Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Ufugaji wa samaki kama ilivyo shughuli nyingine yoyote ya kiuchumi inahitaji usimamizi mzuri ili uweze kuwa na faida. Mbali na hilo, mfugaji wa samaki anatakiwa kuzingatia vigezo vingi kabla ya kuanza ufugaji. Moja ya vigezo hivyo ni soko. Si jambo la busara kuanza shughuli yoyote kabla haujafanya uchunguzi na kujua kama kuna mahitaji ya bidhaa unayokusudia kuzalisha. Wafugaji wengi wameanzisha ufugaji wa samaki lakini wakaishia kupata hasara kutokana na ukosefu wa soko. Na wengine wameanguka kutokana na utunzaji mbovu wa mabwawa ya samaki.
-
*Maji*
Upatikanaji wa maji na ubora wake ni kigezo muhimu katika ufugaji wa samaki. Mtiririko wa maji ni njia rahisi kwa mfugaji. Maji machafu hayatakiwi kwa ufugaji wa samaki. Wafugaji ni lazima wasaidiwe na maafisa kilimo katika eneo lao kama maji yanayopatika yana ubora kwa ajili ya ufugaji wa samaki. Kwa wakazi wa Dar es Salaam, inawezekana pia kufuga samaki kwenye bwawa, endapo maji yana chumvi ya wastani, na kwa kiwango kinachoshauriwa kitaalamu, basi samaki wanaweza kustahimili, na kukua vizuri.
-
*Bwawa*
Bwawa la samaki linahitaji nafasi kubwa ya ardhi, yenye mwinuko pamoja na eneo la samaki kukimbilia. Hii ni njia rahisi ya ufugaji endapo ardhi na maji havina gharama kubwa. Eneo kubwa zaidi linaruhusu uzalishaji usiohitaji nguvu ya ziada na wenye tija.
-
Utengenezaji wa bwawa la samaki kwa maeneo yenye udongo wa kichanga kama Dar es Salaam, mfugaji atalazimika kuchimba na kuweka karatasi ya nailoni. Hii, itasaidia kuzuia upotevu wa maji pamoja na kuzuia bwawa kuporomoka.
-
Ni vyema upande mmoja wa bwawa ukawa na kina kirefu kuliko mwingine. Upande mmoja unaweza kuwa na kina cha mita moja na nusu, na mwingine mita moja. Hii itamsaidia mfugaji kuweza kulihudumia bwawa vizuri, hata kama ni kuingia na kufanya usafi.
-
*Utunzaji wa bwawa*
Inashauriwa kufanyia bwawa usafi mara kwa mara, hasa kwa kuondoa majani ili kuepusha wadudu kufanya makazi na hatimaye wakawadhuru samaki. Pia ukiacha mimea bwawani itatumia virutubisho kwa kiasi kikubwa na kuondoa hewa ya oxijeni.
Hivyo, kila unapoona uchafu, safisha mara moja.
-
*Ulishaji*
Wafugaji walio wengi, wamekuwa hawazingatii kanuni za ulishaji wa samaki. Kwa kawaida inatakiwa kuwalisha samaki mara mbili hadi mara tatu kwa siku.
-
*Aina ya chakula*
Samaki wanaweza kulishwa kwa kutumia pumba ya mahindi, mashudu ya pamba na alizeti, soya, mabaki ya dagaa. Haishauriwi kulisha chakula kilichoko kwenye mfumo wa vumbi, bali kiwe mabonge madogo madogo, kwa wastani wa tambi.
-
*Magonjwa*
Kwa kawaida samaki hawana magonjwa mengi sana yanayowashambulia, ila kuna baadhi ya yaliyozoeleka kama vile magonjwa ya ukungu (fangasi), magonjwa yatokanayo na virusi, pamoja na minyoo.
-
Samaki wanaposhambuliwa na fangasi, huonekana kwa macho kwa kuwa huwa na madoa madoa. Samaki aina ya kambale hushambuliwa zaidi kuliko perege.
-
Pia unaweza kutambua kuwa samaki ni mgonjwa kwa kuwa huzubaa sehemu moja kwa muda mrefu. Magonjwa kwa samaki pia yanaweza kutokana na mrundikano kwenye bwawa. Hivyo, ni muhimu kuwapunguza kila wanapoongezeka.
-
*Tiba*
Tiba iliyozoeleka kwa samaki ni kwa kuweka chumvi kwenye maji, kasha kuwatumbukiza samaki unaowaona kuwa ni wagonjwa, kisha kuwatoa na
kuwarudisha bwawani.
-
*Upatikanaji*

Unaweza kupata vifaranga wa samaki kutoka katika kituo cha kuzalisha na kufuga samaki Kingolwira Morogoro. Bei ya kifaranga cha Perege ni shilingi 50, na Kambale ni shilingi 150.....
 

Umejitaid kutoa maelezo ila ayajajitosheleza.
 
suala kwamba chakula kisichokuwa ktk pellets format kinaisha au kuoza sio issue kwani unashauriwa kuweka mara tatu kwa siku cha kuwatosha muda huo tu na pia unachagua eneo maalum la kusimama na kuwamwagia.

Kwa maelezo yako kilo kumi kwa siku utazigawa mara tatu na kuwamwagia wanakula chote.
 
Habari.

Kupitia jukwaa hili tumekua tukijifunza vitu tofouti juu ya namna ya kujiendeleza kiuchumi ili kujikwamua kutoka katika hali tulizonazo. shukrani kwa wale walionitafuta na wakapata ushauri, nadhani bado tupo pamoja na mtafanikiwa.

Bado nasisitiza uchaguaji wa eneo na uchimbaji wa bwawa unahitajika umakini kwani ndipo ambapo utakua unafanya mladi hivo ikiwa kama initial stage ,inabidi umakini,hivo ujumuisha, uwepo wa maji safi kwa kiasi kikubwa, na uwezekeno wa kupata chakula cha samaki wako.

Mahitaji ni makubwa kulinganisha na wataalamu tuliopo, ivo tuendelee kuwasiliana kwa ajili ya kupeana ujuzi na ushauri, fuga samaki mana ni biashara inayolipa sana. kwa maelezo zaid wasiliana nami 0717451771.
 
Kumekua na shida jinsi ya kuchimba mambwa ya samaki na ufugaji wake kwa ujumla,,hivyo kama unaitaji hiyo project wasiliana nami,0717451771
 
Samaki mpaka anavunwa, sema miezi 3; gharama zake ni kiasi gani na wanakuwa na uzito kiasi gani?
 
Nitakutafuta kwa maelezo ya ziada ila bajeti ya project hiyo ni sh ngapi?
 
Pia kwa wafugaji wa samaki waliopo DSM mkihitaji chakula cha samaki, kinapatikana maeneo ya karibu na mlimani city. Ukihitaji naweza kukuelekeza kwa kiwango unachohitaji.
 
Kumekua na uhangaiko wa wataalamu wa maswala ya ufugaj wa samaki...na kilimo cha majini kwa ujumla..hivo kama una mradi wako au unamfahamu mtu mwenye mradi au anaehitaji kuanzisha mradi basi anitafute...tunaweza kusaidiana kwa gharama nafuu tuu.071745771 .
 
mimi ni mfugaji samaki ili akue anaitaji maji safi na chakula bora nakalibisha maswali
 
Unahitaji bwawa la ukubwa gani kwa ajili ya samaki ili upate faida nzuri na lichukue angalau samaki wangapi?

Linaweza gharimu kiasi gani kulitengeneza? Na linatengenezwaje hilo bwawa la samaki.

Linaweza chukua samaki wangapi?

Hadi samaki kukomaa wanahitaji muda gani?

Malisho ya samaki unayapata wapi? Na yanagharimu kiasi gani?

Kuna madawa utahitaji wakati wa kuwatunza samaki? Kuna magonjwa ya samaki?

Maji gani unatakiwa utumie kwa samaki? Ya bomba au kisima yanafaaa?

Unatakiwa uwe unabadilisha maji? Kama unatakiwa kila baada ya muda gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…