Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

wakuu habari za leo.kwa m

wenye kuwa fahamu bata bukini naomba ushauri.nina bata bukini mwaka wa pili sasa hawajawah kutaga sijui tatizo ni nini.upande wa lishe wana kula vizuri.
 
habari ndungu zangu!namhukuru sana Mungu kwa kuujua uzi huu.Zamani wakati nikiwa kijana mdogo niliamini ili uweze kufanikiwa kwenye ufugaji wa kuku nilazima uwe na kalama au mkono wa kuku,mara nyingi ktk familia yetu huko kijijini tulikuwa tunafuga kuku mimi na ndugu zangu hatahivyo mimi nilikuwa nabaki mwisho kwa kuwa na idadi ndogo au kutokuwa na kuku hata mmoja hii ilisababishwa na kufa kwa vifaranga pia kufa kwa kuku wakubwa kwa magonjwa na sababu zingine ila kuna mdogo wangu yeye alikuwa anafanikiwa sana kwenye ufugaji wa kuku kuliko wote hivyo ikaaminika kuwa huyo mdogo wangu anamkono wa kuku na mimi sina mkono wa kuku.binafsi nilikuwa napenda sana kufuga kuku lakini nikikumbuka kuwa sina mkono wa kuku najisikia vibaya ila siku moja mwanzoni mwanzoni mwa uzi huu mwaka 2013 niliamua kutoa dukuduku langu humu nashukuru nilipata ushauri ambao ulinitia moyo hadi kufikiria kuanza ufugajia.Baada ya kuweka mazingira vizuri nikaanza ufugaji wa kuku wakienyeji na chotara na mrejesho niliuleta humu ndani page na.43.Uwezi amini matokeo ya ufugaji huo hususani nwaka jana yalikuwa mazuri sana kwani tangu nianze kufuga kuku sikiwahi kuwa na kuku wengi kama wale tena nilikuwa nawafuga huria niliwauza xmass,mwaka mpya na pasaka na bado nina kuku ambao wao nimewaacha kama wazazi.Ninacho taka kushauri tuachane na mambo ya imani zinazo katisha tamaa na kutia hofu mimi naamini ukiwa na maarifa ya kutosha juu ya jambo fulani inatosha kwa asilimia 95 kufanikiwau
 

Asante sana Mkuu kwa mrejesho wako ! Ukweli asilimia 95 kufikia mafanikio ni juhudi na maarifa, asilimia 5 tu ndiyo bahati ! Tuko pamoja sana.
 
Mlioko mashambani limeni sana zao la mikunde aina ya soya (soya beans) haya yanaondoa kabisa haja ya kutumia dagaa kwenye utengenezaji wa chakula cha kuku, kinachotakiwa ni kununua amino acid aina mbili ambazo zinakosekana kwenye soya bean lakini zinapatikana kwenye maduka ya kilimo. Ukilima soyabeans na mahindi au mtama kwa ajili ya kutengeneza chakula cha kuku unapunguza nusu ya gharama ya uzalishaji wa kuku. Katika ufugaji wa kuku asilimia 70 ya gharama za uzalishaji ni chakula pekee, ukifanikiwa kutengeneza chakula mwenyewe unapunguza gharama ya uzalishaji sana na hatimae unajipatia faida kubwa zaidi.
 
Huu uzi ndo ulinifanya nikaijua jamii forum enzi hizo nasearch habari flani kwenye Google ndo nkaikuta hii mada. Nliifuatilia sana ndo badaye nkashawishika kujiunga mana nlikuwa natamani kuchangia ila nashindwa. Nlikwmbia harakati za Kubota alivyokuwa anachambua na kuleza magonjwa ya kuku, kisha anatuacha kwanza anaenda kutizama mkaa wake shambani afu tunamsubiri weeee siku kadhaa ndo anarudi teh teh
 
Mungu akujalie maisha marefu bro Kubota. Watu makini wanajua mchango wako hapa JF.
Hakika nlipata sana ujuzi kupitia huyu brother na kama site yeye pengine nsingekuwa jf kabisa ama ngechelewa mda kuifahamu. Cc Kubota thanks in advance my brother.
 
Wanajamvi habari za najukumu, baada ya hapo naomba nisaidiwe kuku wangu wanatabia ya kutaga mayai sehemu moja nimejaribu kuwatengea viota lakini wamekua wakichagua sehemu moja Na kutaga wote naweza Fanya nini ili wote waatamie mayai maana nikimwachia mmoja mayai ni mengi atayaaribu Masada wenu wakuu.
 
natamani sana kufuga kuku wa broiller lkn bei za vyakula zipo juu sana na risk ya kufs kwa vifaranga ni kubwa sana....lkn nitafanya maana siwez kujifunza bila kufanya amakosa.
 
Mm nahamia Tanga mwezi wa saba, nmefika maeneo ya Pande. Naplan kufanya hii biashara make nshaifanyaga...
 
. Mashamba huko wanauzaje kwa heka moja mkuu?
Kwa wale wanaoitaji kuku wakienyeji mim nawauza.
1:Nauza vifaranga kuanzia cha siku Moja mpaka wk
Tatu.
2: Nauza vifaranga vya kuroila kuanzia siku moja mpaka wk tatu:
3: Nauza vifaranga vya kenbro kuanzia siku moja mpaka wk tatu
4: Nauza vifaranga vya Kuchi kuanzia siku moja mpaka wk tatu.
Shamba liko mkoa wa Tanga na Arusha.
Napatikana kwa number 0762355114
 
Kifaranga wa kuchi wa wiki tatu unauza bei gani?
 
elimu tuliyopata hakika ni shule to sha mungu mwema awabariki wote waliotoa yao maoni ktk suala zima la ufugaji wa kuku wa kienyeji. ..ila wengi hawa kurudi kutuelezea walifanikiwa baada ya ufugaji au walifeli?
 
Hakikisha unatanguliza chokaa chini unamwaga kwakutandaza,chokaa hii inayotumika kwenye ujenzi husaidia kukomesha kuzaliana kwa wadudu baada ya kuweka randa.Kwakufanya hivyo utakua umekomesha kabusa habar ya viroboto ioa uwe unabadili randa mara kwa mara.Randa ni nzuri zaidi kuliko pumba ya mpunga.@kurusabha
 
Mada nimeipenda,ila Dawa nzuri kwa viroboto cha kwanza ni usafi wa banda la kuku wa Mara kwa Mara na kuna dawa za kumwagia bandani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…