Habari iwe kwenu wakuu!
Kutokana na yale yanayoendelea kenya , naweza kusema Mheshimiwa Raila Amolo Odinga ndiye mpinzani mwenye nguvu Afrika. Kutokana na mipango yake ya kujiapisha serikali ya jiji la Nairobi walifunga uwanja wa uhuru (Uhuru Park) kwa maelezo kwamba inafanyiwa ukarabati. Lakini jana msemaji wa NASA akihojiwa na VOA alisema hakuna chaguzi nyingine nje ya uhuru park, alisema kama uhuru park itafungwa bado uchaguzi wa pili utabaki uhuru park na hata chaguo la pili likishindikana bado chaguo la tatu ni uhuru park serikali hiyo itake isitake.
Kufuatia msisitizo huo jana mchana maaskari walimwagwa kuzunguka maeno hayo ya uhuru park, lakini hilo halikuwafanya wafuasi wa NASA kurudi nyuma. Usiku kucha wana NASA walikuwa wanamiminika kwenye Uwanja cha UHURU PARK mpaka ikabidi serikali iwatoe wale maaskari. Kwa hali inayoendelea hakuna njia nyingine kumaliza mgogoro huu zaidi ya mazungumzo. Ni vizuri Uhuruto wakakubali kuongea na raila kabla hali haijawa mbaya. Lakini nimegundua raila ana wafuasi watiifu kwake ,wafuasi watiifu kwa chama chake na muungano wao wa NASA, ukiongezea na hoja ya ukabila hapa hali itakuwa mbaya sana UHURUTO wakikaza shingo zao. Hakuna polisi wala jeshi linaweza kuzuia wananchi waliochoka na kukataa tamaa ,wananchi wanaoamini kwamba wanaonewa.
Hoja kwamba anachofanya Raila ni uhaini, inaweza kuwa sawa lakini nani atamshughulikia Raila? si uhuru wala Ruto anayeweza kukubali mchezo wa pata potea wa kuingiza nchi kwenye moto mkali zaidi ya moto wa JEHANAM kwa kumfunga Raila. Kwa hali illivyo na itakavyokuwa kwa masaa machahce yajayo huenda UHURUTO wakaomba mazungumzo.
Kindikwili-Kajiado (Kenya)