Mbona juzi kati kama niliona matangazo kwamba kifafa kinatabika endapo wagonjwa wakizingatia dawa. Ngoja niguatilie hilo tangazo.Nakuja dm.kuna dogo anadondokaga .aisee juzi kati hivi ndo nilimshuhudia kwa mara ya kwanza
Nitamuomba hivyoPole sana kwa masaibu ya wajomba zako ila nakushauri muombe msaada atakaotaka kukupa aupandishe hapa jukwaani sisemi ni tapeli ila ni salama zaidi na utakuwa na msaada kwa wengine
Kifafa kinadawa ambazo zinazuia mgonjwa kuanguka anguka ndo maana recently ni ngumu kuona mgonjwa wa kifafa wapo Ila wanatumia dawa ambazo zinawafanya waishi normal lifePole sana kwa yaliyokukuta
Kuhusu njia za kumsaidia mtu mwenye huo ugonjwa kwanini usiweke hapa kwa faida ya wasomaji wa sasa na wa baadae(miaka ijayo)
Naamini sio siku zote utapatikana PM lakini nyuzi za JF huwa zinaishi
Kifafa kinadawa ambazo zinazuia mgonjwa kuanguka anguka ndo maana recently ni ngumu kuona mgonjwa wa kifafa wapo Ila wanatumia dawa ambazo zinawafanya waishi normal lifeNitamuomba hivyo
Asantee
Sasa kwanini aende ziwani peke yake wakati anajijua ana Epilepsy?Baba mkubwa alifariki kwa sababu ya kifafa alienda ziwani kupunga upepo .kikamkuta akadondoka kwenye ziwa .huu ugonjwa ni pepo kabisa.mjomba wangu pia alikuwa nawo but mungu alimponya yupo mzima sasa
Sasa kwanini aende ziwani peke yake wakati anajijua ana Epilepsy?
Kajitakia mwenyew
Hiyo para ya mwisho inaonesha stori ni yakutunga... kuna watu watapigwa hapa. Mambo ya Dzm.Story au ukweli?nimetoa mchozi broo..pole Sana I can feel your pain !!!!daah..
Pole sana. Kwakweli kifafa ni ugonjwa mbaya sana. Baadhi ya wagonjwa huwehuka mazima kabisa.Nakumbuka ilikuwa mwaka 1986 nikiwa na ufahamu na akili timamu .sikuwa naelewa kifafa ninini . ila nilikuwa na maswali mengi sana Kila nikimtazama mama yangu mzazi ambaye asilimia kubwa mwili wake ulitawaliwa na vidonda. Nakumbuka Kuna wakati tukiwa kisimani mama alitumbukia kisimani si mara Moja na kupata vidonda na siku nyingine anadondoka kwenye moto nakupata majeraha makubwa sana .kutoka kisimani au Mahali alipoanguka ilikuwa ni mpaka wasamalia wamtoe !! Nilikuwa najiuliza Sana kwamba ninini kinamdondosha mama yangu niliekuwa nampenda sana. Kuna wakati niliona waganga wa asili wanapishana nyumbani kumtibia ! Kwa kuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufuatilia hasaa ninini kinamsibu mama! Siku nyingine alidondoka sokoni katikati ya umati wa watu ! Watu wakajaa kushangaa na wasamalia wema wakasaidia kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni hatari angeweza kudondoka Kwa siku hata mara tatu !! Wakati huo nilikuwa darasa la tatu! Alipata ujauzito akafanikiwa kujifungua mapacha WAWILI lakini haikupita miezi tatu alitumbukia nao kisimani hii ni kutokana na baba hakuwa mtu wa kukaa nyumbani muda mwingi alikuwa minadani nakumbuka siku Ile mvua kubwa ilikuwa Ina nyesha!! Mama aliokolewa akiwa hai lakini watoto wale wote walipoteza maisha!! Ilimlazimu mama kuhamishiwa kijijini Kwa Babu mzaa mama na mimi pia nikatakiwa nikakae nae! Kwa kuwa ilikuwa kumtazamia Hali yake Kwa muda mfupi, nilombewa kusoma shule mojawapo hapo kijijini Kwa muda huku tukiendelea kumuuguza ! Babu na bibi walikuwa ni wanywaji wazuri wa pombe hivyo ikifika jioni tu huwezi kuwakuta nyumbani ,,bibi pia alikuwa mkorogaji mzuri sana wa pombe ,hivyo pale nyumbani muda mwingi mizigo ya Kuni ilikuwa haipungii!! Sasa siku Moja niliamka asubuhi mapema kuwahi shule ulipofika muda wa mapumziko nilitoloka shule kurudi nyumbani , Kiukweli siku Ile sikuwa na hamu ya kukaa dalasani kabisa ! Nilipofika nyumbani nikakuta bibi ametenga mapipa makubwa pombe na moto mkali wa makuti akiipika pombe kama kawaida yake .alipiniona tu kaniwakia sana Kwa nini nimetoloka shule ? Akanikatia mahindi shambani nikachoma fasta na kuniamuru haraka niludi shule!! Japo sikutaka kurudi shule lakini kishingo upande nililejea tena shuleni!! Siku hiyo kukawa na michezo tukachelewa kidogo kurudi nyumbani !! Nilifika nyumbani jioni kabisa ila nilishangaa kuona Moshi mzito sana ndani na hakukuwa na dalili ya kuwepo mtu !! Nilizowea kumkuta mama amekaa nje ,lakini hakuwepo .nikajaribu kumuita hakuitika kabisa ! Nilijitahidi kuiingia ndani nikaona Kuna Moshi usio wa kawaida na harufu nzito kama vile mtu amechoma ngozi ya ng'ombe, harufu mbaya mnoo na kulikuwa Giza !! Nikalisogelea dirisha Ile kulifungua tu la haula!! Nikaushuhudia mwili wa mama ukiwa umeteketea kabisa!! Kilichobaki ni miguu ambayo ilikuwa nje ya makaa ya ule moto mkali sana !! Nilitoka mbio kuelekea kilabuni huku nikiwa nimechanganyikiwa hata kuongea siwezi ,nilishindwa kumueleza Babu kilichotokea nyumbani zaidi ya kumshika mkono na kuanza kumvuta Kwa ishara ya kukimbia kuelekea nyumbani Kila mtu pale kilabuni aliduwaa !! Mama ameungua:: hilo ndio neno pekee nililoweza kulitamka hakuna aliyebaki pale kilabuni ! Kufika nyumbani Kila aliekuwa anaingia ndani alitoka meangua kilio huzuni kubwa ilitanda pale nyumbani .Kwa nini mliacha moto bila kuuzima? Watu wengi walikuwa wanahoji swali hilo huku wazee wakianza kuutoa mwili motoni, lakini tayari yalishakuwa majivu !! Nakumbuka wazee wakiwa wanakusanya majivu na kuyatia kwenye kiroba kikubwa hivi!! Lawama zote wakizielekeza Kwa bibi na Babu ! Kwamba Kwa nini hawakuuzima moto baada kumaliza kupika pombe!?? Hakuna tulichookoa !! Tulimzika mama akiwa kwenye kiroba ! Tulizika majivu ! Naweza kusema nauchukia sana ugonjwa huu !! Na usimpuuze mtu yeyote mwenye ugonjwa huu! Popote pale iwe nje au ndani ya familia yenu !!ugonjwa huu Hauna tiba ya Moja Kwa Moja !lakini wagonjwa wake wanahitaji sana uangalizi maalumu !! Katika miaka yangu nimejitahidi Sana kufanya utafiti kuhusu ugonjwa huu !! Nimejifunza mengi na sasa na weza kusema nipo karibu sana na wagonjwa wa kifafa kuwapa elimu na namna ya kuishi Kwa tahadhari na kuepuka hatari zinazowahusu watu Hawa ! Iwe una ndugu ,rafiki au jirani wa karibu ambae anateseka na ugonjwa huu tafadhali njoo dm yangu nitakupa elimu ya jinsi ya kumsaidia ,na jinsi anavyoweza kupona kabisa !! Usiupuuze ugonjwa huu ni hatari kupita kiasi!
[emoji26][emoji26][emoji26][emoji26]Mbaya zaidi unarithiwa,
Duu pole sana kaka.Nakumbuka ilikuwa mwaka 1986 nikiwa na ufahamu na akili timamu .sikuwa naelewa kifafa ninini . ila nilikuwa na maswali mengi sana Kila nikimtazama mama yangu mzazi ambaye asilimia kubwa mwili wake ulitawaliwa na vidonda. Nakumbuka Kuna wakati tukiwa kisimani mama alitumbukia kisimani si mara Moja na kupata vidonda na siku nyingine anadondoka kwenye moto nakupata majeraha makubwa sana .kutoka kisimani au Mahali alipoanguka ilikuwa ni mpaka wasamalia wamtoe !! Nilikuwa najiuliza Sana kwamba ninini kinamdondosha mama yangu niliekuwa nampenda sana. Kuna wakati niliona waganga wa asili wanapishana nyumbani kumtibia ! Kwa kuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufuatilia hasaa ninini kinamsibu mama! Siku nyingine alidondoka sokoni katikati ya umati wa watu ! Watu wakajaa kushangaa na wasamalia wema wakasaidia kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni hatari angeweza kudondoka Kwa siku hata mara tatu !! Wakati huo nilikuwa darasa la tatu! Alipata ujauzito akafanikiwa kujifungua mapacha WAWILI lakini haikupita miezi tatu alitumbukia nao kisimani hii ni kutokana na baba hakuwa mtu wa kukaa nyumbani muda mwingi alikuwa minadani nakumbuka siku Ile mvua kubwa ilikuwa Ina nyesha!! Mama aliokolewa akiwa hai lakini watoto wale wote walipoteza maisha!! Ilimlazimu mama kuhamishiwa kijijini Kwa Babu mzaa mama na mimi pia nikatakiwa nikakae nae! Kwa kuwa ilikuwa kumtazamia Hali yake Kwa muda mfupi, nilombewa kusoma shule mojawapo hapo kijijini Kwa muda huku tukiendelea kumuuguza ! Babu na bibi walikuwa ni wanywaji wazuri wa pombe hivyo ikifika jioni tu huwezi kuwakuta nyumbani ,,bibi pia alikuwa mkorogaji mzuri sana wa pombe ,hivyo pale nyumbani muda mwingi mizigo ya Kuni ilikuwa haipungii!! Sasa siku Moja niliamka asubuhi mapema kuwahi shule ulipofika muda wa mapumziko nilitoloka shule kurudi nyumbani , Kiukweli siku Ile sikuwa na hamu ya kukaa dalasani kabisa ! Nilipofika nyumbani nikakuta bibi ametenga mapipa makubwa pombe na moto mkali wa makuti akiipika pombe kama kawaida yake .alipiniona tu kaniwakia sana Kwa nini nimetoloka shule ? Akanikatia mahindi shambani nikachoma fasta na kuniamuru haraka niludi shule!! Japo sikutaka kurudi shule lakini kishingo upande nililejea tena shuleni!! Siku hiyo kukawa na michezo tukachelewa kidogo kurudi nyumbani !! Nilifika nyumbani jioni kabisa ila nilishangaa kuona Moshi mzito sana ndani na hakukuwa na dalili ya kuwepo mtu !! Nilizowea kumkuta mama amekaa nje ,lakini hakuwepo .nikajaribu kumuita hakuitika kabisa ! Nilijitahidi kuiingia ndani nikaona Kuna Moshi usio wa kawaida na harufu nzito kama vile mtu amechoma ngozi ya ng'ombe, harufu mbaya mnoo na kulikuwa Giza !! Nikalisogelea dirisha Ile kulifungua tu la haula!! Nikaushuhudia mwili wa mama ukiwa umeteketea kabisa!! Kilichobaki ni miguu ambayo ilikuwa nje ya makaa ya ule moto mkali sana !! Nilitoka mbio kuelekea kilabuni huku nikiwa nimechanganyikiwa hata kuongea siwezi ,nilishindwa kumueleza Babu kilichotokea nyumbani zaidi ya kumshika mkono na kuanza kumvuta Kwa ishara ya kukimbia kuelekea nyumbani Kila mtu pale kilabuni aliduwaa !! Mama ameungua:: hilo ndio neno pekee nililoweza kulitamka hakuna aliyebaki pale kilabuni ! Kufika nyumbani Kila aliekuwa anaingia ndani alitoka meangua kilio huzuni kubwa ilitanda pale nyumbani .Kwa nini mliacha moto bila kuuzima? Watu wengi walikuwa wanahoji swali hilo huku wazee wakianza kuutoa mwili motoni, lakini tayari yalishakuwa majivu !! Nakumbuka wazee wakiwa wanakusanya majivu na kuyatia kwenye kiroba kikubwa hivi!! Lawama zote wakizielekeza Kwa bibi na Babu ! Kwamba Kwa nini hawakuuzima moto baada kumaliza kupika pombe!?? Hakuna tulichookoa !! Tulimzika mama akiwa kwenye kiroba ! Tulizika majivu ! Naweza kusema nauchukia sana ugonjwa huu !! Na usimpuuze mtu yeyote mwenye ugonjwa huu! Popote pale iwe nje au ndani ya familia yenu !!ugonjwa huu Hauna tiba ya Moja Kwa Moja !lakini wagonjwa wake wanahitaji sana uangalizi maalumu !! Katika miaka yangu nimejitahidi Sana kufanya utafiti kuhusu ugonjwa huu !! Nimejifunza mengi na sasa na weza kusema nipo karibu sana na wagonjwa wa kifafa kuwapa elimu na namna ya kuishi Kwa tahadhari na kuepuka hatari zinazowahusu watu Hawa ! Iwe una ndugu ,rafiki au jirani wa karibu ambae anateseka na ugonjwa huu tafadhali njoo dm yangu nitakupa elimu ya jinsi ya kumsaidia ,na jinsi anavyoweza kupona kabisa !! Usiupuuze ugonjwa huu ni hatari kupita kiasi!
Imagine... eti njoo dm[emoji848][emoji848]tahadhari ukimuona mtu yoyote anaelezea kitu cha kijamii na hakuweza kutoa faida wazi na kusema munifuatee kwenye Dm yangu nawaombeni muwapuuze ni matapeli wakubwa na ni hatari na wengi wanakuja kwa njia ya matibabu . wewe kama unania ya kusaidia mtu kwanini husemi hadharani kila mmoja apate faida unamwambia aje chumbani kwako ili afanyeje?
Bado yupo mkuu?Itoshe tu kusema umenitonesha kidonda!
Marehemu mama yangu alikuwa na huu ugonwa, naomba nisiongee sana maana madhila yake siyo ya kusimulia.
Dawa yake ipo...
Unione private. Hapo ujue nakupanga kuja kukutapeli. Kama dawa ipo weka hapa.
Tatizo lako wewe ni tapeli ndio maana Kila kitu unakihusianisha na utapeli asilimia mia wewe ni tapeliDawa yake ipo...
Unione private. Hapo ujue nakupanga kuja kukutapeli. Kama dawa ipo weka hapa.
Upo sahihi kabisa. Na mbinu ninayotumia ni kama hii yako ya kuwaambia wanifuate private. Huko ndo naenda kuwaliza mmoja mmoja.Tatizo lako wewe ni tapeli ndio maana Kila kitu unakihusianisha na utapeli asilimia mia wewe ni tapeli