Ugonjwa wa Kisonono (Gonorhea): Dalili, kinga na tiba yake

Ugonjwa wa Kisonono (Gonorhea): Dalili, kinga na tiba yake

attachment.php
​
attachment.php


LEO tutazungumzia ugonjwa wa kisonono ambao umekuwa kama umesahaulika katika jamii ila ni kwamba upo na uambukizo upo kwa kiasi kikubwa sana na wenye hatari kubwa ya kuambukizwa ni wanawake.

Wanawake wana uwezekano mkubwa zaidi wa kuambukizwa ugonjwa wa kisonono kwa asilimia 80, huku wanaume wakiwa katika hatari ya kupata ugonjwa huo kwa asilimia 20 tu.

Dalili

Dalili za ugonjwa huo huwa hazijitokezi kwa uwazi kwa wanawake ikilinganishwa na wanaume na pia ugonjwa huu una madhara zaidi kwa wanawake kwani huweza kuwaathiri watoto walio tumboni kwa wajawazito na anapojifungua. Hayo yote yanaonyesha umuhimu wa kutibiwa ugonjwa huo mapema.

Madhara

Moja ya madhara anayoweza kupata mtu kutokana na ugonjwa wa kisonono ni mwanamke kutoweza kuzaa yaani kuwa mgumba au mimba kutoweza kutunga. Inajulikana kuwa magonjwa ya zinaa ya Chlamydia na kisonono yana mchango katika

kusababisha wanawake kutozaa kwani magonjwa hayo kwa asilimia 15 huweza kusababisha uvimbe kwenye kizazi na hasa kwa kuwa wanawake wengi wenye kisonono huwa hawaonyeshi dalili.

Kwa upande wa wanaume ugonjwa wa kisonono pia huweza kuwafanya wasipate watoto kwani huwasababishia uvimbe katika sehemu ya mbele ya korodani ambako

mbegu za kiume hutengenezwa. Uvimbe huo usipotibiwa husababisha utasa.
Ugonjwa wa kisonono au gono pia huweza kuathiri moyo, ubongo, ngozi na kadhalika

kwa hivyo ni hatari kwa mtu yeyote aliyeambukizwa kutokutibiwa mapema.
Pia ugonjwa huo huleta madhara au uvimbe kwenye maungio ya viungo, ambapo vimelea vinavyosababisha kisonono huweza kusambaa kwenye damu na kuleta

maambukizo kwenye sehemu nyinginezo mwilini. Maambukizo hayo huleta homa, vipele, vidonda kwenye ngozi, maumivu ya viungo na uvimbe. ilevile wanawake ambao ni wajawazito walioambukizwa ugonjwa huu wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla haijatimiza umri wake (preterm labor).

Kwa wale wanaoambukizwa kisonono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa vipofu, homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).

Kinga

Unaweza kujikinga na gonjwa hili la zinaa kwa njia zifuatazo. Kwanza kabisa ni kuwa mwaminifu katika ndoa na kujiepusha na uasherati. Kuchukua tahadhari na kuzungumzia

juu ya ugonjwa huo na dalili zake ili kuweza kufahamu kuwa mshirika wako wa ngono ana ugonjwa huo au la na iwapo anao hatua inayofuata ni kutibiwa na kupata ushauri wa daktari.

Njia nyingine ya kujikinga ni kuepuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono. Vilevile kutumia mipira (kondom) wakati wa kujamiiana na wanawake wajawazito

wanapaswa kuhakikisha kuwa wanahudhuria kliniki mapema ili waweze kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka iwapo watagundulika kuwa na ugonjwa wa kisonono au ugonjwa mwingine wowote.

Wajawazito wanashauriwa kujifungua hospitalini ili kama mtoto ameathirika na kisonono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa ili kuepusha kuwa kipofu na madhara mengine.

Matibabu na ushauri

Tiba ya ugonjwa wa kisonono inahusishwa na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya mawili ya zinaa huambatana pamoja.

Matibabu ya kisonono pia hutegemea umri wa mgonjwa. Kisonono ambacho si sugu kilicho kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, hutibiwa kwa dawa za

Cephalosporin, ambapo mgonjwa hupewa dozi moja ya dawa hizo pamoja na dawa aina ya Macrolide kwa mfano Azithromycin na za jamii ya Penicillin kwa mfano Doxycyclin kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Chlamydia.

Mara nyingi kwa wagonjwa walio na umri wa chini ya miaka 18 na wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano. Mgonjwa hutakiwa kufuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizo kwani nyingi huwa na madhara kwa wajawazito kwa mfano Doxycyclin.
 

Attachments

  • gonorrhea2352.jpg
    gonorrhea2352.jpg
    20.6 KB · Views: 1,371
  • blogGonorrheainfection.jpg
    blogGonorrheainfection.jpg
    29.5 KB · Views: 1,287
attachment.php
​
attachment.php


LEO tutazungumzia ugonjwa wa kisonono ambao umekuwa kama umesahaulika katika jamii ila ni kwamba upo na uambukizo upo kwa kiasi kikubwa sana na wenye hatari kubwa ya kuambukizwa ni wanawake.

Wanawake wana uwezekano mkubwa zaidi wa kuambukizwa ugonjwa wa kisonono kwa asilimia 80, huku wanaume wakiwa katika hatari ya kupata ugonjwa huo kwa asilimia 20 tu.

Dalili

Dalili za ugonjwa huo huwa hazijitokezi kwa uwazi kwa wanawake ikilinganishwa na wanaume na pia ugonjwa huu una madhara zaidi kwa wanawake kwani huweza kuwaathiri watoto walio tumboni kwa wajawazito na anapojifungua. Hayo yote yanaonyesha umuhimu wa kutibiwa ugonjwa huo mapema.

Madhara

Moja ya madhara anayoweza kupata mtu kutokana na ugonjwa wa kisonono ni mwanamke kutoweza kuzaa yaani kuwa mgumba au mimba kutoweza kutunga. Inajulikana kuwa magonjwa ya zinaa ya Chlamydia na kisonono yana mchango katika

kusababisha wanawake kutozaa kwani magonjwa hayo kwa asilimia 15 huweza kusababisha uvimbe kwenye kizazi na hasa kwa kuwa wanawake wengi wenye kisonono huwa hawaonyeshi dalili.

Kwa upande wa wanaume ugonjwa wa kisonono pia huweza kuwafanya wasipate watoto kwani huwasababishia uvimbe katika sehemu ya mbele ya korodani ambako

mbegu za kiume hutengenezwa. Uvimbe huo usipotibiwa husababisha utasa.
Ugonjwa wa kisonono au gono pia huweza kuathiri moyo, ubongo, ngozi na kadhalika

kwa hivyo ni hatari kwa mtu yeyote aliyeambukizwa kutokutibiwa mapema.
Pia ugonjwa huo huleta madhara au uvimbe kwenye maungio ya viungo, ambapo vimelea vinavyosababisha kisonono huweza kusambaa kwenye damu na kuleta


maambukizo kwenye sehemu nyinginezo mwilini. Maambukizo hayo huleta homa, vipele, vidonda kwenye ngozi, maumivu ya viungo na uvimbe. ilevile wanawake ambao ni wajawazito walioambukizwa ugonjwa huu wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla haijatimiza umri wake (preterm labor).

Kwa wale wanaoambukizwa kisonono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa vipofu, homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).

Kinga

Unaweza kujikinga na gonjwa hili la zinaa kwa njia zifuatazo. Kwanza kabisa ni kuwa mwaminifu katika ndoa na kujiepusha na uasherati. Kuchukua tahadhari na kuzungumzia

juu ya ugonjwa huo na dalili zake ili kuweza kufahamu kuwa mshirika wako wa ngono ana ugonjwa huo au la na iwapo anao hatua inayofuata ni kutibiwa na kupata ushauri wa daktari.

Njia nyingine ya kujikinga ni kuepuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono. Vilevile kutumia mipira (kondom) wakati wa kujamiiana na wanawake wajawazito

wanapaswa kuhakikisha kuwa wanahudhuria kliniki mapema ili waweze kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka iwapo watagundulika kuwa na ugonjwa wa kisonono au ugonjwa mwingine wowote.

Wajawazito wanashauriwa kujifungua hospitalini ili kama mtoto ameathirika na kisonono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa ili kuepusha kuwa kipofu na madhara mengine.

Matibabu na ushauri

Tiba ya ugonjwa wa kisonono inahusishwa na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya mawili ya zinaa huambatana pamoja.

Matibabu ya kisonono pia hutegemea umri wa mgonjwa. Kisonono ambacho si sugu kilicho kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, hutibiwa kwa dawa za

Cephalosporin, ambapo mgonjwa hupewa dozi moja ya dawa hizo pamoja na dawa aina ya Macrolide kwa mfano Azithromycin na za jamii ya Penicillin kwa mfano Doxycyclin kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Chlamydia.

Mara nyingi kwa wagonjwa walio na umri wa chini ya miaka 18 na wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano. Mgonjwa hutakiwa kufuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizo kwani nyingi huwa na madhara kwa wajawazito kwa mfano Doxycyclin.

Mbona haujaelezea hizo dalili kwa wanaume zinakuaje?
Mkuu Usisome tu Kichwa cha habari acha uvivu soma habari yote utaona nimesema kwa wanawake na Wanaumme. Angalia Maandishi mekundu hapo juu. Ninanukuu ( Kwa upande wa wanaume ugonjwa wa kisonono pia huweza kuwafanya wasipate watoto kwani huwasababishia uvimbe katika sehemu ya mbele ya korodani ambako

mbegu za kiume hutengenezwa. Uvimbe huo usipotibiwa husababisha utasa.
Ugonjwa wa kisonono au gono pia huweza kuathiri moyo, ubongo, ngozi na kadhalika

kwa hivyo ni hatari kwa mtu yeyote aliyeambukizwa kutokutibiwa mapema.
Pia ugonjwa huo huleta madhara au uvimbe kwenye maungio ya viungo, ambapo vimelea vinavyosababisha kisonono huweza kusambaa kwenye damu na kuleta )
 
Mpenzi wangu alikua anaumwa gono katibiwa bila kuniambia mimi sijui hili wala lile nikasex nae.

Jana nikaanza kuisi maumivu wakati wa kukojoa nilipo mwambia akaniambia ni gono daa nimechanganyikiwa.

Please ni dawa ipi naweza tumia nikapona kwasababu amesex na mimi kabla ya kumaliza dozi na mbaya zaidi sikujua kwasababu alikua mbali.

Msaada wenu jamani
 
Mpnz wangu alikua anaumwa gono katibiwa bila kuniambia mm cjui hili wala lile nikasex nae. jana nikaanza kuisi maumivu wakati wa kukojoa nilipo mwambia akaniambia ni gono daa nimechanganyikiwa. please ni dawa ip naweza tumia nikapona kwasababu amesex na mm kabla ya kumaliza doz na mbaya zaidi sikujua kwasababu alikua mbali. msaada wenu jamani

Hukumuuliza dawa aliyotumia?
 
Nimemuuliza kaniambia kua yy alichelewa hivyo aliandikiwa sindani tano na dawa ameisahau jina. hivyo kanishauri niwahi hospital
 
Unasubili nini kumuacha huyo anayekuambikiza gono?.kama amekuletea gona na ukimwi hauko mbali,mkimbie fasta hakufai


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Mpnz wangu alikua anaumwa gono katibiwa bila kuniambia mm cjui hili wala lile nikasex nae. jana nikaanza kuisi maumivu wakati wa kukojoa nilipo mwambia akaniambia ni gono daa nimechanganyikiwa. please ni dawa ip naweza tumia nikapona kwasababu amesex na mm kabla ya kumaliza doz na mbaya zaidi sikujua kwasababu alikua mbali. msaada wenu jamani
Dah watu wengine bana hospital zipo kwa ajili gani?si uende hospital
 
Nenda hospitali,hao bacteria ni hatari sana utaanza kukojoa usaha soon,after kupona achana na huyo gume gume! Grid ya taifa inakunyemelea!!
 
dawa zipo pia hazina gharama ila sindano zinachomwa kwenye mshipa mkuu, uyo jamaa hafai angekwambia kama alikua na maambukiz
 
Tumieni Condom jaman, na hujamuuliza yeye hilo gonjwa kalitoa wapi?
 
Kama alichomwa sindano hilo sio gono ni kaswende. Wahi hospitali na wewe ukadungwe hizo sindano. Ukipuuza baadae unaeza kuishia kuwa mgumba
 
Pole sana nenda hospital mpenz laa sivyo utakimbiwa kwa kunuka
 
We sema ukweli uling'oa changu kilabuni kwenye komoni huko ukapiga kavu sio kudanganya watu na akili zao eti demu wako. Hiyo ni kaswende kapimwe udungwe sindano na zinauma balaa usitafute tiba za vichochoroni. Kama hadi kesho utakua haujapata matibabu omba sana mkojo usikubane utajuta.
 
We xma ukwl kuwa ww ndo ulie mwambukiza aya kameze CIPROFLAXIN mg 500 au AZYTHROMYCIN note that naisseria gonorrhea wanakuwa sentve na antibiotic wakiwa in effctve stage..!!!! Kazi kwako 2mia kinga kila wakati
 
Back
Top Bottom