Hio sio Pensheni waweke pesa Benki na hapo kutakuwa wala hakuna ulazima kwenye Sheria mwajiri wako kukuongezea hizo asilimia za ziada...
Narudia tena pensheni zilianzishwa kama Social Security na Sio Mtaji kwahio hawa unaosema wapo kwenye ajira na wanafanya biashara kuna mifuko tofauti ambayo wanaweza kuweka ambao wakitaka pesa zao wanaweza kupewa zote bila mfuko kuharibika / kufa...
Cha maana na kigezo ambacho kina-make sense ni watu kulalamika kwamba mtu anachopata kila mwezi hakikidhi mahitaji na wengine watakaokuja kesho watakuwa sio pensionable...; lakini issue ya kila mtu apewe chake chote sio sustainable
Nachukia mawazo yako hivi kwann serikali iendelee kuretain wafanyakazi waliostaafu kwa kuwalipa kidogo kidogo wakati inapaswa kua busy na watumishi wanaofanya kazi,kwanin mtu aliyestaafu asifanye shuguli zingine kwa pesa aliyotunukiwa almost 30 yrs working.na kwanin huu utaratibu hautumiki kwa wabunge na madiwani.
Nachukia mawazo yako hivi kwann serikali iendelee kuretain wafanyakazi waliostaafu kwa kuwalipa kidogo kidogo wakati inapaswa kua busy na watumishi wanaofanya kazi,kwanin mtu aliyestaafu asifanye shuguli zingine kwa pesa aliyotunukiwa almost 30 yrs working.na kwanin huu utaratibu hautumiki kwa wabunge na madiwani.
Watu wamesha elezea uko juu kuhusu wabunge na madiwani, kwanza :-
1. Wabunge na madiwani sio wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii na hawachangii katika mifuko ya hifadhi ya jamii na hawa lipwi na mifuko ya hifadhi ya jamii.. Hawatumii kikokotoo chochote katika kilipwa pesa zao.
2. Utaratibu uko hivyo kwasababu sheria na sera za hifadhi ya jamii duniani kote ziko hivyo PSSSF na NSSF inafuata na kuongozwa na sheria za ILO
Nyie mbwa mnawalipa watu peremende halafu mnawazawadia maelezo yenye utetezi hafifu kama huu.sijajua wewe ni mume wa yule kifutu aliyesema wananchi hawana elimu au ni kaka yake???
Nyinyi miaka 5 tu mnalipana milioni 250 na limshahara la zaidi ya milioni 10 kwa mwezi,halafu mnafanya mzaha na hatma za wazee.watakuja kuwabadilikia siku mshangae.
Kwanza naona wengi wenu akili za funza,huwezi fanya mzaha na hatma za watu kama polisi halafu mnaruhusu wawalinde na silaha,huo ni utaahira,ni kujisahau na dalili ya kuwa kama mazombie,mtu timamu hawezi fanya huo mchezo.
Ni asilimia 19% ya watumishi ndio walikuwa wanalipwa hicho kikokotoo unacho semea niwa PSPF na LAPF.. unawajua walio kuwepo PPF, NSSF na GEPF walitumia kikokotoo kipi...
Ninafahamu Vizuri kama DAS na wengine hawalipwi na PSSSF swali langu kama ilikuwa na faida kipindi wanaunganisha Mifuko kwanini hawakuunganisha Mfuko wao ukawa PSSSF pia..
Najua Pia kuwa NSSF haihusiki na PSSSF na sio Busara kuiunganisha NSSF NA PSSSF
NSSF mpaka sasa wanakikokotoo chao Binafsi na wana fao la Kujitoa pia..
Ninafahamu Vizuri kama DAS na wengine hawalipwi na PSSSF swali langu kama ilikuwa na faida kipindi wanaunganisha Mifuko kwanini hawakuunganisha Mfuko wao ukawa PSSSF pia..
Najua Pia kuwa NSSF haihusiki na PSSSF na sio Busara kuiunganisha NSSF NA PSSSF
NSSF na PSSSF wote wanatumia formula moja kukokotoa mafao ya wanachama wao.
Withdraw Benefit ipo kotekote kwa PSSSF na NSSF kwa wale unskilled labor, hao kazi zao zikifika ukomo wanaruhusiwa kuchukua fedha walizo changia kwenye mfuko kama wamechangia chini ya miezi 180 ( miaka 15.
Hujui kitu, Mjuaji tu wewe PSSSF na NSSF, huwezi zitofautisha kiutendaji kwani zina-fanya kazi pamoja i.e mtu aliye changia NSSF na PSSSF akistaafu analipwa na mifuko yote miwili kwa kutumia tatolization formula, NSSF/PSSSF kabla ya kulipwa mafao ya kujitoa lazima aconfirm NSSF/PSSSF kama ni mwanachama uko au sio mwanachama..
Mawazo yangu ? Nasikitika kusema kwamba sina akili kiasi hicho mimi nilichofanya ni kukuelewesha dhima ya pensheni kwamba ni zaidi ya kibubu ni insurance ya kuhakikisha unapata kitu mpaka siku unafariki.... miaka ya nyuma kwa dunia kuona wazee wanahadhirika uzeeni ndio wakaamua kuja na mfumo kama huu.., ukitaka mifumo ya investment funds pia ipo
Sijakuelewa serikali ina-retain vipi wastaafu ? Serikali imeweke sheria kwa mwajiri yoyote ahakikishe anamkata percent fulani muajiriwa na kumuongezea ili kumuwekea kwenye mfuko..., ili uzeeni wasiwe ombaomba hio ndio dhima nzima
Kwa taifa lililojipanga mtu unastaafu ili kupumzika na sio kubadilisha kazi... ni kipi hicho alishindwa kufanya in thirty years wakati nguvu zipo akifanye ukubwani..., ofcourse akitaka kufanya afanye ila na ufanyaji wake angalau kila mwezi ana kitu kinaingia kwenye akaunti (security) sasa kuondoa security / safety net ni hatari kwa ustawi wa jamii
Sasa hapa ni kama tunaongelea mabovu ya kule kutaka kuharibu huku..., Kumbuka sisemi wanachopata kinatosha nasema kupata / guaratee ya kupata kitu kila mwezi ni muhimu sana, Ufisadi wa wabunge au vinginevyo ni topic nyingine... tena mimi bomu ninaloliona ni hawa machinga na bodaboda wa kesho ambao hata hizo laki na nusu kwa mwezi watakuwa hawana kwahio hata vijisenti vya kuuguza afya zao kwa suluba waliyopata ujanani watakuwa hawana
Kila siku nawaambia watu Pension sio Mtaji wala Akiba bali ni Kinga / Bima / Insurance ya watu wakizeeka / wakikosa nguvu kuweza kusukuma maisha yao mwezi kwa mwezi huku wakingojea siku zao za mwisho....
Pia ninachoogopa na huenda kikaja ni watu / wajanja kubinafsisha / kutengeneza Pension / Security Funds binafsi na kuwashauri watu wawekeze huko kutokana na returns kubwa zaidi na mwisho wa siku kupigwa kama waliopigwa na kina Bernie Madoff
Ila issue a maana zaidi ni kwamba wanachopata ni kwamba hakikidhi mahitaji na sio wao tu mbaya zaidi ni hata kizazi kinachokuja...;
Ni kweli mafao ya wastaafu hayatoshi (si wao tu asilimia kubwa ya wabangaizaji Tanzania either hakuna wanachopata na wakipata hakitoshi)...; Lakini wakati tunachemsha Bongo jinsi ya kuwarekebishia hawa kidogo kiwe kikubwa kidogo, ni vema tukaangalia ni vipi hatari inayokuja kesho ya wazee wa...
Swala la pensheni ya kunchangia ni gumu saana. Nchi zilizoendelea zinatoa pension/social security kama malipo ya mwezi na hakuna malipo ya mkupuo na baadaye malipo ya mwezi. Ukiangalia TZ watu wengi hupewa pesa yote waliyochangia na pamoja ni ile ya mwajiri. Zile wanazolipwa kwa mwezi unaweza ukasema wengi hawastahili maana ziliishachukuliwa kwenye mkupuo (gratuity). Huhitaji rocket science kujuwa hili. Unaweza ukaangalia umechangia kiasi gani kwa miaka ypte na ukajumlisha michango ya mwajiri na utaona tofauti kati ya gratuity na [pesa uliyochangia. Ukibahatika kuishi zaidi ya miaka 10 baada ya kustaafu utajikuta unapokea pesa ambayo ni zaidi ya michango yako na mwajiri katika mfuko wa pension
Ubunge ni kazi ya mkataba wa miaka 5. Hawakatwi fedha za mifuko ya pensheni. Kwa hiyo kisheria hahusiki na mifuko hiyo. Hata hiyo kupata pensheni mpaka uwe umechangia miaka 15.
Sheria ya Hifadhi ya jamii, 1997 inaelezea juu ya pensheni kamili na isiyo kamili. Kwa pensheni kamili, mfanyakazi anapaswa awe amefikia umri wa miaka 60 na walau miezi 180 (miaka 15) ya kuchangia.
na Pension Isiyo kamili ndo ilikuwa na FAO la kujitoa kabla ya Hiyo Miaka 15..
kabla haijabadilishwa na kuondolewa FAO la kujitoa na Kuunganishwa kwa Mifuko yote ya Umma na kufanywa kuwa PSSSF Mwka 2018..
Kipindi wanaunganisha Mifuko na Kubadili sheria ya Pension Kamili na Pension Isiyo kamili kwa nini hawakuconsider Pension isiyokamili kama wabumge???
Kuna watu wanachukua Pension isiyo kamili mpaka Sasa Huko NSSF unawazungumziaje?
Hao ambao walishapewa kwa mkupuo kabla kikokotoo kilichopo walishapata haki yao.
Watendewe haki hawa watarajiwa ili nao wafanyie japo miradi hata midogomidogo.
Bosi nchi hii ina wajinga wengi sana. Badala ya kutafuta ufumbuzi kwenye kuhakikisha watanzania wanapata elimu ya fedha na uwekezaji mapema minitu unakuta ina midevu inasema kikokotoo kibaya. Ukiuliza ubaya wake nini eti apewe hela zote, ukiuliza ukipewa eti nikifa niwe nimechukua hela yako, ukiukiliza je kwani ukiwa unapata kila mwezi ukifa hela yako si watapewa warithi yanasema oh mi nataka hela yangu yaani ni full ujinga mno.
Warithi akina nani? Mtu ameisha somesha watto wake Wana ajira,hiyo pensheni ni ya msaafu na mkewe! Jua Kuna watu wanafanya investment kabla ya kustaafu,wanajitaji pesa zao kwenye miradi Yao. Yaani serikali imeshindwa kulipa mshahara wa maana nikiwa kazini,alafu Leo monthly pension inisaidie? Ujinga mtupu!
Sheria ya Hifadhi ya jamii, 1997 inaelezea juu ya pensheni kamili na isiyo kamili. Kwa pensheni kamili, mfanyakazi anapaswa awe amefikia umri wa miaka 60 na walau miezi 180 (miaka 15) ya kuchangia.
na Pension Isiyo kamili ndo ilikuwa na FAO la kujitoa kabla ya Hiyo Miaka 15..
kabla haijabadilishwa na kuondolewa FAO la kujitoa na Kuunganishwa kwa Mifuko yote ya Umma na kufanywa kuwa PSSSF Mwka 2018..
Kipindi wanaunganisha Mifuko na Kubadili sheria ya Pension Kamili na Pension Isiyo kamili kwa nini hawakuconsider Pension isiyokamili kama wabumge???
Kuna watu wanachukua Pension isiyo kamili mpaka Sasa Huko NSSF unawazungumziaje?
Ni unskilled pekee ndiye anapewa pesa yake yote baada ya kutoka kazini/mkataba wake kufika ukomo na kama hajachangia miezi 180 ( miaka 15 ) kama kachangia miezi 180 atalipwa dIffered pension, monthly pension ataanza kulipwa atakapo fika miaka 55
Kwa skilled labor wao wanalipwa Unemployment benefit wanasubiri two years wakitafuta ajiwa wakikosa wanarudi kwenye mfuko kuchukua michango yao yote ( Withdraw )
Hii ni kote PSSSF na NSSF.
Alafu nimesha kuona vitu vingi hujui ila unaleta ujuaji.
Baada ya kulipwa kiinua mgongo ( CP ) hakuna pesa inayo baki kwenye mfuko, ukisema ulipwe pesa yote... Utalipwa kiinua mgongo tu ndio haki yako.. Hii ya kila mwezi inatoka kwenye mfuko wewe hata hukuichangia.
Warithi akina nani? Mtu ameisha somesha watto wake Wana ajira,hiyo pensheni ni ya msaafu na mkewe! Jua Kuna watu wanafanya investment kabla ya kustaafu,wanajitaji pesa zao kwenye miradi Yao. Yaani serikali imeshindwa kulipa mshahara wa maana nikiwa kazini,alafu Leo monthly pension inisaidie? Ujinga mtupu!
Then waulize wangerudi kwenye utumishi wangetamani kulipwa vipi?
Mimi nadhani changamoto tumeshindwa kubalance story,kati ya Watumishi na wastaafu waliokwishalipwa.
Wapo wastaafu wanatamani hata wasingelipwa mkupuo, pesa yote iende kwenye montly pensheni na iwe kubwa.
Sisi tumeamua kuwa kwenye kelele za Watumishi na wanasiasa.
Tumeamua kuweka taaluma pembeni, sijui na sitaki kuamini wakati tunasoma principles za Hifadhi ya jamii kuna mtu aliwahi kupingana na kile tulichokuwa tunafundishwa.
Leo hii tumeanza kupingana nacho either kwa sababu njia zetu hazijafunguka kuiona na fani yetu kuwa na msaada kwetu direct.
Kuna nchi hata mkupuo hazina kabisa,mtu akistaafu anaunganisha na pensheni ya kila mwezi.
Kuna nchi ukistaafu wanakupa pesa yako yote lakini wao kiuchumi wako vizuri walishakufanyia kila kitu.
Wazee wakishapewa wananunua Annuity ili kila Mwaka walipwe pesa nzuri.
Mnaosema wastaafu wapewe pesa zao zote naombeni leteni mifano ya waliolipwa na wakawekeza na kuwa vizuri kifedha hadi sasa.
Baada ya kulipwa kiinua mgongo ( CP ) hakuna pesa inayo baki kwenye mfuko, ukisema ulipwe pesa yote... Utalipwa kiinua mgongo tu ndio haki yako.. Hii ya kila mwezi inatoka kwenye mfuko wewe hata hukuichangia.
Sasa unataka kiinua mgongo ndio kikujengee nyumba, ununue gari, uongeze mke kwanini ulishindwa kufanya ukiwa na asilimia 95% ya mshaara wako wote, unataka hii uliyo kuwa unachangia 5% ndio ifanye hayo yote...!?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.