Ufafanuzi kuhusu kikokotoo cha mafao ya kustaafu

Hayo ndio maelezo ya kuwaambia watu,sio mtu anakuja hapa kujaribu kusema namna gani vikokotoo ni vitu vya maana ilhali ni wizi na utapeli mtupu.

Ongeza mshahara,ongeza makato.
Kikokotoo hakina shida, shida ni mishaara ya watumishi ni duni.
 
Nachukia mawazo yako hivi kwann serikali iendelee kuretain wafanyakazi waliostaafu kwa kuwalipa kidogo kidogo wakati inapaswa kua busy na watumishi wanaofanya kazi,kwanin mtu aliyestaafu asifanye shuguli zingine kwa pesa aliyotunukiwa almost 30 yrs working.na kwanin huu utaratibu hautumiki kwa wabunge na madiwani.
 
Watu wamesha elezea uko juu kuhusu wabunge na madiwani, kwanza :-
1. Wabunge na madiwani sio wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii na hawachangii katika mifuko ya hifadhi ya jamii na hawa lipwi na mifuko ya hifadhi ya jamii.. Hawatumii kikokotoo chochote katika kilipwa pesa zao.

2. Utaratibu uko hivyo kwasababu sheria na sera za hifadhi ya jamii duniani kote ziko hivyo PSSSF na NSSF inafuata na kuongozwa na sheria za ILO
 
Vitu viwili vinanafanya pensheni ya uzee kuwa kubwa au ndogo ni:-
1. Kiwango cha Mshaara.
2. Miezi ya uchangiaji katika mfuko.

Mishaara ya polisi ni midogo ndio maana pension zao zinakuwa ni ndogo pia, wapambane maslai yao ( mishaara ya iongezwe kwanza )
 
Ni asilimia 19% ya watumishi ndio walikuwa wanalipwa hicho kikokotoo unacho semea niwa PSPF na LAPF.. unawajua walio kuwepo PPF, NSSF na GEPF walitumia kikokotoo kipi...
NSSF mpaka sasa wanakikokotoo chao Binafsi na wana fao la Kujitoa pia..
Kwanza utambue wabunge, RAS, DAS hawalipwi na PSSSF wala NSSF wana mfumo wao wa ulipaji na sio wanachama wa NSSF wala PSSSF.
Ninafahamu Vizuri kama DAS na wengine hawalipwi na PSSSF swali langu kama ilikuwa na faida kipindi wanaunganisha Mifuko kwanini hawakuunganisha Mfuko wao ukawa PSSSF pia..

Najua Pia kuwa NSSF haihusiki na PSSSF na sio Busara kuiunganisha NSSF NA PSSSF
 
UONGO!

NSSF na PSSSF wote wanatumia formula moja kukokotoa mafao ya wanachama wao.

Withdraw Benefit ipo kotekote kwa PSSSF na NSSF kwa wale unskilled labor, hao kazi zao zikifika ukomo wanaruhusiwa kuchukua fedha walizo changia kwenye mfuko kama wamechangia chini ya miezi 180 ( miaka 15.

Hujui kitu, Mjuaji tu wewe PSSSF na NSSF, huwezi zitofautisha kiutendaji kwani zina-fanya kazi pamoja i.e mtu aliye changia NSSF na PSSSF akistaafu analipwa na mifuko yote miwili kwa kutumia tatolization formula, NSSF/PSSSF kabla ya kulipwa mafao ya kujitoa lazima aconfirm NSSF/PSSSF kama ni mwanachama uko au sio mwanachama..

Hujui kitu, una bwabwaja na ujuaji.
 
Nachukia mawazo yako
Mawazo yangu ? Nasikitika kusema kwamba sina akili kiasi hicho mimi nilichofanya ni kukuelewesha dhima ya pensheni kwamba ni zaidi ya kibubu ni insurance ya kuhakikisha unapata kitu mpaka siku unafariki.... miaka ya nyuma kwa dunia kuona wazee wanahadhirika uzeeni ndio wakaamua kuja na mfumo kama huu.., ukitaka mifumo ya investment funds pia ipo
hivi kwann serikali iendelee kuretain wafanyakazi waliostaafu kwa kuwalipa kidogo kidogo wakati inapaswa kua busy na watumishi wanaofanya kazi,
Sijakuelewa serikali ina-retain vipi wastaafu ? Serikali imeweke sheria kwa mwajiri yoyote ahakikishe anamkata percent fulani muajiriwa na kumuongezea ili kumuwekea kwenye mfuko..., ili uzeeni wasiwe ombaomba hio ndio dhima nzima
kwanin mtu aliyestaafu asifanye shuguli zingine kwa pesa aliyotunukiwa almost 30 yrs working.
Kwa taifa lililojipanga mtu unastaafu ili kupumzika na sio kubadilisha kazi... ni kipi hicho alishindwa kufanya in thirty years wakati nguvu zipo akifanye ukubwani..., ofcourse akitaka kufanya afanye ila na ufanyaji wake angalau kila mwezi ana kitu kinaingia kwenye akaunti (security) sasa kuondoa security / safety net ni hatari kwa ustawi wa jamii
na kwanin huu utaratibu hautumiki kwa wabunge na madiwani.
Sasa hapa ni kama tunaongelea mabovu ya kule kutaka kuharibu huku..., Kumbuka sisemi wanachopata kinatosha nasema kupata / guaratee ya kupata kitu kila mwezi ni muhimu sana, Ufisadi wa wabunge au vinginevyo ni topic nyingine... tena mimi bomu ninaloliona ni hawa machinga na bodaboda wa kesho ambao hata hizo laki na nusu kwa mwezi watakuwa hawana kwahio hata vijisenti vya kuuguza afya zao kwa suluba waliyopata ujanani watakuwa hawana
 
Swala la pensheni ya kunchangia ni gumu saana. Nchi zilizoendelea zinatoa pension/social security kama malipo ya mwezi na hakuna malipo ya mkupuo na baadaye malipo ya mwezi. Ukiangalia TZ watu wengi hupewa pesa yote waliyochangia na pamoja ni ile ya mwajiri. Zile wanazolipwa kwa mwezi unaweza ukasema wengi hawastahili maana ziliishachukuliwa kwenye mkupuo (gratuity). Huhitaji rocket science kujuwa hili. Unaweza ukaangalia umechangia kiasi gani kwa miaka ypte na ukajumlisha michango ya mwajiri na utaona tofauti kati ya gratuity na [pesa uliyochangia. Ukibahatika kuishi zaidi ya miaka 10 baada ya kustaafu utajikuta unapokea pesa ambayo ni zaidi ya michango yako na mwajiri katika mfuko wa pension
 
Ubunge ni kazi ya mkataba wa miaka 5. Hawakatwi fedha za mifuko ya pensheni. Kwa hiyo kisheria hahusiki na mifuko hiyo. Hata hiyo kupata pensheni mpaka uwe umechangia miaka 15.
Sheria ya Hifadhi ya jamii, 1997 inaelezea juu ya pensheni kamili na isiyo kamili. Kwa pensheni kamili, mfanyakazi anapaswa awe amefikia umri wa miaka 60 na walau miezi 180 (miaka 15) ya kuchangia.

na Pension Isiyo kamili ndo ilikuwa na FAO la kujitoa kabla ya Hiyo Miaka 15..

kabla haijabadilishwa na kuondolewa FAO la kujitoa na Kuunganishwa kwa Mifuko yote ya Umma na kufanywa kuwa PSSSF Mwka 2018..

Kipindi wanaunganisha Mifuko na Kubadili sheria ya Pension Kamili na Pension Isiyo kamili kwa nini hawakuconsider Pension isiyokamili kama wabumge???

Kuna watu wanachukua Pension isiyo kamili mpaka Sasa Huko NSSF unawazungumziaje?
 
Hao ambao
Hao ambao walishapewa kwa mkupuo kabla kikokotoo kilichopo walishapata haki yao.
Watendewe haki hawa watarajiwa ili nao wafanyie japo miradi hata midogomidogo.
 
Mtu aliyejipanga kabla ya kustaafu,halalamiki alafu huo uongo na visingizio unaleta hapa
 
Warithi akina nani? Mtu ameisha somesha watto wake Wana ajira,hiyo pensheni ni ya msaafu na mkewe! Jua Kuna watu wanafanya investment kabla ya kustaafu,wanajitaji pesa zao kwenye miradi Yao. Yaani serikali imeshindwa kulipa mshahara wa maana nikiwa kazini,alafu Leo monthly pension inisaidie? Ujinga mtupu!
 
Ni unskilled pekee ndiye anapewa pesa yake yote baada ya kutoka kazini/mkataba wake kufika ukomo na kama hajachangia miezi 180 ( miaka 15 ) kama kachangia miezi 180 atalipwa dIffered pension, monthly pension ataanza kulipwa atakapo fika miaka 55

Kwa skilled labor wao wanalipwa Unemployment benefit wanasubiri two years wakitafuta ajiwa wakikosa wanarudi kwenye mfuko kuchukua michango yao yote ( Withdraw )

Hii ni kote PSSSF na NSSF.
Alafu nimesha kuona vitu vingi hujui ila unaleta ujuaji.
 
Mtu aliyejipanga kabla ya kustaafu,halalamiki alafu huo uongo na visingizio unaleta hapa
Baada ya kulipwa kiinua mgongo ( CP ) hakuna pesa inayo baki kwenye mfuko, ukisema ulipwe pesa yote... Utalipwa kiinua mgongo tu ndio haki yako.. Hii ya kila mwezi inatoka kwenye mfuko wewe hata hukuichangia.
 
Hoja yako ni mishaara au ni nini sasa...!?😂
 
Watu wanawekeza kabla ya kustaafu,hiyo pensheni ni haki yangu nipewe Ili niongeze uwekezaji
 
Baada ya kulipwa kiinua mgongo ( CP ) hakuna pesa inayo baki kwenye mfuko, ukisema ulipwe pesa yote... Utalipwa kiinua mgongo tu ndio haki yako.. Hii ya kila mwezi inatoka kwenye mfuko wewe hata hukuichangia.

Mwanzoni mbona walikuwa wakilipa,why now?
 
Mtu aliyejipanga kabla ya kustaafu,halalamiki alafu huo uongo na visingizio unaleta hapa
Sasa unataka kiinua mgongo ndio kikujengee nyumba, ununue gari, uongeze mke kwanini ulishindwa kufanya ukiwa na asilimia 95% ya mshaara wako wote, unataka hii uliyo kuwa unachangia 5% ndio ifanye hayo yote...!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…