Ufugaji wa Nguruwe: Fahamu faida, hasara na mbinu bora za ufugaji

Amoeba

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2009
Posts
3,288
Reaction score
791


- Nguruwe watoto 20 @ 20000 = 400000
- Banda la mabanzi=1,000,000
- Chakula = 1,000,000
- Dawa= 200000

After 1yr: Nguruwe 20 watazaa vitoto kama 160,utachakuwa vitoto jike 100,
mama zao wote watauzwa, huku shambani kwetu nguruwe
mkubwa ni Tsh 200,000 tu, utapata 4,000,000.

After 2yrs: Nguruwe 100 wanaweza kuzaa 700. Kati ya 700 chagua majike 500,(unaweza kuuza watoto dume ukanunua jike).

Year 3: Nguruwe 500 watazaa watoto 3500, chagua watoto 1500 tu
Kutoka hapo unamentein Number 1500, kila mwaka unaweza kuuza
watoto zaidi ya 3000, na nguruwe wakubwa 1500.
1500*200000= Tsh 300,000,000/= kwa mwaka
Nusu ya hiyo pesa ni gharama zingine, unabaki na 150mil.
Welcome to the club

Kabla hujajitumbukiza kaone mifano, au nenda sokoine ukaonane na wataalamu.

Kila mwaka nalima Mahindi, alizeti, maboga ekari 30 kwa ajili ya chakula cha nguruwe tu.

Nakupenda saana mpwa..





==========

USHUHUDA
===
 

Mpwa hii bonge ya deal hata mate yananitoka ila tatizo mimi imani yangu inaniambia nguruwe ni haramu kabisa. lakini hiyo hela naitaka tena sana tu.
 
Mpwa hii bonge ya deal hata mate yananitoka ila tatizo mimi imani yangu inaniambia nguruwe ni haramu kabisa. lakini hiyo hela naitaka tena sana tu.

Hii ni yenyewe mzee, ndg yangu mmoja ameomba nimpelekee, nimeona ni bora niiweke hapa hadharani faida kwa wote. kupanga ni kuchagua kaka, ila sikushauri uende kinyume na imani. na hiyo bei ya nguruwe ni huku shambani kwangu, mjini sijui bei, mm naona maroli yanakuja tu.
 
Nimekuwa interested sana na ushauri wako nami ningependa kujaribu hilo deal. Jambo moja linanisumbua ni jinsi ya kupata sehemu ya kufugia, kama kuna mtu ana idea mashamba ya bei nafuu pembezoni mwa Dar es salaam naomba msaada.
 

Sasa mtani nina maswali kadhaa hapa.
1. Nguruwe anachkua muda gani hadi kuuzwa, umri
2. Nguruwe 500 wakubwa + watoto 3000 wanahitaji wapagazi wangapi
3. Je kama sina shamba la kulima chakula cha nguruwe mikakati inakaa vipi
4. Nguruwe 500 wakubwa + watoto 3000 wanahitaji eneo la ukubwa gani kuwajengea mabanda (zizi)
5. Soko la nguruwe watoto na wakubwa liko vipi
6. Je kuna magonjwa yoyote hatarishi kwa nguruwe ambayo yanaweza maliza zizi zima.

MJ
 

1.Nguruwe anachukua miezi 6 mpaka 12 mpaka kufikia uzito wa kutosha (inategemeanan na malisho)
2.Inategemeana na nafasi yako, ukiwa upo pale full time, wapagazi watatu ni more than enough (kumbuka usipokuwapo watu wanakuwa na uzembe flan). mimi nnao sita chini ya usimamizi mkali.
3.inategemea uko wapi. huku kwetu hata kama haulimi gunia la pumba za mahindi ni Tsh 10,000/=! mashudu ya alizeti gunia ni 20,000/=!
4. Ekari moja wanakaa kwa amani yote. ni vizuri kuwa mbali na makazi ya watu.
5. inategemea uko wapi. kwangu mm nauwezo wa kuuza nguruwe 200 kwa mwezi bila shida. watoto inasumbua kidogo kwa sababu wananunua wafugaji, ukitaka kuwauza kwa urahisi wakuze mpaka miezi mitatu hv.
6. Minyoo na ukurutu. Kikubwa ni chanjo na usafi wa hali ya juu KILA SIKU (nguruwe ni msafi sana akitunzwa, wa kwangu nikimkuta sebuleni nacheka tu-ni WASAFI kama pet)

Nguruwe wanahitaji usimamizi wa karibu sana, uwajue kwa namba ili uweze kufuatilia maendeleo yao kila asubuhi. Ukiona mnyama mmoja amezubaa mwite doctor haraka sana. usiachie wasaidizi kila kitu, kuwa makini na kuhakikisha wanapata milo miwili ya kutosha bila kusahau vegs. nguruwe wanapenda maji-usiwanyime starehe ya kwa kuwabananisha hawatanenepa vya kutosha. Nguruwe ana uwezo wa kuzaa mara mbili kwa mwaka. Mimi sijasoma kilimo na mifugo, ni ubishi tu na kuthubutu vilivyoletwa na maisha magumu. MUHIMU UKUBALI KUKAA SHAMBA, JF UIPATE KWA TTCL NA SOLLAR!
 
Nadhani mdau anataka kujua mchanganuo mzima wa ufugaji wa nguruwe, key issues za ku-take into consideration kama unataka kufuga huyu mnyama!
Wanaojua tunaomba watumwagie data hapa!
Kuna thread ya Amoeba alichanganua vizuri sana yaani ilinitia moyo sana, hawa nadhani nikianza shambani nitawafuga, search au mpm ni nzuri hiyo thread.
 
Inaitwaje?

sorry mkuu, nimechelewa kidogo kuingia pm, hivyo msg yako nimechelewa kuijibu.
Biashara ya ufugaji wa mnyama yeyote inahitaji research na uangalifu wa kutosha, hapa kwenye thread yangu nilieleza kwa haraka tu sababu ya muda. Hata hivyo kama uko srz tafadhali tembelea kwa mtaalamu yeyote wa wanyama aliye karibu nawe, ningependa kuandika kwa undani na kirefu, lakini muda hauniruhusu ndg yangu.

jaribu kucheki hapa https://www.jamiiforums.com/matangazo-madogomadogo/42162-anza-hivi-mpwa-wangu.html
 
safi sana ndugu Amoeba,watu lazima wale kila siku no matter what.
 
wadau nataka nianze ufugaji wa nguruwe wa nyama dsm...sijui chochote kuhusu hawa jamaa ila wanalipa ile mbaya.....give me tips,plz.
 
wadau nataka nianze ufugaji wa nguruwe wa nyama dsm...sijui chochote kuhusu hawa jamaa ila wanalipa ile mbaya.....give me tips,plz.
Naomba ufafanuzi hapo kwenye red:hivi kuna nguruwe wa nyama na ...............................
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…