Uhamiaji Tanzania, lisaidieni Taifa kuhusu Yusuf Manji. Ni raia wa Tanzania au Marekani?

Mwalimu Nyerere alikuwa na waziri Amir Jamal mzungu sijui mhindi sembuse hao wanaowaletea biashara , think twice
 
una maelezo mazuri lakin penda kuheshim sheria. ningekuelewa zaid kama ungepambania sheria yenyewe kubadilishwa na kuruhusu uraia pacha. sumu ya logic yako ikisambaa kwa aspects nyingine hatutaelewana wala kutawalana.
 
Raia wa marekani alipataje udiwani TZ?..kwa sheria zetu hata ww siku adui yako akiwa rais /waziri..unaambiwa ww mkongo
 
Umepita humo humo nilimopita mimi bila kujitambua.

MTanzania wa kuzaliwa, popote alipo duniani atabaki kuwa mTanzania milele. Mkenya wa kuzaliwa popote alipo ataendelea kuwa mkenya tu. Mhindi hata awe si wa kuzaliwa India, popote alipo, atabaki kuwa mhindi tu.

Jibu langu kwako lilikazia huo uraia wa makaratasi ambao hukuthubutu kuugusia hapa.
 
una maelezo mazuri lakin penda kuheshim sheria. ningekuelewa zaid kama ungepambania sheria yenyewe kubadilishwa na kuruhusu uraia pacha. sumu ya logic yako ikisambaa kwa aspects nyingine hatutaelewana wala kutawalana.

Nashukuru serikali imekiri kwamba sheria ni mbaya! sheria za mwaka 1977 ni ngumu kuzitumia 2001 hasa ukizingatia jamii yetu na utamaduni wetu ulivyobadilika. Nashukuru Serikali inaangalia sheria za diaspora upya na nina kubaliana na mapendekezo ya mapema kwamba kama una uraia wa nchi nyingine usijihusishe na siasa za kupiga kura na majeshi yetu. Lakini shughuli nyingine za kimila ikiwa ni mapamoja na maziko, mirathi, uwekezaji nk hakuna sababu za msingi za kuzuia.

Kama mnavyojua kuna ubaguzi ugenini na wanatumia sheria za uraia kunyanyasa wahamiaji hasa kwenye haki za watoto, bima mbalimbali, mafao ya kazi, shule na vyuo, ajira mfano kuna Watanzania zaidi ya 20 wanafanya kazi kama mafundi wa ndege Tusla, Oklahoma kama engineers . Tanzania mafundi hawa bado hawatapata kazi Tanzania maana ndege nyingi ni mpya na zinafanyiwa marekebisho nje ya nchi hakuna approved sehemu ya matengenezo ya ndege Tanzania kwa sasa kwa ujuzi wa hawa wataalamu. Lakini hatuwezi kusema kwasababu ni watanzania wasifanye kazi nje! sasa wanasaidia ndugu zao nyumbani, wanajenga nyumba zao , wanasaidia jumuia za kitanzania kwenye matatizo, wanatangaza jina la nchi, wanapata uzoefu na ipo siku wanaweza kurudi kusaidia sherika letu likikuwa. Kwasababu ya Sept 11, 2001 huwezi kupata kazi hizi kama sio raia sasa hawa jamaa wangeenda wapi waache kazi zao za $80,000 kwa mwaka waende Tanzania ambako hakuna kazi au wachukue uraia na kusaidia nchi yao na familia zao. Hapa sijui swala la mapenzi au kukana nchi yako linatoka wapi!!?? hii ni common sense na Watanzania hao hao ndiyo wanawaambia chukueni kazi acheni ujinga jamaa wawili wazazi wao ni wanajeshi wastaafu!. Hivyo ndugu zangu uzalendo wa nchi ni mapenzi sasa hivi kuna jamaa kama hawa wanatuma pesa za kusaidia ndugu na jamii lakini kuna viongozi wapo Tanzania wanalipwa na serikali kwa pesa za walalahio halafu wanakula rushwa sasa nani kati ya kawa ni mzalendo. Tujue bado tuna shida hakuna mtu anapenda kwenda kufanya kazi kwenye baridi kwa masaa 12 badala ya kukaa bahari beach na kula samaki fresh wa bahari hindi hivyo tujue umasikini wetu na utafutaji ndiyo umetupeleka huko sio mapenzi maana huko huli bila kazi. Kama wewe unabahati ya kusoma Tanzania kulipwa vizuri na una bahati sana sisi wakati tunaondoka hata nafasi za vyuo ilikuwa shida sana kupata hata kama umefaulu. Ulikuwa ukipata Div 3 mbaya au Div 4 wewe unakuwa mtu wa genge au mission town sasa jamaa nafahamu wengine walipata 4 sasa wana masters degree na ni engineers sehemu nyingine sio kwamba walikuwa hawana akili lakini nafasi zilikuwa chache. Hivyo tuweke sheria za kutufaa sisi kwa hali yetu ya sasa na zinaweza kubadilika kama hali yetu itabadilika lakini kwa sasa sheria mpya ya diaspora ni muhimu sana ili tusifanye vitu kwa siri na tujue wanaonufaika na sheria za sasa ni wala rushwa tu sio familia zetu wala serikali
 
Alikuambia amebadilisha uraia, na sio lazima uwe na uraia wa mmarekani ndo uishi marekani hivi tutaacha lini ushamba
 
Kaa kimya ww mkia huna jipya ushabiki wa simba unakusumbua basi na mudi ni muhindi
 
MAKONDA ndiye manager mtarajiwa wakwa Manji?
 
nimekuelewa vyema hasa kwenye economic factor. nchi zetu za kiafrica hata walioko ndan hawana uzalendo zaid ya kutetea tumbo zao. sasa hofu kubwa nadhan ni ya kisiasa. kuwa tutaweka mwanya wa kuibiana, kuhujumiana na kukimbiana bila break. nadhan imekaa kinadharia zaid. haitofautian na sheria ya pf3 na majeruhi.
 
Ujinga dawa yake Elimu! Hebu soma upya ili uelewe hoja ya mwenye thread!
 
Kwahiyo ww ukiukana Utanzania ukija huku tukuchukulie poa kwamba wewe ni mtanzania ilihali ulishajikataa.

Andiko loote hukuambulia hapo chochote .

Kwa mfano Km Manji aliukana Utanzania,leo utanzania wake ni upi ?
Soma tena andiko acha ujuaji na upumbavu uliotukuka.
 
Kwanza wewe kama mtoa mada tuwekee ushahidi wa document kuwa Manji ni raia wa USA. Baada ya hapo mengine yatafuata.
Kasome tena andiko labda utaelewa japo kidogo.
Stone learner's mna vichwa vigumu sana kuelewa hata mambo madogo tu.
Andiko liko wazi.
 
Kuna watu wengi wamezaliwa Tanzania na kubadirisha uraia wawo kwa kutafuta maisha nje, na Zuhura ni mmojawapo. Ni raia wa uingereza. kuwa na passport ya Uingereza kama mwandishi inalahisisha Safari za nje. Zuhura Yunusi ni raia wa Uingereza. Ni vizuri aseme ukweli kuliko kukaa kimya.
 
Hakuna ubishi wowote kuwa Zuhura Yunusi ni raia wa Uingereza. Namushauli aseme ukweli. Huwezi kuwa mwandishi BBC bila kuchukuwa passport ya Uingereza. Sio lazima, lakini kama mwandishi lazima usafiri Safari nchi mbali mbali. Passport ya Uingereza inakubaliwa karibu Nchi zote. Asingeweza kufanya kazi BBC mpaka kufika alipofika bila ya kuwa na passport ya Uingereza hiyo wazi kabisa.
 
Kwa nini Watanzania hatujitambuwi? Kwa nini Watanzania tunaheshimu rangi ya mtu Na kujidharau sisi wenyewe. East Africa ni nchi ambazo wahindi wanaingia na brief case tupu na kuondoka mabilionea, wakisaidiwa na viongozi wetu, bila ya kujali madhara kwa wananchi. Utajiri wa Manji ni fedha za Watanzania, kazipata akisaidiwa na viongozi wetu tuliowaamini na kuwaweka madarakani . Manji ametajilika kwa kupiga tenda hewa wazi wazi haswa wakati wa Kikwete. ManjI siyo muwekezaji bali ni mwizi mmojawapo aliyoitafuna Tanzania na kuiacha mifupa mitupu. Mufano mmoja tu. Japan ilitowa fedha za kuwasaidia wafanya biashara wadogo wadogo. Kikwete akamukabithi fedha hizo Manji. Hakuna machinga hata mmoja aliziona hizo fedha. Manji alitengeneza list ya wafanya biashara anawo wajuwa yeye ikiwa pamoja na wabunge, badala ya kuwapa fedha aliwapa magali
aliyokuwa akiuza na vitu vingine mbali mbali na kuwasainisha kitu cha milioni 40 anaweka saini kuwa wamepokea vitu vya thamani ya milioni 100. Wengi walikubali kusaini wakijuwa hawatalipa, huwo ulikuwa wakati wa ufisadi mkubwa uliokuwa ukifanyika Tanzania. Watu kama Se8th, Rugemalila na raia wengi wakihindi. Wanaiba uganda Na kukimbilia Kenya. Wanaiba Kenya Na kukimbilia Tanzania, kutoka Tanzania wanakimbilia South Africa. Afrika ni tajiri lakini uongozi wetu ni mbaya ndiyo tunataka kwenye umasikini. Wafanya biashara walikuja kupata shock wakati wa Hayati Magufuli wengi wakapelekewa baruwa ya kurudisha fedha hizo. Wengi walipata shock wengine hata kufa. Hiyo ni mojawapo tu. Fedha za Manji ni za Watanzani. Kwa sasa Hayati Maguguli hatunaye tena Manji karudi kama muwekezaji. Kwa Kweli viongozi wetu wamewafanya Watanzania kama wajinga wa kutupwa. Rest in peace our god sent President Magufuli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…