Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Namshukuru Mungu na ushauri wenu ni kweli tukikazana tutaweza tu, changamoto kubwa ni magonjwa ya ghafla kutokea ila nashukuru yaani kila likija hili unakuta mwingine hapa kesha leta na ufumbuzi umejadiliiwa yaani imenisaidia sana sikuwa na Dr yoyote wa mifugo zaidi ya kupata ushauri hapa, kwa RETI na kwenye phamarcy. Sikutaka kuchukua mkopo nilitaka niende taratibu kwa kujibana tu na kupunguza matumizi yasiyo lazima. Naomba nikutie moyo mama Timmy kuku chotara hawana tofauti na hawa kienyeji kwa kulisha na dawa, mimi nimefuga wale wa kisasa ndio nimehamia kwa hawa, ukuaji wa hawa chotara ni wa haraka wakati hawahitaji gharama kubwa kihivyo maana hawali chakula kingi kama wakisasa wala hawahitaji vitamin isipokuwa wiki chache 2 za mwanzo. Kwavile wanakua haraka tayari wakifika kiezi 5 tu unauza kwa 10000 lakini ukiwaacha hadi miezi 8 jogoo ni wakubwa sana na wanauzwa 15000 -20000. Unakuwa huna pressure ya kukubali bei ndogo maana hawali chakula kingi. Faida ya pili wanataga mapema kuliko wa kienyeji hivyo wanaanza kujilisha wenyewe wakiwa na miezi 6 kuendelea na vilevile waweza kuwatumia mayai yao kutotoa vifaranga aidha kwa kuwatumia tetea wa kienyeji pure au incubator na hivyo kutokuwa na haja ya kununua tena vifaranga wengine. Nitajaribu kuweka mchanganuo wa gharama na faida ingawa nikiangalia sio tofauti na iliyowekwa na RETI hapahapa. Lengo langu ni kuongeza aina nyingine ya kuku chotara ili kuwa na aina tofautitofauti, kuanza kutengeneza chakula changu mwenyewe kupitia formula nilipewa na ex SUA lecture na Dr mifugo sasaivi yuko wizarani yeye na mkewe wameitumia na waliniambia inafaa sana ingawa itabidi nipate ushauri wa mwenye mashine kiwango cha usagaji na uchanganyaji wa chakula nitaleta feedback hapa. Nawashukuru wote kwa michango yenu Mungu azidi kuwafanikisha zaidi ktk malengo yenu.
Mama Joe kusema kweli umenitia moyo sana kwa kuweka wazi uzoefu wako khs hawa kuku chotara, nimesoma comments zako zote nimefarijika sana, hata nashindwa niseme nini tu kuelezea furaha yangu!

Naomba kujua namna ya kuwapata na bei zake, manake nataka nianze kuwafuga mwezi ujao kuanzia tar 20 hivi, uzuri banda ninalo so ni kiasi cha kulifanyia usafi tu na kuandaa pesa kwaajili ya kuwanunua. Nalenga kuwafuga kwa ajili ya mayai so nitahitaji majike.
 
Last edited by a moderator:
Asante kama umefaidika na michango yangu. Mimi nilinunua kwa RETI vifaranga. Kuna wengine pia wanatangaza hapa. Pia kuna Bena chicks (website) rafiki yangu alichukua ni wazuri. Kawaida vifaranga robo tatu ni majike. Ukitaka kuchukua majike tu basi chukua wenye umri mkubwa kidogo ili uweze kutofautisha. Karibu tufuge.
Mama Joe kusema kweli umenitia moyo sana kwa kuweka wazi uzoefu wako khs hawa kuku chotara, nimesoma comments zako zote nimefarijika sana, hata nashindwa niseme nini tu kuelezea furaha yangu!

Naomba kujua namna ya kuwapata na bei zake, manake nataka nianze kuwafuga mwezi ujao kuanzia tar 20 hivi, uzuri banda ninalo so ni kiasi cha kulifanyia usafi tu na kuandaa pesa kwaajili ya kuwanunua. Nalenga kuwafuga kwa ajili ya mayai so nitahitaji majike.
 
Last edited by a moderator:
Asante kama umefaidika na michango yangu. Mimi nilinunua kwa RETI vifaranga. Kuna wengine pia wanatangaza hapa. Pia kuna Bena chicks (website) rafiki yangu alichukua ni wazuri. Kawaida vifaranga robo tatu ni majike. Ukitaka kuchukua majike tu basi chukua wenye umri mkubwa kidogo ili uweze kutofautisha. Karibu tufuge.

Nashukuru wana Mama Joe nimetembelea website yao, ngoja nianze kuwasiliana nao sasa

Halafu naomba kujua kwa uzoefu wako hawa kuku chotara wanalipa zaidi ukiwafuga kwa kulenga mayai au kwa kulenga nyama?
 
Mimi naona kwa nyama zaidi. Kwani kwa gharama niliyotumia ningeamua kuuza wote ni faida zaidi ningerudi kuchukua tena vifaranga. Nimeona wengi wanafanya hivyo hadi kuku 600. Lakini pia mayai yao yana soko zuri ingawa kama wa kienyeji kuna kipindi wanasimama kidogo halafu watarudi kutaga then utawauza nao pia.
Nashukuru wana Mama Joe nimetembelea website yao, ngoja nianze kuwasiliana nao sasa

Halafu naomba kujua kwa uzoefu wako hawa kuku chotara wanalipa zaidi ukiwafuga kwa kulenga mayai au kwa kulenga nyama?
 
Mimi naona kwa nyama zaidi. Kwani kwa gharama niliyotumia ningeamua kuuza wote ni faida zaidi ningerudi kuchukua tena vifaranga. Nimeona wengi wanafanya hivyo hadi kuku 600. Lakini pia mayai yao yana soko zuri ingawa kama wa kienyeji kuna kipindi wanasimama kidogo halafu watarudi kutaga then utawauza nao pia.

Nashukuru kwa kuzidi kunipa mwanga zaidi. Kwahiyo hata kama nitaamua kuchukua majogoo tupu ni poa tu? nikiwa namaanisha niwafuge kwa ajili ya nyama tu.
 
Nashukuru kwa kuzidi kunipa mwanga zaidi. Kwahiyo hata kama nitaamua kuchukua majogoo tupu ni poa tu? nikiwa namaanisha niwafuge kwa ajili ya nyama tu.
Mkuu Mito wakati tunasubiri response ya Mzoefu, Mkuu Mama Joe nachomekea hapa kwamba kama umevutiwa kufuga majogoo ili uuze wa nyama changanya na majike kidogo ili ujionee yatokanayo.
 
Mkuu Mito wakati tunasubiri response ya Mzoefu, Mkuu Mama Joe nachomekea hapa kwamba kama umevutiwa kufuga majogoo ili uuze wa nyama changanya na majike kidogo ili ujionee yatokanayo.

nashukuru kwa ushauri Kubota
au vipi kwa mfugo wa kwanza nituchukue batch moja ya kawaida tu (bila kuchagua) ambayo kwa mujibu wa Mama Joe itakuwa vifaranga robo tatu ni majike. Then nikishajionea yatokanayo ndo niwe selective ambapo sasa nitaegemea aidha kwenye nyama, mayai au vyote kwa mpigo
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli hata kwa yote changanya tu kwasababu hata kwa umbo matetea wiki ya sita wanakuwa wakubwa sana ila majogoo watakuja ongezeka miezi inayofata. Hivyo hata matetea kuwauza mmiezi sita poa. Changanya uone mwenyewe kipi faida zaidi kwako.
Mkuu Mito wakati tunasubiri response ya Mzoefu, Mkuu Mama Joe nachomekea hapa kwamba kama umevutiwa kufuga majogoo ili uuze wa nyama changanya na majike kidogo ili ujionee yatokanayo.
 
Wakuu am going to start this soon. Sio mtaalamu Kabisa Ila najua nyie mpo hakuna kitakachoharibika. Chasha you know we meet Saturday for dorep hope kila kitu kitakwenda sawa!
 
Nashukuru sana mkubwa kwa elimu yako kwa sababu umenifumbua sana,so nitafanya kama hivyo soon as possible!
 
Mama Joe (na wengine wenye ufahamu) hivi hawa kuku chotara naweza kuwafuga huria kama wa kienyeji lakini nikawa nawapa supplimentary food mara moja moja? nafikiria kuwafugia kwenye plots (paddocks) zile alizowahi kuweka hapa mkuu Kubota
 
Last edited by a moderator:
Ndio ni vizuri zaidi, ndanoi ni hadi miezi 3 nadhani baada ya hapo ni nje kunawafaa zaidi ila uache milango wazi wakipenda kurudi ndani. Nilimkuta mdau alikuwa nao 600 aliniambia wakipenda usiku wanalala nje ila kutaga wanarudi ndani ila ana fence ya ukuta na mbwa na walikuwa wakubwa tayari.
Mama Joe (na wengine wenye ufahamu) hivi hawa kuku chotara naweza kuwafuga huria kama wa kienyeji lakini nikawa nawapa supplimentary food mara moja moja? nafikiria kuwafugia kwenye plots (paddocks) zile alizowahi kuweka hapa mkuu Kubota
 
Last edited by a moderator:
Ndio ni vizuri zaidi, ndanoi ni hadi miezi 3 nadhani baada ya hapo ni nje kunawafaa zaidi ila uache milango wazi wakipenda kurudi ndani. Nilimkuta mdau alikuwa nao 600 aliniambia wakipenda usiku wanalala nje ila kutaga wanarudi ndani ila ana fence ya ukuta na mbwa na walikuwa wakubwa tayari.

asante sana mama, umenifaa sana kwa kweli. Ila usinichoke kwa maswali yangu manake nitakuwa nakuuliza hapa hapa kila nikihitaji ufafanuzi wa kitu fulani. Ila dah, kuna wadau wako mbali sana, kuku 600!!!
 
Karibu ndugu mie nimejifunzia hapa mengi. Ni kweli 600 na aliuza wote nilipoenda baada ya mwezi nilikuta wameisha. Uzuri wa hawa huna pressure kama broiler maana huku unauza kuku huku unaokota mayai. Wateja wakiishakujua huna haja kuwafata.
asante sana mama, umenifaa sana kwa kweli. Ila usinichoke kwa maswali yangu manake nitakuwa nakuuliza hapa hapa kila nikihitaji ufafanuzi wa kitu fulani. Ila dah, kuna wadau wako mbali sana, kuku 600!!!
 
Nimeipenda sana hii

Wandugu wapenzi Nimeipenda sana hii. Mimi najifunza kufuga kuku wa kienyeji na Batamzinga. Mkuu hapa tutashukuru kama utatukatia ufugaji wa Batamzinga in deatail kama uivyotupa hii ya kuku wa kienyeji. Nina vifaranga 10 vya batamzinga vya umri wa mwezi mmoja hivi. Navifuga kama kuku wa kienyeji tu Je ni sahihi? Ni hasa chakula cha Batamzinga. Wako wanaoniambia kuwa ni Vitunguu maji tu! Nimejaribu kuwawekea hawali! Nifungue kitendawili hiki nataka na mimi siku moja NITOKE na Batamzinga! Tino Mzee wa Shamba
 
Back
Top Bottom