Ufugaji wa Nguruwe: Fahamu faida, hasara na mbinu bora za ufugaji

Kwa muda nimetafuta formula ya chakula kwa ajili ya kulisha nguruwe bila mafanikio. Leo nimefanikiwa kupata hii formula toka chuo cha kilimo na mifugo Tengeru, Arusha. Kutengeneza kilo 100 changanya hivi

Pumba ya mahindi 40kg
Pumba ya ngano 35kg
Mashudu ya alizeti 15kg
Dagaa waliosagwa 5kg
Chumvi 1kg
Pig mix 1kg
Mifupa iliyosagwa 1kg
Chokaa 2kg


Mchanganyiko huu ni kwa nguruwe wa umri wote.
Tafadhali share kama una formula tofauti kwa ulishaji wa nguruwe
 
Nguruwe hata umuweke wapi minyoo haitomuondoka hatta siku moja. Huyu mnyama anakula mavi yake mwenyewe Vipi utaweza kumuepusha na minyoo kwa kutumia hizo drinkers?
 
Acha kuzungumza uzushi.Nguruwe huwa anajitenga na kinyesi chake. Na hizo drinkers si kwa ajili ya kuzuia minyoo, bali ni kufanya maji yasipotee hovyo au kukaa muda mrefu kwenye vyombo vya kuhifadhia maji yao, inayopelekea kuwepo na viluilui.
 
Nguruwe hata umuweke wapi minyoo haitomuondoka hatta siku moja. Huyu mnyama anakula mavi yake mwenyewe Vipi utaweza kumuepusha na minyoo kwa kutumia hizo drinkers?
Hivi wewe na kaunga ndo hanuamini uwepo wa Mungu? Vp katika imani yako, nguruwe ni kitoweo?
 
Hivi wewe na kaunga ndo hanuamini uwepo wa Mungu? Vp katika imani yako, nguruwe ni kitoweo?
Naamini 100 kwa 100 Mungu yupo na Kwa imani yangu nguruwe ni Najisi .
Una swali lingine?
 
Ebu tuambie wapi huko nguruwe Mtoto 20000
 
Nguruwe hata umuweke wapi minyoo haitomuondoka hatta siku moja. Huyu mnyama anakula mavi yake mwenyewe Vipi utaweza kumuepusha na minyoo kwa kutumia hizo drinkers?
Acha unafiki.ni mnyama gani hana minyoo.hata wewe unayo mingi tuu. Na kama hupendi nguruwe sababu ana minyoo au anakula ovyo, mbona kuku anakula kila kitu,bata jee, na samaki af wote unawala hao
 
nataka na fomula ya kulisha kama mtu anayo nasikia hawali sana kuna masaa ya kuwapa chakula ....
 
Acha unafiki.ni mnyama gani hana minyoo.hata wewe unayo mingi tuu. Na kama hupendi nguruwe sababu ana minyoo au anakula ovyo, mbona kuku anakula kila kitu,bata jee, na samaki af wote unawala hao
Bata wala kuku hawali mavi yao wenyewe. We endelea kula tu hio nyamafu siku ukiugua saratani ya tumbo ndio akili itakusogea.
 
Tangu 2009wazazi wang wamekua wakifuga nguruwe kwa mazoea, tupo (mahina) mwanza.
Now nimeludi nyumbani (mwanza) nataka nifanye revolution ya ufugaji nyumbani kwetu.
Kuna nguruwe majike 8 wanalishwa pumba za mchele two times a day.
Wengine manyoya yao yamesimama matumbo yameshuka.
Tu endelee kupeana updates za nguruwe
 
Piglets 0.5kg/day.
Weaners 1.0 kg/day
Growers 1.5kgs/day
Finishers 1.5 - 2kgs/day.
Pregnat and lactating sow 3 kgs/day
Boar 2.5 kgs/day.
 
~piglets ni watoto wa nguruwe,
~weaners ni nguruwe walioachishwa kunyonya (after 8 weeks of age), ~Growers ni nguruwe wanaokuwa (4months of age),
~Finishers ni nguruwe walofikia umri wa kutolewa/kuchinjwa ( 7-9months of age). ~Sow ni nguruwe jike ambae ameshazaa na
~boar ni nguruwe dume ambaye hajahasiwa.
 
Changamka Mapema Mwanza Nguruwe Soko Lao Liko Nje Nje Ukiwafuga Kwa Wingi Ndio Utaiona Faida Ya Ufugaji ... !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…