Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Mkuu,kuku wangu(matetea)hayatotoleshi vifanga vingi tatizo ni nini? au uwingi wa majogoo linaweza kuwa tatizo.ahsante.
Nganu,
Inawezekana kuku wako unawawekea mayai mengi kuliko uwezo wake matokeo yake kuku anashindwa kuyamudu kuyaatamia mayai yote,hivyo kushindwa kutoa joto linalostahili ambalo ni muhimu kwa utotorewaji wa vifaranga.

Kuku wa kienyeji ana uwezo wa kuatamia vizuri mayai kati ya 10-15 kwa wakati moja,vinginevyo hataweza kuyaatamia vyema.

Sababu nyingine ni uwingi wa majogoo unasababisha matetea washindwa kutotoa vizuri kwa kuwa jogoo mmoja anapoenda kumpanda tetea, majogoo wengine wanaenda kumfurumua yule jogoo anayeenda kumpanda tetea matokeo yake yai linakosa kurutubishwa na mbegu ya jogoo.

Yai lisiporutubishwa haliwezi kutotolewa.

Uwiano sahihi kati ya jogoo na tetea ni 1:10 yaani, jogoo mmoja kwa jike kumi.

Mayai yasiyotibiwa pia hupunguza asilimia ya utotorewaji kwa kuwa,wakati mwingine yanaingiwa na wadudu ambao hupenya hadi kwenye kiini cha yai na kukiharibu.Kiini cha yai kikiharibiwa yai haliwezi kutotolewa.
 
Mkuu,kuku wangu(matetea)hayatotoleshi vifanga vingi tatizo ni nini? au uwingi wa majogoo linaweza kuwa tatizo.ahsante.

Mkuu kichwa Mbofu, Hapo kwenye Mvuke sijaelewa kwamba Hayo mayai yanakuwa wapi muda huo unayatibu na Huo mvuke unatokana na nini, je ni hayo madawa ukichanganya ndo yanatoa mvuke au ni unayaweka jikoni, na mayai yana kaa makao gani wakati yanapata huo mvuke?

Chasha,

Hii inakuwa kwa fumigation kwa kutumia potassium permanganate na formalin 40%.Hizi dawa ukiziunguza pamoja kwa uwiano unaostahili hutoa mvuki ambao ndio unaofanya kazi ya kutibu mayai.Wakati wa zoezi la utibuji,mayai yote huwekwa kwenye chumba maalum kidogo ambacho hakiruhusu hewa kutoka nje.

Utibuji wa mayai ni zoezi linalochukua takribani dakika 20 toka formalin na potassium permanganate ulipozireactisha pamoja.

Moto hautumiki hapa.
 
Na hayo fertilized eggs si huhitaji joto fulani? sasa yakikaa kwenye Box wakati unayasafirisha hayawezi kuharibika? au kwa one day hakuna shida?

Na kwa mayai ya Kuku wazazi wa Nyama au wa mayai yanaweza kuliwa? au yale ni specilal kwa ajili ya kutotoa viranga tu?

Mkuu Chasha,

Kwa siku moja hayanashida kitu cha msingi mara yafikapo nyumbani haraka yatibu kisha yaingize kwenye Incubator.

Na kuhusu mayai ya kuku wazazi,yenyewe hayana shida yanaliwa tu kama mayai mengine ya kuku wa kawaida.
 
Je, ni kuku wapi kati ya wa nyama na mayai wana uwezekano mkubwa wa kuingiza faida na risk ndogo katika biashara?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Je ni kuku wapi kati ya wa nyama na mayai wana uwezekano mkubwa wa kuingiza faida na risk ndogo ktk biashara?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

0909Hekima,

Kimsingi kuku wote wanafaida na wote wana risk,ni muhimu kufuata mwongozo wa kanuni bora za ufugaji kwa kuku wote utaepuka risk hasa za magonjwa.
 
Thank you Technology!!

hi kichwa mbovu nimefuatilia hii mjadala nimepata elimu tosha. napenda kuuliza je kuku wa mayai wanachukua muda gani kuanza kutaga? na je kwa kuku mia mpaka watage watakuwa wametumia chakula kiasi gani? na je naweza kufuga kuku wa mayai na nyama kwa wakati mmoja au kutakuwa na muingiliano wa magonjwa?
 
Last edited by a moderator:
Kwa wale wajasiriamali waliohamasika katika zoezi la ufugaji wa kuku hasa kuku wa nyama aina ya broilers ni muhimu kuwa makini kwani tayari nishaanza kupokea malalamiko kutoka kwa baadhi yenu kuwa kuna maagents wa vifaranga wamekuwa wakiwauzia vijogoo badala ya broilers kwa kuwa wote wanafanana kwa rangi.

Vijogoo vinachelewa kukua,mara nyingi mfugaji humchukua hadi miezi 5 kuwahudumia vijogoo ili vifikie uzito wa kuwauza.

Kama unahitaji kuanzisha mradi wa ufugaji wa broilers,ni muhimu ukaenda moja kwa moja kwenye kampuni husika kuliko kuwatumia hawa maagents kwani wengi wao sio waaminifi.Kwa kawaida wasipokupa wote vijogoo,basi watakuchanganyia hadi nusu kwa nusu.

Vijogoo vyenyewa huwa ni bei ndogo sana mpaka wakati mwingine kwa tsh 200 kwa mmoja unaweza ukapata na kwa kipindi fulani hawa vijogoo hutolewa bure kwa makampuni fulani mfano matembwe village company limited. Wakati mwingine hutolewa kama motisha kwa wale wanaonunua kuku wa mayai,mfano mteja anaweza akapata 10% ya layers aliyochukua.

Maagents wanachokifanya ni kwamba, kwa kuwa bei ya vijogoo ni ndogo wanachukua hao vijogoo kutoka kwenye makampuni husika kisha wao wanawadanganya wateja kuwa hao vifaranga ni vya broilers na wanawauzia kwa bei ya broilers.

Ukihitaji broilers nenda amadori utapata vifaranga wengi tu,wala usidanganyike na matapeli,vinginevyo uwe na elimu ya kuwajua vijogoo.
 
Hi kichwa mbovu,

Nimefuatilia hii mjadala nimepata elimu tosha. napenda kuuliza je kuku wa mayai wanachukua muda gani kuanza kutaga? Na je kwa kuku mia mpaka watage watakuwa wametumia chakula kiasi gani?

Na je, naweza kufuga kuku wa mayai na nyama kwa wakati mmoja au kutakuwa na muingiliano wa magonjwa?
 
hi kichwa mbovu nimefuatilia hii mjadala nimepata elimu tosha. napenda kuuliza je kuku wa mayai wanachukua muda gani kuanza kutaga? na je kwa kuku mia mpaka watage watakuwa wametumia chakula kiasi gani? na je naweza kufuga kuku wa mayai na nyama kwa wakati mmoja au kutakuwa na muingiliano wa magonjwa?

Little Angel,

Mimi mzima.Nashukuru kama umepata elimu kutokana na huu uzi wangu,na hilo ndilo hasa lengo langu.Watu waelimike kishe wajiajiri watengeze pesa tuondokane na huu umasikini.

Ukiwatunza vizuri,kuku wa mayai huchukua miezi 5 mpaka kuanza kutaga.Kuku mia wote kwa pamoja mpaka kuanza kutaga watatumia kilo 800,sawa na mifuko 16 ya chakula kila mfuko ukiwa na kilo 50.Kati ya chakula hicho, chicks mash kilo 200 sawa na mifuko 4 na Growers' mash kilo 600 sawa na mifuko 12.

Hata hivyo,katika ufugaji unaweza kuwafuga kuku wa nyama na kuku wa mayai kwa pamoja lakini siyo katika bada moja.Ni muhimu wakatenganishwa mabanda kulingana na asili ya kuku wenyewe.

Broilers wanahitaji saa 18 za kupata chakula tofauti na layers ambao wao wanatakiwa wapewe chakula kwa share maalum kuwazuia kutengeneza mafuta mengi miilini mwao ambayo mara nyingi huja kugeuka kikwazo kwenye utagaji.

Wakati wa ufugaji wa hawa kuku wa kisasa ni muhimu ukafuata kanuni za ufugaji bora zitakazo kufanya ufagaji wako uwe wenye tija.

Nitashukuru kama nitakuwa nimekuridhisha na haya majibu yangu.
 
Little Angel,

Mimi mzima. Nashukuru kama umepata elimu kutokana na huu uzi wangu,na hilo ndilo hasa lengo langu.Watu waelimike kishe wajiajiri watengeze pesa tuondokane na huu umasikini.

Ukiwatunza vizuri,kuku wa mayai huchukua miezi 5 mpaka kuanza kutaga.Kuku mia wote kwa pamoja mpaka kuanza kutaga watatumia kilo 800,sawa na mifuko 16 ya chakula kila mfuko ukiwa na kilo 50. Kati ya chakula hicho, chicks mash kilo 200 sawa na mifuko 4 na Growers' mash kilo 600 sawa na mifuko 12.

Hata hivyo,katika ufugaji unaweza kuwafuga kuku wa nyama na kuku wa mayai kwa pamoja lakini siyo katika bada moja. Ni muhimu wakatenganishwa mabanda kulingana na asili ya kuku wenyewe. Broilers wanahitaji saa 18 za kupata chakula tofauti na layers ambao wao wanatakiwa wapewe chakula kwa share maalum kuwazuia kutengeneza mafuta mengi miilini mwao ambayo mara nyingi huja kugeuka kikwazo kwenye utagaji.

Wakati wa ufugaji wa hawa kuku wa kisasa ni muhimu ukafuata kanuni za ufugaji bora zitakazo kufanya ufagaji wako uwe wenye tija.

Nitashukuru kama nitakuwa nimekuridhisha na haya majibu yangu.

Nashukuru sana kwa majibu yako mazuri.nataka nianze kufuga kuku mwezi wa tano. Ni fedheha sana kutegemea mshahara tu wakati fursa zipo nyingi sana.

Najipanga nikiwa tayari nitakucheki mkuu kwa ajili ya maandalizi ya kupokea vifaranga. Ubarikiwe sana mkuu.
 
Nashukuru sana kwa majibu yako mazuri. Nataka nianze kufuga kuku mwezi wa tano. ni fedheha sana kutegemea mshahara tu wakati fursa zipo nyingi sana.

Najipanga nikiwa tayari nitakucheki mkuu kwa ajili ya maandalizi ya kupokea vifaranga. Ubarikiwe sana mkuu.

Bila shaka Little Angel,

Thank you.
 
Mkuu Kichwa Mbovu, Kuna wale kuku wanao Taga mayaiya Blue vipi? nilikutana nao Jana mahali fulani hivi huku Arusha ila sasa Bei yake make Yai tu ni Tsh 2500 bei ya kuku ndo usiseme, na na try inakwenda kwenye Tsh 85 hivi, ni vipi unawajua?

Na mbona kuna kuku chotara wano atamia mayai?
 
Mkuu Kichwa Mbovu, Kuna wale kuku wanao Taga mayaiya Blue vipi? nilikutana nao Jana mahali fulani hivi huku Arusha ila sasa Bei yake make Yai tu ni Tsh 2500 bei ya kuku ndo usiseme, na na try inakwenda kwenye Tsh 85 hivi, ni vipi unawajua?

Na mbona kuna kuku chotara wano atamia mayai?
Chasha,

Kwakweli hao kuku siwajui na wala sijapata kuwaona. Kuhusu chotara,kuna wale wanaoatamia ambao wanachukua tabia kutoka kwa kuku wa kienyeji na kuna wale ambao hawaatamia kwa kuchukua tabia ya kutoatamia kutoka kwa kuku wa kisasa, kwa kuwa machotara ni mchanganyiko wa kuku wa kisasa na kienyeji.
 
Wanajamii forum hasa jukwaa hili la ujasiriamali,

Nina habari njema kwa watu wa Dar-es-salaam,kuanzia ijumaa ya wiki ijayo tarehe 12,13 na 14 siku ya jumapili nitakuwa huko.Kwa wale watakaonihitaji ili kuwakagulia na kuwashauri juu ya miradi yao ya ufugaji wa kuku tuwasiliane kwa email yangu amanngoma@gmail.com au kwa namba 0767989713 au 0715989713.

Kama mnaweza kujikusanya sehemu watu kadhaa naweza nikawaendeshea mafunzo ya ufugaji wa kuku kwa faida na kama kutakuwa na matatizo mengine yanawasumbua mtapata fursa ya kuyauliza na nitawajibu kwa ufasaha,mfano unafuga kuku wa mayai,wamefikia umri wa kutaga lakini wanataga wachache au hawatagi kabisa,ninao ufumbuzi wa tatizo hilo.

Watakaohudhuria wataweza kujipatia bonus ya feed formula za kuku wa nyama aina ya broilers (aina zote za feed formula) na pia zile za Layers mash. Formula zangu za kutengeneza chakula ni zile za Industrial ambazo ni nzuri na huwezi kuzipata sehemu yoyote. Kwa makampuni au watu binafsi ambao hujishughulisha na utotoreshaji wa vifaranga,pia tuwasiliane nina feed formula za kuku wazazi aina zote.

Kwa kawaida feed formula moja mfano formula za broiler laki moja,lakini tukionana huko itakuwa itakuwa ni bonus.Ukitengeneza mwenyewe chakula inakulipa sana kuliko kununua.

Kwa wanaohitaji gharama kwa washiriki ambao watajikusanya pamoja ni tsh 30,000/=tu.Na pia watakaohitaji mwongozo wa ufugaji bora na wa kisasa wa kuku,kutakuwa na punguzo maalum.

Kwa sababu mifugo ni taaluma yetu,pia kutakuwa na fursa ya kuuliza maswali ya miradi ya ufugaji wa wanyama aina nyingine mfano Ng'ombe, mbuzi, kondoo, nk.

Kuonyesha uko tayari like post kisha nipm au ni email au nipigie.
 
Mkuu Kichwa Bahati mbaya siko Dar Ningekutafuta hata Mimi,

Ila Mkuu nina swali kwenye Chakula Cha Kuku, Mkuu nilipata kusoma Mahali fulani na Baadae nikaja Kuprove ni kweli kabisa.

Tatizo kwenye utengenezaji wa Chakula Cha Kuku Uko kwenye kupima DCP Digestive Crude Protein, na CP kawaida haiwezi pimwa kwa macho wala kwa mizani bali kuna kifaa maalumu na Makampuni ya Kutengeneza vyakula vya Kuku watakuwa nacho na hapo no sehemu ngumu kwa wajasirimali wadogo,

Kwa kenya wao wana Maabara ya Serikali na ukisha Tengeneza chakula unapeleka Maabara kupima Kiwango cha CP,

Tatizo ni kwamba unaweza kuta zao Moja lina CP tofauti kwa kiwango, Mfano. Mahindi yanaweza kutofautina kiwango cha Protein kwa sababu nyingi sana ikiwemo sehemu yalipo limwa, ukame na kazalika, Unaweza kuta Soya inayolimwa Mbeaya ikawa na CP nyingi kuliko my be SOYA inayo limwa DODOMA, naAlzeti hivyo hivyo na kwa macho huwezi tambua kamwe so unaweza pima Kilo 10 za soya kumbe kwa hiyo soya yako ilitakiwa upime Kilo 12 na si Kumi.

Na kwa maelezo niliyo pata tatizo kubwa sana ni jinsi ya Kupima CP na hii ni kwa sababu zao moja linaweza kuwa na CP tofauti na utata uko hapo

Je wewe unafanya nini hapa kwenye kupima DCP?

SO MKUU UTAKUBALIANA NA MIMI KWAMBA HAPO KUNA KAZI KUBWA SANA NA BILA KUPROVE MAABARA HUWEZI TAMBUA DCP ILIYOPO KWENYE HICHO CHAKULA ULICHO TENGENEZA
 
Little Angel,

Mimi mzima. Nashukuru kama umepata elimu kutokana na huu uzi wangu, na hilo ndilo hasa lengo langu. Watu waelimike kishe wajiajiri watengeze pesa tuondokane na huu umasikini.

Ukiwatunza vizuri,kuku wa mayai huchukua miezi 5 mpaka kuanza kutaga.Kuku mia wote kwa pamoja mpaka kuanza kutaga watatumia kilo 800,sawa na mifuko 16 ya chakula kila mfuko ukiwa na kilo 50. Kati ya chakula hicho, chicks mash kilo 200 sawa na mifuko 4 na Growers' mash kilo 600 sawa na mifuko 12.

Hata hivyo,katika ufugaji unaweza kuwafuga kuku wa nyama na kuku wa mayai kwa pamoja lakini siyo katika bada moja. Ni muhimu wakatenganishwa mabanda kulingana na asili ya kuku wenyewe. Broilers wanahitaji saa 18 za kupata chakula tofauti na layers ambao wao wanatakiwa wapewe chakula kwa share maalum kuwazuia kutengeneza mafuta mengi miilini mwao ambayo mara nyingi huja kugeuka kikwazo kwenye utagaji.

Wakati wa ufugaji wa hawa kuku wa kisasa ni muhimu ukafuata kanuni za ufugaji bora zitakazo kufanya ufagaji wako uwe wenye tija.

Nitashukuru kama nitakuwa nimekuridhisha na haya majibu yangu.

Mkuu kichwa mbovu mimi tayari nimeanza kufuga kuku wa mayai na ni kwa uhamasishaji wako! ubarikiwe!
Hapo kwenye masaa ya kuku kula naomba msaada kwani umesema broirer wanakula kwa saa 18 je layers ni masaa mangapi!

Mimi kwa sasa kwa kukuwa wana week kumi na moja kila mmoja nimempigia wastani wa gram 60 tu za chakula kikiisha siongezi tena, je ninakosea?

Asante
Mkuu kichwa mbovu mimi tayari nimeanza kufuga kuku wa mayai na ni kwa uhamasishaji wako! ubarikiwe!
Hapo kwenye masaa ya kuku kula naomba msaada kwani umesema broirer wanakula kwa saa 18 je layers ni masaa mangapi!

Mimi kwa sasa kwa kukuwa wana week kumi na moja kila mmoja nimempigia wastani wa gram 60 tu za chakula kikiisha siongezi tena, je ninakosea?

Asante
 
Asante mheshimiwa

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom