JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Demokrasia dhidi ya uhuru wa kujieleza/vyombo vya Habari
Demokrasia sahihi hutegemea uhuru wa vyombo vya habari vinavyoweza kusimamia maslahi ya jamii. Kimsingi, haki zinazohusiana na uhuru wa kutoa maoni na kujieleza bila ya kuingiliwa, kutafuta, kupokea, na kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali kwa kufuata kanuni chache zilizowekwa, ni haki inayotambuliwa na sheria za kimataifa. Vyombo huru vya habari ni msingi muhimu wa kuhakikisha kupatikana kwa uhuru na haki hizi. Katika kuhakikisha hilo, dhima ya waandishi wa habari ni zaidi ya kazi yao; uandishi ni taaluma inayoweza kusaidia kupatikana kwa mitazamo na maoni ya aina mbalimbali kwenye nchi.
Vyombo vya habari hutoa fursa kwa watu kuhabarishwa na wao kuweza kujenga na kueleza mitazamo yao. Tasnia imara ya habari huwezesha jitihada za kushawishi kupatikana kwa hoja mpya na mabadiliko muhimu, na kufuatilia utendaji wa Serikali ili kuifanya iwajibike kwa wananchi wake.
Waandishi wa habari hutegemea taarifa kutoka kwenye vyombo na taasisi mbalimbali, na vyanzo vinavyoaminika (wakiwemo wafichua uhalifu mbalimbali) ili kuandaa habari na kuiarifu jamii. Sheria zinazowezesha (kuliko kuzuia) juhudi hizo ni muhimu katika utendaji wa waandishi na kushamiri kwa tasnia nzima ya habari. Kwa upande wao, waandishi wa habari na watendaji wengine kwenye vyombo vya habari wana wajibu wa kuhakikisha kwamba wanafuata misingi na maadili ya taaluma zao katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku. Hii ni pamoja na kutoa taarifa za uhakika, kufuata kanuni zote za maadili, na kuhakikisha uhuru wa kiutendaji kwenye tasnia ya habari.
MISINGI YA KISERA NA KISHERIA INAYOSIMAMIA TASNIA YA HABARI – KIMATAIFA
Mikataba mbalimbali ya kimataifa, bara na kanda inalinda tasnia ya habari, waandishi wa habari, na watetezi wa haki za binadamu kutoingiliwa na Serikali. Mikataba hiyo inaweka wajibu kwa Serikali kufuata, kuendeleza, na kulinda uhuru wa kutoa maoni na kujieleza.
TAMKO LA KIMATAIFA LA HAKI ZA BINADAMU (UNDHR)
Kifungu cha 19 cha Tamko hilo kinasema: Kila mtu ana haki ya uhuru wa kutoa maoni na kujieleza; haki hii pia inahusisha uhuru wa mtu kuamini katika maoni yake bila kuingiliwa kwa namna yoyote, na uhuru wa kutafuta na kusambaza taarifa, maoni na mawazo yake kwa njia yoyote bila ya kujali mipaka
Demokrasia sahihi hutegemea uhuru wa vyombo vya habari vinavyoweza kusimamia maslahi ya jamii. Kimsingi, haki zinazohusiana na uhuru wa kutoa maoni na kujieleza bila ya kuingiliwa, kutafuta, kupokea, na kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali kwa kufuata kanuni chache zilizowekwa, ni haki inayotambuliwa na sheria za kimataifa. Vyombo huru vya habari ni msingi muhimu wa kuhakikisha kupatikana kwa uhuru na haki hizi. Katika kuhakikisha hilo, dhima ya waandishi wa habari ni zaidi ya kazi yao; uandishi ni taaluma inayoweza kusaidia kupatikana kwa mitazamo na maoni ya aina mbalimbali kwenye nchi.
Vyombo vya habari hutoa fursa kwa watu kuhabarishwa na wao kuweza kujenga na kueleza mitazamo yao. Tasnia imara ya habari huwezesha jitihada za kushawishi kupatikana kwa hoja mpya na mabadiliko muhimu, na kufuatilia utendaji wa Serikali ili kuifanya iwajibike kwa wananchi wake.
Waandishi wa habari hutegemea taarifa kutoka kwenye vyombo na taasisi mbalimbali, na vyanzo vinavyoaminika (wakiwemo wafichua uhalifu mbalimbali) ili kuandaa habari na kuiarifu jamii. Sheria zinazowezesha (kuliko kuzuia) juhudi hizo ni muhimu katika utendaji wa waandishi na kushamiri kwa tasnia nzima ya habari. Kwa upande wao, waandishi wa habari na watendaji wengine kwenye vyombo vya habari wana wajibu wa kuhakikisha kwamba wanafuata misingi na maadili ya taaluma zao katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku. Hii ni pamoja na kutoa taarifa za uhakika, kufuata kanuni zote za maadili, na kuhakikisha uhuru wa kiutendaji kwenye tasnia ya habari.
MISINGI YA KISERA NA KISHERIA INAYOSIMAMIA TASNIA YA HABARI – KIMATAIFA
Mikataba mbalimbali ya kimataifa, bara na kanda inalinda tasnia ya habari, waandishi wa habari, na watetezi wa haki za binadamu kutoingiliwa na Serikali. Mikataba hiyo inaweka wajibu kwa Serikali kufuata, kuendeleza, na kulinda uhuru wa kutoa maoni na kujieleza.
TAMKO LA KIMATAIFA LA HAKI ZA BINADAMU (UNDHR)
Kifungu cha 19 cha Tamko hilo kinasema: Kila mtu ana haki ya uhuru wa kutoa maoni na kujieleza; haki hii pia inahusisha uhuru wa mtu kuamini katika maoni yake bila kuingiliwa kwa namna yoyote, na uhuru wa kutafuta na kusambaza taarifa, maoni na mawazo yake kwa njia yoyote bila ya kujali mipaka
Upvote
0