Dr Restart
JF-Expert Member
- Jul 15, 2021
- 4,949
- 24,046
- Thread starter
- #2,321
Tutaaaa
Georgia wanapata.
Georgia wanapata.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
best loosers = best losersNaam, ni Hakika!
Wakati ligi mbalimbali duniani zikielekea ukingoni, mashabiki kote duniani wanatarajia kwa hamu kuanza kwa tukio kubwa zaidi la soka barani Ulaya, UEFA EURO 2024.
Mashindano haya ya kusisimua, yanayofanyika mara moja kila baada ya miaka minne, yataanza kutimua vumbi Ijumaa, tarehe 14 Juni, na kumalizika Jumapili, tarehe 14 Julai.
Mwaka huu ni marudio ya 17 ya mashindano haya tangu kuanzishwa kwake mwaka 1960, na ni tukio la kihistoria kwani Ujerumani inaandaa kwa mara ya kwanza tangu kuungana tena. Hata hivyo, mashindano haya yaliwahi kuandaliwa na Ujerumani Magharibi mwaka 1988.
Mashindano ya EURO 2024 yanatarajiwa kuwa ya kipekee, yakifanyika katika miji kumi tofauti na kwenye viwanja kumi tofauti. Miji ikiwemo Berlin, Cologne, Frankfurt, Dortmund, Dusseldorf, Hamburg, Leipzig, Munich, na Stuttgart.
Jumla ya timu 24 zitashindana katika makundi sita, kila kundi likiwa na timu nne. Timu mbili za juu katika kila kundi huelekea hatua za mtoano. Huku best loosers wanne nao hupita katika hatua inayofuata.
View attachment 2964701
Kwa mara ya kwanza, timu ya taifa ya Georgia itashiriki katika mashindano haya, jambo linaloongeza msisimko zaidi.
Kwa taarifa kamili na maelezo zaidi kuhusu UEFA EURO 2024, jiunge nasi kutoka mwanzo hadi mwisho tunapokuletea matukio yote ya kusisimua ya mashindano haya ya kipekee.