Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

nataka nianze kufuga kuku..naomba nijue kati ya kuku wa nyama na mayai bora ipi ,na mtaji wake sh ngapi..masaada please
Mheshimiwa Spinster,

Naomba rudi nyuma anza kusoma uzi wa kwanza hadi mwisho swali lako tayari limeshajibiwa humu ndani
 
Kwa wale wafugaji ambao tayari wamekwisha kuanza ufugaji wa kuku,leteni changamoto zenu tutawasadia kusudi msonge mbele.Sisi ni mkusanyiko wa wataalam wa mifugo by professional lkn pia ni wazoefu wa muda mrefu kwenye hii kada.Pia tuna watu waliobobea kwenye maandiko ya uanzishwaji wa mradi(Project write up) na mpango wa biashara yaani Business plan
Kwa wafugaji waliojikusanya pamoja wanaweza kuwasiliana nasi tukawapa mafunzo ya namna ya ufugaji bora,si tu wa kuku ni kwa mifugo yote.Tutawaeleza kwa uwazi na ufasaha mkubwa wa namna ya kutengeza pesa kupitia ufugaji.Watanzania bila umasikini inawezekana.

Sisi tuko Morogoro,chuo kikuu cha kilimo Sua,but tuko movable kulingana na mahitaji ya anayetaka kuanzishiwA MRADI.
Kumbuka kuanzisha mradi bila kuwa na elimu yake ni sawa na kutembea huku ukiwa umefumba macho.

kwa Makundi haya ya kuku ni kundi lipi ambalo ufugaji wake unalipa zaidi
1) kuku wa nyama
2) kuku wa mayai
3) kuku wa kienyeji
4) kuku Machotara
 
NAFASI INAYOHITAJIKA KWA KUKU 1000 WENYE RIKA TOFAUTI (MABANDA YA KUKU)

[TABLE="class: grid, width: 500, align: center"]
[TR]
[TD]RIKA[/TD]
[TD]CHICKS

VIFARANGA[/TD]
[TD]
GROWERS

KUKU
WANAOKUWA
[/TD]
[TD]LAYERS

KUKU
WANAOTAGA[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]UMRI
KTK
WIKI
[/TD]
[TD]0-6[/TD]
[TD]7-20[/TD]
[TD]20-80[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]KUKU/ENEO LA
M[SUP]2 [/SUP]MOJA ZA MRABA

[/TD]
[TD]12[/TD]
[TD]9[/TD]
[TD]6[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]M[SUP]2 [/SUP]ZINAZOHITAJIKA
/KUKU 1000


[/TD]
[TD]83.7M[SUP]2[/SUP][/TD]
[TD]111.2M[SUP]2[/SUP][/TD]
[TD]166.6M[SUP]2[/SUP][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Eneo watakaloshinda kuku 1000 wakati wa mchana, ambao hufugwa ktk mfumo wa nusu huria ni mita za mraba 10,000 .Hii inamaana kwamba ,kuku mmoja anahitaji eneo lenye mita za mraba 10.Kuhusu utagaji kuku wa kienji hana sifa ya utagaji wa mayai mengi.Kuku wa kienyeji hutaga kwa mzunguko.Kila mzunguko mmoja hutaga hutaga wastani wa mayai 15 na kuanza kuatamia,kutotoa na kulea vifaranga.Mzunguko huo huchukua wastani wa kipindi cha miezi 4 hadi 6 .Hali hiyo hiyo humfanya atage mayai machache kati ya mayai 30 hadi 60 kwa mwaka ukilinganisha na kuku wa kisasa ambao hutaga mayai 270 hadi 300.

Kuku wa kienyeji ukitaka watage mayai mengi wasiruhusiwa kuatamia,kila mayai yanayotagwa yaokotwe na kuhifadhiwa na kama mfugaji atahitaji kutotoresha, kama kuna kuku wengi ,ni vyema ikatumika machine ili kuzalisha vifaranga wengi zaidi.Kuku wa kienyeji anapokuwa kwenye mzunguko wa utagaji,kila siku hutaga yai moja.

Mawasiliano yangu nimekutumia kwenye private message yako ya jf,nenda kwenye notification yako fungua utaona.

Naomba mawasiliano yenu tafadhali
 
Habari zenu wadau.
Natafuta mayai ya kuku wa kisasa kwa jumla. Kwa yeyote mwenye taarifa naomba anijulishe tafadhali.
 
habari wakuu. mimi nimeanza na vijogoo 310. nanimala yng ya kwanza. wana wiki 1 sasa chakula ninacho wapa ni stater. naomba ushauri ktk swala hili la chakula niwapatie chakula kipi ili wawe bora zaid asanten
 
Lambardi chek na watu wa Balton Tanzania wanazo..pia unaweza ongea na watu wa sido au veta wanatengeza..though china na india ni cheap sana
 
Kimsingi kuku wote wanalipa katika ufugaji,mfano kuku wa nyama broilers,kila wiki ukaingiza let say vifaranga 300 ,ukawafuga kwa kufuata kanuni,ukawafuga kwa wiki 8 ili uwauze kwa tshs. 6000/=.Kama kila wiki utaingiza vifaranga ina maana bechi ya kwanza watakapofikia wiki 8,tayari utakuwa na bechi nyingine 7 zinafuata.Chukulia vifo ni 50 katika kuku 300 ingawa inaweza ikawa chini ya hapo.Kwa hiyo katika kila bechi kila wiki utakuwa na kuku 250.

Kimahesababu kuku 250 ukizidisha mara tshs.6000/=,utapata tshs. 1500,000/= kwa wiki na kwa mwezi utapata tshs 6000,000/=.Mapato ya broilers yanaanza baada ya miezi 2 yaani wk 8 ingawa unaweza ukawauza chini ya hapo lkn kwa uzito wa chini kidogo ndio maana inashauriwa wauzwe wk ya nane.

Kuku wa mayai pia nao wanalipa sana tatizo inatakiwa uwe na mtaji mkubwa kwa ajili ya gharama ya kuwanunua na chakula ,mathalani kwa sasa baadhi ya makampuni ya kutotoresha vifaranga wanauza kila kifaranga tshs.2500.Kila kifaranga mpaka atakapoanza kutaga atahitaji kilo 8 za chakula,ukiongeza na madawa,mfanyakazi nk utajikuta unatakiwa uwe na mtaji mkubwa kweli.Mapato ya kuku wa mayai utaanza kupata kwa wastani kuanzia mwezi wa 5 katikati .Baada ya hapo utakuwa na kazi kuuza mayai tu mpaka watakapo choka wiki ya 80 kama umewatunza kwa kufuata misingi na kanuni boro za ufugaji.

Kama ni kuku wa mayai,wakisasa ni wazuri zaidi kwa kuwa wanataga kwa wingi.Kama ni wa nyama ukiweza kufaga machotara ni wazuri zaidi kutokana na kuwa na soko la uhakika.Watu wengi sasa hivi wanapenda kuku wa kienyeji hivyo machota, nyama yake haina tofauti na kuku wa kienyeji,pia ukiweza kuwafuga kwa miezi 6 utaweza kuwauza kila kuku kwa tsh.10000/= bila mteja anayenunua kulalamika.Kuku pure wa kienyeji wana ukuaji hafifu.

mi namachotara 300 wana wiki ya 3. simchezo
 
Dah km zali leo nimefungua nikakutana na hii topic, inaonekana imeanzishwa siku nyingi lakini sikubahatika kuisoma. Nimechoka kuajiriwa na kwa mda mrefu nimekuwa nikifikiria nini cha kufanya ili niondokane na hali ya chini kimaisha na kumtumikia kafiri ambae kila kukicha anazidi kutajirika ilhali mm mfanyakazi wake nazidi kuwa masikini, kwny kibubu changu nina km kamilion10 hivi ila shaka nikihudhuria hii semina naweza kuamua nn nifanye
 
Dah km zali leo nimefungua nikakutana na hii topic, inaonekana imeanzishwa siku nyingi lakini sikubahatika kuisoma. Nimechoka kuajiriwa na kwa mda mrefu nimekuwa nikifikiria nini cha kufanya ili niondokane na hali ya chini kimaisha na kumtumikia kafiri ambae kila kukicha anazidi kutajirika ilhali mm mfanyakazi wake nazidi kuwa masikini, kwny kibubu changu nina km kamilion10 hivi ila shaka nikihudhuria hii semina naweza kuamua nn nifanye

Karibu sana mkuu,
 
habari wakuu. mimi nimeanza na vijogoo 310. nanimala yng ya kwanza. wana wiki 1 sasa chakula ninacho wapa ni stater. naomba ushauri ktk swala hili la chakula niwapatie chakula kipi ili wawe bora zaid asanten

Kimsingi vijogoo kama wanatunzwa vyema ni kuku wenye kukua haraka na kuwa na maumbo makubwa. Ingawa ukuaji wake hauwi sawasawa na broiler kutokana na utofauti wa vinasaba pamoja na kosaafu yake. Vijogoo huhitaji angalawi miezi 4 ili waende Sokoni. Katika umri huu wanakuwa na maumbo makubwa na kukufanya upate tija kubwa unapowapeleka sokoni.

Vijogoo vina soko kubwa kwani wengi hupenda kuwatumia kama mbegu kwa ajili ya kucross na kuku wa kienyeji. Ukipata soko hilo unauwezo wa kuuza hadi tsh 15000 kwa kuku mmoja. Masoko ya vijogoo ni Mashirika binafsi na serikali na NGO'S nk mfano world vision, Halmashauri za wilaya, Care international nk
 
Ndugu wana jamii forum, sasa ni wakati wa kuacha kulalamika, tunapaswa kujituma na kupiga kazi kwa bidii. Vijana graduates kutoka vyuo mbalimbali tuwaze zaidi kwenye kujiajiri kuliko kuajiriwa, kujiajiri kunatoa uhuru wa kufanya kazi na kutoa maamuzi binafsi tena kwa wakati. Kuajiriwa kimsingi hakuna tofauti na utumwa na kama utapiga hesabu vizuri utagundua kuwa kuajiriwa ni hasara na pia huzuia mtu kuitumia elimu yake ipasavyo hasa ukiajiriwa serikalini. Kwa wastaafu pia wana fursa ya kutumia mafao yao vyema kwenye miradi ya ufugaji.

Kwa kuanzia tu naruhusu kuulizwa maswali kutoka kwa wale wote wanaojihusisha na ufugaji wa kuku, kama kuna jambo lolote linasumbua na kutaka kupata ufafanuzi. Pia kwa wanaohitaji kuanzisha mradi wa ufugaji wa kuku,utotoreshaji wa vifaranga,biashara ya uchanganyaji na uuzaji wa vyakula vya kuku nk , kama watanzania tunaweza kusaidiana ili hatimae tuondokane na umasikini. Kila mtu awe msaada kwa watu wengine kwa fani aliyesomea.

Karibuni kwa mjadala.
naweza pata namba yako mkuu...asante kwa elimu nimevutiwa
 
Mkuu me nipo shamba ambako hakuna kabsa mwingiliano wa kuku. Vfaranga wangu nawaona wamevaa mikoti, wengine miguu yao haina nguvu. Je nn shida hapa?
 
Semina ni tarehe ngapi na usajili unafanika wapi

Semina ni tarehe 27/09/2014. Kwa ajili ya usajili nipigie kupitia 0767989713 nitakudarect au ukirudi post za nyuma kuna lile tangazo letu lina namba za mratibu wa haya mafunzo
 
Mkuu me nipo shamba ambako hakuna kabsa mwingiliano wa kuku. Vfaranga wangu nawaona wamevaa mikoti, wengine miguu yao haina nguvu. Je nn shida hapa?

Nipigie kupitia namba 0767989713/0715989713 na 0786989713 nikushauri kwa ufasaha kabisa kabla kuku hawajaanza kufa
 
Kimsingi vijogoo kama wanatunzwa vyema ni kuku wenye kukua haraka na kuwa na maumbo makubwa. Ingawa ukuaji wake hauwi sawasawa na broiler kutokana na utofauti wa vinasaba pamoja na kosaafu yake. Vijogoo huhitaji angalawi miezi 4 ili waende Sokoni. Katika umri huu wanakuwa na maumbo makubwa na kukufanya upate tija kubwa unapowapeleka sokoni.

Vijogoo vina soko kubwa kwani wengi hupenda kuwatumia kama mbegu kwa ajili ya kucross na kuku wa kienyeji. Ukipata soko hilo unauwezo wa kuuza hadi tsh 15000 kwa kuku mmoja. Masoko ya vijogoo ni Mashirika binafsi na serikali na NGO'S nk mfano world vision, Halmashauri za wilaya, Care international nk

dah. nimekusoma mkuu. ila chakula chao je vp lazima niwape vya dukan? kwa wiki 3 izi. nimewapa stater kwa sasa naweza kuwapa mchanganyiko wa pumba na mashudu? Asante
 
Habari wandugu:
Nimejaribu kufuatilia mjadala toka mwanzo, lakini nikiri kwamba kuna uwezekano mkubwa kuna pages sijasoma.

Nimekuwa na hamu ya kuanza hii shughuli ya ufugaji wa kuku wa kisasa wa NYAMA. Na kwa msaada wenu nimeweza kuchanganua kwa kadri niliyoweza na data nilizozipata humu na kwingineko kupata business plan. Huu chini ni mchanganuo wangu, kwa kifupi nimepiga hesabu ya kuku/vifaranga 200, halafu nikajaribu kuangalia kama unaongeza hadi 2000. Na pia nimejichukulia mimi kama muwekezaji kwa maana kwamba mimi nitaweka mtaji na kusimamia pesa lakini mtendaji/mtaalamu ni mwingine.

Kwa Ufupi:

Mahitaji:
[TABLE="width: 255"]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Kuku (Vifaranga) 200[/TD]
[TD]TZS 260,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Madawa na Chanjo[/TD]
[TD]TZS 30,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Chakula jumla gunia 12[/TD]
[TD]TZS 456,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Uendeshaji[/TD]
[TD]TZS 219,000[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 2"]Total[/TD]
[TD]TZS 965,000[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
1. Gharama za kuwafuga/kuwatunza vifaranga 200 hadi unauza ni TZS 965,000
2. Ukiwauza tuseme kuku 200 kwa bei ya 5000 kwa kuku mmoja jumla unapata TZS 1,000,000.
3. Faida ni kiasi cha TZS 35,000.
4.Tuseme basi utafuga/watunza vifaranga 2000 hadi unauza basi gharama itakuwa TZS 905,000 x 10 + 200,000(mshahara) = 9,250,000
5. Faida ya kuku 2000 ni 2000x5000-9,250,000 = 750,000.

Hitimisho:
Maswali niliyonayo:
1. Gharama za madawa na chanjo kwa kuku 200 zinaweza kuzidishwa mara 10 ili kupata gharama ya kuku 2000?
2. Nimeona mshahara kwenye hii thread wa shilingi 100 kwa kuku mmoja kwa mwezi ina maana kuku 2000 kwa mwezi mshahara ni 200,000. je huu mshahara ina maana mfanyakazi anakaa kwake au anakaa na kula kwako? Je ratio ya mshahara na kazi ya kuku 2000 ipo sawa?
3. Kama unaajiri mfanyakazi kwa mwezi je ni kuku kiasi gani mfanyakazi mmoja anaweza kuwaudumia?
4.Kuhusu gaharama za banda au kupangisha banda: Nimeona kwenye hii thread kwamba banda la kuku 1000 kwa vipimo vya 15 x8 m linagharimu kama million 12 huko dodoma. Hizi gharama zipo sahii kweli?
5. Kama unapangisha ardhi ya mtu kujenga banda la size hilo la kuku 2000 inaweza kugharimu kiasi gani?
6. Kama unapangisha banda la size hiyo hapo juu linaweza kugharimu kiasi gani kwa mwezi?
7. Kuna maeneo gani mengine kwenye biashara ya kuku unaweza kupunguza gharama kama unafuga kuku wengi kama 2000 au zaidi?

Nitashukuru kwa msaada wa majibu yenu. Mchanganuo wangu wa hesabu ya kuku 200 upo hapa chini.

Screen Shot 2014-08-27 at 18.32.31.png
 
Back
Top Bottom