Ugumu wa Maisha ni hatari kwa usalama wa Taifa, serikali ichukue tahadhari

Ugumu wa Maisha ni hatari kwa usalama wa Taifa, serikali ichukue tahadhari

RNA

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2013
Posts
1,647
Reaction score
2,803
Ni ukweli mchungu kwamba mtaani hali ni ngumu sana kuanzia upatikanaji wa pesa mpaka bei za bidhaa. Binafsi, mbali na kwamba ni muajiriwa, lakini pia najishughulisha na biashara zinazogusa moja kwa moja wananchi, kwa hiyo ninachoandika nina kifahamu vizuri.

Kwa hali ilivyo sasa, anaweza tokea mtu au mwanaharakati akaunganisha watu kufanya maandamano makubwa sana ambayo yanaweza yasiishe salama.

Watanzania ni wapore sana, lakini njaa inaweza kumfanya mtu afanye chochote kile.

Hivyo, Bunge na serikali kwa ujumla, suala la ugumu wa maisha, hususani bei za vyakula, fanyeni kitu kupunguza ugumu huo.
 
Kati ya CCM na andazi unachagua nini?

Nilishawahi kusema sehemu kuwa, Siku watanzania wakichoka na kuamua kuiingia barabarani, Jumuiya za kimataifa zitaiingiliaa na damu itamwagika na hapata kalika


Iwafikie CCM kwenye jalada
 
Kati ya CCM na andazi unachagua nini?

Nilishawahi kusema sehemu kuwa, Siku watanzania wakichoka na kuamua kuiingia barabarani, Jumuiya za kimataifa zitaiingiliaa na damu itamwagika na hapata kalika


Iwafikie CCM kwenye jalada
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
kwa sasa maisha sio magumu kama yalivyokuwepo kipindi cha mwendazake, wamejitahidi. wafanyabiashara wanajua hili. wanaoendelea kulalamika subirini wawaletee pesa nyumbani kwenu.

wewe mpumbavu unaongea takataka.

Mwaka juzi mwezi wa sita tulikuwa tunanunua mchele kulo 1600 leo unanunua 3200 ongezeko la asilimia 100% ndani ya miezi 24

umeshiba kande unakuja kuongea ujinga hapa.
 
kwa sasa maisha sio magumu kama yalivyokuwepo kipindi cha mwendazake, wamejitahidi. wafanyabiashara wanajua hili. wanaoendelea kulalamika subirini wawaletee pesa nyumbani kwenu.
Na hili ndio jibu lake. Piga kazi kiongozi
 
Mkuu huu ugumu wa maisha ni kwasababu ya
I) Recover ya Covid effect.. Makampuni mengi yalishindwa kufanya kazi

II) Mataifa makubwa kutuma fedha nyingi na vifaa vya kijeshi sehemu moja Ukraine

III) La mwisho ni effect mbaya ya uchumi kwa uongozi wa Magufuli Tanzania... Jamaa alileta uoga kwa wafanyabiashara wakubwa kutumia hela hata kama ni halali.. Suala hili lilidumaza mzunguko wa hela na benki nyingi ziliyumba hasa kwenye kutoa mikopo

Hata hivyo Serikali inajitahidi sana.... Na kiasi fulani Samia anashaurika hasa masuala ya kiuchumi na kubalance mikopo ya nje ...

Hali mbaya itaanza kuimarika kuanzia mwakani tuombe mabalaa ya vita yasiongezeke... na Serikali kujikita kwenye kuongeza bajeti ya kilimo
 
kwa sasa maisha sio magumu kama yalivyokuwepo kipindi cha mwendazake, wamejitahidi. wafanyabiashara wanajua hili. wanaoendelea kulalamika subirini wawaletee pesa nyumbani kwenu.
Wafanyabiashara wanapandisha bei jinsi wanavyotaka
 
wewe mpumbavu unaongea takataka.

Mwaka juzi mwezi wa sita tulikuwa tunanunua mchele kulo 1600 leo unanunua 3200 ongezeko la asilimia 100% ndani ya miezi 24

umeshiba kande unakuja kuongea ujinga hapa.
hizo hasira hadi kunitukana ni kwamba hauna uwezo kununua mchele kili moja 3200? piga kazi mjomba upunguze hasia zisizo na sababu. tafuta hela.
 
Hapa nilipo Mimi vibaka wameongezeka wanaiba kuku masufuria, wanaloa nguo madirishani na kila kitu wanachokiona kinaweza kuuzika,
Hivyo hali ni mbaya mitaani.
Biashara ngumu sababu mzunguko wa hela ni mdogo sana.
Na Kuna akina mama walikopeshwa wengi wao wameshindwa kulejesha na matokeo yake wanakimbia familia zao.
Na wengine wanafirisiwa na kuwa masikini zaidi.!
 
Hapa nilipo Mimi vibaka wameongezeka wanaiba kuku masufuria, wanaloa nguo madirishani na kila kitu wanachokiona kinaweza kuuzika,
Hivyo hali ni mbaya mitaani.
Biashara ngumu sababu mzunguko wa hela ni mdogo sana.
Na Kuna akina mama walikopeshwa wengi wao wameshindwa kulejesha na matokeo yake wanakimbia familia zao.
Na wengine wanafirisiwa na kuwa masikini zaidi.!
biashara ngumu, lakini hapahapo kuna sisi wenzenu tunasema biashara ni nzuri na bora kuliko kipindi kile. kwa watu wanaojishughulisha, kipindi hiki maisha yatakuwa mazuri, ila kwa wale wapenda mteremko na watazama tamthilia, watalalamika kama wewe siku zote. tafuta kazi, tafuta biashara, fanya, sasahivi mazingira yamebadilika. sio kama kipindi kile cha mwendazake ambapo kila mtu aliishi kama mashetani.
 
Hakika
Kati ya CCM na andazi unachagua nini?

Nilishawahi kusema sehemu kuwa, Siku watanzania wakichoka na kuamua kuiingia barabarani, Jumuiya za kimataifa zitaiingiliaa na damu itamwagika na hapata kalika


Iwafikie CCM kwenye jalada
 
Sio kwa watz ninao wajua yaani tz kufa ufufuke hakiwezi tokea kitu kama hicho sababu ni unafiki jamii yawanafiki haijawahi panga jambo likafanikiwa kwahio bro wetetea tumbo lako na familia yako
 
biashara ngumu, lakini hapahapo kuna sisi wenzenu tunasema biashara ni nzuri na bora kuliko kipindi kile. kwa watu wanaojishughulisha, kipindi hiki maisha yatakuwa mazuri, ila kwa wale wapenda mteremko na watazama tamthilia, watalalamika kama wewe siku zote. tafuta kazi, tafuta biashara, fanya, sasahivi mazingira yamebadilika. sio kama kipindi kile cha mwendazake ambapo kila mtu aliishi kama mashetani.
Mimi ninayesema haya nipo field na ushahidi wa haya ninayoyasema ninao.
Wewe pengine ni mwaajiriwa au ni kaka, dada au ni mtoto wa mwaajiriwa, hivyo haya yote huwezi jua.
 
Back
Top Bottom