Black Sniper
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 32,406
- 55,148
Jaribu mkuunajaribu kuweka picha hapa za baadhi ya mifugo wangu lakini naoana mitambo inanigomea nikifanikiwa nitawashirikisha kwa njia ya picha tuendelee kujifunza kwa pamoja.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Jaribu mkuunajaribu kuweka picha hapa za baadhi ya mifugo wangu lakini naoana mitambo inanigomea nikifanikiwa nitawashirikisha kwa njia ya picha tuendelee kujifunza kwa pamoja.
Asante sanaGalla/isiolo huwa wanapatikana majike wakubwa amabao tayari kupandwa na kuzaa ni sh laki 2, madume ndio wana bei ni kuanzia laki 2 mpaka 5 inategemeana na ukubwa na umri wa Mbuzi, napo wakati wakununuwa unapashwa uangalie swala la umri ni muhimu sana hasa kwa Dume usije chukuwa mwenye umri mkubwa sana akashindwa kutumika vyema.
Naomba namba zao mkuu. Au na mimi uniunge kwenye tagofaSisi ni TAGOFA chama cha wafugaji Mbuzi Tz na mletaji ni mwanachama , Mbuzi waliletwa kwa njia ya bara bara na hata ASAS last week kaleta Ngombe kutoka south kwa njia ya bara bara. Msafirishaji anashughulikia vibali vyote wewe unapokea Mbuzi mwenye nyaraka kamili, nawaomba ruhusa niweke number zao humu mtaweza wasiliana nao moja kwa moja.
Vp umeanza kuuza wako kiongozi?najaribu kuweka picha hapa za baadhi ya mifugo wangu lakini naoana mitambo inanigomea nikifanikiwa nitawashirikisha kwa njia ya picha tuendelee kujifunza kwa pamoja.
Bado sijaanza ndugu siku nikianza kuuza nitasemaVp umeanza kuuza wako kiongozi?
Ahsante sanaUshauri wangu jitahidi baba asipande mwanae yaani uchanganye damu usirudie uzao ukapanda uzao unaofuta utapata wanyama bora sana. Japo sio lazima ni wewe na uwezo wako
Ahsante kwa mawazo mazuri sana...Nawasalimuni kwa jina la Mungu. naomba niwapongezeni sana nyote ktk kujenga mawazo ya kutaka kuingia ktk miradi kama hii ya ufugaji. Mimi ni mfugaji wa Mbuzi na nina fuga Mbuzi kwa muda mrefu, niwaombeni kitu ufugaji ni mzuri na una faida na changamoto zake, kikubwa ni kukubali kujifunza na kujijengea umakini ktk ukaguzi na usimamizi wa mifugo yako. Kwa aliyepo Dar namkaribisha kwangu aje tujifunze pamoja na tugawene ujuzi kwa pamoja. Kwa anae anaza kufuga nakuomba sana usinunuwe mbegu kwanza kabla hujapita kwetu wafugaji tulio kutangulia ujifunze vitu halafu ndio uingize Mbegu shambani kwako. Karibuni kwa maswali mbali mba;li nipo hapa tutasaidiana kwa kadiri Mungu atakavyo tujaalia.
Niko mwisho wa reli Kigoma ndugu yangu...Mwalimu ; unapatikana wapi- Unaishi wapi hapa Tz.?
Ahsante Joka.Nimejifunza kitu kutoka kwako.Ubarikiwe!..Pure Boer bei yao ni kubwa sana kuweza kuwasafirisha toka Afrika Kusini.
..Kwa hapa Tanzania sio rahisi mfugaji kukuuzia mbuzi Boer Pure kwasababu wengi wako ktk stage ya kuwa-cross na kuwazalisha ktk miradi yao.
..Kuna wafugaji wakubwa kama Mbogo Ranches nilisikia kwamba wanaweza kuwasaidia wafugaji wadogo kuagiza mbuzi hao.
..Naamini njia nzuri ni watu kuwa ktk kikundi na kuagiza beberu ambaye atatumika ku-cross na mbuzi wa kienyeji.
..Jambo lingine la TAHADHARI ni kwamba beberu la Boer likiwa kubwa sana linaweza kumuumiza mbuzi wa kienyeji wakati wa kupanda.
..Pia mbuzi wa kienyeji anaweza kupata matatizo wakati wa kujifungua baada ya kupandwa na Boer.
..Kwa hiyo ni vizuri kuchagua beberu ambaye ni mdogo-mdogo ili aweze kuwapanda mbuzi wa kienyeji bila kusababisha ajali.
..pia ni vizuri kuwa makini ktk kuchagua majike wakubwa imara watakaoweza kuhimili mshindo wa beberu la Boer.
Nakufata inbox ndugu,Nahitaji namba yako ya WhatsApp kwa ushauri zaidi kuhusu ufugaji wa Mbuzi.Naomba niwasaideni kitu hapa kuagiza Mbuzi south Afrika hakuna urasimu wowowte mimi nazungumzia uzoefu na ninacho kifahamu, mwakajana mfugaji mwenzetu kaleta Red kalahar bila ya shaka na ktk umoja wetu wote walio agiza wamepata, shida ni moja kubwa hata kule south kunawapigaji sana. mnacho takiwa ni kufwata waagizaji wanaojuwa wazalishaji wa ukweli, hata ukienda uganda hata Mubende watakupiga tu ninaushahidi kwakweli. Mbogo Ranchese, Mavuno Farm, Biswalo, Usangu, ASAS. Hao ni waagizaji wa kweli na watakupatia kitu unacho hitaji, wakikuzulumu njoo Nyumbani kwangu nakulipa Mubende 1 bure kabisa.
Kigoma nitakupa somo la Buha wapo kigoma wanazaa vyema hao.Niko mwisho wa reli Kigoma ndugu yangu...
Karibu sana ndugu yangu tujifunze na kufuga kwa pamoja.Nakufata inbox ndugu,Nahitaji namba yako ya WhatsApp kwa ushauri zaidi kuhusu ufugaji wa Mbuzi.
Wanapatikana vijijini ila tu ukubali ghrama muuzaji anaweza kutaja bei isiyo ya kawaida hasa ukimfuata kwake.Ni wazo zuri nami Nafikiria kufanya hivyo ingawa kupata hao wanaozaa mapacha ni bahati nasibu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]sana aisee[emoji38] [emoji23] mbuzi washenzi sana kwanza wakiona shamba utafikiri umewatuma
Kwakweli hapo ungetueleza ukanda ulipowaona hapo labda tungeweza kukusaidia ni aina gani wanapatikana ukanda huo, na picha ingesaidi kusoma hilo.Naomba kufahamu kuna mbuzi nilionaga mahali ni weupee mwili mzima baadhi wana rangi nyeusi kichwani na wanamaumbo makubwa pia wanazaaa mapacha,hawa ni aina gani na wanapatikana sana maeneo gani??