Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

Mkuu ana uhakika kuwa ni vidonda vya tumbo? Amefanya checkup gani akajua kuwa ni vidonda? Wataalam wanasema asilimia kubwa ya vidonda vya tumbo vinasababishwa na bacteria wanaoitwa H-plyori. Aliwahi kupima kama anao? Kama alipima akakuta anao alitumia dawa inavyopaswa? Hawa bakteria ni sugu sana na inabidi utumie mchanginyiko wa antibiotic aina mbili kwa muda wa wiki mbili na zaidi. Halafu baada ya mwezi na nusu au miwili ucheck tena kama wameisha. Halfu jambo la kuzingatia ni kuwa wakati wa kucheck usiwe umetumia antibiotic kwa muda au dawa nyingine zinazozoorodheshwa.
 
Nakuja kwenu wanajamvi kuomba msaada wa mawazo nifanyeje niweze kuondokana na tatizo hili sugu na lililonitesa kwa miaka 22 sasa.

Tatizo hili liligunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1995 hospitalini na nikaanza kutumia dawa na kufuata masharti mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuepuka aina fulani za vyakula na madawa na pia kubadili lifestyle.

Nikiri kuwa baada ya muda fulani baada ya kuanza matibabu nilipata nafuu kubwa hadi husahau maumivu ya tatizo hili lakini nilijitahidi kubaki katika masharti yale.

Baadaye tatizo lilianza upya na nikaanza kutumia dawa zile zile nilizotumia awali lakini sikupata nafuu. Nimebadilisha dawa mbalimbali lakini bado tatizo limeng'ang'ania. Baadhi ya dawa ninazokumbuka nilizotumia mpaka sasa ni: CIMETIDINE, RANITIDINE, OMEPRAZOLE, PANTOPRAZOLE, LANSOPRAZOLE na Antiacids za maji kama MILK OF MAGNESIA na RELCER GEL.

Nimewahi pia kutumia dawa za kienyeji kadhaa bila mafanikio. Mfano: Unga wa mbegu ya parachichi, mafuta ya ubuyu, asali mbichi na mdalasini, kuchemsha mmea wa mbigili n.k.

Nimeshawahi pia kupima H.PYLORI TEST mara 2. Mara moja nilikutwa Positive nikapewa HELIGO KIT dozi ya wiki 2 na nikaendelea na lansoprazole kwa wiki 2 zaidi. Nilipopima tena H.PYLORI ikasoma Negative lakini bado nikindelea kuumwa.

Mwaka jana nilifanyiwa kipimo cha OESOPHAGOGASTRODUODENOSCOPY hospitali moja ya rufaa na ripoti ya Daktari ilisomeka: "Multiple wounds found around the duodenum". Nilipewa dawa lakini bado sikuona nafuu kubwa.

Hivi leo nina siku ya 6 natumia TINIDAZOLE, LANSOPRAZOLE NA CLARITHRIMYCIN kwa pamoja na bado sijisikii nafuu yoyote. Maumivu ni makali, tumbo linauma na kutonesha (painful & tender), nikila chakula kidogo tu nasikia tumbo limejaa. Siwezi kulalia ubavu wa kulia tena sababu ya maumivu.

Usiku wa leo tumbo liliniuma sana mpaka jasho likanitoka japo kulikuwa na baridi.

Kwa ufupi nateseka jamani na nimekuja kwenu kama kuna mhanga kama mimi aliyewahi kuugua tatizo hili na kupona au madaktari mliomo humu jamvini mnisaidie jinsi ya kufanya.

Natanguliza shukurani nikiomba radhi pia kwa post ndefu. Nimelazimika kuandika hivi ili tatizo langu lieleweke vema.
ASANTENI!

Mwanajamvi mwenzenu anayeteseka.
Ndugu hebu tupe mrejesho kama uliweza pata tiba, kama bado nikupe ushauri mwingine.
 
Kingine cha muhimu na wengi tunasahau ni kuanza tiba bila kushughulika na chanzo hasa cha tatizo mara nyingi inakua ngumu kupona, mara nyingi vidonda husababishwa na kuzidi kwa tindikali tumboni hivyo ningekushauri jaribu kutumia vyakula vyenye uwezo wa kuondoa tindikali na kupunguza sumu ndo uanze matibabu na hakika utapona we mwenyewe utashangaa.
Anza kwa kutumia sana juice ya mboga mbichi za kijani, juice ya karoti na tango, watermelon vitakusaidia kwa sana.
Ndugu zingatia sana ushauri wa huyu jamaa. Muhimu sana kutambua chanzo cha tatizo na hakikisha unakiondoa.

Ni muhimu sana ukaweka bayana ni jambo fani unafikiri lilikupelekea kwenye tatizo hili. Kuna mambo kama kukaa na njaa kwa muda mrefu, mawazo yaliyopitiliza n.k

Lifestyle unayosema umeibadili ni muhimu ikawa inaondoa chanzo. Ni muhimu pia ukaweka bayana ni ligestyles fani umebadili ili ushauriwe zaidi.

Zingatia vyakula na kula kwa wakati. Umeshauriwa pia kutumia vyakula kama bamia za kichemsha, kunywa maziwa ya fresh ya viguvugu. Chemsha na kisha yapooze.

Watu wanasema hata mayai mabichi husaidia. Ninaongea haya kwa uzoefu pia. Nilisumbuliwa sana vidonda vya tumbo. Kuna wakati nilipoumwa sana nilikuwa ninakoroga yao bichi kwenye kikombe na kunywa. Jizoeshe pia kula mlenda. Hii inafanana na bamia lakini ukipata ule wa kienyeji kama ule wa singida, itakuwa vyema zaidi.

Epuka vyakula vya nyanya (nyingi) na uji wa ulezi. Unasemekana kukwangua tumbo na hivyo kutonesha vidonda.
 
Niko kwenye mpango wa kujaribu kila dawa hapa.

Mungu asimame. Ndani ya hili Juma moja sijalala mara tatu.
 
Niko kwenye mpango wa kujaribu kila dawa hapa.

Mungu asimame. Ndani ya hili Juma moja sijalala mara tatu.
Pole nimepitia hayo masahibu ninaelewa maumivu yake, ila wakati mwingine inakua ngumu kumshauri mtu atumie nn hasa kutokana na kutojua vidonda vyako vipo kwenye hatua gani. Ila kwa kukusaidia zingatia sana haya...
-epuka vyakula vyenye kusisimua tumbo kama limao, ndimu, pilipili energy drink zote na vyakula vilivyotiwa viungo vingi.
- kama ni mpenzi wa soda, juice za viwandani na pombe zipe talaka muda.
- pia vidonda tumbo husababishwa pia na kuishiwa kwa maji mwilini hivyo jitahidi kila unapoamka asubuhi unywe glass 2 za maji kabla hata ya kupiga mswaki, na uwe unakunywa maji nusu saa au lisaa limoja kabla ya kupata mlo wa mchana au jioni hii husaidia sana kupunguza asidi iliyopo mwilini.
- jitahidi pia kula matunda kama walivoeleza wadau wengine na mboga za majani kwa wingi. Matunda kama parachichi, tikiti tango ni mazuri zaidi.
- japo wengine wanashauri matumizi ya maziwa ila kiuhalisia ni hatari sana kwa wenye vidonda tumbo, tumia soya kama mbadala wa maziwa ile isiyokaangwa.
- achana na kahawa, chai ya rangi nayo si salama, ikiwa unaweza tumia tu mchaichai au soya drink.
- kikubwa zaidi zingatia muda wa kula na kunywa maji ya kutosha, ikiwa utajisikia bado muwako tumboni changanya kijiko kimoja cha chai baking soda(usikijaze sana) na maji glass 1 hii husaidia sana kupunguza tindikali mwilini.
Jaribu kwanza kuzingatia hayo, sikushauri kabisa kukimbizana na madawa ya hospital mie nilishayatumia zaidi ya miaka 10 hayakunisaidia chochote zaidi kutuliza tu maumivu kwa muda na baadae hali inarudi kama mwanzo... Baada ya mwezi mmoja ukiona hali bado tete lete mrejesho nikueleze nini utumie uondokana na hilo tatizo, ila naamini ukizingatia hayo maelezo hapo juu tatizo lako litaisha kabisa.
 
Mkuu ana uhakika kuwa ni vidonda vya tumbo? Amefanya checkup gani akajua kuwa ni vidonda? Wataalam wanasema asilimia kubwa ya vidonda vya tumbo vinasababishwa na bacteria wanaoitwa H-plyori. Aliwahi kupima kama anao? Kama alipima akakuta anao alitumia dawa inavyopaswa? Hawa bakteria ni sugu sana na inabidi utumie mchanginyiko wa antibiotic aina mbili kwa muda wa wiki mbili na zaidi. Halafu baada ya mwezi na nusu au miwili ucheck tena kama wameisha. Halfu jambo la kuzingatia ni kuwa wakati wa kucheck usiwe umetumia antibiotic kwa muda au dawa nyingine zinazozoorodheshwa.
Amepima na kakutwa na hao H-Plyor tena zaid ya Mara mbili kuhusu antibiotic katumia had I za Elfu 40 dose bado wamegoma had I madactar wameimshaur ahamie miti shamba
 
Amepima na kakutwa na hao H-Plyor tena zaid ya Mara mbili kuhusu antibiotic katumia had I za Elfu 40 dose bado wamegoma had I madactar wameimshaur ahamie miti shamba
Alitumia dose gani na ya muda gani? Dawa kuuzwa bei kubwa siyo kigezo cha kuponyesha! Inashauriwa mtu atumie dose ya siku 14 hata ikibidi na zaidi. Halfu iko combination ya dose mbalimbali, hivyo ikikataa moja unajaribu nyingine. Mambo mengine: 1: Anatumia dose kama inavyohitajika? Nauliza hivyo kwa sababu kuna watu wengine ni waoga dawa na anaweza kunywa siku kadhaa halafu akaachilia mbali. Tena unakuta ni mtu mzima kabisa na anajifanya kumeza kumbe hamezi. Hili nalo usilidharau. 2: Dawa anazotumia mna uhakika nazo? Siku hizi kuna dawa nyingi fake. Nunua dawa kwenye maduka yanayoaminika. 3. Una uhakika hapati uambukizo mpya? Hawa bacteria wanaambukiza kwa njia ya kula mboga au matunda yenye vimelea, au kutozingatia usafi wakati wa kutoka chooni au hata kama ana mpenzi/mume/mke anaweza kuwa namwambukiza. Na mwisho anapima na kupata matibabu sehemu ya uhakika? Bongo achana nayo kabisa ina hospital nyingi sana hawajui kupima.
 
Alitumia dose gani na ya muda gani? Dawa kuuzwa bei kubwa siyo kigezo cha kuponyesha! Inashauriwa mtu atumie dose ya siku 14 hata ikibidi na zaidi. Halfu iko combination ya dose mbalimbali, hivyo ikikataa moja unajaribu nyingine. Mambo mengine: 1: Anatumia dose kama inavyohitajika? Nauliza hivyo kwa sababu kuna watu wengine ni waoga dawa na anaweza kunywa siku kadhaa halafu akaachilia mbali. Tena unakuta ni mtu mzima kabisa na anajifanya kumeza kumbe hamezi. Hili nalo usilidharau. 2: Dawa anazotumia mna uhakika nazo? Siku hizi kuna dawa nyingi fake. Nunua dawa kwenye maduka yanayoaminika. 3. Una uhakika hapati uambukizo mpya? Hawa bacteria wanaambukiza kwa njia ya kula mboga au matunda yenye vimelea, au kutozingatia usafi wakati wa kutoka chooni au hata kama ana mpenzi/mume/mke anaweza kuwa namwambukiza. Na mwisho anapima na kupata matibabu sehemu ya uhakika? Bongo achana nayo kabisa ina hospital nyingi sana hawajui kupima.
Duuuuh ngoja nimuulize maana katumia dawa hadi huruma ....Mimi niliona moja inaitwa Omeplazole kitu kama hicho....
 
Duuuuh ngoja nimuulize maana katumia dawa hadi huruma ....Mimi niliona moja inaitwa Omeplazole kitu kama hicho....
Kwangu mimi naona kama tatizo lake kubwa huenda ikawa sehemu anazotibiwa siyo sahihi i.e. anatibiwa vi-hospital visivyo na utaalam wa kutosha. Hao bacteria kama ukienda hosptal yenye wataalam wanaisha. Halafu jambo muhimu ajaribu kuachana haya matibabu ya mtaani. Atajikuta anaongeza matatizo badala ya kupunguza. 1: Combination ya Amoxicillin 1000mgx2, clarithromycin 500mgx2 na lansoprazol 30mgx2 kwa siku 14 ni standard ya matibabu. Au mbadala wake ni combination ya: Tinidazole, clarithromycin na Lansoprazole. Lakini usijinunulie dawa bila kupima sehemu inayoeleweka na dr akuandikie!
 
Nakuja kwenu wanajamvi kuomba msaada wa mawazo nifanyeje niweze kuondokana na tatizo hili sugu na lililonitesa kwa miaka 22 sasa.

Tatizo hili liligunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1995 hospitalini na nikaanza kutumia dawa na kufuata masharti mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuepuka aina fulani za vyakula na madawa na pia kubadili lifestyle.

Nikiri kuwa baada ya muda fulani baada ya kuanza matibabu nilipata nafuu kubwa hadi husahau maumivu ya tatizo hili lakini nilijitahidi kubaki katika masharti yale.

Baadaye tatizo lilianza upya na nikaanza kutumia dawa zile zile nilizotumia awali lakini sikupata nafuu. Nimebadilisha dawa mbalimbali lakini bado tatizo limeng'ang'ania. Baadhi ya dawa ninazokumbuka nilizotumia mpaka sasa ni: CIMETIDINE, RANITIDINE, OMEPRAZOLE, PANTOPRAZOLE, LANSOPRAZOLE na Antiacids za maji kama MILK OF MAGNESIA na RELCER GEL.

Nimewahi pia kutumia dawa za kienyeji kadhaa bila mafanikio. Mfano: Unga wa mbegu ya parachichi, mafuta ya ubuyu, asali mbichi na mdalasini, kuchemsha mmea wa mbigili n.k.

Nimeshawahi pia kupima H.PYLORI TEST mara 2. Mara moja nilikutwa Positive nikapewa HELIGO KIT dozi ya wiki 2 na nikaendelea na lansoprazole kwa wiki 2 zaidi. Nilipopima tena H.PYLORI ikasoma Negative lakini bado nikindelea kuumwa.

Mwaka jana nilifanyiwa kipimo cha OESOPHAGOGASTRODUODENOSCOPY hospitali moja ya rufaa na ripoti ya Daktari ilisomeka: "Multiple wounds found around the duodenum". Nilipewa dawa lakini bado sikuona nafuu kubwa.

Hivi leo nina siku ya 6 natumia TINIDAZOLE, LANSOPRAZOLE NA CLARITHRIMYCIN kwa pamoja na bado sijisikii nafuu yoyote. Maumivu ni makali, tumbo linauma na kutonesha (painful & tender), nikila chakula kidogo tu nasikia tumbo limejaa. Siwezi kulalia ubavu wa kulia tena sababu ya maumivu.

Usiku wa leo tumbo liliniuma sana mpaka jasho likanitoka japo kulikuwa na baridi.

Kwa ufupi nateseka jamani na nimekuja kwenu kama kuna mhanga kama mimi aliyewahi kuugua tatizo hili na kupona au madaktari mliomo humu jamvini mnisaidie jinsi ya kufanya.

Natanguliza shukurani nikiomba radhi pia kwa post ndefu. Nimelazimika kuandika hivi ili tatizo langu lieleweke vema.
ASANTENI!

Mwanajamvi mwenzenu anayeteseka.
mkuu nakushauri mimi nilikuwa nalo hilo sema sio mda mrefu kama wewe kabla ya yote, nenda kanunue dawa za amoeba meza, hata siku mbili haziishi itakuwa sawa. niamini kama ukifata ushauri wangu naomba marejesho. maana mimi nilisumbuliwa hadi nalia kama mtoto mateso yake asikuambie mtu na unaenda hosp dokta anakuambia haoni tatizo ila saizi niko sawa kabisa japo kuna madogo madogo ya ku fix.
 
nilawahi kusumbuliwa sana na tatizo hilo ila nashukuru numepoa. Ila kiukweli siwezi kumbuka nini hasa kilichoniponesha mana nilitapatapa na vitu vingi sana mwisho nikajikuta tu nishapoa. ila kwa vichache ninavokumbuka ni hivi

- nilitumia kunywa mafuta ya habasoda kila siku kijiko kimoja cha chai.
- Juice ya kerotti kila siku glass mbili moja kabla ya kula chochote asubuh na nyengine usiku. (ni karoti tupu na maji kidogo tu yakusagia bila ya sukari)
- nilitumia kula unga wa uwatu kila siku kutwa mara 3 kijiko kimoja cha chakula nachangaya na maji ya uvuguuvugu glass moja.
- na pia nilikua nikitumia kula manjano (japo kijiko kimoja kwenye maji na Thomu japo punje 3
 
Mimi nilikuwa natafuta kabichi mbechi kila siku, ndani ya wiki 2 maumivu yaliisha kabisa
 
Jamaa kapatwa na tatizo symptoms alizonazo ni pamoja na halitosis,bitter test throught the day
Msaada tafadhari medical expert
 
Bacteria that cause stomach ulcers and cancer could also be giving us bad breath, according to research published in the Journal of Medical Microbiology. For the first time, scientists have found Helicobacter pylori living in the mouths of people who are not showing signs of stomach disease.
 
Ahsante sana kwa maelezo na matibabu ya vidonda vya tumbo.

Naomba kuuliza kama kuna dawa ya kutibu homa ya ini HBV ikapona kabisa.
 
Back
Top Bottom