Ufugaji wa Nguruwe: Fahamu faida, hasara na mbinu bora za ufugaji

Ufugaji wa Nguruwe: Fahamu faida, hasara na mbinu bora za ufugaji

View attachment 324772

- Nguruwe watoto 20 @ 20000 = 400000
- Banda la mabanzi=1,000,000
- Chakula = 1,000,000
- Dawa= 200000

After 1yr: Nguruwe 20 watazaa vitoto kama 160,utachakuwa vitoto jike 100,
mama zao wote watauzwa, huku shambani kwetu nguruwe
mkubwa ni Tsh 200,000 tu, utapata 4,000,000.

After 2yrs: Nguruwe 100 wanaweza kuzaa 700. Kati ya 700 chagua majike 500,(unaweza kuuza watoto dume ukanunua jike).

Year 3: Nguruwe 500 watazaa watoto 3500, chagua watoto 1500 tu
Kutoka hapo unamentein Number 1500, kila mwaka unaweza kuuza
watoto zaidi ya 3000, na nguruwe wakubwa 1500.
1500*200000= Tsh 300,000,000/= kwa mwaka
Nusu ya hiyo pesa ni gharama zingine, unabaki na 150mil.
Welcome to the club

Kabla hujajitumbukiza kaone mifano, au nenda sokoine ukaonane na wataalamu.

Kila mwaka nalima Mahindi, alizeti, maboga ekari 30 kwa ajili ya chakula cha nguruwe tu.

Nakupenda saana mpwa..









==========

USHUHUDA

======================================================
mkuu umeniinspire sana ,,lazima nijipange kufanya hii kitu
 
Kwa anayefahamu kuhusu nguruwe jike mwenye mimba anieleze sababu zinazopelekea nguruwe jike kuzaa watoto chini ya watano na tumbo bado kuonekana lina watoto ndani na zipi process inabidi zifwate.
 
Naamini wote mnaendelea vzuri na pia ambao hawajisikii vizuri Mungu awawekee mkono wake,,ndugu zangu mm nataka nianzee kufuga nguruwe na nna mtaji wa laki 800000.swali la kwanza je unatosha kwa gharama za kununulia piglets na gharama zote za vyakula?? Na pia gunia la pumba Na mashudu ntapata wap kwa bei ya chini na soko pia lamaana maana huwezi kufanya Biashara bila soko ,,,Nawatakia kheri ya Christmas na mwaka mpya (samahani kwa watu wa imani za kiislamu kwa hili)
 
Naamini wote mnaendelea vzuri na pia ambao hawajisikii vizuri Mungu awawekee mkono wake,,ndugu zangu mm nataka nianzee kufuga nguruwe na nna mtaji wa laki 800000.swali la kwanza je unatosha kwa gharama za kununulia piglets na gharama zote za vyakula?? Na pia gunia la pumba Na mashudu ntapata wap kwa bei ya chini na soko pia lamaana maana huwezi kufanya Biashara bila soko ,,,Nawatakia kheri ya Christmas na mwaka mpya (samahani kwa watu wa imani za kiislamu kwa hili)
 
Hiyo ni mradi mzuri cha msingi fanya utafiti wapi utapata mbegu nzuri za nguruwe wanao kua haraka na kula kidogo wasiliana na tapifa
 
==========

USHUHUDA

======================================================[/QUOTE]
Habari wanaJF
,
Tafadhali kwa wale wasiopenda jina hilo hapo juu samahani sana.

Mimi nimefuga nguruwe, nilianza nikiwa niko chuo kikuu mwaka wa pili pale UDSM kwa mtaji wa shilingi 500,000/=

Nilianza kujenga zizi kwa shilingi laki tatu tu na nikanunua makinda ya nguruwe mawili jike na dume kila mmoja sh. @40,000 (mradi niliufungua nyumbani mkoani Kigoma). Fedha zilizobakia nilitafuta mfanyakazi wa kuwalisha hao nguruwe. Nilimlipa sh. 40000 kwa mwezi. Kati ya laki 5, zilibaki 80,000 ambazo nilianza kwa kunulia chakula cha nguruwe.

Baada ya hapo nguruwe niliwapandisha wakazaa watoto 10. Kati ya hao madume yalikuwa 4 na jike 6. Baada ya hayo makinda kukua sikuuza makinda ya jike. niliamua kupanua mradi hivyo nilipanua zizi! Hapo ilikuwa baada ya miezi tisa tu.

Baada ya kupanua mradi niliuza madume 3 nikanunua vyakula (maharage yaliyooza na mashudu) ya kulishia nguruwe waliobakia.

Baada ya miezi 18 nguruwe waliongezeka baada ya kuzaa tena (yale majike 6 na dume 1). Nikaendelea kupanua zizi maana nilijikuta nina nguruwe 30. Kumbuka nguruwe sita wote walizaa. Mmoja makinda 6, mwingine 5, mwingine 5 mwingine 4 mwingine 7 na mwingine 2, na lile dume 1. Jumla nguruwe 30.

Nazidi kupanua mradi na chuo nimeshamaliza kwa sasa nasimamia mwenyewe!

Hakika kwa sasa mimi ni tajiri!

Amini usiamini mimi sio masikini tena!

siku njema.
Banda 300,000
Piglets 80,000
Mpagazi 40,000 per month
Umebaki na 80,000

Nguruwe ni atleast afikishe miezi 6 au 7 ili uweze kuuza na wewe umemnunua akiwa na miezi miwili so inakupa muda wa miezi 4 ili apandishwe na mimba ya nguruwe ni miezi 3 wiki3 na siku 3 pia usishau kuwa itabidi anyonyeshe kwa muda wa miezi miwili thus unahitaji kulisha nguruwe huyo jike kwa jumla ya miezi isiyopungua (4+4+2)=10.

Now kwa jike ni miezi 10 ina siku 300
Assume anakula kilo 2-3+maji+majani= Tzs. 600

Then gharama ya chakula ni 600x300= Tzs. 180,000
gharama ya mpagazi ni 20,000x10=Tzs.200,000
gharama ya dawa ni =Tzs. 50,000
Jumla 330,000 kwa jike NB: Bei ya kuuza jike ni 200,000- 300,000

kwa dume atahitaji miezi 4 hadi 5 toka uipo mnunua ambazo assume ni siku 130
Then
gharama ya chakula ni 600x130= Tzs. 78,000
gharama ya mpagazi ni 20,000x5= Tzs.100,000
gharama ya dawa ni = Tzs. 20,000
Jumla = 198,000 kwa dume remind you bei kuuza dume max, ni 200,000

Thus 528,000+420,000= 968,000.



Ushauri ni kwamba gharama za uendeshaji ni kubwa (528,000) kuliko hela uliyobaki nayo (80,000) tafuta njia za kupunguza gharama za uendeshaji wa mradi ili kuweza kupata faida. Pia mbegu nzuri ya nguruwe ndio issue.
Pia nguruwe wanavyozidi kuongezeka na gharama za uendeshi nazo huongezeka sambamba
 
1.mtaji
2.changamoto zake
3.profit and loss calculation
4.market
5.any other advice
Karibuni wajuzi
 
changamoto kubwaa ni garama ya chakula-hasa kama unafugia mjini,,
 
Kuhusu mtaji sifahamu sehemu kama dar kwa nguruwe mkubwa unaetaka kumkuza anauzwa sh ngapi kwa sababu hujaweka bayana kama unaanza na watoto au wakubwa wa kukuza haraka. ila kwa range ya watoto mpaka mkubwa sina uhakika kama itavuka hii range 60,000 - 230,000/= Tsh hapo ondoa gharama ya nyumba kabisa na usafiri na nyingine ndogondogo mpaka wanafika nyumbani.

Hakikisha utafute mbegu nzuri wale warefu kabisa japo wana gharama ila ukiweza kuwatunza watakulipa.

Changamoto zake
hawa wanyama wanakula sana narudia tena wanakula sana, kwa hiyo kama utaamua kuwalisha polard na mashudu ya alizeti peke yake utakula hasara sana. Inakubidi utafute mabaki ya vyakula na matunda mfano buguruni matunda ni mengi na masokoni kama unaweza upate cha kutosha wakaanga chips chukua mabaki ya maganda ya viazi. Pia unaweza kwenda pale kiwanda cha bia ukawaomba kimea cha bia maana wale huwa wanaenda kukitupa ni kizuri huwa wanakuwa haraka sana.Take it from me kama ukiwapunguzia chakula wakawa hawali na kushiba basi kuwa na uhakika watachelewa kukua watachelewa kukupa matokeo unayotaka. Magonjwa ni kawaida uwe karibu na daktari wa mifugo hapa hakuna gharama kubwa sana. Kikubwa zaidi ni gharama ya chakula.

Profit and loss calculation.
Kikubwa zaidi kila unapoenda kuchukua chakula cha nguruwe andika, usafiri n.k pesa inayotoka mfukoni weka pale na pia usiweke siku unazofanya kazi nao. nikisema nikuambie ni magunia mangapi watakula mpaka umeuza kweli hapo sijui. Kama wanakula vizuri miezi 8-9 unaweza kuuza. Tena sehemu kama dar unaweza kuchinja na kuuza kama nyama na utapata hela nzuri.

Market.
Kwa sehemu kama dar silijui soko lake sana ila ukienda maeneo ya tabata na kimara utakutana na sehemu nyingi sana wanauza kitimoto ya kupikwa hao wanaweza kuwa wateja wako.

hayo ndo nayoyajua kutokana na uzoefu wangu
 
Back
Top Bottom