Ugumu wa maisha ni jambo la kusadikika halipo kiuhalisia na sijawahi kuliona na halitatokea

Ugumu wa maisha ni jambo la kusadikika halipo kiuhalisia na sijawahi kuliona na halitatokea

Kwahio kila mtu ana basic needs ? (Chakula, Mavazi na Malazi) nadhani pamoja na gazeti lako ulikuwa unataka kusema kwamba ugumu wa maisha unatokana na uzembe wa mtu kutokurahisisha maisha yake...

Nami nakuuliza wale waliopo vitani sasa hivi..., au waliolima vanilla wakakosa masoko na hata kurudisha gharama ya kununua mbegu na hivyo kufirisika au wale wanaolipa kodi na matozo lakini watunga sera wanashindwa kuwaletea huduma au wale waliouza shamba na kusoma waje wawe wauguzi leo unawaambia wakauze uji.... (Je hao pia ni uzembe wao)?
 
Maisha magumu ni pamoja na mkulima wa Hanang mazao yake kuliwa baada ya mchunga ng'ombe wa Hanang kupitisha ng'ombe shambani kwake.
 
Maisha magumu ni mchungaji ng'ombe wa Hanang aliyepata mtaji wa kufungua biashara kulimbikiziwa kodi na tozo pindi anapoanza biashara tu.
TRA wanasikiliza mtu ambaye anafungua biashara unapewa msahama, wewe nenda kawaeleze ukweli jamaa wanapenda mtu mkweli
 
Maisha magumu ni pamoja na mchunga ng'ombe wa Hanang aliyegeuka fundi umeme kujenga nyumba yake kisha ikabomelewa akiwambiwa amevamia eneo la mtu au serikali.
 
Kiuhalisia kabisa hakuna kitu kinachothibitisha UGUMU WA MAISHA!
Hili ni jambo la kufikirika tu ambalo viumbe na wanadam waliamua kuyabatiza maisha!

Binadamu kaumbwa na akapewa mazingira ayatawale! Sasa unaposema MAISHA Ni MAGUMU mimi huwa simuelewi Magumu kwa kuyalinganisha na yepi?

Binadamu kapewa mazingira ili yampatie chakula, na chakula kipo aina nyingi tu!
Taarifa Alizonazo mtu kuhusu mazingira ndizo humfanya ashibe au aliye njaa!

Lakini kiuhalisia ugumu wa maisha hili jambo halipo!

Kuna watu mtakuja nakusema labda mimi ni mtoto wa kishua!
Story ya maisha yangu nilishwahi kuiweka humu!

Mimi nilipomaliza msingi wazee walilalamika ooh Maisha magumu sijui hawana Ada, Nikawaambia Mbona hatuna maisha magumu sisi!
Nikaondoka nikaenda Hanang'i kuchunga ng'ombe! Pamoja na kuchaguliwa kwenda shule maalum ya vipaji (moshi technical) lakini nilikubali kwenda kuchunga ng'ombe kwanza!

Nikiwa polini maisha yalikuwa matamu sana, nilikula matunda aina nyingi, nilichoma nyama nipendayo, nilicheza michezo ambayo binadamu ilinipa furaha, nilifunza dawa nyingi mno karibia 1200 za kutibu magonjwa mbalimbali!

Wakati wa likizo wala sikushangaa hao waliokwenda secondary waliporudi nakunikuta nachunga ng'ombe!

Hadi pale nilipotosheka nikapatiwa zawadi ya ng'ombe na kwenda kusomea ufundi umeme!

Baada ya kumaliza nilijiajili, nimefanya kazi za umeme ndani ya nchi na inje ya nchi, nimefanya kazi za umeme na wachina, wafrika, wafilipino, wajerumani, wajapan n.k!
Hadi sasa nafanya kazi zangu za umeme sijui kuhusu ugumu wa maisha!

Juzi wakati natokea Dodoma nilipita kwrnge gereza moja hapo morogoro kumsalimia moja ya tuliofaulu nao darasa la saba, wakasoma ngazi za master huko nilimkuta pale jamaa anatumikia kifungo baada ya taasisi aliyokuwa anaisimamia kupata hasara ya mabilioni ambayo inadaiwa kama waliyaiba!...Bado nilipomtembelea nilimwambia jamaa Hakuna ugumu wa maisha nikampatia na mifano hai nikamsihi avumilie kifungo kuna fursa mbele!

Mungu karuhusu tuje hapa duniani tukiwa kama sisi, na mazingira ya kuishi yashaandaliwa!
Tatizo kubwa la wanadamu wengi tunapenda sana kujilinganisha na wengine! Baada ya kujilinganisha ndiyo tunakuja na ubatizo wa MAISHA MAGUMU!

Kiuhalisia hakuna kitu kinachothibitisha maisha magumu! Mimi nafanya kazi za umeme, siku watu wasipojenga naanza kutibu watu ninajua dawa zaidi 1200.

Ukiachilia kujua dawa ninao uwezo wa kuangalia eneo mazingira na mimea ardhini nikagundua uwepo wa maji ukichimba au hakuna!

Nina uwezo wa kukaa msituni na wanyama wakali na wasinifanye chochte kwa kutumia mimea hiyo hiyo iliyopo porini!

Sasa hayo maisha magumu ni kitu gani, unayalinganisha na nini hadi uthibitishe maisha ni magumu?

Narudia tena kushindwa kutumia mazingira ndiko wengi kunawalaza njaa! Lakini hakuna kitu kinaitwa maisha magumu

Mazingira yanasifa kama silaha; Usipojua kuyatumia unaweza kujimaliza mwenyewe!
Maisha magumu yanawekwa na viongozi wa nchi na nchi zinatoka kutawala wengine. Ila ukiingia level flani ya kujitambua unaweza kuona picha yote. Lakini ni wachache watafika huko.
 
Maisha magumu ni pamoja na mchunga ng'ombe wa Hanang aliyegeuka fundi umeme kufungwa kwa kesi ya kuiba vifaa vya umeme mahali alipopewa kazi ya ufundi umeme.
 
Maisha magumu ni pamoja na wachunga ng'ombe walioko Hanang kuumwa mbu msituni kuugua malaria na kushindwa kwenda hospital kupata tiba
Yapo majani ukiyala ladha ya damu inabadilika inakuwa kama na uchungu, baadhi ya vyakula ukila MBU hawakudhuru!
Mambo ya neti nimekuja kuyakuta mjini, miaka yote niko porini sijawahi umwa maralia mimi
 
Maisha magumu ni pamoja na mke wa mchunga ng'ombe wa Hanang kupotelewa na mume wake asijue alipo kama ameliwa na fisi porini, ametumbukia korongoni au ametekwa.
 
Yapo majani ukiyala ladha ya damu inabadilika inakuwa kama na uchungu, baadhi ya vyakula ukila MBU hawakudhuru!
Mambo ya neti nimekuja kuyakuta mjini, miaka yote niko porini sijawahi umwa maralia mimi
Kuna wachunga ng'ombe wengi wa Hanang wanaugua malaria kila siku.
 
Kiuhalisia kabisa hakuna kitu kinachothibitisha UGUMU WA MAISHA!
Hili ni jambo la kufikirika tu ambalo viumbe na wanadam waliamua kuyabatiza maisha!

Binadamu kaumbwa na akapewa mazingira ayatawale! Sasa unaposema MAISHA Ni MAGUMU mimi huwa simuelewi Magumu kwa kuyalinganisha na yepi?

Binadamu kapewa mazingira ili yampatie chakula, na chakula kipo aina nyingi tu!
Taarifa Alizonazo mtu kuhusu mazingira ndizo humfanya ashibe au aliye njaa!

Lakini kiuhalisia ugumu wa maisha hili jambo halipo!

Kuna watu mtakuja nakusema labda mimi ni mtoto wa kishua!
Story ya maisha yangu nilishwahi kuiweka humu!

Mimi nilipomaliza msingi wazee walilalamika ooh Maisha magumu sijui hawana Ada, Nikawaambia Mbona hatuna maisha magumu sisi!
Nikaondoka nikaenda Hanang'i kuchunga ng'ombe! Pamoja na kuchaguliwa kwenda shule maalum ya vipaji (moshi technical) lakini nilikubali kwenda kuchunga ng'ombe kwanza!

Nikiwa polini maisha yalikuwa matamu sana, nilikula matunda aina nyingi, nilichoma nyama nipendayo, nilicheza michezo ambayo binadamu ilinipa furaha, nilifunza dawa nyingi mno karibia 1200 za kutibu magonjwa mbalimbali!

Wakati wa likizo wala sikushangaa hao waliokwenda secondary waliporudi nakunikuta nachunga ng'ombe!

Hadi pale nilipotosheka nikapatiwa zawadi ya ng'ombe na kwenda kusomea ufundi umeme!

Baada ya kumaliza nilijiajili, nimefanya kazi za umeme ndani ya nchi na inje ya nchi, nimefanya kazi za umeme na wachina, wafrika, wafilipino, wajerumani, wajapan n.k!
Hadi sasa nafanya kazi zangu za umeme sijui kuhusu ugumu wa maisha!

Juzi wakati natokea Dodoma nilipita kwrnge gereza moja hapo morogoro kumsalimia moja ya tuliofaulu nao darasa la saba, wakasoma ngazi za master huko nilimkuta pale jamaa anatumikia kifungo baada ya taasisi aliyokuwa anaisimamia kupata hasara ya mabilioni ambayo inadaiwa kama waliyaiba!...Bado nilipomtembelea nilimwambia jamaa Hakuna ugumu wa maisha nikampatia na mifano hai nikamsihi avumilie kifungo kuna fursa mbele!

Mungu karuhusu tuje hapa duniani tukiwa kama sisi, na mazingira ya kuishi yashaandaliwa!
Tatizo kubwa la wanadamu wengi tunapenda sana kujilinganisha na wengine! Baada ya kujilinganisha ndiyo tunakuja na ubatizo wa MAISHA MAGUMU!

Kiuhalisia hakuna kitu kinachothibitisha maisha magumu! Mimi nafanya kazi za umeme, siku watu wasipojenga naanza kutibu watu ninajua dawa zaidi 1200.

Ukiachilia kujua dawa ninao uwezo wa kuangalia eneo mazingira na mimea ardhini nikagundua uwepo wa maji ukichimba au hakuna!

Nina uwezo wa kukaa msituni na wanyama wakali na wasinifanye chochte kwa kutumia mimea hiyo hiyo iliyopo porini!

Sasa hayo maisha magumu ni kitu gani, unayalinganisha na nini hadi uthibitishe maisha ni magumu?

Narudia tena kushindwa kutumia mazingira ndiko wengi kunawalaza njaa! Lakini hakuna kitu kinaitwa maisha magumu

Mazingira yanasifa kama silaha; Usipojua kuyatumia unaweza kujimaliza mwenyewe!
Samico Tanzania 🇹🇿
 
Umeshawahi kuwa mtu mwingine ambaye ni tofauti kabisa na wewe?

Maana umetoa personal experience tu na kufanya kama vile kila mtu anaweza kuishi kama wewe.
Niwe mtu mwingine vipi wakati niliumbwa ili nije kuishi mimi na si mwingine!

Yaani umeumbwa kuwa JUMA ila wewe unataka uishi kama ROSE si ndiyo mwanzo wa mashoga kuwepo kwa style hii
 
Maisha magumu ni pamoja na mchunga ng'ombe wa Hanang kuporwa mifugo yake na wezi wa mifugo huko porini.
 
Maisha magumu ni pamoja na mchunga ng'ombe wa Hanang kuporwa mifugo yake na wezi wa mifugo huko porini.
Mimi nilikwambia yalinikuta mengi, Kuna siku nilikuwa porini wakaja watu na mapanga nikatimua mbio kuelekea nyumbani!
Kundi lote la mifugo lilitimua mbio kunifuata nyuma.. Mifugo wanauwezo wa kusoma alama ya hatari kutoka kwa mchungaji! Hilo nalo ni somo jinngine nitakuja kuwafundisha humu
 
Niwe mtu mwingine vipi wakati niliumbwa ili nije kuishi mimi na si mwingine!

Yaani umeumbwa kuwa JUMA ila wewe unataka uishi kama ROSE si ndiyo mwanzo wa mashoga kuwepo kwa style hii
Sasa mbona wewe unataka watu waweze kulazimisha waishi kama wewe wakati wao si wewe?

Yani wewe una miguu unaweza kutembea bila msaada, unalazimisha kiwete asiye na miguu atembee kama wewe? Unamshangaa kwa nini hawezi kutembea na kusema tatizo la mtu kushindwa jutembea halipo, kwa sababu wewe unaweza kutembea bila msaada?
 
Back
Top Bottom