Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Tembelea Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) hapo Morogoro hakika utapata shule ya uhakika, hasa ukimpata Dr. Mnembuka hakika utapapenda!
 
Mbona sasa unatapatapa,, povu jiiingi utafikri umefungiwa omo mdomoni? Haya mambo ya picha za Ulaya ndizo zinaingiza watu mkenge. Watu waliaminishwa kwa picha kuhusu green house lakini ukija kwenye uhalisia inakuwa tofauti na walivyokuwa wanaona.

Sasa na wewe unatuwekea hydroponic za kwenye mitandao tukueleweje sasa? SUA kwenyewe hizo hazipo na wewe unakuja kutupigisha story hapa!!

Labda hii kitu aje aitetee mwalimu wako Mnembuka au Lamtane ndo kidogo tutawasikiliza, wewe bado mchanga sana nenda kwanza field ukapige kazi upate uzoefu siyo utaalam wa kutumia rejea za kwenye mtandao!!
 
wafundishe yote ila kwa kua hauwauzii Vifaranga .ntawauzia Mimi.Kambale na sato
 
Wadau hebu tujuzane kwa mjadala, ni maeneo gani bei ya samaki iko juu zaidi hapa tanzania?
Hasa kwa samaki aina ya sato na sangara?
 
Inawezekana pia, au waweza chimba kibwawa chako ukubwa unaotaka, badala ya kusakafia unatumia zile plastic liner ili kutoruhusu maji kunyonywa na udongo. Hizi karatasi za plastic waweza zipata kwa urahisi zipo maduka mengi mjini
Naomba kujua namna ya kuonganisha hizi plastic liner katika bwawa iwapo unahitaji mbili ili ziweze kutosha bwawa.

Cellotape haishiki
 
Habari za asubuhi mabibi na mabwana.
Ningependa kufahamu kutoka kwa wale wenye ujuzi zaidi.

Nina bwawa la samaki ambalo ninatala kuweka plastic liner kuzuia maji yasinyonywe na udongo.

Plastic liner zilizopo hazina upana wa kutosha kuweza kutosha bwawa lote.

Je ni mbinu gani nnaweza kutumia?


Nimejaribu kutumia Cellotape lakini haikai hata. Inaachia.

Nimeangalia mtandaoni nimeona kuna machine zinaitwa 'Thermofusion plastic welder' kwa ajili ya kuunganisha hizi plastic liner. Je zinapatikana kweli kwa hapa Tanzania?
 
Nimesikia ufugaji wa Samaki kwa kutumia bwawa dogo la plastiki nyumbani ni mkombozi tosha wa Maisha. Nahitaji msaada wenu wadau. Je bwawa hilo la plastic liwe na vipimo gani? Hayo maplastic yanauzwa bei gani?
Ulifanikiwa mkuu?
 
Inawezekana pia, au waweza chimba kibwawa chako ukubwa unaotaka, badala ya kusakafia unatumia zile plastic liner ili kutoruhusu maji kunyonywa na udongo. Hizi karatasi za plastic waweza zipata kwa urahisi zipo maduka mengi mjini
Zinaunganishwa vipi?
 
Liner ni nzuri sana katika mabwawa kwani hupunguza upotevu wa maji katika mabwawa ,huwa zipo zenye thickness ya 0.5 mm na 1mm,liner huuzwa kwa square meter ,Liner huunganishwa kwa mashine maalum kama blower,extrusion machine na plastic welder na pia machine hizi zipo na kusema ununue kwa ajili ya kuunganishia liner kwa bwawa lako tu ni hasara maana machine hizi huuzwa ghali sana hasa hiyo extrusion machine, sisi tunajishughulisha na kudisign,kuchimba na ku install dam liners na machine zote pia tunazo pamoja na extrusion material.

Pia tuna design na kufunga irrigation system, tunatengeneza greenhouses pamoja na kuuza vifaranga vya kambale (African catfish fingerlings) na Tunapatikana Arusha...kwa mawasiliano tupigie 0752022108
 
Mimi nipo Dar.
Sijui kama mtaweza kutika Arusha hadi Dar kwa ajili ya kuunganisha liner tu

Bwawa limeshachimbwa.

Liner zimeshanunuliwa tayari.

Shida ni kuziunganisha
 
Nani wanauza portable fish tanks?

Nahitaji lenye eneo 50 m2 na kuendelea. Naomba unitumie bei yake hapa
 
kwa wale wanao hitaji huduma ya
kuchimbiwa mabwawa
kujengewa ya sement
kuwekewa yale movable
mantank
huduma zetu ni nafuu sana pia kutafutiwa wanunuzi wa samaki tuwasliane pm(kwa wa kazi wa dar) nitatoa no.
Matank portable bei gani kwa ukubwa gani?
 
Mimi nipo Dar.
Sijui kama mtaweza kutika Arusha hadi Dar kwa ajili ya kuunganisha liner tu

Bwawa limeshachimbwa.

Liner zimeshanunuliwa tayari.

Shida ni kuziunganisha
Toa 200k nimtume kijana aje Na mashine site chap 0763347985
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…