Ufugaji wa Mbuzi, Kanga, Bata Mzinga na Kuku

Ufugaji wa Mbuzi, Kanga, Bata Mzinga na Kuku

Galla huyu kanunuliwa sh laki5
 

Attachments

  • 20210320_180052.jpg
    20210320_180052.jpg
    202.9 KB · Views: 53
  • 20210320_180337.jpg
    20210320_180337.jpg
    313.4 KB · Views: 51
  • 20210320_180340.jpg
    20210320_180340.jpg
    298.7 KB · Views: 46
Ukiwa na huyo inabidi ujiandae na majike wakutosha maana hao Galla sifaya yao madume ni uwezo wa kupanda na kupigana bila ya kuchoka ka Boer, Hapa nyumbani kapiga Dume alilo likuta hapa li mekuwa bwege kabisa sasahivi
 
Uzi wako umekaa vyema sana nakupongeza sana kwa hatua uliyo ifikia, nakushauri tu unapochukuwa Mbuzi mnadani uwapatie huduma za afya kwanza kabla ya kuwachanganya na hao wengine hasa unapokuwa na Mbuzi wachanga.

usiwe mbali na kijana wa kazi hasa hichi kipindi ambacho wana zaa, pili usiruhusu hao watoto kwenda machungani na mama zao mpaka wamalize wiki 4.

Mama anae nyonyesha mpatie pumba na mchanganyiko wa mashudu ya alizeti au pamba, chumvi,chokaa na kuwawekea jiwe la kulamba maana lina madini ya kutosha, na uwapatie dawa za minyoo kwa muda muafaka.
upande wa chanjo za msingi ikoje
 
upande wa chanjo za msingi ikoje
Kwakweli swala la chanjo nilakushirikisha Vet maana unaweza ukafanya chanjo kumbe hujafanya kwa wakati muafaka au ukawa umetoa dozi ndogo au umetumia chanjo isiyo stahiki nisinge penda kutoa ushauri usio wakitaalamu isije kuleta madhara kwenye zizi lako.
Nasisitiza tumia Vet mwenye kuelewa na atakupa elimu nzuri ya chanjo kuliko mfugaji mwenzako.
 
Sorry mdau hv utamjuaje kua huyu ni GALLA? Liko vzr sana!! Sema bei imechangamka sio poa
Galla ana njia kuu za kumtambua. 1, uso wake sio mrefu kama Mbuzi wa kawaida.
2,sehemu zake za siri chini ya mkia ni nyeusi.
3,sehemu za mdomo wake lips ni nyeusi.
4,Ngozi yake juu ikiwa nyeupe chini ya manyoya atakuwa mweusi.
5,Dume la Galla/Isiolo huwa ni kati ya madume yenye nguvu sana ya kupanda bila kuchoka.
6, Chini ya shingo yake baada ya kidevu kuna nyama inashuka hapo kama baadhi ya picha zilivyojionyesha nilizo zituma.
7,Miili yao mikubwa naimejaa nyama sana.
Nafikiri hapo umenielewa ndugu karibu sana tujifunze pamoja.
 
Galla ana njia kuu za kumtambua. 1, uso wake sio mrefu kama Mbuzi wa kawaida.
2,sehemu zake za siri chini ya mkia ni nyeusi.
3,sehemu za mdomo wake lips ni nyeusi.
4,Ngozi yake juu ikiwa nyeupe chini ya manyoya atakuwa mweusi.
5,Dume la Galla/Isiolo huwa ni kati ya madume yenye nguvu sana ya kupanda bila kuchoka.
6, Chini ya shingo yake baada ya kidevu kuna nyama inashuka hapo kama baadhi ya picha zilivyojionyesha nilizo zituma.
7,Miili yao mikubwa naimejaa nyama sana.
Nafikiri hapo umenielewa ndugu karibu sana tujifunze pamoja.

Asante kiongozi!! Mpaka hapo nimekuelewa!! Vp jike lake GALLA linaweza kuzaa watoto mapacha?
 
Asante kiongozi!! Mpaka hapo nimekuelewa!! Vp jike lake GALLA linaweza kuzaa watoto mapacha?
Kwakweli wapo ila mimi bado sijabahatika kuwa nao ila kuna mahala nime agizia ni nunuwe mama pamoja na watoto wake wote
 
Nipo Dar ndugu wanapatikana bila shida wewe upo mkoa gani

nipo dar mzee natamani kuja kuona na kujifunza kwako
Ndugu karibu sana hili ni zawadi yetu sote kwa Mungu njoo chemba tupeane mawasiliano, niko all weekend karibu sana.
 
Niseme kitu kimoja jamani tuliopo kwenye ajira tuanze sasa kutayarisha mashamba yetu kwa anae weza mifugo na kilimo na aliyepo na nafasi ayaendeleze pale alipo fikia kuna maisha ya baadae yanayo tuhitaji hasa sisi waajiriwa baada ya ajira.
 
Tena Sana mkuu hili me nmeliona mapema sana
Niseme kitu kimoja jamani tuliopo kwenye ajira tuanze sasa kutayarisha mashamba yetu kwa anae weza mifugo na kilimo na aliyepo na nafasi ayaendeleze pale alipo fikia kuna maisha ya baadae yanayo tuhitaji hasa sisi waajiriwa baada ya ajira.
 
Nawasalimuni kwa jina la Mungu, poleni na maombelezo ya Rais wetu, lakini tukumbuke Mazizi ya mfugo wetu mpendwa Mbuzi yanatuhitaji, kumekuchaje huko?
 
Mungu ni mwema mkuu harakati zinaendelea vyema
Nawasalimuni kwa jina la Mungu, poleni na maombelezo ya Rais wetu, lakini tukumbuke Mazizi ya mfugo wetu mpendwa Mbuzi yanatuhitaji, kumekuchaje huko?
 
Back
Top Bottom