Tetesi: Ufisadi: Inasemekana kila mwanakikundi wa ngoma kutoka Bagamoyo walioenda Marekani matumizi kwa siku ni milioni 3!

😀 Aliyebandika uzi huu amekula za uso mpaka anatamani kufuta uzi na haufutiki

alitaka wasanii walipwe laki 1 kwa siku jijini New York🤭
 
sasa 3MIL pamoja na hotel kwa siku USA kuna tatizo gani? .... huoni kama wakirudi watakuwa na salio la kutosha mfukoni ambalo watalileta huku beach kidimbwi na kugawana na wazalendo wengine...

Kwani umeambiwa hizo fedha wanazishika wao?
 
Wabongo bhana. Hotel pale New York utalipa chini ya Dola 200 Kwa siku. Huo ni msafara wa Rais he unataka wakalale guest na Kula Kwa mama ntilie?

Hapo utakuta Kati ya hito milion 3 mtu anabak na Laki tano tu Kwa siku
 
Kama Kweli wanalipwa sio Mbaya kikubwa wasiiibe kama kweli inawafikia hao Wana sanaa ni Jambo jema kwani ni intarahamwe si ni watanzania hao
 
Hela ndogo sana kama ni pamoja na gharama za hotel. Waache na wao wale maana wameacha shughuli zao majumbani mwao na familia pia zinawategemea.
Wewe acha uongo, 3,000,000/2300 = dollar 1300 kwa siku hakuna rate ya dollar 1300 serikalini sana sana watakuwa wamelipwa dollar 300 kwa siku na hii inawatosha kwa kiwango chao cha vyeo vyao. hiyo dollar 1000 inakwenda wapi???

Kwa New york hawa wakata viuno hawawezi kuishi mitaa ya Manhattan a.k.a Yankees city, sana sana wataishi Chinese city iliyoko nje kidogo ya Manhattan city
 
Shida iko wapi mpaka kuita ufisadi...
Hebu fafanua ufisadi ni nini..
 
Mil 3 kwa siku nchini Marekani kuna tatizo gani, au unadhani kule Hotel ni shilingi 25,000/= kama Sinza ???
Tena hapo wako New-York inabidi walipwe zaidi. Mtoa mada una nongwa sana wewe......
 
Huu mfumo ccm ni shida ndugu watanzania!
 
Ungeenda wewe ukakate mauno mkuu ulipwe wew, huo ni wivu tuy
 
Kwanza wale misosi gani huko; unapiga mkate na kasoda mambo yanasonga shekeli zingine unarudi nazo kuja kufanya mambo ya kiuchumi!

Nadhani jamaa ameumia kwa kuona kwamba ni wacheza ngoma, dharau tu kwa kazi za watu. Mbona hajasema wengine wanapata kiasi gani.
Nadhani ana wivu aliousema Msekwa mwaka flani!!!
 
Milioni tatu hizo ni dola karibia 1500 kumbuka wako jiji la new york mi naona wamewaonea sana itakua wanalala vichochoroni huko na hamna hata kula bata..

===
Bei ya chumba kwa siku ni Kati ya laki 2 mpaka 4.
Narudi.
 
Ukishaanza habari yako na maneno 'inasemekana' tayari umeshapoteza uhalali wa kuaminiwa. Jifunze sanaa ya uandishi.
 
Milioni tatu hizo ni dola karibia 1500 kumbuka wako jiji la new york mi naona wamewaonea sana itakua wanalala vichochoroni huko na hamna hata kula bata..
Nimerudi.


How much money will you need for your trip to New York City? You should plan to spend around $238 per day on your vacation in New York City, which is the average daily price based on the expenses of other visitors. Past travelers have spent, on average, $37 on meals for one day and $39 on local transportation. Also, the average hotel price in New York City for a couple is $274. So, a trip to New York City for two people for one week costs on average $3,336. All of these average travel prices have been collected from other travelers to help you plan your own travel budget.

===
Laki moja inatosha kwa chakula cha siku moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…