Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

hahaaa kimya tunaomba data watu wa chadema
 
just a piece of advice bana Padri... hebu tumegee kidogo basi yaliyojiri maana si wote tulipata kuona hiyo shughuli

Thanks for this mkuu...

BTW, Hivi ina maana hakuwa na points za kuongelea hadi akumbushwe?
 
Angekuwa hana point mngehujumu hotuba yake?

Hivi kwa busara zako,tatizo la Tanzania yetu sasa lipo kwenye uchumi au ufisadi kwenye uchumi?

By the way,acha kutuzuga.Wenye taaluma ya habari wamebainisha vizuri alichosema Rais Mtarajiwa .Angalia hapa


Slaa's top six agenda

BY POLYCARP MACHIRA
29th August 2010

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) launched its election campaign yesterday, by outlining six top areas on which it would address attention, pledging to deal with pending grand corruption cases within 100 days.

However, the campaign speech by the party's presidential contest flag bearer, Dr Wilbrod Slaa, couldn't be televised live by the State broadcaster, as the latter claimed that the opposition leaders used insulting and abusive language against the government as well as top leaders of the ruling Chama Cha Mapinduzi.

Dr Slaa told mammoth rally attendants at the Jangwani grounds in Dar es Salam that his party plans to restore the lost national glory the country enjoyed during the era of founding president Julius Nyerere.

Improved better education for all Tanzanians tops the aspiring president's agenda. He said his government will make high school education compulsory and free for all students.

Provision of better health facilities and improvement of agriculture are among the projected ambitions, accusing the current government of failing to effect significant changes in the sectors
.

On agriculture, specifically, he said a Chadema-led government would go beyond the power tillers that the current government emphasises, and focus on better tractors that can enhance production.

"Tanzania is losing political, social and economic direction as days go by. This started immediately after the two fathers of the nation, Mzee Nyerere and his successor, Ali Hassan Mwinyi stepped, aside. It is now time to liberate the country through our manifesto," he said.

The outgoing Karatu MP also promised that his party will build a strong economy that provides for the needs of Tanzanians, aiming at moving the country towards tertiary industry to support agriculture.

He lamented that the country had become a dumping ground for foreign companies where cotton is grown locally but the final products are exported from overseas countries. Tanzania, according to the Chadema manifesto, will be a heavy industrialisation point for Africa.

His fifth agenda would be to create more employment opportunities to meet the increased job demand . Dr Slaa blamed the government for failure to provide better jobs for graduates from the universities and other learning institutions.

"University graduates are jobless but the CCM government brags of creating 1,300 jobs in five years, including those of street water vendors. There is need to ensure that educated youths get the right jobs that match their education, " he stressed.

His top last agenda would be to sports, culture and arts as another way of boosting youths in the country, saying artists in the country need government support. On this, he said he would not opt for a foreign coach for the national team but provide training for local coaches to take such opportunities.

Dr Slaa also said he will trim the cabinet from the current 40 plus ministers to less than 20. Comparatively, he said it is quite ridiculous for a country like Tanzania with a population of 40 million people to have 40 ministers while the US with over 100 million people has less than 14 ministers.

He promised that his government would do away with district commissioners and assign the current office bearers other posts.

Other promises include establishment of subway trains by 2020 and liberate the country from a poor transport system that he said retarded national development. He added that workers' problems will be solved within 100 days in office.

He praised former CCM MPs who defected to Chadema, saying they have finally seen the light and joined the ‘commanders' of change in the war to liberate the nation from corrupt a government.

Dr Slaa's running mate, Said Mzee Said, told the gathering that their government will create three governments. There would be governments of Zanzibar, Tanganyika and the union government, saying by so doing; the current contentious matters of the union will be solved.

He said "Let us come together and vote Dr Slaa to State House to bring about the long-awaited changes," he said, adding that by voting yes to his party, all problems of the union will find lasting solutions rather than forming interim governments.

On his part, Party Chairman, Freeman Mbowe, said Chadema is like Real Madrid under the tutorship of Jose Mourinho. "Chadema just liked Real Madrid Football Club collects all talented leaders in the country," he remarked.

He said the party was keen to work in partnership with a serious party on this road to save the nation from what he described as the hands of a few individuals who do not have the nation at heart.

Meanwhile, a prominent Dar es Salaam lawyer and opposition activist Mabere Nyaucho Marando yesterday issued unproved damning attacks about what really transpired during the Central Bank of Tanzania's External Payments Arrears $131million loot(Sh200 billion).

Though the authenticity of his allegations could not be established beyond reasonable doubt, they revive sharp memories on how taxpayers' billions were looted during the third phase regime.

Marando who is among early reformers during the introduction of the multiparty system in 1990s told the campaign rally at Jangwani grounds that the popular ‘EPA scam' was a special project initiated to support election campaign by some of the ruling party leaders.

According to Marando, a former spy turned politician, contrary to what the public was told earlier, EPA was a well calculated move to raise billions of shillings using some vetted businesspeople between July and October 2005.

Marando was reacting to recent media reports, which claimed that he wasn't the right man to fight corruption because he is currently defence counsel of Jeetu Patel who is one of those accused of looting EPA billions through the Bank of Tanzania.

Marando made very damning attacks about the key individuals behind the scam before the public broadcaster, TBC1, suspended its live coverage of Chadema's official campaign rally in Dar es Salaam yesterday.

According to Marando, though the government has arrested and charged some suspects in connection to the EPA loot, the truth about what had happened was beyond what the public was told.

Marando claimed that he has official documents signed by some top party officials instructing the BoT to release the payments as agreed.

EPA was one of the scandals that rocked the fourth phase government, forcing it to award an international auditing firm, Ernst and Young in 2007 to audit the Bank of Tanzania.

Ernst and Young in its auditing revealed how a total of the 22 companies looted $131 million using fake and forged documents under the supervision of the former governor, the late Daudi Balali.

Of those involved, 13 local companies got Sh90, 359,078,804 using forged documents during the 2005/6 financial year. The report also showed that nine unregistered companies were irregularly paid Sh42 billion.

SOURCE: GUARDIAN ON SUNDAY

Sasa uchumi gani unaozungumzia mwenzetu? Tatizo lenu mmeajiriwa kumwaga sumu pasipo maandalizi. Manataka kuzungumzia mambo ambayo hamna idea nayo kabisa.

Shame on you!
 
Kama ule umati wa jana unaitwa "kufunika" na "Jangwani kufurika" basi huo ni ushahidi tosha kuwa hao wanaoripoti hizi habari ni wageni wa mikutano ya kisiasa hapo Jangwani.

Umati wa jana pale Jangwani hauna tofauti na ule wa CUF aliokusanyika kule Kidongo Chekundu juzi. Tofauti ni kuwa CUF hawakujisifia na huo umati kwani walijua kuwa ule umati uliojitokeza kumsindikiza Prof. Lipumba kurudisha fomu ofisi za NEC ulikuwa mara tano mkubwa kuliko huo uliokuwa wakati wa kuzindua kampeni.
 
Muda ulikuwa mchache. Hebu tutafute manifesto yao tuiweke hadharani kisha tuijadili.

Kuna Chadem wengi hapa. TUWEKEENI MANIFESTO YENU TUICHAMBUE.
 
Tatizo ni kukumbushwa sio kuongea, alikazania mahakama ya kisutu, Ruge na Ufisadi

huyo kwani ni malaika, akumbuke kila kitu?, Afterall Tanzania hakuna tatizo la uchumi, kuna rasilimali za kutosha kwa kila mtanzania kuwa na maisha bora, TATIZO NI UFISADI NA UBINAFSI, HAO WANAOCHOTA UCHUMI NA KUWEKA NJE NDIO WA KUWAZUNGUMZIA HAO,

CHA MUHIMU ALIKUMBUSHWA NA AKA-AKASEMA WAZIWAZI, SASA TATIZO LIKO WAPI?
 
Huyu mwanzilishi wa threads hii ni mwongo sana, mimi nimesikiliza hotuba yote. Nilipata hasira sana baada ya kuona hotuba inakatishwa bila saba ya msingi na kuanza kutuwekea ndombolo. John Shibuda alimpa kikaratasi akimweleza kwamba hajataja suala la KILIMO. Katika maaelezo yake akasema kwamba hakutaka kutaja kilimo kama issue moja kwani alipozungumzia uchumi na suala la KILIMOliko humo humo. Padri anataka kuhalalisha negative reaction aliyonayo kwa chaema tu.
 
msisahau wananchi kwa maelefu waliojaa pale jangwani na kufurika ......umati ule ni mkubwa sana...wote wamekuja kwa nauli zao ...wala hawajalipwa pesa .....zaidi ..wamekuja kuchangia pesa ...na hata uchangamfu uliokuwapo ni mkubwa sana....huwezo kulinganisha na umati wa kukodiwa wa ccm....hata kura zao ni za kununua....wao walitumia mamilioni kuwalipa wananchi waliohudhuria pale pesa ...[kama hukupata kwamdai balozi wako ].....walipeleka mabasi kila kata ....na magari mengine kubeba watu.......ukipanda unapewa kifuta jasho .....ie elfu mbili na fulana .......ndio maana watu waliohudhuria mkutano wa ccm walikuwa hawajachangamka kabisa.......hata pamoja na kuwa na bendi na wasanii wa bongo fleva kama 50 .....mood was too dull..

Ukiongeza na tukio la "aiseee" ndio basi tena,wakawa kama wako msibani,na kila mtu aliondoka na njia yake,pole ni kwa wale walioletwa na mabasi/Fuso ambao walitegemea kurudishwa,ilikula kwao.
 
Tuko pamoja Mkuu. asanteni wote.

Regia pia ameonyesha ushirikiano mkubwa sana. Anastahili pongezi.

Mkuu Invisible, in case kutahitajika Video Camera aanytime, na mimi pia naungana na Indume, naweza kutoa yangu pia.

Naamini sana JF inafanya kazi yake vema kipindi hiki.
Mimi pia nitachangia,sitaki habari za kuchakachuliwa na akina Marin Hassan,matokeo yake wanaishia kupata vipigo lol!
 
Wera wera weraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa Ubungo Letu Ukuuu wa nchi wetu majimbo asilimia 51% yetu sasa mnaaka nini tena wera wera weraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa:welcome😀r.Slaa kwenye Kiti cha ukuu wa Nchi(Urais)
 
Nimeisoma ilani ya Chadema na mwanzoni kabisa nimeanza kuona tatizo lile lile ambalo Chadema wanasema wanapingana nalo.Longolongo na kutoweka jambo wazi kwa mapana yake.Sehemu iliyoanza kunipa mashaka kabla hata sijafika mbali ni hii:

Ufisadi ni nini?

Tunapozungumzia Ufisadi tunazungumzia mfumo na muundo wa utawala ambao umetengeneza utamaduni wa kuishi kiujanja ujanja, matumizi mabaya ya madaraka na vyeo, ufujaji wa mali ya umma, wizi wa fedha za umma, utaratibu wa kubebana na ajira zinazotegemea kujuana, na mahusiano ya watawala na watawaliwa ambayo msingi wake ni woga, vitisho, na kujiona watu wanastahili zaidi kuliko wengine. Ni mfumo uliodidimiza tawala mbalimbali duniani na ambao pasipo kuushughulikia kwa makusudi unasimama kama tishio lilopo na la hatari kwa Tanzania kuliko vita. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema kuwa "ufisadi na rushwa ni adui mkubwa zaidi wa maslahi ya wananchi wakati wa amani kuliko vita" (Bungeni, Mei 17, 1960, kikao cha 35 cha bajeti).

Ufisadi ndio kizuizi kikubwa cha kuboresha maisha ya watu wetu; ni kikwazo kikubwa katika kujenga na kuimarisha utawala bora, utawala wa sheria na haki za raia. Ufisadi ndio kikwazo kikubwa kabisa cha maendeleo ya nchi. Ndio kusema, juhudi zetu za kujiletea maendeleo kama nchi haziwezi kufanikiwa bila kwanza kukomesha ufisadi.

Tumekuwa na miaka takribani 50 ya CCM. Wameahidi kila aina ya ahadi na wamefanya kila makosa, lakini tukawavumilia na tukawapa nafasi nyingine tukiamini kwamba mambo yatabadilika. Kila tulipowapa nafasi, hali ilizidi kuwa mbaya, tukasogea kutoka kubaya kwenda kubaya zaidi. Lengo lao kubwa limekuwa ni kushinda uchaguzi, ili waendelee kutumia madaraka tunayowapa kwa ajili ya kujinufaisha kwa njia ya ufisadi.

Ni wakati wa mabadiliko, na fursa ya kufanya mabadiliko ni huu uchaguzi wa 2010 na siyo 2015. Tukisubiri wakati mwingine tutakuwa tumechelewa sana. Na tukiwapa nafasi nyingine moja CCM ya kututawala tena tutakuwa tumewapa leseni ya kuendelea kutawala wapendavyo na tutakuwa tumejihukumu sisi wenyewe na uzao wetu katika maisha ya umaskini wa kudumu.
Katika sehemu hiyo ni wazi kuwa Chadema wanataka umma uamini kwamba matatizo yote tuliyo nayo yanatoka na utawala!

Wanataka tuamini hata wale watu wanaotumia vyandarua kufugia kuku badala ya kujikinga na malaria kuwa ni tatizo la watawala.

Wanataka tuamini kuwa serikali inawafuatilia wakwepa kodi sugu kuwa ni unyanyasaji simply kwa sababu JK kapita mahali basi hata kama TRA walitaka kudai kodi basi wasidai tena.

Wanataka tuamini hata kushindwa kwetu kuweka akiba na kujaa kwenye sehemu za starehe siku za kazi,kuchangia mambo ya burudani zaidi kuliko elimu na maendeleo yote hayo kuwa ni tatizo la serikali!!!!!

Ilani haisemi kwamba hakuna chama kinachoweza kuwaondolea watu umasikini kwa asilimia mia. Natumaini Chadema watajipanga zaidi miaka ijayo kuelezea wananchi kwamba elimu ya kujitambua binafsi ni muhimu sana kabla ya lolote.On top of that Chadema inasema kwamba 2010 ndo wakati muafaka!!!

What are the justifications kwa hili??U mean 2010 ndo Chadema imeona nchi inaporomoka au ni ile "I wana be the boss too"!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Chadema wanasema kitu cha kwanza kubadilisha ni mfumo mbovu wa utawala (bad governance)unaowafanya viongozi wasiwajibike pale wanapopaswa. Ukimweka malaika kwenye mfumo mbovu wa utawala atakuwa malaika mbaya pia. Lakini ukiweka mfumo mzuri wa uwajibikaji hata 'vuvuzela' atawajibika.

Mind you, sera siyo kila kitu ni dira inayoelekeza wapi chama fulani kinapoelekeza nguvu zake na baada ya hapo kutafuata marekebisho ya sheria ili viongozi waweze kuwajibika kwa kiwango cha hali ya juu. Mfumo uliopo sasa hivi haumfanyi kiongozi awajibike kwa wananchi bali wananchi wawajibike kwake.

Pili, Chadema inajinadi kuwa ina mkakati wa kuwarudisha Watanzania kwenye maadili. Sasa hivi Watanzania wanaabudu pesa na siyo utu. Ukiwa na pesa unaweza kufanya kila kitu: unaweza kumlipa mtu amvue mtu usiyempenda, unaweza kuagiza bidhaa feki nje na kuja kuwauzia wananchi (bila kujali madhara kwa afya zao), unaweza kununua vyeti na kuonekana una elimu nzuri na unafaa kupewa wadhifa fulani, nk.

Ni wazi kuwa Watanzania tulio wengi tunajisikia vizuri tukibaki ndani ya mfumo wa sisiemu unaoruhusu wenye nacho kuwa nacho na wasio kuwa nacho kuendelea kuahidiwa maisha mema huku wakilia na kusaga meno. Kuna wakati Mwalimu Julius Nyerere alitoa hotuba yake kwa maskitiko sana. Alisema ni wazi kwamba serikali ya wamu ya kwanza imefanya madudu mengi na mazuri pia. Yale mazuri yangeendelezwa na mabaya yakaachwa lakini cha kushangaza, alisisitiza, hayo mabaya ndiyo yanayokumbatiwa na mazuri yanaachwa mfano maadili ya viongozi yameachwa.

Binafsi kwa sasa vyama vya siasa vinajinadi kwa sera zao na baadhi ya watu wanadhihaki sera za vyama vingine wakisema watafanya nini. Bila kuwapa baadhi ya wanasiasa wapya fursa ya kuongoza ni wazi hatutajua uwezo wao. Lakini je, nani alijua uwezo wa Ali Hassan Mwinyi, nani alujua uwezo wa William Mkapa? Nani alijua uwezo wa Jakaya Kikwete? Na ni kiongozi yupi atakaa madarakani karne zote?

Nashauri sisi Watanzania tumeona uwezo wa wanasisiemu na udhaifu wao. Tujaribu pia kuona uwezo wa wanasiasa kutoka vyama vyama vingine na hasa tuchague watu wenye sifa bila kujali mtu huyo anatoka chama gani. Tukifanya hivyo, in the long run tutakuwa na idadi ya kutosha ya viongozi wema na hao wataunda serikali ya watu wema - wawajibikaji. Tatizo kubwa liko kwetu sisi wapiga kura kwa vile tunapigia chama kura na siyo viongozi wenye sifa.
 
Mimi ni fuasi wa Chadema ila kwa hili wameniacha hoi kwa kweli. Sina hamu!!!!!!!!
 
King ebu nyosha maelezo u mean mpaka apo Jangwani hamna mawasiliano,wamekata umeme.
Ebu fafanua pls.
CCM mwaka huu imekula kwao.
Amenifurahisha Marando kuwa vyombo vya habari kesho wasije sema Makani ameanguka kam Kikwete,wajue fika Makani ana 80 something na JK is only 57 so ni kama first born wake
Wameshasema mbona. Kwami watachelewa. Mfa maji hukamata hata nyasi!!
 
MwanaHaki, ni vizuri kwenye UKWELI kutoongopa, haisaidii kitu kuongopa. Naijua vizuri familia ya kina Halima Mdee, Halima ni MKRISTO, kama alivyo Baba na Mama yake, bali ndugu wengi wa Baba yake ni WAISLAMU. Nikija kwa Anna Komu, alikuwa anaitwa Maulidah kabla ya kubadili dini na kuwa Mkristo. Hivyo Halima Mdee na Maulidah Anna Komu wote ni Wakristo.

Ukiwa katika haki uongo wa nini?.
Hebu rudi kwenye shimo ulilotokea haraka!
 
Kushiri SASA kuna Njoia Nne:
1. Muda wa Kutoa Sadaka kwenye Mikutano yote - Sadaka ya Ukombozi
2. Accounti 2 za Benki : CRDB Bank: CHADEMA M4C (Sadaka zinakusanywa)
A/c 01J1080100600; NMB: A/C CHADEMA: No. 2266600140
IBAN/SWIFT codes kwa waliopo nje ya nchi tafadhali.
 
Katika uzinduzi wa kampeni za chadema jana nilishangazwa na tukio la mgombea urais wa chadema kusahau kuzungumzia uchumi wa taifa. Ambapo ndio kitu muhimu sana. Yeye alijikita na habari za ruge na house of talent, badala ya kujadili issue za kitaifa. Wao ugomvi wa watu wawili wameufanya ndio sera za chama. Akajikita na uendeshaji wa kesi mahakama ya kisutu.

Kama chama chadema kingezungumzia suala za uendeshaji kesi zote yaani mfumo wa sheria nchini, sio kujadili kesi moja au mbili za mahakama ya Kisutu.

Slaa ameshindwa kusema kuwa JK amechagua majaji wangapi kurahisisha mfumo wa sheria.

Nilivunjwa mbavu pale John Shibuda alipompelekea desa bwana slaa kuwa mzee umesahau kuzungumzia uchumi. Slaa kwa ufahamu wake mdogo akatamka hadharani akisema 'nakushukuru ndugu yangu Shibuda kwa kuniletea karatasi kunikumbusha nizungumzie uchumi"

Chama makini kingezungumzia uchumi kutokana na mambo kadhaa yaliyojiri hivi karibuni dunian na hapa nchini mambo kama credit crunch na mengi ya mfano huo. Riba na uchumi wa nchi. Yeye alikuwa busy kuzungumzia neno moja tu ufisadi.

Sasa kama shibuda angekuwa hayupo jana ingekuwaje? Hilo ndio tatizo la chama kuwa na watu wenye elimu ya darasa la saba na kidato cha nne kama mbowe na mgombea mwenza wa Slaa.

Mgombea mwenza angekuwa msomi au mwenye uelewa angemsaidia Slaa.

Chadema mshukuruni sana Shibuda kafanya kazi nzuri ingawa hamkumpa nafasi ya kuzungumza.

huu nao ni upupu mwingine. Mbona watu mnakuwa na mawazo mepesi na kunukuu vitu hafifu hivyo? Mbona haukuendeleza nukuu ya slaa? Wengine msitafute sifa kujaza jukwaa tu
 
Kama ule umati wa jana unaitwa "kufunika" na "Jangwani kufurika" basi huo ni ushahidi tosha kuwa hao wanaoripoti hizi habari ni wageni wa mikutano ya kisiasa hapo Jangwani.

Umati wa jana pale Jangwani hauna tofauti na ule wa CUF aliokusanyika kule Kidongo Chekundu juzi. Tofauti ni kuwa CUF hawakujisifia na huo umati kwani walijua kuwa ule umati uliojitokeza kumsindikiza Prof. Lipumba kurudisha fomu ofisi za NEC ulikuwa mara tano mkubwa kuliko huo uliokuwa wakati wa kuzindua kampeni.

He he heee! Hii nayo. Mko wengi maji ya shingo.
 
Back
Top Bottom