Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Mimi kuna vifaranga vinajaa maji kichwani na kufa
 
Mimi kuna vifaranga vinajaa maji kichwani na kufa

Kuna jamaa atakupa ushauri. Ila nahisi wanakula sijui mavi au labda maji machafu! Mie banda langu dairy nasafisha mkali balaa! Bora room kwangu kusipigwe deki lakini bandani naua mtu! Naingia humo bandani mara 20 kwa siku nawapenda sana kuku wangu! Leo nilienda kupata supu nikabeba mabaki nikanunua na dagaa za buku mbili aisee hadi raha wananipandia hadi kichwani! Nawapenda sana!
 

Nina vifaranga wawili wa mwezi mmoja wa kienyeji naanza kuwafuga,nimewapa kabichi na matembele waliishia kuangalia tu ila nilipowapa mchicha aisee waliugombania kama hawana akili nzuri,niliwapa machicha ya nazi ambayo yamekamuliwa tui kuna akanitisha eti itawasababishia kifua,je? Kuna ukweli wowote.
Nalog off
 
Pamoja kaka! Tujitume man! Nina target ya kuku 200 by Xmas this year! Mungu atanisaidia

huwa nacheka sana mambo yako ila nimefurahi kuwaona kuku wako poa. Ukiamini utafika hadi elfu moja na zaidi. Pambana
 
Mimi kuna vifaranga vinajaa maji kichwani na kufa

Inawezekana ni ugonjwa uitwao fowl coryza.

Dalili moja wapo macho kuvimba na ukijaribu kuyafikicha kuna kitu cheupe kilichoganda kitatoka

Ikiwa ni hivyo basi hakikisha unawatenga wale wanao umwa kisha vaa gloves mikononi mwako kisha fikicha taratibu jicho moja baada ya jingine (ikiwa yote yamevimba)
Kisha futa na pamba na umuwekee dawa iitwayo O.T.C EYE/WOUND POWDER hii ni antibiotic ya unga kwa ajili ya wanyama ama kama sio waweza wapatia OXYTETRACYICLINE 20% kwenye maji wakanywa kwa siku 5
 

Ee bhana ee, hilo ni banda la kukuzia vifaranga teknolojia niliyoicopy na kuipaste home kutoka maonyesho ya nanenane.
Kama inavyoonekana banda lina sehemu 2. Upande wa kulia ni banda la mduara lililosanifiwa mahsusi kwa ajili ya vifaranga kulala. Kwa nje kama linavyoonekana limezungushiwa sheet za ceiling boards na kufunikwa juu yake kwa material yaleyale. Kwa ndani limewekwa pumba za mpunga kuzunguka mzingo wote pamoja na kifuniko chake. Ilielezwa muundo huu unasaidia kuhifadhi joto linalohitajika kwa ajili ya vifaranga hivyo kuviepusha na baridi na ni mbadala wa joto ambalo vingepata kutokana na kulaliwa na mama yao.
Upande wa kushoto ni sehemu ya chakula na kunywa. Haina usipesheli wowote mwingine zaidi ya kuwa na uzio huo kuzuia vifaranga hivyo kutoroka.
Sehemu hizo mbili zinaunganishwa na mlango mdogo tu kwa ajili ya kuruhusu vifaranga kuingia na kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Ilielezwa kuwa banda hili linaweza kutumika kuhifadhi vifaranga vya umri wa kuanzia siku 2 na kuendelea.
Bhana ee, nilicopy nikapaste na ndo hilo mnaloliona.
Heheee, kwani limefunction!! Kila kifaranga tuliyeweka humo hajakatiza. Limeua vifaranga wa home na wengine nilionunuanunua hapa kijijini zaidi ya 30.
Ama basi kuna step nakosea? But I bet I did it right, but why then?
Kama kuna watalaam walokuwa wakinadi teknolojia hii waseme walifake au nini, maana hii sasa hasara tupu jamani!!!
 
Mshawa
Nimekuelewa na nitafata ushauri wako pia asante sana
 
Last edited by a moderator:
aah hiyo sijawai sikia, me nawapaga machicha wanayala sana tu sijawai ona wakiumwa kifua,
unaishi wapi ww mkuu, ninahitaji kuku wa israel.
 

Ushaangalia prison break? Waweke uone dehydration hata ww humalizi siku moja humo ukiwa hai
 
Nahisi kitendo cha kuwafunika kimekupa matokeo hayo'vifaranga wanahitaji hewa safi pia najoto likizidi ni hatari pia.
 
Jela imefanya kazi nduguzangu! Nimemtoa kuku wangu sasa hivi naona hana dili kabisa na vifaranga! Hadi raha
 
Ushaangalia prison break? Waweke uone dehydration hata ww humalizi siku moja humo ukiwa hai

Dah!! ndg yangu yaani majanga. Sasa hawa watalaam walikuwa wananadi upuuzi au nao hata hawajawahi kufanya. Halmashauri zetu kweli zina mazezeta tu. Najuta kwa kweli...
 
Nahisi kitendo cha kuwafunika kimekupa matokeo hayo'vifaranga wanahitaji hewa safi pia najoto likizidi ni hatari pia.
Kwa hiyo hii teknolojia ni fake? Mkuu kama ulibahatika kuhuzuria maonyesho ya nanenane nadhani uliona baadhi ya mabanda ya halmashauri mbalimbali yalikuwa yanatoa elimu kuhusu teknolojia hii.
 
Habarini wadau

Mimi nimejenga nyumba ya kawaida kwny eneo la 20x20,na hapohapo nimeanza kufuga kuku 8,matetea sita,kiwango cha juu kwa eneo langu km nikifuga huria ni kuku wangapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…