Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Kupitia maswali na majibu ya uzi huu nimejitengenezea Kijarida kidogo ambacho kitakuwa very useful especially kwenye changamoto za Ufugaji wa Kuku ...Ahsanteni sana Wadau kwa spirit hii ya Mafanikio ya Pamoja...Mungu aendelee kuwabariki kadri ya kujitoa kwenu..
 
  • Thanks
Reactions: Qj_
Wakuu, nimeanza tena ufugaji wa kuku wa kienyeji. Mara hii natumia mfumo
wa NUSU HURIA nimeanza na kuku 15 mwaka Jana mpaka sasa wako 369
Nimeuza kuku 271 kwa bei za kati ya Tsh 17,000 mpaka 23,000 namshukuru
Mungu nimeweza kupunguza ukata.

Mwakahuu kuna ttizo kubwa limejitokeza nashindwa jinsi ya kulikabili, Kuna ndege
Mdogo kwa umbo anafanana sana na njiwa, anakamata vifaranga balaa. Tena
anakamata wale vifaranga wakubwa ambao wanajitegemea. Ndani ya wiki mbili
hizi amekamata vifaranga 18.

Sijajua jinsi ya kumdhibiti yaani huyu mshenzi ananipa hasira si mchezo.
Huyo anaitwa kipanga mkuu,tafuta nyavu umtegeee lazima anase.
 
Habari wanajamii forums,mimi nimgeni humu natokea Geita. Wanajamii naomba kufahamu changamoto katika, ufugaji wa kuku wa kienyeji,na je, ni ufugaji unaofaa kibiashara?Naombeni ushauri kidogo watanzania wenzangu.
 
Changamoto katika biashara yoyote ipo...
Kwa case yako ni magonjwa, Masoko, usimamizi wake n.k

Hiyo biashara ukiisimamia vizuri inalipa..Kila la heri mkuu
 
"Uandaaji wa chakula cha mifugo kwa njia ya hydroponics fodder",kuna mtu anaandaa hii kwa malisho ya kuku?kama yupo naomba atupatie uzoefu.
 
Naomba kufahamishwa kuhusu tabia hii ya kuku wa kienyeji
Nina kuku wangu wa kienyeji pure ametaga kafikisha mayai 10 na ndio mtago wake wa kwanza lakin ameanza tabia ambayo sijaielewa ikifika jion anaenda kwenye kiota chake cha mayai analalia ikifika asubui wakati nafungua banda anatoka na harud tena kulalia mpaka ikifika jion muda wa kuingia bandani na leo ni siku ya pili kafanya hivyo :
1.sasa nilitaka kujua ndio inavyokuwa kwa kuku anaeanza kulalia/kuatamia kufanya hivi kwa siku za kwanza au sio mlaliaji mzuri
2.je mayai yatakua salama kwa style hii aliyoifanya kulalia usiku tu kwa siku mbili
3.je nifanye nini kuyaokoa mayai yasiharibike kama itakua bado hayajaharibika?
 
kuku wa kienyeji ... da nilidhani kuku wa kienyeji ninayemjua mimi....
 
Naomba kufahamishwa kuhusu tabia hii ya kuku wa kienyeji
Nina kuku wangu wa kienyeji pure ametaga kafikisha mayai 10 na ndio mtago wake wa kwanza lakin ameanza tabia ambayo sijaielewa ikifika jion anaenda kwenye kiota chake cha mayai analalia ikifika asubui wakati nafungua banda anatoka na harud tena kulalia mpaka ikifika jion muda wa kuingia bandani na leo ni siku ya pili kafanya hivyo :
1.sasa nilitaka kujua ndio inavyokuwa kwa kuku anaeanza kulalia/kuatamia kufanya hivi kwa siku za kwanza au sio mlaliaji mzuri
2.je mayai yatakua salama kwa style hii aliyoifanya kulalia usiku tu kwa siku mbili
3.je nifanye nini kuyaokoa mayai yasiharibike kama itakua bado hayajaharibika?
SIYO KAWAIDA MTENGE NAYO UYAKAGUE VINGINEVYO YATAHARIBIKA
 
Naomba kufahamishwa kuhusu tabia hii ya kuku wa kienyeji
Nina kuku wangu wa kienyeji pure ametaga kafikisha mayai 10 na ndio mtago wake wa kwanza lakin ameanza tabia ambayo sijaielewa ikifika jion anaenda kwenye kiota chake cha mayai analalia ikifika asubui wakati nafungua banda anatoka na harud tena kulalia mpaka ikifika jion muda wa kuingia bandani na leo ni siku ya pili kafanya hivyo :
1.sasa nilitaka kujua ndio inavyokuwa kwa kuku anaeanza kulalia/kuatamia kufanya hivi kwa siku za kwanza au sio mlaliaji mzuri
2.je mayai yatakua salama kwa style hii aliyoifanya kulalia usiku tu kwa siku mbili
3.je nifanye nini kuyaokoa mayai yasiharibike kama itakua bado hayajaharibika?
Kuku wanatofautiana mkuu, ndomana kabla ya kutaka kufuga kuku unashauliwa kutafuta breed yenye sifa nzuri ya kuweza kulalia, hivo huyo wako hana sifa hiyo na ni vigumu kumbadili, labda endapo utaamua kutengenezea banda na kutoruhusu atoke nje na chakula uwe unampa wewe na sio kujitaftia

Issue ya mayai, ni kweli akiendelea hivo mayai yataharibika, sasa ili kuyanusuru inabidi uyapeleke kwenye mashine ya kutotoresha
 
anajiandaa kulalia huyo,toa mayai muachie matatu mpaka atakapochanganya kulalia,pia muandalie sehemu nyingine nzuri ya kulala,kuku hata asiyetaga anapenda kulala kwenye kiota kizuri
 
Kama humpi chakula unategemea nini mkuu? Lazima akatafute msosi ashibe kwanza
 
Kuku wanatofautiana mkuu, ndomana kabla ya kutaka kufuga kuku unashauliwa kutafuta breed yenye sifa nzuri ya kuweza kulalia, hivo huyo wako hana sifa hiyo na ni vigumu kumbadili, labda endapo utaamua kutengenezea banda na kutoruhusu atoke nje na chakula uwe unampa wewe na sio kujitaftia

Issue ya mayai, ni kweli akiendelea hivo mayai yataharibika, sasa ili kuyanusuru inabidi uyapeleke kwenye mashine ya kutotoresha

Unataka kuniambia hiz siku mbili alizolalia usiku tu mayai yatafaa kwenda kwenye incubator na vifaranga nikapata?
 
Back
Top Bottom