Ufafanuzi: The Royal Tour, filamu ya Rais Samia inayolenga kukuza utalii

Ufafanuzi: The Royal Tour, filamu ya Rais Samia inayolenga kukuza utalii

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Royal Tour pic.jpg

Rais Samia Suluhu Hassan akiwa katika moja ya ziara zake kurekodi The Royal Tour, 2021

Tumesikia na kuona Rais Samia akiwa katika kile kilichojulikana kama The Royal Tour, lakini huenda kuna baadhi yetu hatujaelewa ni kitu gani hiki.

Wapo wanaodhani Rais kajitungia jina na kutafuta wapiga picha kadhaa anaoambatana nao. La hasha!

Wapo waliopendekeza kwamba Rais angetumia watu wenye ushawishi nchini kufanya kazi hiyo - lakini je, inafaa kuwa hivyo? Hapana.

Wapo pia tuliodhani Royal Tour ni ile picha moja iliyobadilishiwa background mara nyingi na kusambazwa mtandaoni.

Royal Tour ni mfululizo wa vipindi vya televisheni vinavyorushwa na chaneli ya PBS (Public Broadcasting Service) huko nchini Marekani.

Mtayarishaji wa The Royal Tour ni nani?
The Royal Tour inazalishwa/tayarishwa na Peter Greenberg ambaye -- kwa mujibu wa vyanzo kadhaa -- ni mmoja wa waandishi wa habari wa musuala ya utalii wanaojulikana na kuheshimiwa zaidi nchini Marekani. Anajulikana katika tasnia ya utalii kama “The Travel Detective”.

Bw. Greenberg pia ni Mhariri wa Masuala ya Utalii wa kituo cha CBS News kwa sasa.

Maandiko yake yamechapishwa na Forbes.com, CBS.com, Oprah.com n.k. Pia amewahi kushirikishwa kama mgeni na vyombo vya habari na vipindi vikubwa kama vile CNN, The Oprah Winfrey Show, Late Night with Conan O'Brien, Larry King Live n.k

Peter-Greenberg-Featured-Blog-Image.jpg

Peter Greenberg
Greenberg ni Mtaalam wa masuala ya usalama wa anga na pia ndiye mtayarishaji mwenza wa Secrets of the Black Box, mfululizo wa vipindi vinavyorushwa na kituo cha History, ambavyo huchunguza majanga mabaya zaidi ya anga. Mnaofuatilia mambo mtakuwa mnakifahamu hiki.

The Royal Tour inafanyikaje?
Kipindi kinalenga kumhusisha mkuu wa nchi husika ambaye ndiye anakuwa mwenyeji au “tour guide” akionesha maeneo mbalimbali ya kuvutia kwa mgeni wake Peter Greenberg. The Royal Tour inatoa fursa ya kuonesha nchi na watu wake na kutoa uelewa bora - na wa kuaminika - juu ya utamaduni wake na watu kupitia uzoefu wa kiongozi wake. Well, ndiyo maana nikasema Rais hawezi kuwakilishwa na mtu maarufu ama kiongozi mwingine katika hili. Lengo kuu hapa ni Kiongozi Mkuu wa Taifa kushiriki na kumtembeza Bw. Greenberg maeneo ambayo ni muhimu na yenye kuvutia watalii pamoja na kujibu maswali anuai kuhusu nchi anayoiongoza. Je, Rais anajua zaidi ya kila mwananchi? Huenda hapana, lakini kwakuwa kipindi kinamlenga yeye, basi hana budi kushiriki katika nafasi hiyo.

Je, Rais Samia ni wa kwanza kushiriki The Royal Tour?
Hapana. The Royal Tour tayari imewashirikisha viongozi kadhaa duniani ikiwa ni pamoja na wafuatao:
  • Helen Clark, aliyekuwa Waziri Mkuu wa New Zealand (1999 - 2008)
  • Benjamin Netanyahu, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Israeli (1996 – 1999/ 2009 – 2021)
  • Mfalme Abdullah II wa Jordan (tangu 1999)
  • Alejandro Toledo, aliyekuwa Rais wa Peru (2001 - 2006)
  • Felipe Calderón, aliyekuwa Rais wa Mexico (2006 – 2012)
  • Rais Paul Kagame wa Rwanda
  • Mateusz Morawiecki, Waziri Mkuu wa sasa wa Poland (tangu 2017)

peter-greenberg-and-the-prime-minister-at-jerusalem.jpg

Peter Greenberg akiwa na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu wakati wa kurekodi The Royal Tour, Jerusalem, 2014

Mafanikio yake kuwavutia watalii yapoje?
Kwa uchache tu ni kwamba, ingawa The Royal Tour imechukuliwa na baadhi ya watu kama jukwaa la PR Stunts za wakuu wanchi, lakini pia kumekuwapo “ripoti” za mafanikio, tofauti na zile zinazoonekana kulenga kubadili narrative kuhusu viongozi wa nchi na tawala zao.

Baada ya The Royal Tour iliyomshirikisha Mfalme Abdullah II kurushwa, “iliripotiwa” kuwa utalii ulipanda karibu asilimia 20 nchini Jordan, huku Mexico, Peru na Jamaica zikishuhudia ongezeko la 10%

Wizara ya Utalii ya Israeli pia ilisema kuwa baada ya filamu hiyo kuoneshwa, nchi hiyo ingepata ongezeko la watalii 200,000 zaidi. Hata hivyo, si kila mmoja alipendezwa na filamu hiyo nchini Israel. Lakini Greenberg alisisitiza kwamba filamu hiyo si PR kwa Israeli, na kwamba wafanyakazi wa Waziri Mkuu hawakuruhusiwa kukagua baada ya production kukamilika.

Kwa upande wa Rwanda, pamoja na kutembelea vivutio mbalimbali, pia Rais Kagame alipata fursa ya kueleza kuhusu mambo mbalimbali likiwemo la tuhuma za kung’ang’ania madarakani. Siku kadhaa baada ya kuzinduliwa, ilioneshwa katika eneo la umma huko Rwanda.


Hii ni trailer ya The Royal Tour iliyomshirikisha Rais wa Rwanda, Paul Kagame mwaka 2018


Hii ni trailer ya The Royal Tour iliyomshirikisha Waziri Mkuu wa Poland, Mateusz Morawiecki mwaka 2019



Hii ni trailer ya The Royal Tour iliyomshirikisha Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu mwaka 2014
 
Jamaa atakuwa kalipwa mkwanja mrefu teha sio huu wa pesa ya madafu bali ni ule mkwanja wa Biden, sijui hii itenda imetoka vipi, mzungu kawa mtaalamu wa wanyama wetu na sisi tumebaki kung'aa macho na sifa zote zitamwendea yeye.
 
Pamoja na ufafanuzi huo, bado kuna walakini mkubwa sana juu ya hicho mnachoita utalii wa kifalme, kwa kawaida huyo muandaaji wake lazima atakuwa na historia ya eneo na mlengwa au muhusika kulingana na tukio.

Hapa kwetu bimkubwa ndo hata mwaka hana kwenye cheo leo ghafla anatakiwa kufanya shooting kwa kigezo gani?

Marais waliofanya production huko nyuma tunaona hakuna aliyekaa madarakani kwa mwaka ni zaidi ya miaka ndiyo walifanyiwa coverage, hapa kwetu kuna nini huko?

Mimi binafsi nawaza anayeendesha hii nchi kwa upande wa pili huyo ndiye anaweza kuwa Royal Tour kwa kutengeneza deals akiwa ni mmoja wa ten per, although sisi nchi yetu inajitangaza yenyewe bila nguvu.

Kama jana nimeulizwa na mwafrika mwezangu kutoka Namibia; nyie (watanzania) mna mlima gani mrefu kuliko ule wa Kenya? Wakimaanisha Kilimanjaro!

Hapo ndipo naona kuna tatizo kwa hiyo VIP Tour na something hiden!
 
Hivi kweli Tanzania hii inahitaji mkuu wake wa nchi akatangaze vivutio vyetu lukuki vinavyojiuza vyenyewe badala ya kushughulikia mambo ya msingi? Wizara husika inapangiwa bajeti ya nini?

Kwa vyovyote vile mtahalalisha upuuzi huu, na mmefanikiwa. Aidha Peter Greenberg ana agenda yake ya siri ya kusaka umaarufu au ni ule mwendelezo wa kinachoitwa New World Order.
 
Mwaka ule walimtumia Steve Nyerere kuutangaza utalii wetu. Sijui walifikia wapi
 
..is the government of Tz paying Peter Greenberg to record this program, or this is done for free?

Well, as producer of the program he has to make sure he’s got some substance for his audience, no?
 
Well, as producer of the program he has to make sure he’s got some substance for his audience, no?

..Is the government / tax payers of Tanzania paying Peter Greenberg?

..how was the conclusion that tourist numbers in Peru, Mexico, and Jamaica, increased by 10% after filming Royal Tour arrived at?

..do you know the organization that did the study and its credibility?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom