Ugonjwa wa kifafa usikilizeni redioni. Simulizi yake ni ya kutishaa!

Ugonjwa wa kifafa usikilizeni redioni. Simulizi yake ni ya kutishaa!

Nakumbuka kuna bint mmoja alikuwa na kifafa sasa walienda shambani kulima yeye akawa ameenda kwenye mto jirani na shamba lao, asee yule bint alifia pale pale kwenye mto baada ya kuangukia kwenye mto
 
Duh pole mno, Ila inasemekana mgonjwa wa kifafa akianguka na akaungua moto hata kidogo tu basi kupona Ni km haiwezekani tena
 
Sitokuja kusahau mwaka 1998 nasafiri na basi dogo DCM toka Tukuyu kwenda Ushirika, nimekaa siti ya mlangoni ghafla nikamuona konda anakakamaa ameshika chuma cha pembeni ya mlango na mlango upo wazi na gari ipo kwenye spidi ya kawaida, anauma ulimi wake anatoa mate anakakamaa kashika chuma kile cha kushika kama unapanda kwenye daladala bahati alikuwa amegeuka anaangalia ndani ya gari anahesabu pesa zake.
Nilichomoka kama komandoo kipensi kabla hajaachia chuma kumdaka na kumshikilia kwa nguvu sana huku nikimpeleka kwa ndani ya gari asianguke nje na kugonga kichwa chini na gari kumpitia na tairi ya nyuma.
Alinishika kwa nguvu sijawahi ziona toka nazaliwa alinishika mikono chini ya mabega lakini mimi nilishika shingo badae akaachia mikono akashika nguo kwa nguvu za ajabu mpaka zikatatuka mifuko ya kifuani.

Kuna mama mmoja akamwekea kanga mdomoni mimi nimemshika yule jamaa kama dakika 15 hizi nikaona ameanza kulegea. Shati lake limetapakaa mate na mimi nimetapakaa mate na mambo mengine ya kibinadamu.

Niliambiwa nimuache pale pale atulie na tukafika ushirika stendi jamaa akiwa bado amepoteza fahamu. Lakini lile tukio siwezi kulisahau maishani mwangu. Nilipewa sifa nyingi sana kwa tukio lile. Kuna jamaa alikuwa anaitwa Mwakibete alininunulia shati pale ushirika maana la kangu lilichanika kwenye kwapa ile vuta nkuvute na kidogo nilitapakaa mate ule mgusano wa nguvu kama tunacheza mieleka vile.

Jamani kifafa ni ugonjwa hauna mfano kwa kuogofya,kustua na kutesa watu wa Mungu.

Mwenyezi Mungu atusaidie sana sisi waja wake. Amina
ubarikiwe
 
tahadhari ukimuona mtu yoyote anaelezea kitu cha kijamii na hakuweza kutoa faida wazi na kusema munifuatee kwenye Dm yangu nawaombeni muwapuuze ni matapeli wakubwa na ni hatari na wengi wanakuja kwa njia ya matibabu . wewe kama unania ya kusaidia mtu kwanini husemi hadharani kila mmoja apate faida unamwambia aje chumbani kwako ili afanyeje?
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka 1986 nikiwa na ufahamu na akili timamu .sikuwa naelewa kifafa ninini . ila nilikuwa na maswali mengi sana Kila nikimtazama mama yangu mzazi ambaye asilimia kubwa mwili wake ulitawaliwa na vidonda. Nakumbuka Kuna wakati tukiwa kisimani mama alitumbukia kisimani si mara Moja na kupata vidonda na siku nyingine anadondoka kwenye moto nakupata majeraha makubwa sana .kutoka kisimani au Mahali alipoanguka ilikuwa ni mpaka wasamalia wamtoe !! Nilikuwa najiuliza Sana kwamba ninini kinamdondosha mama yangu niliekuwa nampenda sana. Kuna wakati niliona waganga wa asili wanapishana nyumbani kumtibia ! Kwa kuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufuatilia hasaa ninini kinamsibu mama! Siku nyingine alidondoka sokoni katikati ya umati wa watu ! Watu wakajaa kushangaa na wasamalia wema wakasaidia kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni hatari angeweza kudondoka Kwa siku hata mara tatu !! Wakati huo nilikuwa darasa la tatu! Alipata ujauzito akafanikiwa kujifungua mapacha WAWILI lakini haikupita miezi tatu alitumbukia nao kisimani hii ni kutokana na baba hakuwa mtu wa kukaa nyumbani muda mwingi alikuwa minadani nakumbuka siku Ile mvua kubwa ilikuwa Ina nyesha!! Mama aliokolewa akiwa hai lakini watoto wale wote walipoteza maisha!! Ilimlazimu mama kuhamishiwa kijijini Kwa Babu mzaa mama na mimi pia nikatakiwa nikakae nae! Kwa kuwa ilikuwa kumtazamia Hali yake Kwa muda mfupi, nilombewa kusoma shule mojawapo hapo kijijini Kwa muda huku tukiendelea kumuuguza ! Babu na bibi walikuwa ni wanywaji wazuri wa pombe hivyo ikifika jioni tu huwezi kuwakuta nyumbani ,,bibi pia alikuwa mkorogaji mzuri sana wa pombe ,hivyo pale nyumbani muda mwingi mizigo ya Kuni ilikuwa haipungii!! Sasa siku Moja niliamka asubuhi mapema kuwahi shule ulipofika muda wa mapumziko nilitoloka shule kurudi nyumbani , Kiukweli siku Ile sikuwa na hamu ya kukaa dalasani kabisa ! Nilipofika nyumbani nikakuta bibi ametenga mapipa makubwa pombe na moto mkali wa makuti akiipika pombe kama kawaida yake .alipiniona tu kaniwakia sana Kwa nini nimetoloka shule ? Akanikatia mahindi shambani nikachoma fasta na kuniamuru haraka niludi shule!! Japo sikutaka kurudi shule lakini kishingo upande nililejea tena shuleni!! Siku hiyo kukawa na michezo tukachelewa kidogo kurudi nyumbani !! Nilifika nyumbani jioni kabisa ila nilishangaa kuona Moshi mzito sana ndani na hakukuwa na dalili ya kuwepo mtu !! Nilizowea kumkuta mama amekaa nje ,lakini hakuwepo .nikajaribu kumuita hakuitika kabisa ! Nilijitahidi kuiingia ndani nikaona Kuna Moshi usio wa kawaida na harufu nzito kama vile mtu amechoma ngozi ya ng'ombe, harufu mbaya mnoo na kulikuwa Giza !! Nikalisogelea dirisha Ile kulifungua tu la haula!! Nikaushuhudia mwili wa mama ukiwa umeteketea kabisa!! Kilichobaki ni miguu ambayo ilikuwa nje ya makaa ya ule moto mkali sana !! Nilitoka mbio kuelekea kilabuni huku nikiwa nimechanganyikiwa hata kuongea siwezi ,nilishindwa kumueleza Babu kilichotokea nyumbani zaidi ya kumshika mkono na kuanza kumvuta Kwa ishara ya kukimbia kuelekea nyumbani Kila mtu pale kilabuni aliduwaa !! Mama ameungua:: hilo ndio neno pekee nililoweza kulitamka hakuna aliyebaki pale kilabuni ! Kufika nyumbani Kila aliekuwa anaingia ndani alitoka meangua kilio huzuni kubwa ilitanda pale nyumbani .Kwa nini mliacha moto bila kuuzima? Watu wengi walikuwa wanahoji swali hilo huku wazee wakianza kuutoa mwili motoni, lakini tayari yalishakuwa majivu !! Nakumbuka wazee wakiwa wanakusanya majivu na kuyatia kwenye kiroba kikubwa hivi!! Lawama zote wakizielekeza Kwa bibi na Babu ! Kwamba Kwa nini hawakuuzima moto baada kumaliza kupika pombe!?? Hakuna tulichookoa !! Tulimzika mama akiwa kwenye kiroba ! Tulizika majivu ! Naweza kusema nauchukia sana ugonjwa huu !! Na usimpuuze mtu yeyote mwenye ugonjwa huu! Popote pale iwe nje au ndani ya familia yenu !!ugonjwa huu Hauna tiba ya Moja Kwa Moja !lakini wagonjwa wake wanahitaji sana uangalizi maalumu !! Katika miaka yangu nimejitahidi Sana kufanya utafiti kuhusu ugonjwa huu !! Nimejifunza mengi na sasa na weza kusema nipo karibu sana na wagonjwa wa kifafa kuwapa elimu na namna ya kuishi Kwa tahadhari na kuepuka hatari zinazowahusu watu Hawa ! Iwe una ndugu ,rafiki au jirani wa karibu ambae anateseka na ugonjwa huu tafadhali njoo dm yangu nitakupa elimu ya jinsi ya kumsaidia ,na jinsi anavyoweza kupona kabisa !! Usiupuuze ugonjwa huu ni hatari kupita kiasi!



Itoshe tu kusema umenitonesha kidonda!

Marehemu mama yangu alikuwa na huu ugonwa, naomba nisiongee sana maana madhila yake siyo ya kusimulia.
 
Itoshe tu kusema umenitonesha kidonda!

Marehemu mama yangu alikuwa na huu ugonwa, naomba nisiongee sana maana madhila yake siyo ya kusimulia.
Pole sanaa broo
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka 1986 nikiwa na ufahamu na akili timamu .sikuwa naelewa kifafa ninini . ila nilikuwa na maswali mengi sana Kila nikimtazama mama yangu mzazi ambaye asilimia kubwa mwili wake ulitawaliwa na vidonda. Nakumbuka Kuna wakati tukiwa kisimani mama alitumbukia kisimani si mara Moja na kupata vidonda na siku nyingine anadondoka kwenye moto nakupata majeraha makubwa sana .kutoka kisimani au Mahali alipoanguka ilikuwa ni mpaka wasamalia wamtoe !! Nilikuwa najiuliza Sana kwamba ninini kinamdondosha mama yangu niliekuwa nampenda sana. Kuna wakati niliona waganga wa asili wanapishana nyumbani kumtibia ! Kwa kuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufuatilia hasaa ninini kinamsibu mama! Siku nyingine alidondoka sokoni katikati ya umati wa watu ! Watu wakajaa kushangaa na wasamalia wema wakasaidia kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni hatari angeweza kudondoka Kwa siku hata mara tatu !! Wakati huo nilikuwa darasa la tatu! Alipata ujauzito akafanikiwa kujifungua mapacha WAWILI lakini haikupita miezi tatu alitumbukia nao kisimani hii ni kutokana na baba hakuwa mtu wa kukaa nyumbani muda mwingi alikuwa minadani nakumbuka siku Ile mvua kubwa ilikuwa Ina nyesha!! Mama aliokolewa akiwa hai lakini watoto wale wote walipoteza maisha!! Ilimlazimu mama kuhamishiwa kijijini Kwa Babu mzaa mama na mimi pia nikatakiwa nikakae nae! Kwa kuwa ilikuwa kumtazamia Hali yake Kwa muda mfupi, nilombewa kusoma shule mojawapo hapo kijijini Kwa muda huku tukiendelea kumuuguza ! Babu na bibi walikuwa ni wanywaji wazuri wa pombe hivyo ikifika jioni tu huwezi kuwakuta nyumbani ,,bibi pia alikuwa mkorogaji mzuri sana wa pombe ,hivyo pale nyumbani muda mwingi mizigo ya Kuni ilikuwa haipungii!! Sasa siku Moja niliamka asubuhi mapema kuwahi shule ulipofika muda wa mapumziko nilitoloka shule kurudi nyumbani , Kiukweli siku Ile sikuwa na hamu ya kukaa dalasani kabisa ! Nilipofika nyumbani nikakuta bibi ametenga mapipa makubwa pombe na moto mkali wa makuti akiipika pombe kama kawaida yake .alipiniona tu kaniwakia sana Kwa nini nimetoloka shule ? Akanikatia mahindi shambani nikachoma fasta na kuniamuru haraka niludi shule!! Japo sikutaka kurudi shule lakini kishingo upande nililejea tena shuleni!! Siku hiyo kukawa na michezo tukachelewa kidogo kurudi nyumbani !! Nilifika nyumbani jioni kabisa ila nilishangaa kuona Moshi mzito sana ndani na hakukuwa na dalili ya kuwepo mtu !! Nilizowea kumkuta mama amekaa nje ,lakini hakuwepo .nikajaribu kumuita hakuitika kabisa ! Nilijitahidi kuiingia ndani nikaona Kuna Moshi usio wa kawaida na harufu nzito kama vile mtu amechoma ngozi ya ng'ombe, harufu mbaya mnoo na kulikuwa Giza !! Nikalisogelea dirisha Ile kulifungua tu la haula!! Nikaushuhudia mwili wa mama ukiwa umeteketea kabisa!! Kilichobaki ni miguu ambayo ilikuwa nje ya makaa ya ule moto mkali sana !! Nilitoka mbio kuelekea kilabuni huku nikiwa nimechanganyikiwa hata kuongea siwezi ,nilishindwa kumueleza Babu kilichotokea nyumbani zaidi ya kumshika mkono na kuanza kumvuta Kwa ishara ya kukimbia kuelekea nyumbani Kila mtu pale kilabuni aliduwaa !! Mama ameungua:: hilo ndio neno pekee nililoweza kulitamka hakuna aliyebaki pale kilabuni ! Kufika nyumbani Kila aliekuwa anaingia ndani alitoka meangua kilio huzuni kubwa ilitanda pale nyumbani .Kwa nini mliacha moto bila kuuzima? Watu wengi walikuwa wanahoji swali hilo huku wazee wakianza kuutoa mwili motoni, lakini tayari yalishakuwa majivu !! Nakumbuka wazee wakiwa wanakusanya majivu na kuyatia kwenye kiroba kikubwa hivi!! Lawama zote wakizielekeza Kwa bibi na Babu ! Kwamba Kwa nini hawakuuzima moto baada kumaliza kupika pombe!?? Hakuna tulichookoa !! Tulimzika mama akiwa kwenye kiroba ! Tulizika majivu ! Naweza kusema nauchukia sana ugonjwa huu !! Na usimpuuze mtu yeyote mwenye ugonjwa huu! Popote pale iwe nje au ndani ya familia yenu !!ugonjwa huu Hauna tiba ya Moja Kwa Moja !lakini wagonjwa wake wanahitaji sana uangalizi maalumu !! Katika miaka yangu nimejitahidi Sana kufanya utafiti kuhusu ugonjwa huu !! Nimejifunza mengi na sasa na weza kusema nipo karibu sana na wagonjwa wa kifafa kuwapa elimu na namna ya kuishi Kwa tahadhari na kuepuka hatari zinazowahusu watu Hawa ! Iwe una ndugu ,rafiki au jirani wa karibu ambae anateseka na ugonjwa huu tafadhali njoo dm yangu nitakupa elimu ya jinsi ya kumsaidia ,na jinsi anavyoweza kupona kabisa !! Usiupuuze ugonjwa huu ni hatari kupita kiasi!
Binam zangu wawili waliteseka sana na huu ugonjwa...
Kama unavyosema mda wote miili yao ina majeraha ya kutisha.
Mmoja alifariki tu akiwa amelala...
Mwingine bado yuko hai. Nakuja dm utusaidie dawa
 
bibi na babu yako walikuwa wazazi wa hovyo kupata kutokea,hawakustahili lawama tu bali hata adhabu.ukute mambo ya kimila walimsindikiza mtoto wao(mama yako).
mgonjwa wa kifafa ni kilema kama wengine,anahitaji ukaribu wa hali ya juu,yaani hata kama ni kazi anafanya hatakiwi kufanya akiwa peke yake.

kifafa kimeua dogo niliyekuwa naye,amekua nacho kwa muda mtefu alivyokua mtu mzima akaanza kuachwa peke yake,nilikuja kuambiwa alitumbukia kisimani akakutwa ameshapoteza maisha.

kilimkosa kosa mshkaji ambaye ana kovu kubwa mguuni mpaka leo baada ya kuangukia jiko la kuni,yaani aliiva kabisa sehemu ya mguu.


kifafa kibaya kabisa ni cha uzazi,maana kwanza mnakuwa hamjui kama ndugu yenu anacho,mpaka ashike mimba,tarehe za mwisho mkitarajia atashikwa na uchungu kama wanawake wengine aombe msaada,pale pale anakula kabali.ilibaki kidogo nipoteze dada yangu kwa aina hii ya kifafa,aliyemuokoa ni rafiki yake ambaye huja kushona naye nyumbani pale,kaja amekuta sister anakoroma tu mapovu sakafuni.

pole sana mkuu.
 
Binam zangu wawili waliteseka sana na huu ugonjwa...
Kama unavyosema mda wote miili yao ina majeraha ya kutisha.
Mmoja alifariki tu akiwa amelala...
Mwingine bado yuko hai. Nakuja dm utusaidie dawa
Pole sana kwa masaibu ya wajomba zako ila nakushauri muombe msaada atakaotaka kukupa aupandishe hapa jukwaani sisemi ni tapeli ila ni salama zaidi na utakuwa na msaada kwa wengine
 
Back
Top Bottom