Ugali wa Rowe unafaa sana kutumiwa na wanajeshi vitani, Chakula asili cha Wamanyema na Waha hapa kwetu Kigoma

Ugali wa Rowe unafaa sana kutumiwa na wanajeshi vitani, Chakula asili cha Wamanyema na Waha hapa kwetu Kigoma

Kigoma Region Tanzania

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2021
Posts
230
Reaction score
611
Huu ni ugali usioharibika hata ukikaa mwezi mmoja, Ugali huu unaitwa Rowe hapa kwetu Kigoma.

Unatengenezwa kutokana na muhogo, Masharti yake usihifadhiwe kwenye jokofu ama sahani. Unaandaliwa kwa siku 4 mpaka 7.

Ugali wa Rowe baada ya kusongwa unahifadhiwa kwenye majani maalum ya mgomba, unaliwa kwa mboga ama bila mboga, unaweza kusafiri nao popote kwenye begi. Ni chakula cha asili cha watu wa Kigoma hasa kabila la Waha na wamanyema.

Ugali huu ni biashara inayopata umaarufu mkubwa siku hadi siku, magharibi mwa Tanzania na nchi za Rwanda, Burundi na Congo.

_107895524_1.jpg


_107895528_4.jpg
 
Maprofesa wa Tanzania badala ya kushindana kuja na njia mbali mbali za kurahisisha maisha yetu wamejazana kwenye siasa huko wanapiga porojo tu.

Ona sasa Ugali tu unapikwa Kwa siku saba.

Kule Kwa wazungu wangetafuta mashine ya kupika Kwa masaa machache tu,

Elimu ya kukaririshana madesa haina tija.
 
Tuendelee kuombea amani ya nchi yetu, nchi yetu ina tofauti kubwa sana na nchi nyingi.

Nchi majirani zetu na nchi nyingi zina mila lakini mila zetu kama watanzania ni tofauti na mila.zao,tunajuana makabila tunheshimiana tunataniana tunaoleana

Nchi nyingi zina dini lakini jinsi watu wenye imani tofauti wanavyokaa kwa upendo, kuvumiliana, kuheshimiana kuoleana Tanzania ni tofauti kbisa kiistoria na kijamii kuhusu imani na mataifa mengi hata kule dini hizo zilipotoka. Ukiona mtu anaanzisha chokochoko za kidini au kikabila ujue hana asili ya Tanzania ama ana backup ya watu ama taasisi kutoka nje yenye lengo la kuharibu umoja wetu.

HUU UGALI wa LOYA una asili ya nchi zilizowahi kupigana civil war na umewafanya waweze kupona kufa njaa misituni kwa kuwa unadumu muda mrefu

Sisi watanzania mbinu hizo hatuna kwa sababu tumezaliwa kwenye amani na tunakulia kwenye amani. Tuheshimu tunu zetu za amani ili kuepuka matumizi ya vyakula kama hivi. MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Hizo siku 4 unakua upo tu jikoni?
Hapana, mchakato upo namna hii...

Unachimba mihogo mibichi kutoka shamba, kisha unaimenya halafu unaiwekea maji kwenye sufuria kubwa (kilindaa), inakaa humo kwenye maji kwa siku 4 hadi 5. Ukiitoa kwenye maji hayo inakuwa na ladha flani tamu sana kwa huku tunaita ''Mitewe au Mitebwe'' ni mihogo iliyowekwa kwenye maji kwa siku 4 hadi 5 huja na ladha nzuri sana.

Sasa mitewe hiyo ambayo ni mihogo huchukuliwa na kuoshwa, halafu hurejeshwa kwenye sufuria kubwa (Kilindaa) na kuwekewa maji na kisha huanza kupikwa hadi itapoiva. Sufuria hilo hufunikwa kwa majani ya migomba ya ndizi. Ikishaiva vizuri hutolewa na huanza kutwangwa (kusagwa) kwenye kinu, inasagwa hadi inalainika kabisa na kuwa unga ulioiva mfano wa ugali, kumbuka hiyo ni mihogo iliyopikwa tayari.

Baada ya kusaga ndio unaanza kuibumba (kuibanda) na kuwa mfano wa ugali na kisha unaiweka kwenye majani ya migomba ya ndizi halafu unafunga vizuri kabisa kwa ajili ya matumizi ya chakula kuanzia sasa hadi siku 30 zijazo.
 
Maprofesa wa Tanzania badala ya kushindana kuja na njia mbali mbali za kurahisisha maisha yetu wamejazana kwenye siasa huko wanapiga porojo tu.

Ona sasa Ugali tu unapikwa Kwa siku saba.

Kule Kwa wazungu wangetafuta mashine ya kupika Kwa masaa machache tu,

Elimu ya kukaririshana madesa haina tija.
Ni kweli ndugu
 
Nasikia ukila huo ugali bc umeshiba mwezi mmoja.
Hapana mwezi haufiki kwa kushiba, bali ukiula ugali huo unakuwa na nguvu sana na unaweza chukua muda mrefu bila ya kula chochote kitu, ni ugali uliotumika kwenye safari ndefu kutoka Kigoma hadi Dar es salaam kwa njia ya treni au kutoka Kigoma hadi Zambia kwa njia ya Meli.
 
Tuendelee kuombea amani ya nchi yetu, nchi yetu ina tofauti kubwa sana na nchi nyingi.

Nchi majirani zetu na nchi nyingi zina mila lakini mila zetu kama watanzania ni tofauti na mila.zao,tunajuana makabila tunheshimiana tunataniana tunaoleana

Nchi nyingi zina dini lakini jinsi watu wenye imani tofauti wanavyokaa kwa upendo, kuvumiliana, kuheshimiana kuoleana Tanzania ni tofauti kbisa kiistoria na kijamii kuhusu imani na mataifa mengi hata kule dini hizo zilipotoka. Ukiona mtu anaanzisha chokochoko za kidini au kikabila ujue hana asili ya Tanzania ama ana backup ya watu ama taasisi kutoka nje yenye lengo la kuharibu umoja wetu.

HUU UGALI wa LOYA una asili ya nchi zilizowahi kupigana civil war na umewafanya waweze kupona kufa njaa misituni kwa kuwa unadumu muda mrefu

Sisi watanzania mbinu hizo hatuna kwa sababu tumezaliwa kwenye amani na tunakulia kwenye amani. Tuheshimu tunu zetu za amani ili kuepuka matumizi ya vyakula kama hivi. MUNGU IBARIKI TANZANIA
Ahsante ndugu, lakini unakosea sana. Ugali huo asili yake ni Kigoma na wala sio nchi hizo zenye machafuko, ispokuwa soko kuu liko kwenye nchi hizo za vita. Tunatengeneza kisha tunakwenda kuwauzia wakati wa machafuko. Lakini asili yake haswa huo ugali ni hapa kwetu Tanzani mkoani Kigoma.
 
Huu ni ugali usioharibika hata ukikaa mwezi mmoja, Ugali huu unaitwa Rowe hapa kwetu Kigoma.

Unatengenezwa kutokana na muhogo, Masharti yake usihifadhiwe kwenye jokofu ama sahani. Unaandaliwa kwa siku 4 mpaka 7.

Ugali wa Rowe baada ya kusongwa unahifadhiwa kwenye majani maalum ya mgomba, unaliwa kwa mboga ama bila mboga, unaweza kusafiri nao popote kwenye begi. Ni chakula cha asili cha watu wa Kigoma hasa kabila la Waha na wamanyema.

Ugali huu ni biashara inayopata umaarufu mkubwa siku hadi siku, magharibi mwa Tanzania na nchi za Rwanda, Burundi na Congo.

View attachment 1831816

View attachment 1831820
Nimewahi kula huu ugali kwenye kijiji kinaitwa Mzenze. Ukila kwa nyama ya mbuzi ya kuchoma safi sana
 
Huu ni ugali usioharibika hata ukikaa mwezi mmoja, Ugali huu unaitwa Rowe hapa kwetu Kigoma.

Unatengenezwa kutokana na muhogo, Masharti yake usihifadhiwe kwenye jokofu ama sahani. Unaandaliwa kwa siku 4 mpaka 7.

Ugali wa Rowe baada ya kusongwa unahifadhiwa kwenye majani maalum ya mgomba, unaliwa kwa mboga ama bila mboga, unaweza kusafiri nao popote kwenye begi. Ni chakula cha asili cha watu wa Kigoma hasa kabila la Waha na wamanyema.

Ugali huu ni biashara inayopata umaarufu mkubwa siku hadi siku, magharibi mwa Tanzania na nchi za Rwanda, Burundi na Congo.

View attachment 1831816

View attachment 1831820
Muwape na kayoga.😝😝😝
 
Kwahio huu ni kama biscuits / cookies; preservation ni ukavu au wanaweka chumvi pia

Huwa kuna biscuit fulani za jeshi ngumu kama mbao, ila zinashibisha
Hapana, ugali huu hauwekewi chumvi bali una ladha yake ya asili ambapo hukufanya wewe mlaji uweze kuula bila hata mboga, na pia unaweza kuukata kata kwa vipande mfano wa beskuti kama picha hii

12642470_1549240578721430_648170975695804560_n.jpg
 
Nimewahi kula huu ugali kwenye kijiji kinaitwa Mzenze. Ukila kwa nyama ya mbuzi ya kuchoma safi sana.
Ndio, unaweza kuula kwa nyama ya kuchoma, au kwa samaki wa kuchoma au kwa dagaa wa bichi wa Kigoma (Masembe na Nyamnyam) au hata bila mboga unalika.
 
Back
Top Bottom