Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

wapendwa
wafugaji nisaidieni ushauri nimekwama.
ni njia ipi rahisi ya kusafirisha kuku, nawatoa rombo to dsm?

wako 18, wamewekwa kwenye tenga, naona watu wa mabasi ya abiria
wanasumbua sumbua.. je kuna alternative nyingine? Your advice plz! Mama Joe chasha Kubota Zogwale na wafugaji wengine
 
Last edited by a moderator:
VIFARANGA WA KIENYEJI WANAUZWA
VIFARANGA BORA WA KUKU WA KIENYEJI (ASILI NA MALAWI) WANAUZWA KWA BEI NAFUU KAMA IFUATAVYO
UMRI
BEI
SIKU MOJA
1,800/=
MWEZI MMOJA
2,500/=
MIEZI MIWILI
5,000/=
MIEZI MITATU
7,500/=
MIEZI MINNE
10,000/=

SIFA ZA VIFARANGA HAWA:

  1. WANATAGA MAYAI MENGI (WASTANI WA MAYAI 5 KWA WIKI)
  2. WANAUWEZO MKUBWA WA KUSTAHIMILI MAGONJWA
  3. WAMEPEWA CHANJO DHIDI YA MAREK’S DISEASE
  4. KUKU HAWA NI WAZITO NA WANAFAA KWA NYAMA NA MAYAI
  5. WANAKUA TAYARI KWA NYAMA NDANI YA MIEZI MINNE NA NUSU TU
  6. SOKO LA MAYAI NA NYAMA YA KUKU HAWA NI KUBWA
MTEJA ATAPATA USHAURI MUDA WOTE JINSI YA KUWALEA MPAKA WANATAGA

WASILIANA NASI KWA NJIA ZIFUATAZO:
EMAIL: irpoultry2014@gmail.com
PHONE: +255685637670
TANZANIA, IRINGA, MTWIVILA, KITUO CHA KWA MSHONA VIATU

Unasafirisha kwa qharama zako mikoa yote? Je unaweza kuweka picha tuone
 
wapendwa
wafugaji nisaidieni ushauri nimekwama.
ni njia ipi rahisi ya kusafirisha kuku, nawatoa rombo to dsm?

wako 18, wamewekwa kwenye tenga, naona watu wa mabasi ya abiria
wanasumbua sumbua.. je kuna alternative nyingine? Your advice plz! Mama Joe chasha Kubota Zogwale na wafugaji wengine
Pole sana binti mzuri neggirl. Nilikuwa busy kidogo sikuwa na muda wa kupitia notofications. Ila pia mimi nimfugaji wa kuku ila sijawahi kusafirisha toka mbali na tenga. Kuku wangu nilichukua kidogokidogo kwenye box kutoka kijijini na wengine nikanunua Dar wakazaliana na sasa wako kama 150 na zaidi kwa ajili ya kitoweo tu.
 
Last edited by a moderator:
Kwa wale wa Morogoro sasa najiandaa kuanza kuzalisha vifaranga wa kuku wa kienyeji...........nauza na mayai ya kienyeji pia
 
Pole sana binti mzuri
neggirl. Nilikuwa busy kidogo sikuwa na muda wa
kupitia notofications. Ila pia mimi nimfugaji wa kuku ila sijawahi
kusafirisha toka mbali na tenga. Kuku wangu nilichukua kidogokidogo
kwenye box kutoka kijijini na wengine nikanunua Dar wakazaliana na sasa
wako kama 150 na zaidi kwa ajili ya kitoweo tu.

asante Zogwale.
niliamua kuanzisha thread baada ya kuona nakawia hapa. But nashukuru nimepata mawazo ya watu tofauti na Mungu akijalia wiki hii nategemea nitawasafirisha.

by the way.. wewe wafuga 150 wote hao kwa ajili ya kitoweo? mmh!
 
Last edited by a moderator:
asante Zogwale.
niliamua kuanzisha thread baada ya kuona nakawia hapa. But nashukuru nimepata mawazo ya watu tofauti na Mungu akijalia wiki hii nategemea nitawasafirisha.

by the way.. wewe wafuga 150 wote hao kwa ajili ya kitoweo? mmh!

Ha ha ha ni kweli ni kitoweo tu kwa kuwa sili nyama nyekundu. Hivyo kuna wakubwa na wadogo na inafika idadi hiyo. Mayai nauza kwa oda ya jumla. Na ndugu zako nao wanachukua kwenda kula kwa kuwa hawana muda wa kufuga, si mnajua tena nyie vijana. Ila wanachukua kwa market price!!! Hakuna vya bure eti.
 
Kuku wa kienyeji kama unawafuga kwa mtindo wa free range waweza kufuga wengi kulingana na ukubwa wa shamba lako,na hautingia gharama kubwa ya kuwalisha. Na ukitaka kuuza utauza taratibu bila shinikizo lolote
nakubaliana na wewe
 
nashkuru nimepata somo kubwa sana.hii ni baada y kutafuta kaz kwa muda mrefu na kukosa.wana jf juuuuuuuuuuuu!
 
nina sh.100000 kutokana na somo lenu nataka nifuge kuku wa mayai na nyama.inawezekana kama ndio.naomba procedures kibot
 
Kaka uliyosema ni kweli, sisi watanzania hatuna umoja na ndiyo maana production zetu ni hafifu zikiingia sokoni - mfano nilioutoa hapa ni kwamba
Wafugaji wa kuku nchini kenya wananunua Mashudu ya alzeti, Pumba za mahindi na Mahindi kutoka Tanzania - Then wanarudi kutuuzia mayai tena yenye ubora. Najiuliza je tukiingia kwenye soko huria si watatumaliza kabisa.

Mtu anaweza kusema tusiogope kuingia kwenye soko la pamoja la africa mashariki lakini ndugu zangu wakenya wapo juu sana karibu katika kila sekta. Watanzania tujifunze umoja.

Kwa mafano juzi nilimsikia mama mmoja anasema yeye anapekeka kuku ya nyama somalia na arabuni - wana soko kubwa sana huko - sasa vitu kama hivi ndivyo vya kuanzia kufanyia kazi. Mnaungana watu kama 10 ambao ni wafugaji wa kuku lets say, then mnatengeneza kitu chenye quality mnauza n'gambo.

Kwa sasa mayai mengi sana yanatoka Mombasa na yanauzwa tray kwa Tshs 5000 tena yana ubora mzuri. sisi mayai ya hapa TZ ni 5500 kwa bei ya jumla lakini mengine hayana uzito na ukubwa unaotakiwa sokoni.

Watanzania tuamuke - tusaidieane - tusipende kufanya vitu kipekee pekee - HATUFIKI POPOTE. mfano unakuta wafugaji karibia kumi na ni majirani kila mtu anafuga kuku wa nyama mia mbili, mia tatu tatu hivi - je kama hawa watu wangekuwa na umoja na kutengeneza kitu chenye ubora na kutafuta soko lenye uhakika. Inawezekana, tatizo hatuna hii culture ya kuungana.
mkuu umenena kweli ubnafsi unatuuwa Watanzania hasa vijana aisee na twaishia kulalamika..mimi now ni kijana nadhan by November ntakuwa na mtaji wa almost one million anaetaka kuungana na mie npo tayari tushirikiane tondokane na umaskin
 
mkuu umenena kweli ubnafsi unatuuwa Watanzania hasa vijana aisee na twaishia kulalamika..mimi now ni kijana nadhan by November ntakuwa na mtaji wa almost one million anaetaka kuungana na mie npo tayari tushirikiane tondokane na umaskin
safi, kinachotakiwa usichague nini cha kufanya, kwa mfano vijana wenye degree moja na zaidi wanaona uwekezaji kwenye sekta ya kilimo na ufugaji ni kwa wazee wastaafu na kina mama wajane. hii dhana ikifutika vijana wengi watajiajiri hasa kwenye hii sekta ya kilimo na ufugaji ambayo ipo wazi kabisa katika nchi yetu.

Kuna msemo kijana ukianza kufunga ngombe wa waziwa au kuku - eti unajiandaa kustaafu.
 
Jamani mimi nimenunua incubator bado mpya, nimeitest kwa siku mbili hivi.
Nauliza je kuna dawa yoyote ya kuoshea mayai kabla ya kuyaweka kwenye incubator?
Na je ikitokea umeme ukakatika kwa muda wa masaa manne je mayai yataharibika?
Naomba ujuzi wandugu kesho ndio nataka weka mayai kwenye mashine, nimepata ya kuku wa malawi
 
nlikuwa sijui incubator ni nini kumbe ndo mashine ya kutotolea vifaranga wa kuku ten wa kisasa .
 
nlikuwa sijui incubator ni nini kumbe ndo mashine ya kutotolea vifaranga wa kuku ten wa kisasa .

sio wa kisasa tu hata mayai ya kuku wa kienyeji yanatotolewa na incubator pia. Halafu sio mayai ya kuku tu hata kanga, bata na ndege wengine wanaofugwa.
 
Jamani mimi nimenunua incubator bado mpya, nimeitest kwa siku mbili hivi.
Nauliza je kuna dawa yoyote ya kuoshea mayai kabla ya kuyaweka kwenye incubator?
Na je ikitokea umeme ukakatika kwa muda wa masaa manne je mayai yataharibika?
Naomba ujuzi wandugu kesho ndio nataka weka mayai kwenye mashine, nimepata ya kuku wa malawi

1: Kuhusu dawa ya kusafishia mayai sina uhakika kama ipo au lah. Ninachojua kwa mazingira niliyotumia hiyo incubator nilikuwa nahakikisha mayai ni masafi tu na yale machafu kiasi yalikuwa yanafutwa kwa kitambaa.
2: umeme unapokatika hakikisha joto la ndani ya incubator halishuki chini ya nyuzi joto 37 centigrade. Kama umeme umekatika chini ya masaa manne na upo sehemu za joto kama Dar unaweza kulitunza joto la ndani ya incubator na linaweza lisishuke sana na kuwa na madhara. Kwa kuwa hakuna uhakika katika umeme wetu ni muhimu kuwa na jenereta itakayoweza kusaidia la sivyo ipo siku utapata hasara.

Lingine la kuzingatia hakikisha mayai hayajakaa zaidi ya wiki 2 tangu yalipotagwa au yametunzwa vizuri.

Kila la heri.
 
Back
Top Bottom