KWA mujibu wa Kitabu cha ZUGRIL GALAYO (Nguvu Iliyodunu Katika Jadi)
Mtu wa Kwanza Alitambulika kwa Majina yaliyotokana na mazingira na jambo lililomuhusu katika kuishi kwake.
1. FUMBA KASA - lilipatikana ktk kipindi cha kukusanywa kwake.
2. SABKORODAMS - lilipatikan alivyoanza kula
3. MID ERA - Alivyoanza kuvaa nguo (kujisitiri)
4. MUNDU - Alivyoanza kuwa na Lugha
5. ZUNDRAGA - Alivyoanza kufanya matembezi
6.MASON KWATA - Alivyopata jinsia ya pili iliyotokana na yeye
7. ABE EI - alipoanza kuzaa na kulea
8. ESTONE - Alipoanza ujenzi wa vitu
GOWESHAN - Alipanza kuweka hifadhi kwa ajili ya familia yake
9. MTALAY - wakati anaacha wosia kwa watoo wake.
ALIUMBWAJE SASA!!?
Mtu huyu aliumbwa kwa mkusanyiko wa vumbi kutoka mabara saba lillokusanyika katika eneo la SHANKOMBOLUZU Ambalo leo hi linatambulika kama URUSI.
Aliumbwa akiwa na urefu wa Km Nne (4) upana wa kifua Mita mia tatu akiwa na rangi nyeusi na mwenye asili ya Nywele Ngumu zisimamazo kwa umbile lake.
NAWAOMBENI MKITAFUTE HIKI KITABU SANA SANA SANA MAANA NDANI YAKE KINAMUELEEZEA HADI ADAM ALIVYOKUJA KUPATIKANA NA HAKIMUELEEZEI KAMA ALIKUA MTU WA KWANZA KUUMBWA.
Nilibahatika kukipata na kwa kuwa sikuwa na muda wakuweza kutulia na kukisoma kutokana na uharaka wa aliyekuwa nacho, nilimuomba japo nikinakili ingawa pia sikuweza kukimaliza chote kukichapa kwa uharaka wa mwenye nacho.
Kina mengi mengi yakuyatafakari, na ni kitabu cha asili ya Muafrika na kina hadi namba na herufi za kibantu achana na hizi alfabeti tuzijuazo, humo ndio namba zinaandikwa mosi mpaka kenda nk, namna makabila na nchi mbalimbali duniani zilivyoanza....
nilijaribu kushare na watu wengi hawakua wakikifaham nikaona nisije kuonekana mimi ndio mtunzi ila nilipomsikia Mwanamuziki akijiita Ibrozama nikajua ni kitabu kijulikancho kwa wengine maana jina hilo linapatikana ndani ya kitabu hiko na lina historia yake.
sipo vizuri kukieleezea sana ila nitapenda kukishare na Mshana Jr, then atatusaidia kama kina lolote la kujifunza au kukipuuza japo kina typing error kidogo kutokana na kukichapa mwenyewe na mpaka sasa sijapata muda wakutulia kukiedit coz hard copy yake bado naendelea kuhangaika niipate tena.
Mshana Jr ukiridhia nitakutumia PM!
Sent using
Jamii Forums mobile app