Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Dawa ni hii

Wapake rangi ya Ukili au ile rangi inayopakwa kwenye Mikeka yaani wapake kiwiliwili chote, kuna rangi nyekundu,blue manjano au yeyote ile hii itamfanya kuku aonekane kiumbe cha Ajabu
fc914dc56828ab49a721ece007f1ee43.jpg
cec46d97edd1722ea647eba139c0a8bd.jpg
 
Hugo no kipanga mkuu,mbaya sana Hugo kiumbe,akikosa vifaranga atahangaika na hao kuku wakubwa hata anyofoe bwawa tu.
Na hivi keshajua hapo kuna ulaji hachomoki ng'o, fugia bandani hata kwa muda skate tamaa kuja hapo.
 
Dawa ni hii

Wapake rangi ya Ukili au ile rangi inayopakwa kwenye Mikeka yaani wapake kiwiliwili chote, kuna rangi nyekundu,blue manjano au yeyote ile hii itamfanya kuku aonekane kiumbe cha Ajabu
fc914dc56828ab49a721ece007f1ee43.jpg
cec46d97edd1722ea647eba139c0a8bd.jpg
Umenikumbusha mbali sana hii pic
 
1. Huu kwa juu ni wavu?
2. Wanakaa humu kwa muda gani baada ya kutotolewa?
3. Unaweza taa au chungu chenye moto ili wapate joto?
4. Chakula unawapa kiasi gani kwa siku let's say wapo 15 kwenye box?

Samahani kwa maswali mengi mkuu.
Nilikuwa sijaliona hili swali (Samahani)
Kwanza haya unayoyaona ni mabox ya pikipiki, huku tunanunu 5000 mpaka 10,000
na wakati mwingine huwa yanatupwa na wauzaji. (Uliza kwa watengenezaji au wauza pikipiki)

1.Hayo maboksi yanakuja na mifuniko, mimi nimekata sehemu ya juu ya mfuniko nikaziba
kwa waya wa Dirishani kama unavyoonekana.

2. Wengi huwaweka hadi pale wanapoweza kuruka na kutoka nje ya box, binafsi sina mudaa maalumu
Wakishatotoa wengine huwa naangalia box ambalo wamekomaa nawaondoa na kuwaweka wapya

3. Wakati wa joto siweki chohote, wakati huu wa baridi huwa nawawekea hiyo mitungi
ambayo nimeiweka kwenye picha huku tunanunua kwa 3000 mpaka 5000. Kunambinu nili
fundishwa ya kuufanya mkaa udumu muda mrefu bila kuzimika au kuisha, huwa njaza unga
unga au chenga za mkaa hapo juu, pia huwa naloweka jivu na kuliweka (Uliza kwa wauza kahawa
watakuelekeza vizuri zaidi)

4.Huwa nawakadiria tu, wakimaliza nawaongezea tena. Machicha ya nazi, pumba za mahindi
' Pumba za dagaa n.k isipokuwa siku 3 za mwanzo naweza kuwapa kile kilichochanganywa kwa
ajili ya vifaranga, maa nyingi nanunua kwenye maduka ya kilimo.
 
Nilikuwa sijaliona hili swali (Samahani)
Kwanza haya unayoyaona ni mabox ya pikipiki, huku tunanunu 5000 mpaka 10,000
na wakati mwingine huwa yanatupwa na wauzaji. (Uliza kwa watengenezaji au wauza pikipiki)

1.Hayo maboksi yanakuja na mifuniko, mimi nimekata sehemu ya juu ya mfuniko nikaziba
kwa waya wa Dirishani kama unavyoonekana.

2. Wengi huwaweka hadi pale wanapoweza kuruka na kutoka nje ya box, binafsi sina mudaa maalumu
Wakishatotoa wengine huwa naangalia box ambalo wamekomaa nawaondoa na kuwaweka wapya

3. Wakati wa joto siweki chohote, wakati huu wa baridi huwa nawawekea hiyo mitungi
ambayo nimeiweka kwenye picha huku tunanunua kwa 3000 mpaka 5000. Kunambinu nili
fundishwa ya kuufanya mkaa udumu muda mrefu bila kuzimika au kuisha, huwa njaza unga
unga au chenga za mkaa hapo juu, pia huwa naloweka jivu na kuliweka (Uliza kwa wauza kahawa
watakuelekeza vizuri zaidi)

4.Huwa nawakadiria tu, wakimaliza nawaongezea tena. Machicha ya nazi, pumba za mahindi
' Pumba za dagaa n.k isipokuwa siku 3 za mwanzo naweza kuwapa kile kilichochanganywa kwa
ajili ya vifaranga, maa nyingi nanunua kwenye maduka ya kilimo.
Asantee sana kwa majibu yako yaliyoshiba na kujitosheleza...kwa kweli umenipa elimu kubwa sana sana,Mungu akubariki mno...
 
Hao vipanga kuwazuia ni rahisi mno. Tengeneza fensi na uweke wavu wenye matundu madogo kama tunazoweka madirishani na juu pia uweke hizo wavu, umemaliza.
 
Ni hivi Kuku wa Kienyeji wanapenda Kujiachia Tengeneza Vidude Vya Kutagia juu. Kuku wakishatotoa wakae na Watoto Wiki Moja Nenda kwa wauza Dawa za Mifugo mwambie akupe Dawa ya Makoti na Baadhi ya Dawa za Vitamin

Baada ya Hapo wale Watoto wanatunzwa Tofauti wakuu hasa Ujiku inatakiwa wakae kwenye Joto sasa kuna Mawili Unaweza ukawasha jiko la mkaa Usiku na Asubuhi au Ukafunga Bulb zenye Joto hadi wapate Mikia tetea huwa wana mikia mirefu vijogoo vina mikia mifupi utaviona tuu na vichwa Huwa vikubwa vikipata mikia Hapo Uwezekano wa Kupona Vyote upo

Chakula Please Usiwalishe Pumba Mwanzo Mwisho na hizo Dawa watakua wanakunywa kila baada ya siku tatu Isikae masaa 24 huwa ni Sumu ikae Masaa 8 tuu then Unabadilisha

Walishe
-Pumba
-Mboga za Majani Fungu hata Moja la Chinese

Sasa baada ya Kuwapa hivyo vyakula Mimi kimsingi huwa nafurahia wanavyokula vikishashiba Unaweza Ukawapa Chenga za Dagaa ndo uwape Maji au Ukawapa Maji ndo ukawapa Dagaa.

Kuna Siri Moja Dagaa hata kama kinaumwa kitakula tuu ni chakula ambacho Watoto wanakipenda sana na wanakua haraka ukiwapa Dagaa

Mara Moja Moja vipe Mchele pia vinaupenda Mahindi hawawezi Kumeza

Ukizingati ndani ya mwezi vinakua Vikubwa tayari kwa kutoka Nje

Hakikisha Banda lako Unasehemu za Kuwatenga kutokana na Umri si vizuri Kuku wadogo unaenda kuwachanganya na Waliozeeka kuna baadhi ya Jogoo huwa wanawaua Watoto.

Hakikisha Vyombo vya Maji Unavisuuza na wakiwa watoto usiwape Pumba uliyoloweka kwenye maji, pia Wakishakunywa Maji toa Yale Maji At least wapewe Mara 3 kwa Siku lakini kama uko Busy Maji yasikua na Dawa wanaweza Kushinda Nayo

Mkuu ukizingatia hayo kama Una matetea 15 wakitaga wote Nategemea Utawaponesha Kuku 160. Pia control Kwenye kuatamia at least atamie Mayai 13 hadi kwenye 10 pia uwe Mjanja kuchagua koo za Kuku kuna wengine wanataga sana wengine wao kufikisha Mayai 12 issue kuna wengine wanatotoa sana kuna mwingine akiatamia Mayai 14 anatotoa Watoto 2 Kuku hawa ni stress na Ukishaona Hivyo subiri anenepe tuu Umle Kuku wa aina hii Mara Nyingi Ni wale uliowanunua wakiwa wakubwa na Unajua mbongo anauza Kitu Kikiwa kina matatizo.
Ahsante kwa maelezo mazuri mkuu...
Mimi nina kamtaji ka 2.2m, je katatosha kuanza ufugaji wenye tija mkuu.
Pia naomba kujua ni kipi bora kati ya kufuga kuku wa kienyeji na wale matahira(wa kisasa)?
Note: nahita kufuga kwaajili ya biashara na sio kitoweo tu.
 
Ahsante kwa maelezo mazuri mkuu...
Mimi nina kamtaji ka 2.2m, je katatosha kuanza ufugaji wenye tija mkuu.
Pia naomba kujua ni kipi bora kati ya kufuga kuku wa kienyeji na wale matahira(wa kisasa)?
Note: nahita kufuga kwaajili ya biashara na sio kitoweo tu.
Uko wapi? Unafanya Nini? Nataka nijue mwingine yupo kwenye Nyumba za Kupanga anataka Kufuga Kuku
 
Nipo Dar mkuu....
Na nipo kwenye nyumba ya kupanga,
Kama Dar Hakuna Ulazima wa Kukaa nakushauri hii Shughuli itapendeza zaidi Mikoani na 2.2M ni Kiasi Kikubwa sana Kama haujaoa hauna Kazi yeyote unaweza ukaachana na Dar na Kwenda hata hapo Mkurunga Utafanikiwa.
 
Tafuta sehem ujenge banda kubwa tu na lakutosha watazurura humo ndani kwa usalama
 
Kama Dar Hakuna Ulazima wa Kukaa nakushauri hii Shughuli itapendeza zaidi Mikoani na 2.2M ni Kiasi Kikubwa sana Kama haujaoa hauna Kazi yeyote unaweza ukaachana na Dar na Kwenda hata hapo Mkurunga Utafanikiwa.
Nashukuru kwa ushauri mkuu... Kwa sasa kuondoka Dar haitakuwa rshisi maana kuna sehemu bado fanya kazi japo kipato sio kikubwa sana lakini nashukuru kimeniwezesha kuweka akiba ya hicho kiasi mkuu... Pia nimeoa mkuu........!!
Pengine itapendeza ukiendelea kinipa mawazo mkuu hata ambayo ni tofauti na ufugaji maana naona option hii inanilazimu kuwa kijijini.
Nawasilisha mkuu
 
1.Vifaranga vya kuku bei gani,,
Jibu:
Umri Bei (Tsh)
Siku 1 2,000/=
Wiki 2 3,000/=
Mwezi 1 3,500/=

2.ni vya umri gani
Jibu:
Kulingana na uhitaji wa mhusika tunaanza kuuza kuanzia wa siku moja na kuendelea

3.mnaanza kumplkea mtu kwake akichukua idadi kuanzia vingap
Jibu:
Order yeyote hata 1,000pcs tunapokea

4.je kuna ushauri wowote mnatoa kwa mtu hasa anaeanza ufugaji mara ya kwanza namn ya kufuga

Jibu:
Ndio tunatoa ushauri kabisa

5.Pia chanjo za mwanzoni mnazo hapo kwenu au mpka mtu aende duka la madawa ya mifugo kupata hizo chanjo,,,,asante…!!

Jibu:
Chanjo zote zinazotakiwa kabla hujawachukua tunakuwa tumewapa.


1
 
Back
Top Bottom