawrenco Ravasco na baadaye ilishambuliwa pemba na Francisco da Seixas De'Cabrera.kama ilivyokuwa Kilwa ilivamiwa Fransisco De Almeida akishiriana na vasco Da Gama Mwaka 1505,)
kushambuliwa Unguja kuanzia mwaka 1503 Unguja ilishambuliwa Miezi Miwili Mfululizo na Wareno chini ya Laurenso ravasco hata ilipofika mwaka 1508, Don Duarte Delemos, Gavana Wa Kireno Nchini Ethiopia Alifika Unguja ili kukusanya Kodi, akakataliwa
watu wa Unguja wakapambana Kiume wakishirikiana na wenzao kutoka visiwavywa Pemba na katika mwaka 1631 Francisco de sexas Cabreira alipiga Bomu kasri ya Malkia Mwana wa Mwana na kuifukia kama ilivyopigwa bomu Kiilwa na bagamoyo.
Malkia Mwana wa Mwana alikimbilia na kuhamia Yenen na hakufanikiwa kurudi tena Mpaka Umauti ulipomfika akiwa Jiddah Saud Arabia Mwaka 1638.)
Kasri yake wakaivamia Wareno na kuifanya kuwa kanisa dogo la mwanzo, lakini baadaye kanisa hilo lilivunjwa na I mamu Seif wa Oman alipokuja kuikomboa Zanzibar ' ngome kongwe ndio ilokuwa ikulu ya Malkia Mwana wa mwana hapo zamani ,
katika Unguja baada ya tukio hilo watu wengi sana walikimbilia Oman ili kwenda kujipanga vizuri na kufundishwa mbinu na kupambana na mreno, mwaka 1632 Yusuf bin hassan bin Ahmed kutoka pemba aliishambulia ngome ya Wareno Mombasa,
kushambuliwa pemba kwamara ya mwanzo,kwa mujibu wa waraka wa Jamba Ngome ulioandikwa mwaka 1606 na Mmoja kati ya wazee wa pemba chini ya usimamizi maelekezo wa Sharif bin yusuf bin burhan
waraka huo ulikutwa katikati ya Msahafu (Qur an) na Shekh Theniya bin Khalfan ambaye aliupiga Copy nakala kisha ukatafsiriwa kwa kiingereza na Shekh Abdur rahman bin muhammad bin Jidawy wa kahkama kuu ya Zanzibar na kuhifadhiwa katika makumbusho ya taifa ya beitul Aman. waraka huo unasema hivi,
Baada ya Francico De sexas Cbreira kuivamia Pemba akiwa na kisoni bin jojo ambaye aliingia pemba na meli tano na wanavita wa msalaba wa kireno kutaka kulipwa kodi.
wenyeji wa pemba walikusanyika pamoja na maalimu Juma bin kombo na kiongozi wa pemba akasema tazama hapa wewe kisoni hatutakupa chochote,hatukujui wewe ni nani? sisi sio watumwa wako, kwanza wewe ni nani?
kwa sababu hii kisoni akatangaza Vita lakini wenyeji wa pemba wakapambana kwa muda wa siku 32 kisoni akashindwa kwa mshikamano huo akakimbia na kuondoka katika mwaka 1652, kisoni alirudi tena na meli 65 za wana vita kudai kodi kutoka kwa wenyeji wa pemba lakini walikataa kata kata na walipigana kwa muda wa siku 60, waliua Wareno 1304 na wenyeji 364 walikufa mashahidi, Kisoni hakupata kitu akarudi na watu wake,'
katika mwaka 1656. Kisoni alikuja na Meli 70 za kijeshi zikatua Ras-Mkumbuu zikajipanga kwa mapambano ya siku saba wenyeji wa pemba walijikusanya kutoka kona zote za pemba,ilikuwa ni maadalizi ya kujitolea muhanga zidi ya wareno kufa kupona,
wakati kisoni alipotaka kodi majlis Shura iliyowajumuisha maalimu juma kombo Shsme bin ali, Mfalme haruna bin hassan bin ali na Mwinyi bin Sharif bin Qutb bin mahaz Al Baalawy ,
maalim juma kombo alimwambia Kisoni tumekubaliana kwamba hatukulipi kodi yoyote Kisoni akasema Mkubali msikubali Mtalipa kodi kama kawaida maalim akasema hatuogopi sieee'...
Waraka unaendelea kusema kuwa mwisho walikubaliana kiujanja kuwa watalipa Dirham 12000 na baadaye wataongeza Dirham 16000, lakini zitaanza kulipwa mwaka utakaofuatia
waraka huo unabaini kuwa walifanya hivyo ili bwana kisoni aondoke wapate kujipanga zaidi kwa mapambano, na alipoondoka walisoma Ahlal badri kumuomba mwenyezi mungu kwa tawasul ya watu waliopigana vita vya badr ndani ya wakati mgumu wa mwezi wa Ramadhan...pamoja na nyiradi mbanimbali
husemwa kuwa hiyo ndio dua iliyoombwa kuwa asipatikane Mzanzibar yeyote kuritadi kutoka katika Uislamu ikiwa ataritadi apatwe na madhara na hii imetokezea mara nyingi katika vizazi vya zanzibar,
Mwisho ilishambuliwa pemba na wareno kutamalaki Hollings Worth anahitimisha kwa kusema
hakuna shaka yeyote wala ubishi kkkkwamba wareno walikuwa na hamu kubwa ya ajabu kuhakikisha kuwa wanausambaratisha Utawala wa kiislamu na Ustaarabu wake katika kisiwa cha pemba
na katika Mwaka 1651 Oman ikiongozwa na imamu nasir bin murshid al yaaroud ambapo alifanikiwa kuukomboa Mji wa ormuz mwaka 1622 na Mwanawe imam seif ibm nasir ibn murshid alyaarod alifakiwa kuwatowa kabisa wareno katika mwaka 1631/
Lakini zanzibar ilikaa chini ya Utawala wa kireno tena mpaka mwaka 1696 baada ya kushindwa kwa majaribio mengi ya kutaka kujikomboa, yaani mwaka 1585 waliposaidiwa tena na Utawala wa Uturuki Ottoman Empire/ na kupitia kwa Shambulizi kubwa alilofanya yusuf Ahmed mwaka 1630 ambalo halikuzaa matunda/
Lakini ilipokombolewa Oman mwaka 1632 ndio Chachu ya kukombolewa kwa Zanzibar kwani machifu wa kizanzibar kutoka tumbatu na peeemba wakishirikiana na watu wa Kilwa
waliteua wajumbe kwenda Oman jahazi lilichogwa chwaka Uguja nakwenda kukutana Imam seif ili afanye Ukombozi wa kuwasaiidia zanzibar nae alikubali pale alipokusanya majeshi na kutangaza vita dhidi ya mreno kuanzia mwaka 1696-1698 alipofanikiwa kuikamata Ngome kuu ya mombasa
wakati huo zanzibar katika kasr ya Fatma na Mwinyi Mkuu tayari wareno walishajenga kanisa digo ndani ya ngome kogwe , unaweza kuyaona makombora aliyotumia Imam seif kumtowa mreno yamewekwa mbele ya ndome hiyo kogwe na sasa mengine mbele wa forodhani ikiwa kama kumbukumbu ya tukui hilo,
baada ya kumaliza kuikomboa Zanzibar Imamu seif bin murshid alikuwa tayari kuyarejesha majeshi yake nyumbani kwake oman kama walivyofanya waturuki Ottoman Empire mwaka 1585. lakini Wazanzibar walijikushanya nakuweka shura ya kukubaliana kwamba majesshi ya oman yasirudi kwanza
hivyo kwa kuhofia kwamba wareno watarudi kama walivyorudi mwaka 1586 baada ya waturuki Ottoman empire''walivyorudi kwao, walimsihi imamu sei ayabakishe majeshi yake hapo na washirikiane katika Uamuzi wa zanzibar hivyo basi imamu seif alikubali tena maombi ya ndugu zake katika iman akabakisha majeshi yake hapo, bali akiwa oman aliteua magavana mbali mbali wenye kufanya kazi katika mwambao wa Africa mashariki kupitia Zanzibar na pia wapo Wazanzibar waliteuliwa kwenda kufanya kazi oman chini ya mashirikiano hayo,.
kadhalika alianza kuitumikia zanzibar kwa misaada kuendeleza kilimo bora cha minazi ni yeye ndio aliyeanzisha ukarabati wa njia na kuttawenya visima vywa maji safi na kufanya rutuba iliyowezesha zao la minazi na miti mingine
imamu seif alifariki mwaka 1711, akateuliwa imam seif II kushika Uimamu, lakini naye alifariki mwaka 1728)
akaja Inan said ibn Ahmed ibn ssultan ibn said al Busaid
(sayyid said)
Uchaguzi wa mwaka 1741ulimuweka madarakani imam Ahmed bin said bin sultan al busaid Ambaye naye alishika Uimamu yeye alibadili mfumo wa Utawala na kuwateua magavana (maliwali) wapya na huko mombasa ambayo ilikuwa chini ya uliwali wa Mazrui na huko pate walikuwa ma- al harth
katika mwaka 1746 imam Ahmed alimteua Addullah bin Djad kuwa Liwali Mpya wa Zanzibar, na mombasa na pate,ndipo mazrui wa mambasa na ma-al harth wa pate walipokataa na kujitangazia utawala wao (mombasa Sheikhdom)
katika mwaka 184 sayyd said alikamata madaraka ya Oman na Zanzibar kwa taratibu za kisheria kwa mujibu wa dhehebu lake la ibadhi ni yeye aliyefanikiwa kuumaliza mzozo wa mombasa na pate lakini baadaye mwaka 1826 aliwapa tena indhar
wakati yote yanatendeka mwinyi mkuu wa zanzibar Hassan ambaye ndio Mtawala wa kienyeji aliyewakaribisha wa- Oman zanzibar akimsihi sana sayyid said bora ahamishe makao makuu kuyatoa Oman aje kuishi zanzibar ili ijengeke kama makao makuu au mji mkuu sayyid said hakufanya khiyana aliitikia wito wa nduguye katika iman hatimaye mwaka 1833 alianza kuikarabati Ngome kongwe na 1840 kuhamia ambapo mwanzo aliitumia Mwinyi Mkuu mara baada ya kuondoka wareno
john middleton na jane Campbell wanalezea vizuri tukio hilo la kiungwana kinyume na wale wanaosema sayyid said amekuja kuteka nchi ya zanzibar
sayyid said bin sultan hakuwa ni mwenye kuteka lakini kuitikia wito wa ndugu zake wa iman
Ndio hapo ukaimbwa wimbo wa kibuzi buzi, kuwa ni fumbo la kuimbwa na watoto kueleza
(Njama za kwenda manga omaaan uitwae fumo mkuki na Upanga huku sinba mreno karegea karegea kongwe Mzee hajiwezi)''
mwinyi Mkuu akajenga dunga bweni na kuhamia huko ili kumpisha sayyid said.
mwinyyi mkuu wa zanzibar hassan bin sultan bin Alawy Mtoto wa Mwinyi Mkuu wa kwanza kuhamia hapa Unguja alikuwa Mfalme mwwwaka 1710... na mwinyi mkuu hassan bin Ahmed ndie wa kwanza kuhamia Dunga, kaskazini ya dunga Bweni akimpisha Sayyid said bin sultan mjini,.
kwani fahari wawili hawakai zizi moja ingawa akija sana Mjini kumtembelea na wakisikilizana na akipendwa sana na wananchi mpaka Nyimbo ya kkumbembelezea Mtoto ikimbwa kwa jina lake
karatasi nakupeleka
kwa Mfalme Hassani
na fimbo ya Henzirani,
makosa niliyokosa
nina muombeazi kweani,
Mwombezi wangu nyota
na baraka ramadhani...'''
Lakini pia viongozi hawa walikuwa ni viongo muhimu katika baraza la mawaziri wa sayyid said


Tuwashukuru wa Oman kwa kuwatoa Wareno..

askari wa Malkia baada ya vita ya saa dakika 38.....
View attachment 341277
Thank you very much for the useful information.
 
Mkuu Crabat ukisikia ilmu ndio hii, uzi wako huu umenifundisha mengi ambayo sikuyajua na miongoni mwa haya ni kuwa kumbe Sultan Said Sayyid alipohamisha makao makuu ya sultanate yake toka Oman na kuyahamishia Zanzibar ile mwaka 1832, hakuivamia Zanzibar bali alikaibishwa na mtawala wa Zanzibar aliyeitwa Mwinyi Mkuu!. Wajerumani na Waingereza, Wabelgiji, Wareno, Wataliano, Wahispania, etc kila wakishika maeneo, waliingia mikata na wenyeji, hivyo lazima kuna mkataba Mwinyi Mkuu aliingia na Waarabu kuitawala Zanzibar, hata kama sio mkataba wa maandishi, lakini there must be something, haiwezekani Mwenyeji ampishe tuu mgeni!, kwa mujibu wa bandiko lako, sababu kuu ya Wenyeji wa Zanzibar chini ya Mwinyi Mkuu, kuwakaribisha Waarabu Zanzibar, ni ulinzi wa visiwa hivyo visivamiwe tena na Wareno!.

Hivyo basi pia kuna uwezekano Mwinyi Mkuu aliwaeleza uzao wake, hivyo tishio la uvamizi wa Wareno lilipoisha kabisa, wajukuu wa Mwinyi Mkuu wakawafuata wajukuu wa Said Sayyid, kuwaambia sasa imetosha, tupisheni nyumbani kwetu, na nyinyi rudini kwenu Oman?!, Yaonesha Waarabu walikataa na sijui waliwafanya nini hao waliodai chao! (nahisi waliwafunga mawe shingoni na kuwatosa baharini, na ndio maana Karume kuna watu aliwafanza vivyo hivyo!). Inawezekana kabisa walio organize yale Mapinduzi Matukufu ya 1964 ni masalia ya familia ya Mwinyi Mkuu!, hivyo mapinduzi yale ni haki na halali kabisa ya wenye haki kudai chao kutoka kwa wageni waliowakaribisha tuu kwa makubaliano fulani?!.

Kama Mwinyi Mkuu alivyowakaribisha Waarabu ili kuwalinda dhidi ya Wareno, ndivyo Karume aliwakaribisha Tanganyika kuingia muungano ili kuvilinda visiwa hivi visivamiwe tena na Waarabu?!, hivyo kama ilivyokuwa halali kwa Sultan Mkaribishwa kuitawala Zanzibar kama yake, vivyo hivyo ni halali Mtanganyika mkaribishwa kuitawala Zanzibar ili Mwarabu asithubutu kurejea kwa mlango wa mbele wa kukaribishwa, au kwa mlango wa nyuma wa vikaratasi vya kura?!.

Asante nimejifunza kitu, ila mada yangu katika uzi huu iko based kwenye taarifa hii A report on slavery and the slave trade in Zanzibar, Pemba, hivyo ukiisoma na kuichambua lipi ni la kweli na lipi ni la uongo au limetiwa chumvi utanisaidia sana kukubali kumbe wazungu hawa ni waongo, wanawasingizia tuu Waarabu ukatili!.

Ahsanta.

Pasqwa.
Wewe Pasco, naona sasa unaandika pumba tu, eti nahisi nahisi.

Huna hoja wewe.

Kuhisi sio hoja au sio Historia.

Unaweza kuhisi kitu lakini ikawa sio kweli unayohisi.

Dear members, asiwapotezee wakati wenu huyu Lofa Pasco mbaguzi wa rangi (mwenye chuki kwa Waislamu, tena sana).
 
Huu mzunguko wa mapinduzi, waislamu, John Okello ni kwenda mbali sana ili kutaka kuvuruga kinachojadiliwa.
Eleza kwa ufupi biashara ya utumwa ya Afrika Mashariki na Maziwa Makuu.

Kwa kukusaidia tu, biashara ya utumwa imetokea miaka mingi sana katika mazingira, jamii na hali tofauti. Kubwa zinazokumbukwa Africa ni Trans- Antlantic Slave Trade iliyohusisha misafara sehemu kubwa ya Afrika Magharibi, Americas na Ulaya, na kuna hii ya East African Slave Trade iliyohusisha pwani ya Afrika Mashariki na Uarabuni. Hebu jadili hii ya Afrika Mashariki utupe labda ukweli ambao sisi wengine hatuujui
Watu wote waliosoma wanajua vyema kwamba meli za wazungu ndio zilikuwa zikiwachukua watumwa wa Africa na kuwapeleka south American, Europe na North America (mpaka leo wapo huko). Acha kujidanganya.
 
Watu wote waliosoma wanajua vyema kwamba meli za wazungu ndio zilikuwa zikiwachukua watumwa wa Africa na kuwapeleka south American, Europe na North America (mpaka leo wapo huko). Acha kujidanganya.
Mkuu Mandago, haya usemayo ni kweli, ila biashara hii iliitwa Trans Atlantic Slave Trade, na pia ni kweli sio tuu vizazi vya watumwa hao vipo hadi leo, bali pia baada ya kusitishwa biashara hiyo, watumwa waliokuwepo Marekani na Uingereza walipewa fursa ya kurejeshwa Afrika, Wamarekani wakaja Afrika, wakatafuta pori, wakalifyeka, wakajenga makazi, na kuunfa nchi ya Liberia na kuwarejesha watumwa waliokuwa Marekani, Uingereza nao wakaunda Siera Leone na kuwarejesha watumwa wake waliotaka kurejea Afrika kwa idhaa zao.

Biashara ya utumwa iliyofanywa Afrika ya Mashariki, soko kuu la watumwa lilikuwa Zanzibar eneo la Mkunazini, watumwa hawa walipelekwa Arabuni, na India na wengine walibakizwa Zanzibar kwa matajiri wa Kiarabu. Watumwa hawa wa soko la Zanzibar, hatua ya kwanza waliyofanyiwa ni kuhasiwa!. Huu ni ukatili wa hali ya juu kwa binadamu kuliko ukatili mwingine wowote!, afadhali hata kuuliwa!. Hii genocide ilipelekea kusiwe na kizazi cha watumwa Zanzibar, Arabuni na India. Ila mabwana wa Kiarabu walkiwatumia watumwa wa kike kama wajakazi, hivyo kuwaingilia kwa nguvu. Wale walioshika mimba, waliuwawa kwa kutobolewa matumbo kiumbe kilicho tumboni tuu ndicho kilizikwa kama sii rizki na mwili wa mtumwa alifukiwa tuu kama mzoga!.

Ila kufuatia baadhi ya wanawake wa bara, kukolea kuliko wanawake wa Kiarabu katika mambo yale, ilitokea kwa mabwana wengi wa Kiarabu kuridhika na huduma za hao wajakazi watumwa, hivyo wakawapenda kwa dhati, na wakawaoa, hivyo kupanda cheo, kutoka ujakazi na kuwa masuria. Mtumwa akiishapanda cheo kuwa suria, anakuwa sio mtumwa tena!. Hawa masuria walipopata ujauzito, hawakuuliwa, bali waliendeleza ukoo, na ndio kisa cha kuwapo machotara Unguja, Pemba na Arabuni. Hili la mtumwa kugeuka suria, liliukumba hadi ukoo wa Sultani, ambapo yupo Sultani mama yake alikuwa mtumwa, na pia yupo mwana Sultani mwingine aliyezaliwa na mjakazi kwa siri, baada tuu ya mjakazi huyo kushika ujauzito, aliondolewa kwenye kasri, na kwenda kuozeshwa mahala pengine, ambapo mwana sultani alizaliwa huko, na kuonekana ni mtoto wa familia ya huko alikozaliwa, ila ukoo wa sultani uliokimbilia Uingereza, umeendelee kuihudumia familia ile hadi leo!, mwana huyo yungalipo hadi leo!.

Pasco
 
Watu wote waliosoma wanajua vyema kwamba meli za wazungu ndio zilikuwa zikiwachukua watumwa wa Africa na kuwapeleka south American, Europe na North America (mpaka leo wapo huko). Acha kujidanganya.
Kule mashariki ya kati walipelekwa na meli ya nani?
 
Hii ni hatari, nilidhani una makengeza pekee lakini natongo pia. Hiyo historia iliosema Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika iliomeguka umeisoma Kisonge au Lumumba. Basi na mie nakwambia Tanganyika ni sehemu ya Zanzibar kwa kuitawala kwa karne mpaka akaja mjerumani kukomboeni

Waliomkaribisha mwarabu kuja kuuondoa utawala dhalimu wa kireno ni jopo la maulamaa ( masheikh) kutoka Zanzibar( Mafia, Kilwa,Mombasa, Pemba) waliosafiri kwenda Oman kuwaomba ndugu zao katika imaan, kuja kuwasaidia kuondoa dhulma na fitina ya wareno ambayo ilishanza kuota mizizi.


Nakumbuka mwaka 1974 wakati wa utawala wa Alhaj Jumbem kwenye uwanja wa Amani, Mwl. Nyerere katika hotuba zake za " kisungura" alipoitaka Zanzibar kuchangia shughuli za Muungano si kwa ukubwa la eneo lake lakini kwa mujibu wa ustawi wa Uchumi wake.Huko nyuma Karume alikuwa kagoma kutoa senti kuipa Tanganyika, akilipiza kisasi kuwa Benki ya Tanzania kuilazimisha Zanzibar kununua pesa za madafu za Tanzania kwa fedha za kigeni.

Tanganyika uliuporomosha uchumi wa Zanzibar kutoka kisiwa tajiri kuwa ombaomba. Mafuta yetu mnayakodolea macho. Watu 1.5 Million na rasilmali tuliokuwa nazo ni rahisi kuifanya Zanzibar kuwa Singapore ya Afrika. Lakini hili linawezekana tu tukiwa na Mamlaka kamili ya nchi yetu.
Mkuu hamna ushahidi wa wenyeji kuenda Oman kuomba msaada et kwa wenzao toka lini sisi waaafrica nyie waarabu mkawa wenzetu? Kamma however ni watawala wa city states za pwani walioomba uma wa waislam kuwasaidia kupambana na wareno,na aliengoza jahazi ni Mir Ali Bey ambaye ni mturuki na sio mwarabu
 
Historia inasema Nchi zote zilizoko ktk Fukwe za Bahari ya Hindi zilihusishwa ktk biashara ya Utumwa.
Hatq BIBLIA book of Leviticus INAELEZEA UTUMWA uliokuwa Huko ETHIOPIA Wakati huo hata Somalia ilikuwa ndani ya ABYSSINIA. Na kabla ya hapo ikiitwa THE Kingdom of Kush(1070 BC–AD 350)

Sasa unaposema Wasomali na Wahabesh hawakuwemo Ungeambatanisha na Ushahidi wa HISTORIA Inaokubalika ili tukufahamu Vizuri vinginevyo utakuwa Unaleta vitu kutokana na Fikra zako binafsi. NA Hili ni kosa Kubwa sana Ktk Kuandika Historia.


Sikatai hoja yako ili umeipeleka kale mno ndio mana nimesema modern slavery sasa kama ni ya kale hata Genghis Khan aliwakamata waasia wakiwemo warabu na waturuki na kuwapeleka Mongolia utumwani
 
Wakamata watumwa, walikamata watu ambao ni makabila ya majembe kazi!, watu wa makabila ya nyanya hawakushughulika nao kabisa, ndio maana hata huko Zenj, hawakukamata watumwa!.

Pasco

Mkuu pasco kwenye nyanya sijakuelewa unaweza fanya ufafanuzi
 
Mkuu pasco kwenye nyanya sijakuelewa unaweza fanya ufafanuzi
Kuna makabila ni majembe kazi, watu wa makabila hayo ni wagumu, wachapakazi kutokana na kula vitu vigumu vigumu kama ugali maharage, mihogo, magimbi. Makabila nyanya ni makabila laini laini, watu wake wako legelege kutokana na kula vitu laini laini, kama tende, halua, chips, wali, urojo, chapati maji, visheti etc.

Pasco
 
Haahahahhahah mkuu pasc
Kuna makabila ni majembe kazi, watu wa makabila hayo ni wagumu, wachapakazi kutokana na kula vitu vigumu vigumu kama ugali maharage, mihogo, magimbi. Makabila nyanya ni makabila laini laini, watu wake wako legelege kutokana na kula vitu laini laini, kama tende, halua, chips, wali, urojo, chapati maji, visheti etc.

Pasco
mkuu Pasco kwanza nashukuru kwa ufafanuzi yakinifu lakini pembeni naona umewachokoza kina ritz,faiza zamilun,barghash etc
 
Back
Top Bottom