Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Kaka asante sana kwa elimu nzuri natumaini utakua umetusaidia wadau wengi tu wenye ndoto kama zako.....hamna kitu kizuri kama kufanya ujasiriamali kwa kujifunza kutokea kwa waliokutangulia.
 
hii habari ya chakula inabidi kuifanyia kazi hii hebu Kubota atwambie kama aliweka kila kitu kinachohitajika na kwa uwiano halisi? mimi naona tukikwamuka hapa kwenye chakula itakuwa mteremko sana maana mfuko wa chakula unafika hadi 45000 kipindi sasa vifaranga vikiwa vingi itakuwaje?

Umesema kweli kabisa kwamba kumudu kujitengenezea chakula hasa hiki cha vifaranga ni ukombozi mkubwa! Wajuzi wanasema katika gharama za uzalishaji wa kuku 70% ni chakula! Niliweka ingredients zote muhimu! Mimi nimeafikiana na ushauri wako tuendelee kufanya ubunifu na utundu hadi tuweze! Na kama kuna alieweza atatuongoza! Kwa maneno yako Mama Joe nitarudi tena kambini kwa nguvu zaidi nijaribu tena kutengeneza na kuchanganya kichinachina!
 
Mama Joe kwenye chakula na hicho kipindi cha mwezi mmoja wa kwanza kweli kuna changamoto.na nahisi tatizo sio kuweka kila kitu na kwa ratio inatakiwa.Inawezekana matatizo yakawa mawili makubwa.mosi, ni size ya punje za mahindi, dagaa na pumba.katika hali ya uchanganyaji wa mikono ni ngumu hivi vitu kusagika na kuwa katika punje ndogondogo kwa kifaranga wa siku moja hadi wiki tatu kuweza kula.mara nyingi inatokea punje za mahindi ni kubwa hata kama zimeparazwa.Tatizo la pili nahisi ni uchanganyaji wenyewe mana kwa kuchanganya na mikono ili vichanganyio vyote vichanganyike vizuri nayo sio rahisi sana hata kwa kuchanganya kilo 50 tu.Kwa mtazamo wangu nahisi hivyo ndo vinavyochangia.Asante.

Asante sana Mkuu Dafo yaani ulivyoandika ni kama nilikushikia kalamu, na mimi nawaza hivyo hivyo, siongezi wala kupunguza hata nukta! Ukiona hivyo ujue hapa kunatatizo! Sasa tutaepukaje hiyo 45,000 kwa mfuko wa chakula cha vifaranga? Hiyo ni changamoto!
 
Katika Utengenezaji wa Chakula cha Kuku, Kwenye vifaranga wa One day old, huwa inashauriwa kutumia Unga wa Dona ambao tiyali umesgwa ndo utumike badala ya Pumba,au mahindi, so kwenye kuchanganya unashauriwa kutumia unga wa Dona, Ila hakikisha mahindi hayana Dawa make unaweza ua vifaranga,

Ukiachiulia mabali formula ya ratio ya kila kimoja, kwenye ku changanya napo kuna Formula ya Kuchanganya si kuchanganya tu ilimuradi unachanganya, Kuna makundi unatakiwa kugawa vyakula katika makundi kama mawili hivi na kila kundi lina changanywa kivyake na mwisho unacompail pamoja hayo makundi mawili

Ushauri mzuri sana.mdogo mdogo ndio mwendo.Tutafika tu.Kubota endelea basi kutupa shule.
 
Mkuu kuna Ile Manula ya RLDC kama sijakosea speling, wana manual nzuri sana ya jinsi ya kutengeneza chakula cha kuku, niliipenda sana Manual yao, na kuna moja wa Kenya nao walikuwa na ya maelezo ya kila chakula na altenative yake, ukisoa Damu utumie nini, ukikosa hiki utumie nini,

Asante mkuu kwa maelezo yako...ningependa kama ungeweza kutwekea hiyo manul ingekuwa vizuri sana.na pia kwenye damu kwa sasa naona baadhi ya wataalaamu wanashauri damu isitumike baada ya kutokuwa na uamnifu kwa wauzaji kutoka machinjioni wamekuwa wakiweka kinyesi ili kuongeza uzito.ambayo ni inaweza pelekea maambukizi kwa kuku.
 
Jamani shule nzuri sana asanteni wadau wote kwa micahngo mizuri sana, ngoja niwahi kuku wangu.
Hizo doc Chasha anazosema nawawekea hapa,
weekend njema

Mhh! Wakuu Mama Joe na Chasha huu ukarimu wa kudumbukiza hizi documents hapa you make me crazy!! Mungu awabariki kwa ukarimu huu ambao mitaani ni adimu isipokuwa JF pekee!
 
Chasha; Hebu tuwekee mawasiliano ya hawa jamaa hapa tafadhali!


Mkuu kuna Ile Manula ya RLDC kama sijakosea speling, wana manual nzuri sana ya jinsi ya kutengeneza chakula cha kuku, niliipenda sana Manual yao, na kuna moja wa Kenya nao walikuwa na ya maelezo ya kila chakula na altenative yake, ukisoa Damu utumie nini, ukikosa hiki utumie nini,
 
Last edited by a moderator:
Chasha; Hebu tuwekee mawasiliano ya hawa jamaa hapa tafadhali!

Wapi hao wa RLDC au jamaa wa Mashine ya Kuchanganya chakula Cha kuku? Hawa wa RLDC wako Dom na wanaproject za kuku huko Singida, zinazo fadhiliwa na wathungu,
Ila wa Mashine ya Chakula cha kuku yuko A town, nita wekana namba yake baada ya kuwasiliana naye, make si kila mtu anapenda namba yake kuwa open si unajua, ila kwa PM utapata
 
Kubota; Mama Joe;

Msisite kutujuza hata kwa vifaranga wenye kutotolewa na mpaka miezi miwili dawa stahiki ni ipi?

Na hata dawa nzuri kwa hawa kuku wakubwa hasa kuhusu dawa ya minyoo kuku kuhara njano na hata nyeupe ni nini haswa chanzo ya hilo? Kubota; pitia kipande hii!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kubota nakusubiri kwa hamu kwenye magonjwa, kwakweli shule hii ni kiboko. Nimiekuwa nikifuga kwa sasa ni miezi mitatu. Tatizo ni vifaranga nimekuwa nikiwalisha starter toka kutotolewa mpaka week ya tano. niliwachanja chanjo ya jicho. wakakua vizuri mpaka wakaanza kuota manyoya. week ya tano nikaanza kuwatoa nje, mara nikaona kama watatu hivi ghafla wakaanza kuvaa makoti. kwanini wakati nimewachanja na wataalamu waliniambia nikiwachanja chanjo ya jicho hawatapata huo ugonjwa. nimechanganyikiwa maana nategemea kupata vifaranga wasiopungua arobaini maana kuna kuku wanne wanaatamia mayai 15 kila mmoja.
 
Last edited by a moderator:
guta;
Hapo kwenye red nakwambia mwaka jana niliwapoteza vifaranga kama 120 hivi na hapo Mi nasema wamevaa SUTI! Kha ha ha ha ha ha ha ha haaaaa!

Mkuu Kubota nakusubiri kwa hamu kwenye magonjwa, kwakweli shule hii ni kiboko. Nimiekuwa nikifuga kwa sasa ni miezi mitatu. Tatizo ni vifaranga nimekuwa nikiwalisha starter toka kutotolewa mpaka week ya tano. niliwachanja chanjo ya jicho. wakakua vizuri mpaka wakaanza kuota manyoya. week ya tano nikaanza kuwatoa nje, mara nikaona kama
watatu hivi ghafla wakaanza kuvaa makoti.
kwanini wakati nimewachanja na wataalamu waliniambia nikiwachanja chanjo ya jicho hawatapata huo ugonjwa. nimechanganyikiwa maana nategemea kupata vifaranga wasiopungua arobaini maana kuna kuku wanne wanaatamia mayai 15 kila mmoja.


Kubota; Usitusahau hata kwa post hii!

Hakuna kulala mpaka kieleweke!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom