Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata kesi za ujambazi sio poa Mkuu.Kesi ambazo naomba Mungu nizikwepe ni mauaji na ubakaji.
Nisihusike Wala nisishirikishwe
Issue zenye chain links zinazohusisha vigogo huwa zinafyeka wanyonge wengi sana ili ku clear any possible tracks,humo wengine hupewa adhabu ya kifo kwa kuwa tu wanamjua mhusika flani papa, huko Mexico wanaharakati wa mazingira wanauawa kila kukicha,mbaya zaidi wanaohusika na mambo hayo wengi ni viongozi wa serikali wanaoshirikiana na majangili wanaopora Maliasili hasa magogo na kuyauza kwa faida kubwa kwenye viwanda via ndani na nje ya Mexico,sasa hata hapa naona kama hiyo michezo inapiga hodi,kuna na helicopter ilishushwa huko mikumi miaka kadhaa nyuma,God forbidTatizo la hizi ishu zinaishia kwa Washiriki wadogo wa mwisho...kama hapo wanamaliza tu na hao Wauwaji.
Laiti kama watafuata chaneli mpaka wafike juu kabisa kwa Wahusika wakuu.
Sasa rasmi nimethibitisha pasipo shaka yoyote kuwa wewe ni mpumbavu, yaani pamoja na mwandishi kuandika kwa mtiririko mzuri kabisa ila wewe ulikuwa busy kutafuta jina lenye asili ya kaskazini ulipigie kambi?what a stupid creature?Kuna wakaskazini hapa wafanya biashara pale Arusha, lakini mtasikia tu wakaskazini wanajua kubana budget mpaka wanapata pesa, waaapi..... Kuna mtu anajua kubana pesa kama Muhindi na Muha wa Kigoma? Watu ni majambazi, yaani kundi lote hili kumuua mtu mmoja tu tena siyo Raia kwa faida za ujambazi wao!!! Dunia hii
Mi mwenyewe nimejiuliza,nikakosa jibu,kuna issue behind this one,amini tu hivyoInamaana michongo yote hiyo na wahusika wote hao walikuwa wanapambania 20m!!!!
Huo mgao utakuwaje wajameni?
Shithole kbs huyu.kaskazin inamuwasha sanaSasa rasmi nimethibitisha pasipo shaka yoyote kuwa wewe ni mpumbavu, yaani pamoja na mwandishi kuandika kwa mtiririko mzuri kabisa ila wewe ulikuwa busy kutafuta jina lenye asili ya kaskazini ulipigie kambi?what a stupid creature?
Una chuki na wivu wa kisichana.Kuna wakaskazini hapa wafanya biashara pale Arusha, lakini mtasikia tu wakaskazini wanajua kubana budget mpaka wanapata pesa, waaapi..... Kuna mtu anajua kubana pesa kama Muhindi na Muha wa Kigoma? Watu ni majambazi, yaani kundi lote hili kumuua mtu mmoja tu tena siyo Raia kwa faida za ujambazi wao!!! Dunia hii
Ana nafasi ya kuchomoka akipata wakili mzuriYaani watu 11 wananyongwa kwa kuhusika kumuua mtu 1?
Dada Rahma ananyongwa kwa kutunza silaha na kuwapikia hao wana?
Dooh!
Madawa ya kulevya je?money laundering?Kesi ambazo naomba Mungu nizikwepe ni mauaji na ubakaji.
Nisihusike Wala nisishirikishwe
Mnapata dhambi sana kuchafua watu kama hakuna ushahidi wa tuhuma hizo.Msoga & Msomali wapo kazini.
Mpiga kampeni ya kukomesha biashara haramu ya pembeHuyo Lotter alikuwa nani??
We jamaa unakipaji cha kuchekesha.Hata kesi za ujambazi sio poa Mkuu.
Ile kuvunja nyumba na kuiba hukumu zake zimechangamka.
Asante sana mkuu kwa mrejesho huu. Huyu Lotter bila shaka ni yule mzungu aliyeuawa Masaki kama sikosei. Kuna waliodhani kuwa alikuwa ameuawa na watu wa kitengoWatuhumiwa 11 wamehukimwa na Mahakama kuu ya Tanzania kwa kumuua Wayne Lotter.
Ingawa mfadhili kuu wa kesi hii alikuwa Mchina , bado haijajulikana hakukamatwa au alikamatwa akawa deported. Mwingine Fahmi Karama alikamatwa lakini haijulikani yupo wapi, hata kwenye kesi hakuletwa Kama mtuhumiwa:.
Uhusika kwenye mauaji ya Lotter Ni Kama ifuatavyo:
1. Wa kwanza, Ismail Issa Machips yeye ndio alipewa dili na mchina na kutakiwa kutafuta hitman wa kumuua Lotter. Machips na huyo mchina walikutania Arusha. Kwenye kutafuta hitman akamuhusisha Makoi.
2. Wa pili ni Makoi, yeye alimtafuta Hitman baada ya kushirikishwa na Issa Machips. Na Makoi akapendekeza mtu anayeweza hiyo kazi ni Fahmi Karama. Hivyo Hawa wawili ndio chimbuko hasa la dili lote.
3. Wa tatu Rahma Mwinyi, yeye kazi yake ilikuwa kutunza silaha zilizotumika kumuua Lotter. Na silaha hizo alikuwa anaficha makaburini huko Temeke. Pia huyu Rahma aliingizwa kwenye hili dili na kaka yake Fahmi Karama na alikuwa saa zingine anawapikia msosi watuhumiwa wengine waliokuwa wanakuja hapo kwao Temeke.
4. Wa nne Chambiie Juma, huyu alikuwa dereva taxi kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa KIA. Na Marehemu Wayne Lotter alikuwa mteje wake alipokuwa akifika KIA au kuondoka KIA. Yeye ndio alitoa taarifa kwa wauaji kwamba Mr Lotter ameshapanda ndege na anaelekea Dar.
5. Wa tano, Allen Mafue. Huyu ameingia kwenye hi kesi Kama mfadhili wa mauaji. Yeye ndiye aliyewalipa kiasi Cha millioni 20 za kitanzania akina Karama na ongiste. Na aliwalipa hizo fedha kwenye bureau de change yake.
6. Wa sita Ayoub Selemani Kihoi, yeye kazi yake kubwa ilikuwa kuwafuatilia kwa ukaribu Lotter na mwenzake na kuwapa taarifa wauaji. So kazi yake ilikuwa ni kumonitor na kuwafatilia akina Lotter wanapotoka na kwenda siku hiyo ya mauaji. Na kuwapa attention wauaji wawe tayari.
7. Wa Saba ni Abou Omary mchingile, yeye pamoja na Kihoi walikuwa pamoja kumonitor taxi waliyoitumia akina Lotter na kutoa taarifa imefika wapi na inaelekea wapi ili wauaji wawe attention.
8. Wa nane, Michael David Kwavava, huyu ndio alikuwa dereva taxi wa Mr Lotter ndio aliyemtoa JKIA kumpeleka Baobab Village Masaki. Huyu dereva taxi alikuwa na mawasiliano na Fahmi Karama kabla siku ya mauaji hayajatokea. Na Fahmi alikuwa na mazungumzo naye kwa nusu saa kuhusu huo mpango wake.
9. Wa tisa ni Ndui mana ongiste raia wa Burundi. Huyu ndie aliyetekeleza mauaji kwa kumpiga Risasi Marehemu Lotter. Pia dereva taxi kwavara alimtambua kwenye identification parade iliyofanyika polisi, kwamba ndiye aliyefyatua risasi. Pia alikuwa akishirikiana na Fahmi Karama kwenye mipango yote.
10. Wa kumi ni Godfrey Peter Salamba, huyu ndio alikuwa dereva aliyewaendesha wauaji. Ndio alikuwa dereva wa gari lilobeba wauaji.
11. Wa kumi na moja Hibonimana Augustine Nyandwi, raia wa Burundi . Yeye ndiye aliyeleta silaha iliyomuua huyo Lotter na pia aliratibu mambo mengine ya kufanya mauaji hayo.
Kwenye hao wote wenye ahueni ya kukata rufaa ni wawili dereva taxi, maana mwanzoni kwenye kesi alikuwa Kama shahidi wa Jamhuri ila baadae ikagundulika naye alikuwa na mawasiliano na Karama. Na waliomtaja ni watuhumiwa wengine. Anaweza kubisha kwamba watuhumiwa walimtaja Kama kumkomoa baada ya kusema alimuona ongiste akimpiga risasi Lotter.
Mwingine ni Erick Mafue amabaye bureau de change yake ilitumika kufanya malipo kwa watuhumiwa. Je alitumiwa tu pesa za kigeni abadilishe au pesa zilikuwa za kwake za kufadhili mauaji hayo. Na je alijuwa fedha hizo zitatumika kwenye mauaji?. Wengine kwenye kuchomoka kwenye rufaa ni kazi.
This is too low my dear. Try another method to relieve your frustration.Kuna wakaskazini hapa wafanya biashara pale Arusha, lakini mtasikia tu wakaskazini wanajua kubana budget mpaka wanapata pesa, waaapi..... Kuna mtu anajua kubana pesa kama Muhindi na Muha wa Kigoma? Watu ni majambazi, yaani kundi lote hili kumuua mtu mmoja tu tena siyo Raia kwa faida za ujambazi wao!!! Dunia hii
Hata kesi za ujambazi sio poa Mkuu.
Ile kuvunja nyumba na kuiba hukumu zake zimechangamka.
Madawa ya kulevya je?money laundering?