Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ni check Kwa vitabu vya ufugaji wa kuku wa kisasa na kienyeji
 
Karibu Kwa vitabu vya ufugaji wa kuku wa kisasa na kienyeji
 
Nauza kuku wa kienyeji majogoo 20000 makubwa na majike kuanzia 12000 na mayai yao trei moja ni 15000
 
salaam greathinkers!

sasa nimeamua kuacha woga, na nataka kuanza kufuga kuku wa kienyeji rasmi. Kwa sasa najenga banda litakamilika next saturday (26/4), kwa kuanzia banda langu lina ukubwa wa mita 25 kwa 11.

Je kwa ukubwa huo naweza kufuga mpaka kuku wangapi wa kienyeji?
 
Kitabu bora cha ufugaji wa kuku wa kienyeji kinapatikana kwangu 0758303090
 

Tupo pamoja sana mkuu

Nafikiria kuanza kufuga kuku wa kienyeji kwa large scale pale Rufiji huku niki-intergrate na ufugaji samaki japo bado nakusanya ushauri wa ufugaji wa samaki , maana seems utaalamu wa tilapia aquaculture kwa hapa Bongo bado ni kidogo na watu wanafuga kimazoea sana.

Vipi mkuu kulikoni kukimbia kuku wa kienyeji na kuhamia kwenye chotara??

Mie wa kienyeji siwaachi maana ni wavumilivu mno na watanifaa sana kama nitafanikiwa kuwaunganisha na mabwawa ya samaki
 
Mm naomba ushauri ,nimenunua kuku wa mayai 26 size ya miezi mitatu cha kushangaza nimewaweka ktk chumba ambacho muna godoro ukutani leo nimeamka wamelitoboatoboa wanakula je hakuna madhara yeyote?

Mkuu hao kuku unawalisha chakula cha kutengeneza mwenyewe au ni cha kununua??

Kama ni cha kutengeneza hakikicha unaweka na madini ya chokaa ya wanyama(ni tofauti na chokaa ya kupaka nyumba), ukienda duka lolote la mifugo watakupa hii kitu.

Kama ukishidwa kabisa , wachanganyie majani ya mlongelonge yaliyokaushwa bila kuanikwa juani i.e yaliyokaushwa kivulini, tatizo lako litaisha kabisa
 
Mkuu kuku wako anavimba usoni kwa kukosa madini ya vitamini A. Tiba ya dharura ni kuwapaka mafuta ya alizeti kama ilivyokwishaelezwa humu, lakini kwa long run solution tafuta vyakula vyenye wingi wa madini ya vitamini A ambavyo vingi ni majani jamii ya mikunde kunde, au majani laini mapana yanayopendwa na kuku. Lakini pia kama unapata muda tafuta majani ya mlonge longe uwachanganyie kwenye chakula chao ni tiba murua sana, utasahau hili tatizo forever
 
mradi wa ufugaji kuku ni mzuri nina kuku wa kienyeji 11 ambao nafuga tu kwa ajili ya kula nyama ila nimevutiwa kuwafuga kibiashara baada ya kusoma uzi huu hata ivyo changamoto kubwa kuliko zote ni wizi juzi jirani yangu kaibiwa kuku 61.
 
Hivi mkuu wale wadudu wanaokula mayai mfano .vicheche au kenge dawa yao ni nini maana wamenitia hasara sana mayai km ishirini waliyala yote karibu wiki waweze kuangua iliniuma sana
 
MI nimeanza na kuku 11 jike 10 dume moja mwezi sasa umeisha,
wamekufa wawili kwa ugojwa na mmoja kaliwa na mbwa.
wamebaki 8 mmoja tu ndio anataga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…