Ufahamu kuhusu nyota za angani

Ufahamu kuhusu nyota za angani

Matikuu Kifyatu naomba unieleweshe ni nishati gani inayowezesha satelite kuwa kwenye motion.

Nishati ya kuiongoza:

Satellite ikishaingia kwenye orbit na kupata spidi stahiki basi haihitaji kusukumwa tena. Itaendelea tu kama ulivyo mwezi wetu (mwezi ni satellite ya dunia yetu). Isipokuwa satellite zote zinakuwa na mitungi ya hewa ya hydrogen na Oxygen ambazo zikichanganywa zinalipuka na kutoa msukumo (thrust) kama unataka kuirekebisha au kuipunguzia mwendo ili uidondoshe.

Nishati ya matumizi ya kila siku:
Satellite zote zinatumia nishati kubwa sana kuendeshea mitambo yake ya mawasiliano na dunia, kupiga picha, kompyuta na electronics zote. Kupata nishati hii Satellite nyingi hutumia solar panels kutengeneza umeme. Pia ndani ya hizi satellite kuna rechargeable batteries ambazo zinachajiwa na hizi solar panels ili kuhifadhi nishati kwa matumizi ya baadae.

Vyombo vinavyokwenda mbali sana ambako muanga wa jua ni hafifu sana wanatunia nishati ya nyuklia kutengeneza umeme wa matumizi ya kila siku.
 
Iv kwann waliokoo kwenye ISS hawahisi ile spidi kbs kwa mfano ISS inatembea 7km/sec lakn sidhan kama wanahis io spid
Unahisi Upo kwenye spidi unapojilinganisha Na stationary objects. Ndio maana hujihisi upo kwenye spidi kubwa kwenye ndege Kwani huoni vitu kama Miti wakati ukiwa angani. Ikiwa usiku utafikiri ndege imesimama Kwani huoni vitu unavyovipita.
 
Mkuu Kifyatu naomba unieleweshe ni nishati gani inayowezesha satelite kuwa kwenye motion.
Ni Gravity au nguvu ya mvuto wa dunia. Huwa "inaanguka" ila haifiki duniani. Dunia ina "curve" mita 5 kila kms 8 sasa mfano kama inachukua sekunde moja kuanguka chini urefu wa mita 5 na katika sekunde moja unasafiri Kwa spidi ya kms 8, Ina maana utakuwa unaanguka bila kufika chini. Soma hapa A Satellite as a Projectile Spidi ya kuanzia ni hiyo inayotokana Na roketi iliyoipeleka juu. Jua kwamba huko juu hakuna msuguano kutokana na hewa (atmosphere) kwani haipo. My two cents....
 
View attachment 318903Tazama hii sketch apa hizo ni sayari ambazo kila moja ina mzunguko wake binafsi na kila moja inazunguka jua kwa muda wake tofauti, Mchana na usiku ni matokeo ya dunia kuzunguka katika muhimili wake na mwaka ni dunia kuzunguka jua

Kifyatu; nadhani unaiyona hiyo picha vzr, swali hivi hicho chombo ama object yoyote ile iliyokuwa inatoka dunian kwenda sayari nyingine may be mars kikiwa njiani chombo hicho kikafeli lakini kikiwa kimeshatoka dunian je chombo hicho kitaangukia wapi? Ni hiyo sehemu nyeusi nyeusi au kitaporomoka kuelekea kwenye jua.

Umbali wa sayari moja na nyingine ama umbali wa hizo njia(orbit) sayari moja na nyingine ni kias gani? Elezea kwanini watu wanatembea kwa kujifunga kamba huko sayari za mbali yaani wanakuwa km wanaelea kama ile Picha la john carter.

Na je ipo sayari inayokaribia kufanana na hii ya dunia ukiwa unatembea unakuwa free kama huku ulimwenguni?
 
Jamani samahani ndugu zangu wote Mimi mkristo ila na soma sana Quran kujifunza mambo, katika Quran MUNGU MKUU anasema kuna mbingu saba ambazo ameziumba na anasema mbingu ya kwanza ambayo niyakwetu ndio aliyoipamba sana kwa nyote ili hali hizo mbingu sita azijapambwa kama hiii, na Ulikuwa maalumu kwa ajili yetu, pia Mola anasema anaendelea kuujenga kila Siku ulimwengu, kumbuka haya yamezungumzwa kwenye Quran Tukufu ata kabla sayansi ya juu kutambulika je Ina maana tunaposema kuna nyote katika galaxy nyingine tunapingana na MUNGU MKUU!?
 
Jamani samahani ndugu zangu wote Mimi mkristo ila na soma sana Quran kujifunza mambo,katika Quran MUNGU MKUU anasema kuna mbingu saba ambazo ameziumba na anasema mbingu ya kwanza ambayo niyakwetu ndio aliyoipamba sana kwa nyote ili hali hizo mbingu sita azijapambwa kama hiii,na Ulikuwa maalumu kwa ajili yetu,pia Mola anasema anaendelea kuujenga kila Siku ulimwengu,kumbuka haya yamezungumzwa kwenye Quran Tukufu ata kabla sayansi ya juu kutambulika je Ina maana tunaposema kuna nyote katika galaxy nyingine tunapingana na MUNGU MKUU!?
Ukichanganya dini na sayansi unaweza ukatia DOA imani yako kwa kujiuliza maswali mengi tena kwa dini zote mbili.
 
Jamani samahani ndugu zangu wote Mimi mkristo ila na soma sana Quran kujifunza mambo,katika Quran MUNGU MKUU anasema kuna mbingu saba ambazo ameziumba na anasema mbingu ya kwanza ambayo niyakwetu ndio aliyoipamba sana kwa nyote ili hali hizo mbingu sita azijapambwa kama hiii,na Ulikuwa maalumu kwa ajili yetu,pia Mola anasema anaendelea kuujenga kila Siku ulimwengu,kumbuka haya yamezungumzwa kwenye Quran Tukufu ata kabla sayansi ya juu kutambulika je Ina maana tunaposema kuna nyote katika galaxy nyingine tunapingana na MUNGU MKUU!?

Kwanza Hongera kwa kupenda kusoma mkuu lakini maarifa yaliyopo katika kila kitabu either Quran au Bible au kitabu chochote sio kuwa ndio usahihi wa hicho kinachoelezewa Maarifa yanaongezeka mkuu watu wanafanya Research na kuandika vitu vipya kila uchao nakushauri jiweke huru unapotaka kujifunza wakati Quran hio inandikwa hapakuwepo na technology hii iliyopo sasa kama satellite, Telescope hivo walio andika hawakuwa na clearly understanding ya ulimwengu Tunaheshimu mawazo yao but hatuwezi kusema yako sahihi 100% na yatufunge kuchunguza zaidi.

Galileo Galilie italian astromer aliwa kuingia katika ugomvi na Kanisa la Roma kwa kujaribu kueleza dunia sio Flat kama kanisa lilivyo dai ali show scientific method ya kuelezea Kuwa the Earth is sphere not Flat leo tunahakikisha kazi yake kwa wataalamu kwenda anga za mbali nakuutazama dunia really ni sphere
 
Ukichanganya dini na sayansi unaweza ukatia DOA imani yako kwa kujiuliza maswali mengi tena kwa dini zote mbili.
Doa linakuja baada ya kimoja kutotoa maelezo sahihi kati ya Science au Dini yani incompetence ya kimoja wapo Ndio inapelekea kuwe hq doubts. science inakua haijajifunga ila Dini wameweka limits
 
Ukichanganya dini na sayansi unaweza ukatia DOA imani yako kwa kujiuliza maswali mengi tena kwa dini zote mbili.
uploadfromtaptalk1453634306434.jpg
 
Jamani samahani ndugu zangu wote Mimi mkristo ila na soma sana Quran kujifunza mambo,katika Quran MUNGU MKUU anasema kuna mbingu saba ambazo ameziumba na anasema mbingu ya kwanza ambayo niyakwetu ndio aliyoipamba sana kwa nyote ili hali hizo mbingu sita azijapambwa kama hiii,na Ulikuwa maalumu kwa ajili yetu,pia Mola anasema anaendelea kuujenga kila Siku ulimwengu,kumbuka haya yamezungumzwa kwenye Quran Tukufu ata kabla sayansi ya juu kutambulika je Ina maana tunaposema kuna nyote katika galaxy nyingine tunapingana na MUNGU MKUU!?
Quran ndo nin???!!!!
 
Quran ndo nin???!!!!
Ni kitabu cha jamii ya kiarabu kinachoelezea Kanuni za maisha na baadhi Mambo katika ulimwengu kiko basic Spiritual zaidi kama kilivo Bibles cha Wayahudi ni Vitabu vya Zamani vizuri kabisa vilivyotoa muongozo wa maisha kwa zama izo na Mpaka sasa kwa baadhi ya matabaka
 
Quran ndo nin???!!!!
Ni kitabu cha jamii ya kiarabu kinachoelezea Kanuni za maisha na baadhi Mambo katika ulimwengu kiko basic Spiritual zaidi kama kilivo Bibles cha Wayahudi ni Vitabu vya Zamani vizuri kabisa vilivyotoa muongozo wa maisha kwa zama izo na Mpaka sasa kwa baadhi ya matabaka
Jamani Jamani msije mka divert mjadala ambapo tunapata elimu ya nyota,mambo ya imani tuyaache na kila mtu afate imani yake.
 
Kifyatu; nadhani unaiyona hiyo picha vzr, swali hivi hicho chombo ama object yoyote ile iliyokuwa inatoka dunian kwenda sayari nyingine may be mars kikiwa njiani chombo hicho kikafeli lakini kikiwa kimeshatoka dunian je chombo hicho kitaangukia wapi? Ni hiyo sehemu nyeusi nyeusi au kitaporomoka kuelekea kwenye jua.... Umbali wa sayari moja na nyingine ama umbali wa hizo njia(orbit) sayari moja na nyingine ni kias gani?
Elezea kwanini watu wanatembea kwa kujifunga kamba huko sayari za mbali yaani wanakuwa km wanaelea kama ile Picha la john carter,
Na je ipo sayari inayokaribia kufanana na hii ya dunia ukiwa unatembea unakuwa free kama huku ulimwenguni?!.

1. swali hivi hicho chombo ama object yoyote ile iliyokuwa inatoka dunian kwenda sayari nyingine may be mars kikiwa njiani chombo hicho kikafeli lakini kikiwa kimeshatoka dunian je chombo hicho kitaangukia wapi?
Kitaendelea tu mpaka kitakapovutwa na gravity ya sayari nyingine kama Mars, Jupiter, nk. Kikivutwa na hiyo sayari nyingine mambo matatu yanaweza kutokea kutegemea kinaikaribia katika muelekeo (angle) gani:
  • Kitavutwa na kuangukia kwenye anga la hiyo sayari. Mara nyingi kitaungua kama kimondo.
  • Kitaingia katika orbit ya hiyo sayari na kuwa satellite yake.
  • Kitatupwa kama na manati (sling-shot) na kuongeza kasi yake kuelekea muelekeo tofauti na ule wa awali. Hii ndio njia muhimu inayotumiwa na wanasayansi wanapopeleka chombo kwenye masafa ya mbali.
2. Umbali wa sayari moja na nyingine ama umbali wa hizo njia(orbit) sayari moja na nyingine ni kias gani?
Masafa ya sayari haya hapa chini.
upload_2016-1-24_12-6-48.png



3. Elezea kwanini watu wanatembea kwa kujifunga kamba huko sayari za mbali yaani wanakuwa km wanaelea kama ile Picha la john carter,
Sayari zote zina gravity na ukiwa kwenye ardhi ya sayari yoyote ile utaweza kubaki ardhini bali utakuwa na uzito tofauti na ulionao hapa duniani. Hiyo Table hapo juu inakuonesha utakuwa na uzito gani ukiwa sayari nyingine. Sasa kama mko kwenye space ambako hakuna gravity, ili msiachane kujifunga kamba ni jambo zuri. Watu hawajafika huko mbali bali kwenye space station, ISS, wanaanga wanapokwenda nje ya chombo kwa matengenezo ni muhimu wajifunge kamba kwenye hiyo ISS.

4. Na je ipo sayari inayokaribia kufanana na hii ya dunia ukiwa unatembea unakuwa free kama huku ulimwenguni?!
Mars
inafana sana na dunia yetu kimazingira bali utakuwa na uzito mdogo kuliko uliokuwa nao hapa. Venus inalingana kiukubwa na dunia yetu na uzito wako utakaribia na ulionao hapa lakini joto lake litakuua haraka sana.
Masafa ya Sayari.png

upload_2016-1-24_11-45-36.png

upload_2016-1-24_12-6-48.png
 
Ukipata seson 1 series ya Cosmos odyssey utapa info nzuri sana about stars, sun, planet galaxy... Na vitu vingi amizing abot our galaxy
 
Ukipata seson 1 series ya Cosmos odyssey utapa info nzuri sana about stars, sun, planet galaxy... Na vitu vingi amizing abot our galaxy

Mkuu, Cosmos Odyssey Series (Session) 1 ziko nyingi sana mtandaoni kutoka vyanzo mbalimbali. Ni ipi mojawapo unayoipendekeza kwa wanaoanza kujifunza haya mambo. Tafadhali tuwekee link yake hapa nadhani itawasaidia wengi.
 
1. swali hivi hicho chombo ama object yoyote ile iliyokuwa inatoka dunian kwenda sayari nyingine may be mars kikiwa njiani chombo hicho kikafeli lakini kikiwa kimeshatoka dunian je chombo hicho kitaangukia wapi?
Kitaendelea tu mpaka kitakapovutwa na gravity ya sayari nyingine kama Mars, Jupiter, nk. Kikivutwa na hiyo sayari nyingine mambo matatu yanaweza kutokea kutegemea kinaikaribia katika muelekeo (angle) gani:
  • Kitavutwa na kuangukia kwenye anga la hiyo sayari. Mara nyingi kitaungua kama kimondo.
  • Kitaingia katika orbit ya hiyo sayari na kuwa satellite yake.
  • Kitatupwa kama na manati (sling-shot) na kuongeza kasi yake kuelekea muelekeo tofauti na ule wa awali. Hii ndio njia muhimu inayotumiwa na wanasayansi wanapopeleka chombo kwenye masafa ya mbali.
2. Umbali wa sayari moja na nyingine ama umbali wa hizo njia(orbit) sayari moja na nyingine ni kias gani?
Masafa ya sayari haya hapa chini.
View attachment 319046

3. Elezea kwanini watu wanatembea kwa kujifunga kamba huko sayari za mbali yaani wanakuwa km wanaelea kama ile Picha la john carter,
Sayari zote zina gravity na ukiwa kwenye ardhi ya sayari yoyote ile utaweza kubaki ardhini bali utakuwa na uzito tofauti na ulionao hapa duniani. Hiyo Table hapo juu inakuonesha utakuwa na uzito gani ukiwa sayari nyingine. Sasa kama mko kwenye space ambako hakuna gravity, ili msiachane kujifunga kamba ni jambo zuri. Watu hawajafika huko mbali bali kwenye space station, ISS, wanaanga wanapokwenda nje ya chombo kwa matengenezo ni muhimu wajifunge kamba kwenye hiyo ISS.

4. Na je ipo sayari inayokaribia kufanana na hii ya dunia ukiwa unatembea unakuwa free kama huku ulimwenguni?!
Mars
inafana sana na dunia yetu kimazingira bali utakuwa na uzito mdogo kuliko uliokuwa nao hapa. Venus inalingana kiukubwa na dunia yetu na uzito wako utakaribia na ulionao hapa lakini joto lake litakuua haraka sana.
Uzito kuwa Mdogo kwenye mars unaadhiri nin binadam kuishi humo?

Kama uzito ni tatizo je zipo kasoro nyingine zinazopatikana ktk sayari hiyo ya mars mbali na hiyo?

Mars inaonekana ina kipindi kirefu cha mwaka, je ni zaidi ya miezi 12 kutokana na njia yake kuwa ndefu.

Tuelezee khs lile Pete lililopo pembezoni mwa mars asili yake mpk kuwepo hapo, je ni baki la sayari nyingine iliyogongana nayo.?!
 
1. Uzito kuwa Mdogo kwenye mars unaadhiri nin binadam kuishi humo?

2. Kama uzito ni tatizo je zipo kasoro nyingine zinazopatikana ktk sayari hiyo ya mars mbali na hiyo?

3. Mars inaonekana ina kipindi kirefu cha mwaka, je ni zaidi ya miezi 12 kutokana na njia yake kuwa ndefu.

4. Tuelezee khs lile Pete lililopo pembezoni mwa mars asili yake mpk kuwepo hapo, je ni baki la sayari nyingine iliyogongana nayo.?!

Majibu:
  1. Uzito mdogo kwenye Mars sio tatizo bali viumbe vitakavyoishi huko vitakuwa na mifupa na musuli hafifu (density).
  2. Uzito sio tatizo bali hakuna hewa ya Oxygen wala maji yanayotiririka kama hapa.
  3. Mwaka wa dunia ni siku zetu 365, mwaka wa Mars ni siku zetu 687. Siku ya dunia yetu ni masaa 24, siku ya Mars ni masaa 24 na dakika 40.
  4. Mars haina pete kama ilivyo Saturn isipokuwa ina miezi miwili Phobos na Deimos. Inatabiriwa kuwa siku za usoni hii miezi inaweza kupigwa dhoruba na vimondo na kuwa vumbi ambalo linaweza kutengeneza pete kama ilivyo Saturn. Kitu hicho kinaweza kutokea hapa kwetu pia kama mwezi wetu utapigwa na dhorubwa kubwa hivyo.
 
Back
Top Bottom