Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Tuwasiliane mkuu,nanavyo.Ni pamphlects zinazotoa mwongozo wa ufugaji bora wa kuku wa kienyeji,chotara na wa kisasa.

Kichwa mbovu kama hizo pamphlets ni tofauti na kile kitabu, basi nami nazihitaji. Elimu haina mwisho, si unajua! Nitakupigia wakati wowote tuongee. Namba na email yako umenipa. Asante sana.
 
Nimependa sana jinsi ulivyo weza kufafanua kuhusu ufugaji wa kuku, ila mimi bado nahitaji maelezo ya kiundani zaidi juu ya ufugaji wa hao kuku wa kisasa {nyama}, maana ndo kwanza nataka nianze na idadi ya kuku mia mbili, ila chakushangaza nimepiga hesabu ila naona hailipi hata kidogo, labda unaweza kunisaidia juu ya ilo.
 
Amani kwenu,

Nawashukuru wote mnaonipigia na kuhitaji maelekezo mbalimbali na miongozo ya ufugaji bora wa kuku. Nawashukuru pia wadau wote wa Songea mara baada ya kupata taarifa kuwa nipo Songea walitumia kila njia ili kuonana na mimi kwa ajli ya mazungumzo.

Kwa sasa namshukuru mungu nimerejea tena Morogoro tayari kuendelea na majukumu yangu ya kawaida.Kwa sasa nimerudi tena hewani maana Songea moderm inayoshika vizuri ni ya voda nami sinayo hiyo.

Asanteni sana!
 
Mkuu kichwa nina swali kwenye swala la Kutotoresha, Ulisema unaweza gawa Incubators ya mayi 1000 mara mbili yaani ukaweka mayai 500 baada ya wili mbili ukaweka mengine 500, Ia ninavyo jua mimi Joto na Humidity ndani ya Incubators inatakiwa kubadilika pale inapo fikia kuanguliwa yaani siku ya 18 inatakiwa Humidity ipande juu kidogo na unaacha au unachomo Eggs turining susteam make siku ya 18 ndo inatakiwa wisho kugeuza mayai, so ukifanya hivyo inakuwa vipi katika swala la kugeuza mayai na humidity? kwa sbabau mayai yanatakiwa kugeuzwa angalau mara Tatu kwa siku,
 
Mkuu kichwa nina swali kwenye swala la Kutotoresha, Ulisema unaweza gawa Incubators ya mayi 1000 mara mbili yaani ukaweka mayai 500 baada ya wili mbili ukaweka mengine 500, Ia ninavyo jua mimi Joto na Humidity ndani ya Incubators inatakiwa kubadilika pale inapo fikia kuanguliwa yaani siku ya 18 inatakiwa Humidity ipande juu kidogo na unaacha au unachomo Eggs turining susteam make siku ya 18 ndo inatakiwa wisho kugeuza mayai, so ukifanya hivyo inakuwa vipi katika swala la kugeuza mayai na humidity? kwa sbabau mayai yanatakiwa kugeuzwa angalau mara Tatu kwa siku,

Chasha,

Ni kweli kabisa mkuu, inawezekana kuitumia mashine moja na kuigawa sehemu tatu sio mbili kama ambavyo umeeleza. Sehemu ya kwanza utaweka mayai kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba,kisha utayashusha sehemu ya pili kuanzia siku ya 8 hadi 14 na sehemu ya tatu yatakaa mayai kuanzia siku ya 15 hadi 18, kisha siku ya 19 mayai utayahamishia kwenye hatcher.Kwa baadhi ya Incubator setter na hatcher zote ziko pamoja.

Mashine hizi ni zile zinazotengenezwa nje .Kama umenunua incubator yenye uwezo wa kutotoresha mayai 3000,jua kwamba kwa wakati mmoja unatakiwa uigawe sehemu tatu,vinginevyo utakosa sehemu ya kutotorea kwani kwa kawaida
Setter yenye uwezo wa kubeba mayai 3000, hatcher yake inakuwa na uwezo wa kutotoa mayai 1000.

Mashine ya kutotoa vifaranga(Incubator) imegawanyika sehemu mbili, moja Setter ambayo ni kiatamishi na mbili hatcher ambayo ni kitotoreshi.Mfano wa machine hizi ni zile zinazotengenezwa nchini Italy na kampuni ya Victoria.

Incubator hizi hutengenezwa kwa kadiri ya joto na unyevunyevu unavyohitajika kwa mujibu wa idadi ya siku ambayo mayai yamekaa kwenye machine. Kuanzia pale unaposhusha kwenye hatcher,joto na unyevunyevu lazima vyote kwa pamoja vipande.
 
Mkuu nimekupata vyema kabisa, Kuna sehemu nilisoma huwa inawezekana kutotoresha Vifaranga kabla ya siku 21 yaani unaweza ongeza joto na hivyo kufanya mayai yatotorewe yakiwa na hata siku 19, hii vipi?
 
Mkuu nimekupata vyema kabisa, Kuna sehemu nilisoma huwa inawezekana kutotoresha Vifaranga kabla ya siku 21 yaani unaweza ongeza joto na hivyo kufanya mayai yatotorewe yakiwa na hata siku 19, hii vipi?

Chasha,

Kwakweli hii sijapata kuisoma kokote, ila ninachofahamu ni kuwa mayai yakiwekwa kwenye chumba chenye joto kabla ya kuingizwa kwenye incubator,vifaranga huanza kujitengeneza matokeo yake ukiyaweka mayai hayo kwenye mashine yatawahi kutotoa kabla ya siku 21 kutimia.

Kiitaalam kifaranga huhiji siku 21 zilizokamilika katika uumbikaji wake,ni kama ilivyo kwa mbuzi miezi 5, ng'ombe miezi 9, bata siku 35, kanga siku 28 na nguruwe siku 114 nk.Ukiongeza joto utaua kifaranga kilicho jitengeneza ndani ya yai.Joto linalotakiwa kutotoresha vifaranga ni nyuzijoto 67.6.
 
Dawa inayotumika kutibia mayai kabla ya kuwekwa kwenye incubator kwa ajili ya kutotolewa ni Potassium parmanganate pamoja formolin 40% zote zikichanganywa pamoja kwa uwiano sahii.
 
Mkuu kwenye kutibu Mayai, ni lazima utibu yote kabla ya kuweka kwenye mashine/Incubators? na ukisha changanya hayo madawa unaosha kama unavyo osha vyombo vya chakula? au kuna mtambo mwingie wa kutibu?
Na je kama source ya mayai ni wewe mwenyewe means kutoka kwenye kuku wako ni lazima kuyatibu?
 
Mkuu kichwa, vipi kuhusu kusafirisha Fertlized eggs, yaani ni njia zipi nzuri za kusafirisha mayai ya kwenda kuatamisha? mfano umepata mayai Mbeya na unataka kuyapeleka Arusha, je utatumia Tray kama kawaida au kuna njia nyingine ya kuyabeba.
 
Mkuu kichwa mbovu

Hivi kwa hapa Tanzania ni wapi naweza kupata kuku wazazi kwa ajili ya broilers?
 
Mkuu kichwa mbovu
Hivi kwa hapa Tanzania ni wapi naweza kupata kuku wazazi kwa ajili ya broilers?
King kingo,

Kwa hapa Tanzania huwezi kuwapata kuku wazazi wa Broilers. Kwa Afrika mashariki kuku hawa wanapatikana nchini Kenya ambako kuna kituo cha kuzalisha na kuuza kuku wazazi wa Broilers kinachomilikiwa na Aviagen ya uingereza ambao ni wazalishaji wakubwa wa Hybro parent stock.
 
Mkuu kichwa, vipi kuhusu kusafirisha Fertlized eggs, yaani ni njia zipi nzuri za kusafirisha mayai ya kwenda kuatamisha? mfano umepata mayai Mbeya na unataka kuyapeleka Arusha, je utatumia Tray kama kawaida au kuna njia nyingine ya kuyabeba,

Chasha,

Nakushukuru kwa maswali yako mazuri,ila sorry kwa kuchelewa kurispond.Njia nzuri za kusafirisha mayai ya kwenda kuatamishwa ni ile ya kutengeneza box la mbao ambalo linakuwa karibu sawasawa na tray za mayai ambazo utazitumia kwa ajili ya kutumbukiza tray za mayai zilizofungwa vizuri kwa pamoja kisha unatumbukiza kwenye box.

Hakikisha unapopanga mayai kwenye tray,kwa chini unaweka tray 3 na juu pia tatu kisha unafunga pamoja then unaweka kwenye box la kusafirishia mayai. Unaweza ukatengeneza mabox makubwa yanayoweza kuruhusu kuuingia bundle za tray zilizofungwa pamoja zaidi ya moja.

Box huzuia tray za mayai kupata misukosuko wakati zinasafirishwa hivyo kupelekea kuvunjika.Mayai yenye ufa hayafai kwa ajili ya utotoreshaji.
 
Mkuu, kuku wangu (matetea) hayatotoleshi vifanga vingi tatizo ni nini? au uwingi wa majogoo linaweza kuwa tatizo.

Ahsante.
 
Mkuu kwenye kutibu Mayai, ni lazima utibu yote kabla ya kuweka kwenye mashine/Incubators? na ukisha changanya hayo madawa unaosha kama unavyo osha vyombo vya chakula? au kuna mtambo mwingie wa kutibu?

Na je kama source ya mayai ni wewe mwenyewe means kutoka kwenye kuku wako ni lazima kuyatibu?

Chasha,

Ni muhimu kuyatibu mayai yote kabla ya kuingizwa kwenye Incubators kwa kuwa mayai toka yatagwa na kuku huchukua siku 7 hadi 10 mpaka kuingizwa kwenye Incubator.

Yai linapotagwa linakuwa limejiweka kwenye mazingira rahisi kuingiwa na wadudu ambao huenda kuharibu kiini cha yai matokeo yake husababisha yai kushindwa kutotolewa na hivyo kupunguza percentage of harcherbility.

Hata kama mayai unazalisha mwenyewe lazima uyatibu. Utibuji wa mayai husaidia kuzuia pia manjwa ya kuambukiza toka kwa mama kwenda kwa vifaranga. Ndio maana wakati mwingine unakuta vifaranga wanazaliwa baada ya muda mfupi wanakufa wote. Hali hii inatoka na mayai kutotibiwa.

Dawa ya kutibu mayai ni ya kuunguza na mvuke wake ndio unaotibu mayai.Mayai yote hutibiwa kwa pamoja.Wakati mwingine unaweza ukailamu Incubator yako kuwa sio nzuri kumbe mayai yako hukuyatibu hivyo yanakuwa yameharibiwa na wadudu.Wadudu hawa ni wadogowadogo sana ambao hawana uwezo wa kuonekana kwa macho na wana uwezo mkubwa sana wa kupenya hadi kwenye kiini cha yai na kukiharibu.

Dawa zinazotumika kwa ajili ya utibuji wa mayai ni dawa mbili ambazo hutumika zote kwa pamoja kwa ya fumigation. Dawa hizo ni Potassium parmananate pamoja na fomalin 40%.
 
King kingo,
Kwa hapa Tanzania huwezi kuwapata kuku wazazi wa Broilers.Kwa afrika mashariki kuku hawa wanapatikana nchini Kenya ambako kuna kituo cha kuzalisha na kuuza kuku wazazi wa Broilers kinachomilikiwa na Aviagen ya uingereza ambao ni wazalishaji wakubwa wa Hybro parent stock.


Mkuu Asante kwa maelezo yako naweza kupata contact zao kama unazo?
 
Chasha,
Ni muhimu kuyatibu mayai yote kabla ya kuingizwa kwenye Incubators kwa kuwa mayai toka yatagwa na kuku huchukua siku 7 hadi 10 mpaka kuingizwa kwenye Incubator.

Yai linapotagwa linakuwa limejiweka kwenye mazingira rahisi kuingiwa na wadudu ambao huenda kuharibu kiini cha yai matokeo yake husababisha yai kushindwa kutotolewa na hivyo kupunguza percentage of harcherbility.

Hata kama mayai unazalisha mwenyewe lazima uyatibu.Utibuji wa mayai husaidia kuzuia pia manjwa ya kuambukiza toka kwa mama kwenda kwa vifaranga.Ndio maana wakati mwingine unakuta vifaranga wanazaliwa baada ya muda mfupi wanakufa wote.Hali hii inatoka na mayai kutotibiwa.

Dawa ya kutibu mayai ni ya kuunguza na mvuke wake ndio unaotibu mayai.Mayai yote hutibiwa kwa pamoja.Wakati mwingine unaweza ukailamu Incubator yako kuwa sio nzuri kumbe mayai yako hukuyatibu hivyo yanakuwa yameharibiwa na wadudu.Wadudu hawa ni wadogowadogo sana ambao hawana uwezo wa kuonekana kwa macho na wana uwezo mkubwa sana wa kupenya hadi kwenye kiini cha yai na kukiharibu.

Dawa zinazotumika kwa ajili ya utibuji wa mayai ni dawa mbili ambazo hutumika zote kwa pamoja kwa ya fumigation.Dawa hizo ni Potassium parmananate pamoja na fomalin 40%.

Mkuu kichwa Mbofu, Hapo kwenye Mvuke sijaelewa kwamba Hayo mayai yanakuwa wapi muda huo unayatibu na Huo mvuke unatokana na nini, je ni hayo madawa ukichanganya ndo yanatoa mvuke au ni unayaweka jikoni, na mayai yana kaa makao gani wakati yanapata huo mvuke?
 
Na hayo fertilized eggs si huhitaji joto fulani? sasa yakikaa kwenye Box wakati unayasafirisha hayawezi kuharibika? au kwa one day hakuna shida?

Na kwa mayai ya Kuku wazazi wa Nyama au wa mayai yanaweza kuliwa? au yale ni specilal kwa ajili ya kutotoa viranga tu?
 
Back
Top Bottom