Ufahamu kuhusu nyota za angani

Ufahamu kuhusu nyota za angani

Hii itatokea for sure, labda dunia yetu iangamizwe na kitu kingine kabla ya siku hiyo ya mwisho.

Jua letu kwa sasa linachoma hewa ya Hydrogen kutengeneza Helium. Itachukua mabilioni ya miaka kuimaliza hii Hydrogen. Hydrogen ikimalizika itaanza kuchoma helium kutengeneza element nyingine nzito.

Jua litakapoanza tu kutengeza chuma (Iron) basi hilo jiko la nuklia linakufa mara moja na kishindo kikubwa kitatokea (soma maelezo yangu ya awali kuhusu Super-Nova katika uzi huu huu). Jua letu halitakufa kwa kishindo kikubwa kama cha supernova bali kitatosha kutimua vumbi lenye joko kali litakaloimeza Mecury, Venus, sisi (Earth) na hata kuikaribia Mars.

Jibu rahisi la swali lako ni "NDIO", dunia yetu itakujamezwa na jua siku moja (hakuna utata hapa). Lakini itachukua mabilioni ya miaka kufikia huko.

Kwa sasa, wewe jivinjari tu na moja moto moja baridi ukijua wazi kuwa wewe, watoto wako, wajukuu, vilembwe, nk. wataamka kila asubuhi yao na kiliona jua kama lilivyo leo.
Maelezo mazuri!....Naonba utufafanulie hapa ya kuwa ni kitu gani kingine utafiti wa kisaysnsi umebaini kuwa huenda kikaangamiza dunia?.Kuna Sayari mojawapo siikumbuki nilisoma mahali kuwa inapigwa sana na vimondo je kwa nature ya mifumo ya sayari hili haliwezi kutokea kwa Dunia yetu?
Cc kifyatu!
 
Majibu:
  1. Uzito mdogo kwenye Mars sio tatizo bali viumbe vitakavyoishi huko vitakuwa na mifupa na musuli hafifu (density).
  2. Uzito sio tatizo bali hakuna hewa ya Oxygen wala maji yanayotiririka kama hapa.
  3. Mwaka wa dunia ni siku zetu 365, mwaka wa Mars ni siku zetu 687. Siku ya dunia yetu ni masaa 24, siku ya Mars ni masaa 24 na dakika 40.
  4. Mars haina pete kama ilivyo Saturn isipokuwa ina miezi miwili Phobos na Deimos. Inatabiriwa kuwa siku za usoni hii miezi inaweza kupigwa dhoruba na vimondo na kuwa vumbi ambalo linaweza kutengeneza pete kama ilivyo Saturn. Kitu hicho kinaweza kutokea hapa kwetu pia kama mwezi wetu utapigwa na dhorubwa kubwa hivyo.
Samahani kifyatu Uzi ni wa zamani sijui kama bado unaupitia mkuu!,Mimi nauliza tu ikiwa mwezi wetu wa hii dunia kama utapigwa na dhoruba ya vimondo na kuwa kama vumbi vumbi linaloizunguka hii dunia,Ni yapi yatakuwa mabadiliko ya matokeo hayo hapa duniani?
 
Daaa aiseee tunakosa maarifa kwa sababu ya wajinga wachache.
Wapenda anga tuandamane mpaka aje 😂😂😂😂.
Mwenyewe alisema aliishia pale wengine waendeleze, ila tuseme ukweli alijitahidi mno , hakosi comment zaidi ya mia kwenye uzi huu na zote zimeshiba haswa, hata ingekuwa ni mimi ningeishia pale.
 
Mwenyewe alisema aliishia pale wengine waendeleze, ila tuseme ukweli alijitahidi mno , hakosi comment zaidi ya mia kwenye uzi huu na zote zimeshiba haswa, hata ingekuwa ni mimi ningeishia pale.
Ngoja nizipitie maana mimi nimesoma mwanzo nikarukia page ya mwisho.
Ahsante sanaaa kwa kujali kwako mkuu.
 
Ngoja nizipitie maana mimi nimesoma mwanzo nikarukia page ya mwisho.
Ahsante sanaaa kwa kujali kwako mkuu.
Mhh, mbona upo kwenye uzi huu toka 2019 huko, upitie my dear, ni uzi ambao ukisoma hauta hauta baki kama ukivyokuwa kabla, ume jaa makubwa mno .
 
Back
Top Bottom