Uhamiaji ianze uchunguzi jinsi watoto wa Lissu, ambao ni raia wa Marekani walipata passport za Tanzania, kama Lissu alidanganya, ashughulikiwe

umeleta hoja dhaifu, dunia iko mbali sana kuliko unavofikiria wewe endelea na mawazo yako ya kijamaa na wana ccm wenzako ndio maana kwenye andiko lako unazomewa na kila mtu ujue umefanya utoto
 
Tafuta pesa brooo,wenye pesa hawafikiriii kura utumbo wa kuku
 
Acha kelele zako hapa. Una uhakika gani kama kada yote ya CCM haina passport za Tanzania na za nchi za nje? Watoto wao ndiyo usiseme. Wewe unafikiri Rais wako Samia hana Passport ya Oman? Je, watoto wake umewafawanyia uchunguzi?

Sasa kama waziri wa nchi za nje AD Mulamula watoto wake wapo Marekani itashindikana kwa Rais wetu na baadhi ya Makada wakubwa wa chama tawala watoto wao kuwa na status hiyo?

Kama huna cha kuandika afadhali nenda kalale na mkeo, anakusubiri. Kujikombakomba kwa namna hii ili uonekana kwa ajili ya position serikalini ni ugonjwa usioponyeka kama hujui. Utakuwa umepungukiwa na neuron ya ku reason vitu. Kwa maana nyingine hauko sawa kichwani.

Nchi yetu imeuzwa tayari na inashikiliwa na majasusi wanaojiita wana CCM.

CCM imewateka watanzania kimabavu kwa kutumia vyombo vya Dola na kuwalazimisha watanzania kumsujudu mwenyekiti wa chama chao ambaye ndiyo Rais wa nchi kuwa Mungu. Samia ni Mungu wa watanzania kwasababu hakuna kitu kina fanyika bila yeye.

Halafu mnadanganywa eti Tanzania kuna amani! Kuna amani Tanzania? Huo ni ukandamizwaji. Amani gani ambayo inawafanya watu wasiwe na mlo? Amani gani ambayo inawafanya watu pia wasiwe na basic things kama maji na nishati? Amani gani hiyo ambayo watu hawaruhusiwi kupaza sauti zao kwenye Demonstration?

Hujui kumzuia mtu kudai haki zake za maisha kwa kufanya peacefull Demonstration ni violation ya haki za binadam?

Hujatambua tu bado kuwa wale mabalozi wa nchi kubwa za Ulimwengu walio kuwa wakibwata kuhusu haki za binadam enzi za hayati Magufuli, hawabwati tena? Hujatambua bado kuwa hivi sasa wapinzania wako kimya hawapigi kelele tena?

Kama hujui na hujalitambua hilo, basi ujue kuwa nchi imeshaachiwa walaji wa kimataifa ambao walikuwa wanavuna nchini bila kupanda. Tanzania imekuwa shamba la bibi tena. Yule aliyekuwa anawazuia wamesha mpeleka ahela tayari.

Sasa nchi imerudi tena mikononi mwa Mungu mtu ambaye ana determine kila kitu cha watanzania. Na wageni ndiyo wanaofaidika na rasilimali zetu.

Watanzania amkeni na tuanze kudai haki zetu colectivelly. Twendeni tuka anadamane ndugu zangu kudai haki zetu. Nchi yetu lazima irudi mikononi mwetu.
 
mtu mzima unapata wapi muda wa kuandika utumbo wa namni hii.
Samahani mkuu, article yangu sikukulenga wewe. Nili ku-refer kimakosa. Nimeyasaihihisha sasa.

Pole sana ndugu yangu. Nafikiri ulilielewa lengo lango. Pole Pole sana. [emoji120]
 
Mtoto wa Mtanzania hata kama amezaliwa nje, anaweza kupewa passport ya TZ. Isipokuwa akipewa passport, ukomo wa passport ni kabla ya kutimiza miaka 18.

Baada ya kutimiza miaka 18, mtoto anaruhusiwa kuomba passport mwenyewe kama mtu mzima. Kwa hiyo kusema achunguzwe baba au mama, tunaingia kwenye siasa mno kuliko kutumia sheria. Mchukie Lissu, lakini usiwachukie au kuwahusisha watoto wake kwenye chuki ambazo si zao! Raisi Mwinyi aliita hii "wivu wa kike".
 
Unaelewa Nini maana ya uraia au umetumwa na Machawa kuleta uzi.
Lini Lissu aliishi Marekani na akapata watoto huko.

Ndio kunazo njia unaweza kuwazalia huko. Ila hii ya kwako haina mantiki yote ni Uchawa tuu.
Tafuta pesa ya kutunza mko na watoto wako haya hayana mantiki kwako kalaghabaho!
Unaifundisha uhamiaji kazi!!
 


Tatizo tuna mambu mbu mbu wengi sana siku hizi hapa JF. Watoto wa chini ya miaka 18 wanaweza kuwa na Uraia wa nchi zaidi ya moja mpaka waamue wanataka kuwa raia wa wapi wakifikisha miaka 18.

Ili mradi mzazi mmoja awe na passport ya TZ. Watoto wa ndugu yangu miaka 7 wana passport ya canada, US na Tanzania . Baba yao ana uraia wa US, Mama TZ na wamezaliwa Canada
 
Uzalendo unaanzia nyumbani. Ajiuzulu uongozi wa chama chake na siasa za Tanzania kiujumla. Wapo Watanzania wengi kwenye situation kama yake wanafanya aliyofanya kwa manufaa ya watoto wao, lakini hawafanyi maigizo ya kujifanya Wazalendo namba moja kama yeye hadi kufikia kuusaka uongozi wa nchi.
 
Matoto ya Lissu ni mazee kabisa
 
Naona umelewa chimpumu
 
Alisema mzee Lowassa-
Elimu,
elimu,
elimu
Elimu duni imekuwa ni changamoto kubwa sana. Unakuta mtu kashupalia jambo ambalo hana uhakika nalo na anakuwa mbishi hata anapoelimishwa wakati ni mjinga tu.

Ujinga unapozidi unageuka na kuwa upumbavu hasa mjinga anapojifanya mjuaji na hataki kuelimishwa.
 
Matoto ya Lissu ni mazee kabisa

Hata kama wana Uraia wa US so what? Ujue tu Tanzania bado kuna katiba ya kikoloni kuliko hata za hao wakoloni! . Kenya haya mambo ya kijinga ya uraia wamesha weka sawa sisi tuna baki kuangaliana na kushindana na diaspora kama watoto
 
Bila kuweka umri hapa, hatuwezi jenga hoja, kisheria/katiba, mtoto chini ya miaka 18 anaweza kuwa na passport au uraia pacha. Anatakiwa atakapofikisha miaka 18, aukane mmoja kati ya hizo 2.

Je watoto hao wa Lissu wana umri gani?
 
mleta uzi utakuta hata umeme wala maji ya kuoga halina linapoishi, na linaishi kwa upigaji tuu
 
Haya ndiyo matatizo ya kuwa mgombea binafsi, hujui kama Tundu Lissu siyo Mmarekani. Akishinda Urais wa Tanzania halafu Mungu apishie mbali akafa, "warithi" wake, first of kina, ni wanawe wa Marekani, watarithi mali zake zikiwemo nyaraka zake na other private documents zinazohusu Taifa, zikaangukia mokononi mwa adui.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…