Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Hy
Naomba mwenye kujua kuhusu ufugaji wa samaki anisaidie. Nina sato 400 wanakaa kwenye bwawa kubwa na kuna kisima nlikuwa na kambale 100 ila wamekufa nimebakia na 10 hii ni ndani ya mwezi. Maji yao yanakuwa meusi na kunuka sana kila baada ya siku 3 baada ya kubadilisha.

1.Je naweza kuwachanganya sato na kambale nataka kuchukua vifaranga vya kambale?

2. Zile mashine za kuingiza hewa kwenye bwawa zinaitwaje na gharama zake au kama kuna njia nyingine naomba kujuzwa?

3. Chakula gani niwape hawa kambale maana nlikuwa nawapa chakula sawa na sato ila ndio hivyo hawakukaa hata mwezi.
Asanten
 
Da pole sana, wasiliana na JKT Mgulani watakusaidia, kama uko Dar
 
Wakuu,

Mabwawa ambayo ni movable yanaweza kuwana ukubwa wa kiasi gani? Hakuna limit? Pia naomba kujua watengenezaji wenye bei nzuri kwa dar es salaam
 
Kambale ni bottom feeder tofauti na sato wao ni surface feeder, kwaio ukiwa unalisha hakikisha unatumia chakula ambacho kitazama chini ili kambale waweze hula mfano ukiwa unawalisha walishe pellets ziwe na uwezo wa kuzama chini na sio chakula cha powder form ambacho kinaelea juu, pia unaweza kuwachanganya sato na kambale hii system inaitwa polyculture lakin kambale anakula sato kwaio tegemea idadi ya sato kwenye bwawa kupungua tofauti na hivi unaweza kutengeneza Earthen pond kwa ajili ya kufuga hao kambale, mashine za oxygen zinaitwa Aerators machine ila gharama yake siifahamu.

Note: Chakula ulichokuwa unawalisha kimesababisha maji kunuka kwa sababu kilikuwa hakiliki na hao kambale ikapelekea maji kuwa machafu ambapo ikapelekea dissolved water oxygen kuwa ndogo, kambale ni wavumilivu wa oxygen kuliko sato ndomana wana uwezo wa kukaa kwenye matope kwa muda.
 
Chakula gani kingine kinweza kuwafaa maana huwa nawpa uduvi na mavi ya ng'ombe mabichi na samaki wenyewe ni kambare
 
Yes

_@@@-------------@@-----------@@@
""In life its important to know when to stop urging with people and simply let them be Wrong""
 
nawazaga kuandaa project ya ufugaji wa hawa samaki ila sina elimu juu ya samaki kwa ujumla. ila natamani kuwafuga tena kwa wingi japo nasikia wana cost mtaji mkubwa ila huwa sijali nisha wekaga malengo

mwenye elmu ya kutosha juu ya ufugaji anaweza kuja pm akanisaidia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nawasalimu wote humu, natafuta ushauri mzuri wa jinsi ya kufuga Samaki kwa kutumia vyakula vya asili.

Tafadhali nisaidieni Mimi nipo Arusha
 
Nawasalimu wote humu, natafuta ushauri mzuri wa jinsi ya kufuga Samaki kwa kutumia vyakula vya asili.

Tafadhali nisaidieni Mimi nipo Arusha
naona wadau labda watakuja ila jaribu kupitia posts za nyuma kuhusu samaki waweza pata kitu
 
Kwa mujibu wa Mhadhiri Mwandamizi kutoka Idara ya Sayansi ya Wanyama ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUAambaye pia ni mtaalamu wa lishe ya samaki na uzalishaji Dr. Berno Mnembuka, ili kujua aina za vyakula vya samaki ni lazima mfugaji ajue tabia za ulaji wa samaki, tabia hizo zipo katika makundi 3.

Kundi la kwanza ni samaki wanaokula nyama, hili ni kundi linalonufaika na vyakula vilivyo na asili ya nyama, mfano wa samaki waliopo kwenye kundi hili ni pamoja na sangara na kambale.

Kundi la pili ni samaki wanaokula mimea vipando kwa mfano samaki aina ya ‘carps’. Kundi hili la samaki ustawi wake hutegemea vyakula vilivyo na asili ya mimea vipando kwa maana ya masalia ya mabaki ya mazao ya mashambani na mazao ya bustani.

Kundi la tatu ni samaki wanaokula vyakula mchanganyiko kama perege, sato na mwatiko (samaki wa maji chumvi). Kundi hili la samaki hutegemea zaidi upatikanaji wa vyakula vyenye asili ya nyama na mimea.

Baada ya kuyaangalia makundi hayo matatu ya tabia za ulaji wa samaki, sasa tuangalie aina za vyakula vya samaki. Kuna aina mbalimbali za vyakula vya samaki kama anavyotueleza mtaalamu wa lishe ya samaki na uzalishaji Dr. Mnembuka.

Aina ya kwanza ya chakula cha samaki ni mabaki ya nafaka ambayo yanahusisha pumba za mahindi, ngano na mpunga. Hapa mtaalamu huyu anawataka wafugaji kuchukua tahadhari pindi wanapotumia pumba za kununua kwa sababu wakati mwingine pumba zinazotokana na nafaka hizo huwa na dawa(sumu ya kuulia wadudu) ambayo iliwekwa wakati nafaka hizo zinahifadhiwa, dawa hizo zinaweza kuleta madhara kwa samaki hivyo cha msingi ni mfugaji kuwa na chanzo cha uhakika cha kupata pumba hizo.

Aina nyingine za vyakula vya samaki ni pamoja na dagaa, damu iliyokaushwa, unga wa mifupa, machicha ya pombe, mboga mboga (kama vile tembele, mchicha na kabichi), matunda (kama maembe na ndizi zilizoiva sana), chumvi na chokaa.

Ili mfugaji aweze kujua namna ya kuchanganya vyakula hivyo hana budi kuwasiliana na wataalamu kwa kuwa mchanganyiko wa vyakula hivyo unategemea aina ya samaki, umri wake na hali yake kwa mfano samaki mzazi mahitaji yake ni tofauti na samaki wengine.

Muongozo wa mahitaji ya viinilishe vya samaki

Kwa ujumla samaki huhitaji viini lishe vile vile ambavyo wanahitaji wanyama wengine, viini lishe hivyo ni protini, wanga, mafuta, madini na vitamini. Mpaka sasa kuna aina 210 za samaki wafugwao ambapo kwa mujibu wa Dr. Berno Mnembuka,Mhadhiri Mwandamizi kutoka Idara ya Sayansi ya Wanyama SUA, muongozo wa kutayarisha vyakula vya samaki hao ni lazima uzingatie viwango vifuatavyo;

(i) Vyakula vyenye asili ya wanga viwe kati ya wastani wa asilimia 20 hadi asilimia 25

(ii) Vyakula vyenye mafuta viwe kati ya wastani wa asilimia 10 hadi asilimia 15

(iii) Vyakula vyenye vitamin viwe kati ya wastani wa asilimia 1 hadi asilimia 2

(iv) Vyakula vyenye madini viwe kati ya wastani wa asilimia 1 hadi asilimia 2

(v) Maji – hapa ifahamike kuwa wakati tunazunguzia viwango vya maji vinavyohitajika kwa wanyama wengine wafugwao, hitaji la maji kwa samaki ni ubora wa maji anayofugiwa na sio wingi wake.
 
Wadau nimefurahi Sana kupata maelezo ya ufugaji WA samaki. Maana nataka kuanza kufuga Ila naomba msaada Wa kujua gharama za uchimbaji mabwawa na masiliano tafadhali

Kuna seminar itatolewa tarehe 10/09/2018 up to 22/09/2018




Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Wadau nimefurahi Sana kupata maelezo ya ufugaji WA samaki. Maana nataka kuanza kufuga Ila naomba msaada Wa kujua gharama za uchimbaji mabwawa na masiliano tafadhali

Kuna document natamani nikuwekee hapa ila nashindwa kuattach!



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom