Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

inasemekana kuwa vijana wenye hasira kali walimtandika vibao Marine Hassan Marine baada ya kuona kusikia kuwa TBC wamekatisha kurusha mkutano.Nilikuwa jukwaani hivyo sikuona tukio hili.
 
Ingalikuwa vyema iwapo Chadema itakuwa imenunua muda kwa hivi vituo vyetu vya TV kwa ajili ya sisi tuliokuwa mbali kushuhudia tukio hilo muhimu. Ila sidhani kama kuna Kituo cha TV kitadiriki kurusha matangazo hayo jinsi walivyo waoga!

tbc walikuwa wanarusha bana ila huku kwetu umeme ulikuwa umekatika nikawa nasikiliza kwenye redio ya simu alipoanza kuonge mabere arando wakakatisha matangazo kwasababu za kiufundi ila wali inyima mengi nilipokatiza maeneo ya tauni nikakuta watu wanaendelea kuangalia kwenye tv wakati huo mkuu wa anga ya saba alikuwa anaongea
 
inasemekana kuwa vijana wenye hasira kali walimtandika vibao Marine Hassan Marine baada ya kuona kusikia kuwa TBC wamekatisha kurusha mkutano.Nilikuwa jukwaani hivyo sikuona tukio hili.

Asantea Regia.

Vyovyote ilivyokuwa message imewafikia wahusika. na ufasadi aliousema Marando sasa ni black and white.

Tunasubiri ama wampeleke mahakamani ama watoe maelezo ya kutosha juu ya tuhuma nzito kama hizi za kutingisha dunia.
 
Kikwete anaposema atawalipa fidia walioathirika na machimbo, mbona hujauliza atafanyaje ili kulipa fidia hiyo? na ahadi nyingi alizozitoa. Tatizo ukishakuwa shabiki wa CCM hata akili ya kufikiri huna. Mimi niliye wahi kufanya kazi serikalini katika position ya juu ninakubaliana kabisa na silaa kwamba kupunguza wizara kutaokoa fedha nyingi sana. wewe pengine uelewi.
Ni sehemu ya walafi wale wale ambaye anaona kitumbua kinaondoka
 
TBC news ..saaa mbili:

Tido Muhando anakubali kuwa ni kweli kuwa ni wao waliokata matangazo

WHY?

...eti kulikuwa na matusi ya nguo....

.... Wanasema inawezekana siku zijazo watashindwa kurusha matangazo ya kampeni za CHADEMA...

.... anaogea na vituvingine visivyoeleweka... lakini kwlei wameigwaya CHADEMA...
 
Dr. Slaa na CHADEMA hongera sana kwa uzinduzi wa kampeni yenu.

Ila tu hizo siku 100 utafanya mangapi? Kwa kutumia pesa zipi? Kwa kutumia sheria zipi? Kwa kushiriiana na watu gani? Wanasiasa acheni kutudanganya Watanzania.

Itafaa CCM wakidondoshwa ili tujipange upya lakini ahadi zote hizo ni utapeli wa kisiasa tu. Hata kubadili katiba tu itatuchukua zaidi ya mwaka.

vitu ambavyo dr slaa atavifanya kwa siku zake 100 za kwanza haviitaji pesa za wahisani au nini, vinahitaji nia na maamuzi....
2010 hatudanganyiki......
 
Wewe...wewe...Superman sasa unataka sifa :becky: yaani unaanza kuandika fasta zaidi ya ninavyoweza kusoma...duuh, wee mtu nuksi kichizi, una vigurudumu nini kwenye vidole vyako?? lol :smile-big:

Superman, Superman, Superman, Superman, Superman OOOyeeeeah!! Live Event Reporter Of The Year (LEROTY) !!!!! Come to think of it, an award could be in the making... lol

huyo ni Superman
 
Huyu mgombea udiwani 'anaetafutwa' tukimwona tuwajulishe polisi au?
 
TBC news ..saaa mbili:

Tido Muhando anakubali kuwa ni kweli kuwa ni wao waliokata matangazo

WHY?

...eti kulikuwa na matusi ya nguo....

.... Wanasema inawezekana siku zijazo watashindwa kurusha matangazo ya kampeni za CHADEMA...

.... anaogea na vituvingine visivyoeleweka... lakini kwlei wameigwaya CHADEMA...
pale mkutanoni tuliambiwa ni itilafu ya mitambo, sasa hivi kwenye taarifa tido anasema kwa ajili ya lugha chafu
alikata pale marando alipokuwa anataka kuanika kila kitu, kwa nini hawakukata wakati ambapo wanasema palikuwa na matusi.
safari watake wasitake mabadiliko yatatokea tuuuu
 
Tunawashukuru wote walioshiriki kutuletea matangazo haya moja kwa moja toka Jangwani. Tunaomba moyo huu uendelee, na mabadiliko ya kweli yaja Tanzania kama kila mmoja wetu atajisikia kuguswa na udhalimu tuliotendewa kwa miaka yote hii toka Uhuru, tuikomboe nchi yetu kutoka mikononi mwa walioteka hatutaki kulipa ransom, ni kura yako na ya jirani zako, ndugu zako na rafiki zako!
Hongera Superman, tunaomba walioweza kuchukua clips watuwekee!!
 
nimeisoma ilani ya chadema na mwanzoni kabisa nimeanza kuona tatizo lile lile ambalo chadema wanasema wanapingana nalo.longolongo na kutoweka jambo wazi kwa mapana yake.sehemu iliyoanza kunipa mashaka kabla hata sijafika mbali ni hii:

ufisadi ni nini?

tunapozungumzia ufisadi tunazungumzia mfumo na muundo wa utawala ambao umetengeneza utamaduni wa kuishi kiujanja ujanja, matumizi mabaya ya madaraka na vyeo, ufujaji wa mali ya umma, wizi wa fedha za umma, utaratibu wa kubebana na ajira zinazotegemea kujuana, na mahusiano ya watawala na watawaliwa ambayo msingi wake ni woga, vitisho, na kujiona watu wanastahili zaidi kuliko wengine. Ni mfumo uliodidimiza tawala mbalimbali duniani na ambao pasipo kuushughulikia kwa makusudi unasimama kama tishio lilopo na la hatari kwa tanzania kuliko vita. Baba wa taifa mwalimu julius nyerere alisema kuwa "ufisadi na rushwa ni adui mkubwa zaidi wa maslahi ya wananchi wakati wa amani kuliko vita" (bungeni, mei 17, 1960, kikao cha 35 cha bajeti).

ufisadi ndio kizuizi kikubwa cha kuboresha maisha ya watu wetu; ni kikwazo kikubwa katika kujenga na kuimarisha utawala bora, utawala wa sheria na haki za raia. Ufisadi ndio kikwazo kikubwa kabisa cha maendeleo ya nchi. Ndio kusema, juhudi zetu za kujiletea maendeleo kama nchi haziwezi kufanikiwa bila kwanza kukomesha ufisadi.

tumekuwa na miaka takribani 50 ya ccm. Wameahidi kila aina ya ahadi na wamefanya kila makosa, lakini tukawavumilia na tukawapa nafasi nyingine tukiamini kwamba mambo yatabadilika. Kila tulipowapa nafasi, hali ilizidi kuwa mbaya, tukasogea kutoka kubaya kwenda kubaya zaidi. Lengo lao kubwa limekuwa ni kushinda uchaguzi, ili waendelee kutumia madaraka tunayowapa kwa ajili ya kujinufaisha kwa njia ya ufisadi.

ni wakati wa mabadiliko, na fursa ya kufanya mabadiliko ni huu uchaguzi wa 2010 na siyo 2015. Tukisubiri wakati mwingine tutakuwa tumechelewa sana. Na tukiwapa nafasi nyingine moja ccm ya kututawala tena tutakuwa tumewapa leseni ya kuendelea kutawala wapendavyo na tutakuwa tumejihukumu sisi wenyewe na uzao wetu katika maisha ya umaskini wa kudumu.
katika sehemu hiyo ni wazi kuwa chadema wanataka umma uamini kwamba matatizo yote tuliyo nayo yanatoka na utawala!

Wanataka tuamini hata wale watu wanaotumia vyandarua kufugia kuku badala ya kujikinga na malaria kuwa ni tatizo la watawala.

Wanataka tuamini kuwa serikali inawafuatilia wakwepa kodi sugu kuwa ni unyanyasaji simply kwa sababu jk kapita mahali basi hata kama tra walitaka kudai kodi basi wasidai tena.

Wanataka tuamini hata kushindwa kwetu kuweka akiba na kujaa kwenye sehemu za starehe siku za kazi,kuchangia mambo ya burudani zaidi kuliko elimu na maendeleo yote hayo kuwa ni tatizo la serikali!!!!!

Ilani haisemi kwamba hakuna chama kinachoweza kuwaondolea watu umasikini kwa asilimia mia. Natumaini chadema watajipanga zaidi miaka ijayo kuelezea wananchi kwamba elimu ya kujitambua binafsi ni muhimu sana kabla ya lolote.on top of that chadema inasema kwamba 2010 ndo wakati muafaka!!!

What are the justifications kwa hili??u mean 2010 ndo chadema imeona nchi inaporomoka au ni ile "i wana be the boss too"!!!

Mungu ibariki tanzania.

pole mzee
 
pale mkutanoni tuliambiwa ni itilafu ya mitambo, sasa hivi kwenye taarifa tido anasema kwa ajili ya lugha chafu
alikata pale marando alipokuwa anataka kuanika kila kitu, kwa nini hawakukata wakati ambapo wanasema palikuwa na matusi.
safari watake wasitake mabadiliko yatatokea tuuuu

Nilikuwa nimesahau.
Shirika la habari la taifa linadanganya umma! Kwa nini walisema ni mitambo hapo uwanjani kama kweli walikatisha kwa haki si wangesema tunakatisha matangazo kutokana na matumizi ya lugha chafu?

Walijua reaction ya wananchi ingekuwaje
 
nilikuwa nimesahau.
Shirika la habari la taifa linadanganya umma! Kwa nini walisema ni mitambo hapo uwanjani kama kweli walikatisha kwa haki si wangesema tunakatisha matangazo kutokana na matumizi ya lugha chafu?

Walijua reaction ya wananchi ingekuwaje


guilds!

Kifo cha nyani miti huteleza
 
Huyu mtu anaitwa michuzi (MZEE WA LIBENEKE) anazidi kujipotezea umaarufu kwa kutumia blogu yake kuipigia kampeni CCM tu kila kukicha utadhani hakuna vyama vingine!!!. Nilitegemea basi hata aweka japo ka habari kamoja ka CHADEMA leo, lakini badala yake anapiga mapicha ya CCM na akina Mama Rwakatare(maombi ya Kampeni),. Chakusikitisha kote ughaibuni anakoenda anaendela kujifagilia kuwa yeye ndie mwenye "blogu ya jamii"" inayowapasha wanatanzania wote habari bila upendeleo.. Inasikitisha kwa msomi kuwa "bias".

UNCLE MICHUZI Kama hujui mkuu unapoteza, jaribu kwenda na wakati wa kutofungamana na upande wowote, vinginevyo utapoteza wasomaji wa blogu yako kwa itikadi zako za upendeleo, ana utajikuta huna nyimbo pale ambapo wapinzani watachukua inchi !!!. Kama hulipwi na CCM katika safari zako au kuihudumia blogu yako, tafadhari toa nafasi sawa kwa vyama vyote kaka kwani ni vya watanzania!!!
 
uzuri wa SIASA siku zote mtu yoyote anaweza ongea chochote kama MC. Ni wajibu wa kila mmoja kivyakevyake kutafuta kilichojiri.

Huyu jamaa amemwaga upupu hapa Jangwani leo lakini hakuna hata sehemu moja alikoelezea jinsi gani;

1. Atakavyo-badilisha mikataba ya madini iliyopo na kwa kutumia sheria ipi? Hii Uranium au reserves mpya za madini yeye anataka kufanyaje tofauti na wengine wote Duniani wanavyofanya?
2. Namna gani serikali yake ya mawaziri 20 itaweza ku-run bila kuongeza kurugenzi na taasisi zaidi ambazo ni gharama zaidi. Angekuwa muwazi angetuambia hao mawaziri watakuwa zizara gani na namna gani taasisi za serikali zitakuwa zinaendeshwa na hao mawaziri 20.
3. Jinsi gani na kwa namna gani anaweza badilisha hali ya wafanyakazi wa TZ kwa siku 100? Aeleze mkakati ulivyo na si kutifuka tifuka. je hali ya wakulima itakuwaje?

Hata hivyo, kuna elements za idea nzuri ambazo CCM tutazitumia baada ya kuapishwa Novermber 5. Mojawapo hii ya watu kutojua katiba na kudhibiti zaidi wimbi la ujambazi. CCM itahakikisha inaweka sawa sawa mambo yote katika miaka mitano ijayo.

Kidumu chama. Idumu CCM hapa JF

idiota
 
uzuri wa SIASA siku zote mtu yoyote anaweza ongea chochote kama MC. Ni wajibu wa kila mmoja kivyakevyake kutafuta kilichojiri.

Huyu jamaa amemwaga upupu hapa Jangwani leo lakini hakuna hata sehemu moja alikoelezea jinsi gani;

1. Atakavyo-badilisha mikataba ya madini iliyopo na kwa kutumia sheria ipi? Hii Uranium au reserves mpya za madini yeye anataka kufanyaje tofauti na wengine wote Duniani wanavyofanya?
2. Namna gani serikali yake ya mawaziri 20 itaweza ku-run bila kuongeza kurugenzi na taasisi zaidi ambazo ni gharama zaidi. Angekuwa muwazi angetuambia hao mawaziri watakuwa zizara gani na namna gani taasisi za serikali zitakuwa zinaendeshwa na hao mawaziri 20.
3. Jinsi gani na kwa namna gani anaweza badilisha hali ya wafanyakazi wa TZ kwa siku 100? Aeleze mkakati ulivyo na si kutifuka tifuka. je hali ya wakulima itakuwaje?

Hata hivyo, kuna elements za idea nzuri ambazo CCM tutazitumia baada ya kuapishwa Novermber 5. Mojawapo hii ya watu kutojua katiba na kudhibiti zaidi wimbi la ujambazi. CCM itahakikisha inaweka sawa sawa mambo yote katika miaka mitano ijayo.

Kidumu chama. Idumu CCM hapa JF

.
Kifilie mbali chama cha majambazi.
Unataka darasa la namna ambavyo chadema itafanya kazi na mawaziri 20, na jinsi ya kuzigeuza hali za wafanyakazi kwa siku 100, na mengineyo mengi? Basi njoo chadema usomeshwe ukiwa umetulia chamani.
 
Nimeisoma ilani ya Chadema na mwanzoni kabisa nimeanza kuona tatizo lile lile ambalo Chadema wanasema wanapingana nalo.Longolongo na kutoweka jambo wazi kwa mapana yake.Sehemu iliyoanza kunipa mashaka kabla hata sijafika mbali ni hii:

Ufisadi ni nini?

Tunapozungumzia Ufisadi tunazungumzia mfumo na muundo wa utawala ambao umetengeneza utamaduni wa kuishi kiujanja ujanja, matumizi mabaya ya madaraka na vyeo, ufujaji wa mali ya umma, wizi wa fedha za umma, utaratibu wa kubebana na ajira zinazotegemea kujuana, na mahusiano ya watawala na watawaliwa ambayo msingi wake ni woga, vitisho, na kujiona watu wanastahili zaidi kuliko wengine. Ni mfumo uliodidimiza tawala mbalimbali duniani na ambao pasipo kuushughulikia kwa makusudi unasimama kama tishio lilopo na la hatari kwa Tanzania kuliko vita. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema kuwa "ufisadi na rushwa ni adui mkubwa zaidi wa maslahi ya wananchi wakati wa amani kuliko vita" (Bungeni, Mei 17, 1960, kikao cha 35 cha bajeti).

Ufisadi ndio kizuizi kikubwa cha kuboresha maisha ya watu wetu; ni kikwazo kikubwa katika kujenga na kuimarisha utawala bora, utawala wa sheria na haki za raia. Ufisadi ndio kikwazo kikubwa kabisa cha maendeleo ya nchi. Ndio kusema, juhudi zetu za kujiletea maendeleo kama nchi haziwezi kufanikiwa bila kwanza kukomesha ufisadi.

Tumekuwa na miaka takribani 50 ya CCM. Wameahidi kila aina ya ahadi na wamefanya kila makosa, lakini tukawavumilia na tukawapa nafasi nyingine tukiamini kwamba mambo yatabadilika. Kila tulipowapa nafasi, hali ilizidi kuwa mbaya, tukasogea kutoka kubaya kwenda kubaya zaidi. Lengo lao kubwa limekuwa ni kushinda uchaguzi, ili waendelee kutumia madaraka tunayowapa kwa ajili ya kujinufaisha kwa njia ya ufisadi.

Ni wakati wa mabadiliko, na fursa ya kufanya mabadiliko ni huu uchaguzi wa 2010 na siyo 2015. Tukisubiri wakati mwingine tutakuwa tumechelewa sana. Na tukiwapa nafasi nyingine moja CCM ya kututawala tena tutakuwa tumewapa leseni ya kuendelea kutawala wapendavyo na tutakuwa tumejihukumu sisi wenyewe na uzao wetu katika maisha ya umaskini wa kudumu.
Katika sehemu hiyo ni wazi kuwa Chadema wanataka umma uamini kwamba matatizo yote tuliyo nayo yanatoka na utawala!

Wanataka tuamini hata wale watu wanaotumia vyandarua kufugia kuku badala ya kujikinga na malaria kuwa ni tatizo la watawala.

Wanataka tuamini kuwa serikali inawafuatilia wakwepa kodi sugu kuwa ni unyanyasaji simply kwa sababu JK kapita mahali basi hata kama TRA walitaka kudai kodi basi wasidai tena.

Wanataka tuamini hata kushindwa kwetu kuweka akiba na kujaa kwenye sehemu za starehe siku za kazi,kuchangia mambo ya burudani zaidi kuliko elimu na maendeleo yote hayo kuwa ni tatizo la serikali!!!!!

Ilani haisemi kwamba hakuna chama kinachoweza kuwaondolea watu umasikini kwa asilimia mia. Natumaini Chadema watajipanga zaidi miaka ijayo kuelezea wananchi kwamba elimu ya kujitambua binafsi ni muhimu sana kabla ya lolote.On top of that Chadema inasema kwamba 2010 ndo wakati muafaka!!!

What are the justifications kwa hili??U mean 2010 ndo Chadema imeona nchi inaporomoka au ni ile "I wana be the boss too"!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Hivi watanzania mnataka Tanzania ya namna gani? Mbona nchi hii imeshiriki kwenye ukombozi wa nchi jirani lakini kujikomboa bado ni kitendawili? Unapokuwa na mawazo ya kupinga watu wenye mtazamo mbadala (CHADEMA) basi wewe una mawazo mgando. Hebu tuachilie mbali na Ilani ya CHADEMA, na tuzingatie nchi hii, kwa miaka mitano iliyopita, chini ya utawala huu imevuna mambo mangapi?
  • Umaskini unaoongezeka kwa kasi, kuliko Rwanda na Burundi ambao nusu ya wananchi waliteketea
  • Viongozi ambao hata kujua kuwa wako pale sababu ya wapiga kura ni sawa na kuandika Thesis ya PhD
  • Hadhi ya Elimu imekuwa ikishuka kila idadi ya shule/vyuo zinapoongezeka
  • Watawala hawana cha kuwaeleza wapiga kura, bali kutumia takwimu zisizo sahihi, au zisizoendana na hali halisi
  • Mifumuko ya bei na kuporomoka kwa shilingi, inahusishwa na vigezo(indicators) visivyostahili
  • Tofauti za kidini kuonekana ni tija, kuliko maendeleo na umoja wa kitaifa
Nchi hii imegubikwa ulemavu wa kifikra zaidi kuliko ulemavu wa kimwili, na kama kizazi kipya kinaendana na hiyo syndrome basi tumekwisha, na sitashangaa kwa sababu, watawala wanageuza uongozi wa nchi kuwa wa kurithishana na sio wa kuchaguliwa kidemokrasia. Tukae chonjo saa mbaya, fanya maamuzi sahihi.
 
Back
Top Bottom