Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Mkuu Kanyagio, umenivunja mbavu jioni ya leo, Elnino amejikita ktk ufugaji wa Mayai. na kilimo cha mahindi alipoanza kilinitia moyo nami nikaanza kuota ndoto za kulima mahindi,nadhani sasa atakuwa akivuna na kutengeneza chakula cha kuku wa mayai

Wakuu, ni vugumu kutenganisha kilimo na ufugaji, kwa mafano kwenye ile formulla ya Kuku wa mayai unaona kabisa mahindi ni kilo 500 katika kila tani. soko la sasa hapa dar kilo ni sh 490 - jumla ni Tshs. 245,000.

Sasa mimi badala ya kununua haya mahidi ninaji - supply mwenyewe. Kifupi bado nafanya Kilimo na ufugaji kwa pamoja. Kilimo changu pia kinaendana sambamba na ujasiliamali kwamba wakati wa mavuno pia nanunua mazao toka kwa wakulima wenzangu na kuweka kwenye stoo zangu, ampamo chakula hiki hutumia kulishia mifugo yangu.
 
wakuu,

katika pita pita yangu mitaani nimekutana na fuso nyingi tu za mayai, nikauliza wanasema zinatoka Mombasa kenya na mayai wanauza tray kwa 4200/- vipi nyie wafugaji wa kuku wa mayai mmejiandaa vipi na ushindani huu?

naanza kuwa na wasiwasi juu ya ushindani huu - tutauweza kweli kwa bei hii? average ya bei ya tray hasa hapa dar ni kati ya Tshs. 5500/- mpaka 6000/-
 
ngoja tufanye mahesabu hapa ..... okay

let say body ya fuso ina upana = 2.5 meters urefu 5.0 meters na kina =3.0 meters

hivyo basi tray ya mayai ina urefu sawa na upana = 30 centimeters = 0.3 meters

2.5/0.3 = 8.3

5/0.3 = 16

3/0.3 = 10

then 8x16x10 = 1280 , roughly total number of trays of eggs fuso can carry is 1280

if the farmer sells and get 1000 per tray as profit he gets 1,280,000 per fuso times three fuso at a time = TZS 3,840,000 (say per week)

assume that this is the farmer and not a broker and all costs of keeping the layers chicken and transportation cost(fuso from mombasa) is 4200 - 1,000(profit) = 3,200 (investment cost and transportation)

price of Tsh 4,200 per tray was suggested by FUSO

is it a good business?
 
wadau naomba kuuliza,
watalaam wa ufugaji kuku wa mayai. naomba kujua eti kwa vifaranga unapoviweka bandani, kwenye sakafu unatanguliza maranda au unaweka kwanza magazeti. nataka nijue namna ya kutengeneza chick bedding!!
nitashukuru!!
 
Habarini wana JF, nina furaha kuwataarifu wanajamvi hasa wale wapenzi wa jukwaa la uchumi kuwa nilianza mazoezi ya mradi ambao ulitambulishwa na mwanajamvi mwenzetu GAZETI kwa title ya je unataka kuwa tajiri. Ukweli ni kwamba mradi unaendelea vizuri sana na unaleta matumaini makubwa tena zaidi ya vile alivyokadiria muheshimiwa gazeti. Kwa wale ambao hawakubahatika kuisoma post hiyo wafanye hima kuisoma kwani njia alizofundisha ndizo ninazotumia nimeongeza utaalamu kidogo tu kutoka kwa mshauri wa Kilimo. Kwa wale ambao hawakubahatika kusoma mwongozo huo wafungue hapa https://www.jamiiforums.com/business-and-economic-forum/113459-unataka-kuwa-tajiri.html

Nimependa ulivyorudisha feedback ya matokeo,hii inajenga zaidi.
 
wadau naomba kuuliza,
watalaam wa ufugaji kuku wa mayai. naomba kujua eti kwa vifaranga unapoviweka bandani, kwenye sakafu unatanguliza maranda au unaweka kwanza magazeti. nataka nijue namna ya kutengeneza chick bedding!!
nitashukuru!!

Lazima ujiulize maswali machache tu

a) Kwa nini unaweka maranda?
b) Kwa nini unaweka magazeti?
c) Kwa nini unafanya cover kwenye madirisha kwenye banda la vifaranga na kuachia sehemu za kupitisha hewa?

Vitu hivi ni basic na lazima kila mfugaji aelewe maana ya kila hatua.

Malanda: tunapunguza phyical contact kati ya kifaranga na sakafu, by asumming sakafu ina ubaridi na pia inatuza bacteria kwa urahisi wakati wa unyevu. kwa ku apply malanda juu ya sehemu watayoishi vifaranga basi unapunguza contact hence kupunguza magonjwa kwa vifaranga / kuku.

Magazeti unaweka juu ya malanda, hasa kupunguza vumbi, wote tunajua vifaranga hukimbia kimbia na watatimu vumbi ambalo litawafanya waugue mafua - sasa ukiweka magazeti unapunguza case hii. hakikisha hakuna phisical contact kati ya kifaranga na sakafu, pia hakikisha banda ni kavu muda wote.

Utaziba madirisha kuweka joto la kawaida la vifaranga arround 35 - 38C. kama huna umeme (Dowans) kwa ajiri ya kuongeza joto basi unaweka kutumia chemli. Jiko la mkaa ni hatari kwani carbon inayotoka hapo inaweka kuwa sumu usipokuwa mwangalifu.


Mi si daktari wa mifugo ila majarida na vipeperushi vinasaidia sana. Madaktari wataongezea.
 
FUSO umesema kwamba nisitumie jiko la mkaa, bali nitumie chemli.. ahsante kwa kunielimisha hiki kitu maana mimi nilishanunua majiko hayo
 
FUSO umesema kwamba nisitumie jiko la mkaa, bali nitumie chemli.. ahsante kwa kunielimisha hiki kitu maana mimi nilishanunua majiko hayo

unaweza kutumia hayo majiko ya mkaa ila uwe mwangalifu sana - unaweza kuua vifaranga vyote sababu moshi wake una carbondioxide ambayo ni sumu wa viumbe hail - kuepuka hilo we nunua chemli, nenda kariakoo soko kuu utazikuta kibao.
 
hongera sana mkuu, labda mimi kwa kukusaidia nikupe namba ya mtu fulani wa dodoma anatengeneza incubeter nzuri sana kama utataka lakini
Kaka Komandoo nimekuwa nafuatilia issue hii kwa umakini na nitakuwa Dodoma next week. Je unaweza nipatia namba ya huyo mtaalamu wa incubator?
 
Kaka Komandoo nimekuwa nafuatilia issue hii kwa umakini na nitakuwa Dodoma next week. Je unaweza nipatia namba ya huyo mtaalamu wa incubator?

mkuu unataka incubator ya kutumia mafuta ya taa au umeme? mbona zipo dar kibao - nenda SIDO makao makuu idara ya umeme mdogo (electronics department) utakutana na wataalam.
 
mkuu unataka incubator ya kutumia mafuta ya taa au umeme? mbona zipo dar kibao - nenda SIDO makao makuu idara ya umeme mdogo (electronics department) utakutana na wataalam.
Kaka Mie naishi mwanza nod maana nikataka kumwona huyu ndugu yetu wa Dom
 
Tukutane nane nane kesho wote mliko Dom...........ni PM niwapeni contacts zangu
 
Asante jamani wote kwa ushauri na michango yenu! nimejifunza mengi sana, ngoja tukatafute mtaji tuingie kwenye ligi tupambane na umaskini. Mungu awabariki sana!
 
price of Tsh 4,200 per tray was suggested by FUSO

is it a good business?

Mkuu unajua wenzetu wa Kenya wana busara sana.., ufugaji wao sio mkulima mmoja mmoja wanafuga kwa ushirika.., hivyo basi wanakuwa na guarantee ya production ya mayai sababu mtu mmoja ukiomba contract ya kuuza mayai au nyama kwenye kampuni kubwa huenda wasikupe sababu kunakuwa hakuna guarantee kwamba utaweza ku-supply big quantity kila watakapohitaji.

Lakini wenzetu sababu ya umoja wao wanakuwa na uhakika wa ku-supply amount yoyote wakati wowote pia hata chakula wananunua kwa volumes kwahiyo inakuwa cheaper...

Kila kitu ni soko, mfano mimi ninajua mtu anafuga kuku wa nyama na anajua kwamba baada ya miezi kazaa watakuwa wamekuwa wakubwa kwahiyo kunakuwa kuna soko tayari la kuwauza wote pindi wakikuwa tu, sio mwingine kuku ameshakuwa mkubwa ready for market yeye ndio anaanza kutafuta soko baada ya kupata soko anajikuta kuku amekula chakula kingine cha mwezi mzima ambacho hakutakiwa akile
 
Mkuu unajua wenzetu wa Kenya wana busara sana.., ufugaji wao sio mkulima mmoja mmoja wanafuga kwa ushirika.., hivyo basi wanakuwa na guarantee ya production ya mayai sababu mtu mmoja ukiomba contract ya kuuza mayai au nyama kwenye kampuni kubwa huenda wasikupe sababu kunakuwa hakuna guarantee kwamba utaweza ku-supply big quantity kila watakapohitaji.

Lakini wenzetu sababu ya umoja wao wanakuwa na uhakika wa ku-supply amount yoyote wakati wowote pia hata chakula wananunua kwa volumes kwahiyo inakuwa cheaper...

Kila kitu ni soko, mfano mimi ninajua mtu anafuga kuku wa nyama na anajua kwamba baada ya miezi kazaa watakuwa wamekuwa wakubwa kwahiyo kunakuwa kuna soko tayari la kuwauza wote pindi wakikuwa tu, sio mwingine kuku ameshakuwa mkubwa ready for market yeye ndio anaanza kutafuta soko baada ya kupata soko anajikuta kuku amekula chakula kingine cha mwezi mzima ambacho hakutakiwa akile

Kaka uliyosema ni kweli, sisi watanzania hatuna umoja na ndiyo maana production zetu ni hafifu zikiingia sokoni - mfano nilioutoa hapa ni kwamba
Wafugaji wa kuku nchini kenya wananunua Mashudu ya alzeti, Pumba za mahindi na Mahindi kutoka Tanzania - Then wanarudi kutuuzia mayai tena yenye ubora. Najiuliza je tukiingia kwenye soko huria si watatumaliza kabisa.

Mtu anaweza kusema tusiogope kuingia kwenye soko la pamoja la africa mashariki lakini ndugu zangu wakenya wapo juu sana karibu katika kila sekta. Watanzania tujifunze umoja.

Kwa mafano juzi nilimsikia mama mmoja anasema yeye anapekeka kuku ya nyama somalia na arabuni - wana soko kubwa sana huko - sasa vitu kama hivi ndivyo vya kuanzia kufanyia kazi. Mnaungana watu kama 10 ambao ni wafugaji wa kuku lets say, then mnatengeneza kitu chenye quality mnauza n'gambo.

Kwa sasa mayai mengi sana yanatoka Mombasa na yanauzwa tray kwa Tshs 5000 tena yana ubora mzuri. sisi mayai ya hapa TZ ni 5500 kwa bei ya jumla lakini mengine hayana uzito na ukubwa unaotakiwa sokoni.

Watanzania tuamuke - tusaidieane - tusipende kufanya vitu kipekee pekee - HATUFIKI POPOTE. mfano unakuta wafugaji karibia kumi na ni majirani kila mtu anafuga kuku wa nyama mia mbili, mia tatu tatu hivi - je kama hawa watu wangekuwa na umoja na kutengeneza kitu chenye ubora na kutafuta soko lenye uhakika. Inawezekana, tatizo hatuna hii culture ya kuungana.
 
Asante kwa kutufungua macho, na ninashukuru kwa mchango wako.
Kuna tatizo la mahesabu kidogo. Jumla ya gharama ni 1,590,277 na siyo 1,490,277 na kufanya faida kuwa 1,702,523. Kwa kuwa unatumia Msexcel
nakushauri utumie formulas badala ya kutype figures zote:
Column ya mapato( e3)andika =b3*d3 press enter, jibu litakuja pale. Then click kwenye E3 then kwenye right hand lower corner itakuja alama ya msalaba (+), press your left side mouse usiachie na vuta kwenda chini. Fomula itakuwacopied hadi chini yaani E4 itakuwa =b4*d4 nk. Kuweka jumla mwishoni click kwenye cell unayotaka jibu liwe e34 halafu nenda juu kwenye tool bar click
∑ basi jibu la jumla ya namba hizo itakuja,kwanza itajionyesha kwa kuhighlight, au andika =sum(e3:e33) press enter. Fanya hivyo hivyo kwa upande wa gharama, utapata jibu sahihi. Na profit ni =e34-f34. Hii inapunguza makosa madogo madogo ya kimahesabu
Pili tungefurahi zaidi kama ungetueleza una kuku wangapi? na sikuelewa eggies!
Thanks again

Mkuu.thread #12 kasema anao 900.Hiyo nyingine I think alikusudia eggs,may be somebody else did it for him/her lol!
 
wanajamvi, wapi nitapata kuku wa kienyeji wa miguu mifupi (kuna sehemu wanaitwa CHING'WEKWE). nasikia wanapatikana Morogoro, ila kwa kuwa sina contacts za uhakika huko; naomba mwenye kufahamu contact ya mtu mwenye nazo aturushie hapa.

sifa za kuku huyu ni: Majogoo wana wastani wa kg 1.6, Mitetea wastani kg 1.2, mayai wastani wa gm 37. Kuku hawa wenye umbo dogo hupatikana zaidi maeneo ya CHAKWALE mkoani Morogoro na pia sehemu za umasaini. Kuku hawa hutaga mayai mengi sana kuliko aina nyingine ya kuku wa kienyeji waliopo Tanzania, kwa hiyo wanafaa sana kwa biashara ya mayai (source ni hapa hapa JF).
 
Back
Top Bottom