Uhamiaji Tanzania: Bila dhumuni la safari hakuna kupewa pasi ya kusafiria (Passport)

Uhamiaji Tanzania: Bila dhumuni la safari hakuna kupewa pasi ya kusafiria (Passport)

Tunarudi miaka mingi nyuma kwa kasi
Labda baadhi ya Viongozi wanawaza kinyume nyume, badala ya kufocus mbele.

Tatizo ni uongozi.
Ndiyo maana Dr. John C. Maxwell kasema, " Everything rises and falls on leadership"

Kama viongozi wanawaza kwa kurudi nyuma badala ya kusonga mbele, na matunda ya kazi zao yatakuwa vivyo hivyo.

Hiyo inatoa picha ya mitazamo ya Viongozi. Baadhi yao wangali wakiwaza kijima.
 
Ujue HUU NI UPUMBAVU.

Passport ni haki ya kila raia kuwa nayo.haijalishi una safari au hauna. Passport sio mali ya uhamiaji.

Acheni UKOLONI.

Yaani siku nikipata safari ndo nianze kuhangaika kutafuta passport?
Sidhani kama Wakoloni wangefanya ukatili kama huo! Wanaojua faida ya watu kutoka.
 
H
Man!!!!!!!!! Jamani mbona kila kukicha kila aliepewa madaraka anajifanya kuwa mbabe na kutoa amri za ajabu sana?

Hivi alitoa uamuzi huu hata alifikiri kwanza? Mtu tuseme anataka kwenda kusoma au kutembea nchi fulani, inabidi uombe visa, utaombaje visa bila ya kuwa passport. Mtu hatoki tu akaenda kununua tiketi ya kusafiri bila ya kuwa na uhakika wa kupata visa ya huko anakotaka kwenda.

Hawa jamaa hivi kweli wao wenyewe walishajaribu hata kusafiri nje ya nchi? Mfumo mzima wa kusafiri kwanza ni kuwa na lengo na uwezo wa kusafiri, unapata passport kisha unaomba visa. Unapoomba visa ndio unapoonyesha kwa ubalozi husika uwezo wako wa kununu ticket, lengo la safari yako, mdhamini wako, unapofikia n.k. Unapokubaliwa na kupewa visa ndio unanunua ticket ya kuondoka nchini.

Sasa hawa wanaotaka mtu anunue ticket ya safari ilhali hujui lini utaipata passport au hata akama utaipata si wana vichaa. infacts, mashirika mengi duniani siku hizi unaponunua ticket za ndege unatakiwa ujaze details zako na za passport yake, sasa mtu atajaza nini ikiwa hana passport?
Hata tiketi za mabasi yanayoenda nchi za nje, details za passport zitahitajika.
 
Hii ndio taarifa mpya kutoka Uhamiaji iliyotolewa leo na Msemaji wake Paul Mselle.
View attachment 1727162
Paul Mselle amesema haya...

Pasi ya kusafiria ni 'document' ya kiusalama na ni haki ya kiusalama na ni mali ya Serikali, pale ambapo mtu ataitumia vibaya basi anaweza akanyang’anywa

Pasi ya kusafiria sio kitambulisho kusema mtu achukue abaki nayo ndani ni lazima kuwe na dhumuni la safari, kama hauna safari hatuwezi kukupa pasi ya kusafiria

Mtu atakayepoteza Pasi yake ya kusafiria (Passport), itamlazimu kutoa taarifa Polisi pamoja na kutangaza kwenye gazeti na kwamba ni lazima atoe kiasi cha shilingi Laki tano kwa kupoteza Passport hiyo, na ili aweze kupata nyingine.

Kumekuwa na changamoto ya kuchelewa kwa pasi ya kusafiria sababu unakuta mtu hajakamilisha vigezo vya kupata pasi ya kusafiria. Kuna wengine wanawasilisha vyeti vya kuzaliwa ambavyo haviko kwenye mfumo wa RITA na ukimuuliza alikipataje anasema alimtuma mtu kwa maana ya vishoka na hawa unakuta wengine ni raia wa Tanzania na wengine sio raia wa Tanzania

Wengine nao unakuta taarifa za cheti cha kuzaliwa zinatofautiana na taarifa za vitambulisho vya Taifa, unakuta kwenye Kitambulisho cha TAIFA(NIDA) kazaliwa Temeke kwenye cheti kazaliwa Morogoro.

Passport.png
Yaani hawa watu weusi hawaamini kabisa kama mkoloni alishaondoka na Mwafrika yuko huru sasa, walichorithi ndio wanasimama nacho. wanachobhana hata ukiwauliza wenyewe hawajui
 
Sisi tunatafuta scholarships, kwenye Application wanataka namba za passport itakuaje
Hawafikirii hivyo wenzio.
Wapo pale kuwapa wahindi na wachina vibali vya kuja kuchoma mahindi kariakoo na kufanya kazi ambazo watz wanaziweza.
Unajua Tanzania Kuna Malaya wengi Sana wa kichina na kihindi.
 
Na hiyo ni mbali na pesa ambazo wangeziingiza nchini watakapofanikiwa huko nje.

Wana ndugu zao Tanzania, wakiwatumia pesa haitaadhiri kwa namna chanya mzunguko wa pesa nchini?

Kuna watakaohitaji kujenga. Huoni huko nako ni faida kwa Watanzania na Tanzania kwa ujumla.

Je kwa wale watakaorejea nchini kuwekeza baada ya kukusanya mtaji huko nje, hawatakuwa wamesaidia kukuza uchumi wa nchi?
Biashara zao hazitatoa ajira kwa Watanzania na pia Serikali kupata mapato kupitia kodi?

Wakati mwingine nawaza na kuishia kusema, TANZANIA HAINA UPUNGUFU WA WATU, LAKINI INA UPUNGUFU WA WATU WANAOFIKIRIA.

Hata kama PASSPORT zingetolewa bure, bado faida ambayo ingepatikana ingeizidi gharama ya kuziandaa.

Angalia nchi ya watu WANAOFIKIRIA.
Nigeria HAINA dini. Lakini kipindi fulani, mmoja wa wahubiri maarufu nchini humo alitaka kuhamishia huduma yake nchi nyingine. Ilibidi Serikali imbembeleze asiondoke.

Serikali ya Nigeria ilikuwa inahitaji mahubiri yake? Noo! Lakini ilipopiga hesabu ya watu mbali mbali kutoka mataifa mengine yanayoenda kanisani kwa huyo muhubiri, ilibaini kuwa ingepoteza mapato makubwa sana.

Wageni waliokuwa wakienda kwa huyo muhubiri walikuwa wakiingizia Nigeria fedha nyingi za Kigeni.
Watu wapumbavu walihubiri na kuingia kwenye globalisation huku wakizuia raia wao kuingia kwenye hiyo globalisation. Namna yao ya kufikiri inatia kichefuchefu kabisa.
 
Ujue HUU NI UPUMBAVU.

Passport ni haki ya kila raia kuwa nayo.haijalishi una safari au hauna. Passport sio mali ya uhamiaji.

Acheni UKOLONI.

Yaani siku nikipata safari ndo nianze kuhangaika kutafuta passport?
Bro umesema kile nilichotaka kusema hawa immigration ni watu wajinga sana ndio maana uraia wanapewa watu wa jirani ni watu hovyo sana tuko ktk ulimwengu wa DOT COM lakini hawa wako nyuma sana kila ukenda immigration mijitu mingi sana inafaa serikali wafungue vituo zaidi ya kumi kwa Dar na mambo yende speed .PAUL MSELLE Nenda kasome tena wewe na wote ni watumishi wetu uko pale kwa ajili yetu sisi Raia .Pasport ni haki ya Raia wote usituletee ushamba wako kama hujawahi kusafiri hebu safari kidogo uone wacheni roho zenu mbaya immigration.
 
Kama ni msafiri ukipitia huu uzi ndo utajua watu ambao wanauzoefu na safari na wanaozungukia humuhumu tu. Hii imetolewa kuwakumbusha watu Ila miaka yote ukiomba passport lazima uonyeshe madhumuni ya kuomba passport kama invitation letter, I-20,letter of acceptance ya chuo, barua ya daktari kwa wagonjwa, reference ya malipo ya hotel kwa wanaotalii etc. Na ipo hivyo miaka yote. Ukiruhusu kila mtu aombe passport uhamiaji hapatakalika. Halafu kama huna mpango wa kusafiri passport ya nini!?.. kuwatambia watu uswahilini kwenu!?... Nina uhakika anayebishia hili hajawahi kuomba passport ndo maana hajui ipo hivyo siku zote.
Bora nilifanya mapema...
Nikapata bila usumbufu
 
Hili neno Pasipoti ni haki ya kila raia liondolewe, ibaki ni haki ya kila msafiri
 
HIVYO VIGEZO HAVIWAHUSU WAHAYA

SISI WAHAYA UKISHAZALIWA UNAHAKI YA PASSPORT KWA MAANA SAFAR HUWA TUNAZO NYINGI
 
Hili neno Pasipoti ni haki ya kila raia liondolewe, ibaki ni haki ya kila msafiri
Tafsiri mbovu sana

Tofauti ya kitambulisho cha NIDA na Passport ni moja tu

Kitambulisho cha NIDA ni kitambulisho local kinachotambuliwa locally kwa local people au taasisi local

Passport ni kitambulisho cha NIDA cha kimataifa kinachotambuliwa kimataifa

Kimataifa huwezi muonyesha mtu kitambulisho cha NIDA hiki local kikadi cha NIDA

Passport ni kitambulisho tu cha kawaida tu sema immigration hawajielewi wala kuelewa kwa nini Passport inatamkwa kuwa ni haki ya kila raia!!!

Kitambulisho cha NIDA ni haki ya kika raia na Passport pia ni haki ya kila Raia

Vyote vitambulisho tu

Mtu akitaka Passport apewe tu awe ana safari au la apewe tu kama kitambulisho cha NIDA whether atakitumia popote kwa lolote au la

Akiomba kitambulisho apewe
 
Kama ni msafiri ukipitia huu uzi ndo utajua watu ambao wanauzoefu na safari na wanaozungukia humuhumu tu. Hii imetolewa kuwakumbusha watu Ila miaka yote ukiomba passport lazima uonyeshe madhumuni ya kuomba passport kama invitation letter, I-20,letter of acceptance ya chuo, barua ya daktari kwa wagonjwa, reference ya malipo ya hotel kwa wanaotalii etc. Na ipo hivyo miaka yote. Ukiruhusu kila mtu aombe passport uhamiaji hapatakalika. Halafu kama huna mpango wa kusafiri passport ya nini!?.. kuwatambia watu uswahilini kwenu!?... Nina uhakika anayebishia hili hajawahi kuomba passport ndo maana hajui ipo hivyo siku zote.
Hapatakalikaje mkuu? Kwamba kutakuwepo na utitiri wa watu?

Eboo! Sasa hiyo si fursa ya ajira? Ni Watanzania wangali wanaosaka ajira, na wengine hata kutafuta pa kujitolea bure bila mafanikio?

Passport inalipiwa. Kama idadi ya wateja itaongeza, na nguvu kazi ziongezwe.
 
Passport ni haki ya kila raia mtanzania.kwanini wafanye kama ni mali yao?.kuna mmalawi ni shamba boy yupo huku kitaa.anakwambia kwao malawi PASSPORT sio ishu.
Ila hapa tanzania mpaka unakufa unaweza usiwe na passport.
Mtu akiwa na passport hata akili ya kutoka nje ya nchi kutafuta maisha inafunguka.
Lakini wao wanataka kila siku tuwe humu humu kama makondoo.
"...mtu akiwa na passport hata akili ya kutoka nje kutafuta maisha inafunguka..."

Uko sahihi mkuu. Hiyo inaitwa "ACT AS IF!"

Mtu akishakuwa na passport, akili itaanza kutafuta fursa ya kusafiri.
 
Kufanikiwa kwa tanzania ni dili au jambo la ajabu,kuna maisha tanzania tunaishi kama zama za mawe.alafu tunashangalia tukisema wakombozi.
Uchumi wa kati wa mlipa kodi ya mwaka shilingi 20k
Inawezekana aliyetunga hiyo sera ni darasa la pili ambaye hajawahi kutoka nje ya kijiji chake

Haiakisi usomi hata kidogo.
 
Back
Top Bottom