Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Ufunuo usiosemwa: Je, Lilith ndio nyoka wa Eden? Je, ni mke wa kwanza wa Adam?

Nilirejea kuisoma Mwanzo sura 1:26ff na 2 (nzima) na kubaini jambo ambalo limenipa kuuliza swali kwa mleta uzi huu kwamba kama mke 'wa awali' wa Adam alikuwa ni Lilith (Is. 34:14) ni vigezo gani vimetolewa kudhibitisha hilo beyond doubt?
 
Nilirejea kuisoma Mwanzo sura 1:26ff na 2 (nzima) na kubaini jambo ambalo limenipa kuuliza swali kwa mleta uzi huu kwamba kama mke 'wa awali' wa Adam alikuwa ni Lilith (Is. 34:14) ni vigezo gani vimetolewa kudhibitisha hilo beyond doubt?
Na mimi niko kwenye hilo hojaji lakini kuepuka marudio naomba usome replies za zitto junior zina ufafanuzi mzuri sana
 
Na mimi niko kwenye hilo hojaji lakini kuepuka marudio naomba usome replies za zitto junior zina ufafanuzi mzuri sana
Nimemsoma na tangu Mwanzo wa Uzi huu hata sasa sijaacha kitu hata dot; hata inputs za Zitto jnr nimezihifadhi kabisa; ila bado hajadadavua vya kutosha.

Kwa mfano, ktk Mwanzo 1:27-30 Biblia inazungumzia uumbwaji wa me & ke na umilikishwaji wa raslimali zote; lkn ktk Mwanzo 2:7 tunaona Bwana ANAMFANYA mtu!

Je, na huyo wa mwanzoni kwenye Mwanzo 1:27 ndio nani?
 
Hapa kwenye huu mstari ulio unukuu kilichokuwa kinaongelewa ni ugumu wa mioyo ya hao walio kuwa Kapranaum. Kuwa pamoja na miujiza yote na mambo makuu ya Mungu bado hawakuamini. Miujiza hiyo ingefanyika hata sodoma na gomora wangali badili mioyo ya iliyojaa kutenda uovu na dhambi wakamgeukia Mungu.


Kwa staili hii hautawahi ongeza maarifa.... unaposema ni uongo mbona Yesu anaitambua embu soma hapa

Matthew 11:23
"And you, Capernaum, will not be exalted to heaven, will you? You will descend to Hades; for if the miracles had occurred in Sodom which occurred in you, it would have remained to this day.

Na kuna mistari mingine 10 inamtaja huyo hades mtoto wa cronus ambaye alifungwa Tertullus huko chini ya dunia mpaka leo ssa unaposema ni uongo tukueleweje ilihali Yesu alimtambua?? Bado kusahau Matendo 14 utaona zeus na hermes hawa wanatajwa..... Je unaposema ni uongo kivp watambulike na paulo na barnaba???

Mkuu panua ufaham kejeli hazisaidii





Kwanza hakuna upotoshaji maana lilith kajadiliwa na maprofessor wengi tu na kwa ushahidi wa ancient sumerian texts ndio maana hata kwenye biblia ametajwa...... Kwahiyo anajadili kitu ambacho kipo sio stori za mdomoni kma popobawa!!!

Kingine unadai mwanadamu hawezi kuficha jambo ambalo Mungu anataka lijulikane?? Je unajua mangapi kwenye historia ya imani tumefichwa hata kma ni kwa nia njema

1. Maisha ya Yesu kwenye biblia yapo 10% pekee ila ujana wake wote na maisha binafsi haupo katika biblia hii ya kiprotestant ila vitabu vilvyoandika maisha ya Yesu in details vilitolewa unajua na nani na kwanni??

2. Kuna kitabu kimejadili masuala kabla dunia haijaumbwa wala kuwepo ila kilitolewa je unajua kwanni na nani alikitoa?? Je mshana jr akisema kuna vitu tumefichwa utakataa

3. Hivi unajua paulo aliandika nyaraka takribani 60 ila biblia unayotumia ina barua zake 21 pekee!! Unajua lini zilitolewa na kwanni???

Dah ni mengi mkuu tumefichwa ni vzuri ufanye utafiti kuliko kumkejeli mtoa mada ambaye ana nia nzuri ya kutufikirisha
 
Soma Biblia yako vizuri sababu ya Yakobo kupewa jina la Israel iko wazi. Soma pia maongezi ya wale Abraham na wale watu watatu anapo wasihi. Mwanzo 18:3. Watu watatu anawambiaje "Bwana wangu"? Si ange wa ambia bwana zangu.

Mwanzo 18:9 Wakamwambia...
Mwanzo 18:10 Akamwambia... Ukitulia na kutafakari haya maongezi na majibizano utaona ni Mungu katika zile nafsi zake tatu abawasiliana na Ibrahim.


Kwahiyo aliyepigana na Yakobo hakuwa malaika???

Kwahiyo waliokula kwa abraham walikuwa sio malaika??

Nachouliza kma malaika waliweza fanya yote ya mwilini kwanni huamini anaweza lala na mwanamke na kupata mtoto???
 
Kwa lugha yako hii ni ngumu kujadiliana.. Na huna kifua cha mijadala mizito kama huu

Hamna mjadala mzito hapa ila niufinyu wa akili zenu za kibinadamu ambazo mwafikiri kwa kuzitumia hizo bila kuomba msaada wa Mungu mtayaelewa Maandiko Matakatifu bila kuyapotosha.
 
Tanua fikra usiwe kama pakacha unameza tu bila kuchuja ukiambiwa ukweli utakuweka huru tafuta ukweli sio kuamini tu unachohubiriwa jiongezee

Wewe msukule wa shetani utanishauri nini? Maana umepita darja la kuwa mfuasi wa ibilisi wewe ni msukule wa shetani.
 
Hamna mjadala mzito hapa ila niufinyu wa akili zenu za kibinadamu ambazo mwafikiri kwa kuzitumia hizo bila kuomba msaada wa Mungu mtayaelewa Maandiko Matakatifu bila kuyapotosha.
Okay sawa asante kwa kushiriki mjadala... Kwangu mimi kila mchango ni somo bila kujali kama una mtazamo hasi au chanya
 
Soma Biblia yako vizuri sababu ya Yakobo kupewa jina la Israel iko wazi. Soma pia maongezi ya wale Abraham na wale watu watatu anapo wasihi. Mwanzo 18:3. Watu watatu anawambiaje "Bwana wangu"? Si ange wa ambia bwana zangu.

Mwanzo 18:9 Wakamwambia...
Mwanzo 18:10 Akamwambia... Ukitulia na kutafakari haya maongezi na majibizano utaona ni Mungu katika zile nafsi zake tatu abawasiliana na Ibrahim.
MWANZO 19
1 Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi.
2 Akasema, Bwana zangu, karibuni nawasihi mwingie nyumbani mwa mtumwa wenu, mkalale, mkanawe miguu yenu, hata asubuhi mwondoke na mapema mkaende zenu. Wakasema, Sivyo, lakini tutakaa uwanjani usiku kucha.
3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala


Mkuu ukifuatilia mistari hii utagundua malaika walimtembelea lutu na waliweza kufanya mambo yote wanayofanya binadamu

Walikula walikunywa walitaka kulala na walioga pia ssa najiuliza kma walikuwa na ubavu wa kufanya mambo yote ya mwilini kwanni huamini kwamba walikuwa na uwezo wa kufanya ngono???

Kwanni mengine waweze ngono washindwe embu tuanzie hapo
 
Hapa kwenye huu mstari ulio unukuu kilichokuwa kinaongelewa ni ugumu wa mioyo ya hao walio kuwa Kapranaum. Kuwa pamoja na miujiza yote na mambo makuu ya Mungu bado hawakuamini. Miujiza hiyo ingefanyika hata sodoma na gomora wangali badili mioyo ya iliyojaa kutenda uovu na dhambi wakamgeukia Mungu.
Wewe ulisema greek mythology ni stori za kufikirika hiyo mistari inamtaja zeus hades na Hermes sasa ndio nakuuliza kma Yesu aliwataja hao Miungu wa kigiriki kwanni wwe unasema ni story za kufikirika?? Je nikuamini wwe au Yesu
 
Okay sawa asante kwa kushiriki mjadala... Kwangu mimi kila mchango ni somo bila kujali kama una mtazamo hasi au chanya
Mkuu mshana jr we ni mmoja wa viungo muhimu sana huku jukwaa la intelligence kwa thread zako zenye madini.... Huyo hayuko tayari kujifunza ila asikuvunje moyo maana tulio wengi tunakusupport
 
Maelezo marefu eti unajenga hoja. Kabla ya kufanya hivyo unge jiuliza maswali haya, wanyama si nyama na mifupa,? Je nyama na mifupa yao ilitoka kwa Adam? Haikudhaniwa wangempa kampani Adam? Lengo hilo lilifanikiwa/lilitimia? nk nk.


Labda mimi sijui sana kiswahili fasaha kama maprofeseri wa kiswahili but na uhakika mtu anaposema SASA anamaanisha hicho anachokiongela alishakiona kingine kama hiko kabla na ndio maana anatumia neno Sasa kutofautisha....huwezi tumia neno sasa kwa kitu ambacho hujawahi ona Wanyama ni tofauti na Mwanamke hawafanani hata chembe na adam hakiwahi hata kuwa na wazo wala ndoto akiwaza picha ya mwanamke...
Plus pia anamdadavua huyo mwanamke kuwa huyu ni nyama wa nyama yangu[emoji53][emoji53][emoji53] swali jingine hilo......Kama huyo ni nyama kutoka kwake Je kuna ambaye hakuwa wa Nyama yake[emoji53][emoji53][emoji53]????
Bado kuna viulizo hapo
 
Wewe ulisema greek mythology ni stori za kufikirika hiyo mistari inamtaja zeus hades na Hermes sasa ndio nakuuliza kma Yesu aliwataja hao Miungu wa kigiriki kwanni wwe unasema ni story za kufikirika?? Je nikuamini wwe au Yesu

Niangalie tena vizuri, utakuwa umenifananisha.
 
Mkuu mshana jr we ni mmoja wa viungo muhimu sana huku jukwaa la intelligence kwa thread zako zenye madini.... Huyo hayuko tayari kujifunza ila asikuvunje moyo maana tulio wengi tunakusupport
[emoji120] [emoji120] [emoji120] am humbled.. Nimekualika tayari kwenye mada ya laana naye namualika. Tujifunze pamoja
 
Nilirejea kuisoma Mwanzo sura 1:26ff na 2 (nzima) na kubaini jambo ambalo limenipa kuuliza swali kwa mleta uzi huu kwamba kama mke 'wa awali' wa Adam alikuwa ni Lilith (Is. 34:14) ni vigezo gani vimetolewa kudhibitisha hilo beyond doubt?
Mkuu TRIPLE H hakuna mstari direct kwenye biblia unathibitisha kuwa lilith alikuwa ndie mke wa adam kabla ya Hawa ila nje ya biblia zaidi ya jamii nyingi za kale zilitambua uwepo wa Lilith kuanzia Egyptians Assyrians greeks mpaka sumerians bila kusahau babylon wote wanaitambua hii stori na imeandikwa kwenye vitabu vyao vingi ila kwenye biblia kama nilivyoeleza hapo mwanzoni wanaipa hoja yao mashiko kupitia kulinganisha mwanzo 1 na mwanzo 2

Hivyo basi kwa kuwa wana conclude mwanamke aliyetajwa mwanzo moja ni tofauti na mwanzo 2 basi inatoa fursa kwa hoja ya kwamba lilith kweli alikuwepo Eden sababu kuna ka upenyo kameachwa apo

Na mstari wenyewe ni hapa tu

22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu BWANA Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.

23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume


Hivyo kwa hitimisho lao ni kwamba kama lilith asingetajwa popote basi wasingediriki kusema mwanzo 1 na 2 zinaongelea wanawake 2 tofauti.... Ila kwakuwa kuna story ya jamii karibu zote za mashariki ya kati kuwa lilith alikuwepo eden afu muda huo huo biblia imeacha huo mwanya hivyo walioanzisha nadharia hii wameishia KUCONNECT dots kuwa lilith existed

Cjui inaeleweka ama bado
 
Back
Top Bottom