Uingereza: Waziri mwingine mwenye asili ya Afrika ajiuzulu huku Serikali ikionesha dalili za kuelekea kuanguka

Uingereza: Waziri mwingine mwenye asili ya Afrika ajiuzulu huku Serikali ikionesha dalili za kuelekea kuanguka

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
1666214058938.png


Suella Braveman ambae alikuwa akiongoza wizara ya mambo ya ndani amejiuzulu leo jioni baada ya kukiuka kanuni za usalama wa habari mitandaoni kwa kutumia anuani binafsi ya barua pepe badala ya anuani maalum ya serikali.

Waziri huyo anadaiwa kutumia anuani binafsi kutuma taarifa nyeti katika mitandao ya serikali jambo ambalo linaweza kupoteza taarifa hizo kwa wale wasokusudiwa.

Bi Suella alituma ujumbe wa barua pepe uloonyesha mswaada uloongelea sera ya uhamiaji kupitia simu yake ya mkononi jambo lilokikuka kiufundi suala zima la usalama wa mitandao ya serikali.

Lakini katika kinaochoonekana kwa bi Suella kutokubali uongozi wa waziri mkuu Liz Truss, katika barua yake ya kujiuzulu amedai kutokuwa na imani na serikali na mwelekeo wake na pia serikali kutokufanya yake ambayo iliyaahidi kwa wapiga kura.

Pia katika barua hiyo bi Suella amedai kuwa serikali bado imeshindwa kushughulikia suala la uhamiaji ulozidi kipimo ambapo idadi kubwa ya wahamiaji wamekuwa wakiingia nchini humo kinyume cha sheria na kushindwa kuzuia mitumbwi inotumiwa na wahamiaji hao kuingia nchini humio kupitia mkondo ujulikanao kama "English Channel".

Katika barua yake alomjibu bi Suella, waziri mkuu Liz Truss amekubali kujiuzulu huko na kusisitiza umuhimu wa viongozi wa serikali kutii maadili ya uongozi na kulinda siri za baraza la mawaziri.

Serikali ya Uingereza bado ipo matatani ambapo waziri mkuu Liz Truss amekuwa akabiliwa na madai ya kutakiwa kujiuzulu jambo ambalo amekuwa akipingana nalo kwa wiki zaidi ya mbili sasa.

Hali kadhalika ndani ya chama cha wafahidhina kumekuwepo mipasuko na mikanganyiko ambapo wapo wanachama wanotaka Liz Truss ajiuzulu na wapo pia wanotaka bwana Boris Johnson arejeshwe ili kukiokoa chama hicho dhidi ya mashambulizi kutoka vyama vya upinzani vikiongozwa na chama cha Labour.

Hata hivyo kitendo cha bi Suella Braveman bado kimeendelea kuleta masuali mengi juu ya uwezo wa baadhi ya viongozi katika chama cha wahafidhina hususan wale ambao badi umri wao ni mdogo kisiasa.

Hadi sasa Bi Liz Truss amewateua katika baraza lake la mawaziri wale ambao walikuwa wakimuunga mkono mhasimu wake bwana Rishi Sunak ambae walichuana katika kinyang'anyiro cha kuongoza chama cha wahafidhina. Siku chache zilopita, Bi Liz Truss alimteua bwana Jeremy Hunt kuwa waziri wa fedha na leo jioni amemteua bwana Grant Shapps kuwa waziri wa mambo ya ndani.

Bi shaka mambo haya yaendelea kuwapa wakati mgumu wapiga kura wa nchi hiyo ambao mpaka sasa wakabiliwa na baridi kali ijayo kuanzia mwezi ujao wa November na kupanda kwa kasi kwa gharama za maisha.
 
Uwajibikaji huko ni mkubwa sana.Kwa Tanzania waziri anaweza kuiba bilioni za umma na asijiuzulu.Mfanao Tanesco kuingia mkataba wa kihuni na kampuni ya kihindi wenye thamani zaidi ya bilioni 60 na hamna ufanisi wowote ulioonekana na waziri anakula kiyoyozi tu ofisini
 
Uwajibikaji huko ni mkubwa sana.Kwa Tanzania waziri anaweza kuiba bilioni za umma na asijiuzulu.Mfanao Tanesco kuingia mkataba wa kihuni na kampuni ya kihindi wenye thamani zaidi ya bilioni 60 na hamna ufanisi wowote ulioonekana na waziri anakula kiyoyozi tu ofisini
Aeeee Afrikaaa eee Africa eeelisambeeee🤸🤸
 
Kwan ungesema waziri UK kajiuzulu pengine kuna kitu kingepungua? Au kuleta maswala ya race unadhan inasaidia ku-shape argument? This is racism.
 
Uwajibikaji huko ni mkubwa sana.Kwa Tanzania waziri anaweza kuiba bilioni za umma na asijiuzulu.Mfanao Tanesco kuingia mkataba wa kihuni na kampuni ya kihindi wenye thamani zaidi ya bilioni 60 na hamna ufanisi wowote ulioonekana na waziri anakula kiyoyozi tu ofisini
Umeenda mbali sana unaongelea wizi kule hubaki salama watu wanajiuzulu kule kwa tabia binafsi tu wala sio kazi Boris Johnson kufanya party tu wakati wa corona hakuachiwa kule ukikutwa sehemu tu haina maadili umekaa kama kiongozi ujue safari huku hakuna hayo labda utumbuliwe tu na hata akitumbuliwa sio mwisho wa safari baada ya muda tu usishangae karudi kwa nguvu tena. Ok tatizo liko wapi?

Huku kwetu ukiwa mkubwa unaamini utumikiwe na watu kule wewe unatumikia watu na huna madaraka juu ya watu na wengi hawako kwa ajili ya pesa maana wengi ni matajiri ila wanajisikia ufahari kuhudumia nchi na kufanya jambo.

Hapa leo waziri anasimamia hili kesho anaruka utasema sio yeye alisema na wala hawajibiki. Kweli yule Mama alikuwa waziri wa afya wakati wa corona leo bado waziri pamoja na drama zake zote zile kuongea uwongo hadharani leo anaukana maneno yake.

Kwetu ukiwa kada mzuri na mtiifu inatosha maana watanzania wako busy na umbea na mambo ya kijinga ndio tunapenda.
 
Kwan ungesema waziri UK kajiuzulu pengine kuna kitu kingepungua? Au kuleta maswala ya race unadhan inasaidia ku-shape argument? This is racism.
Ndugu, ukisoma mfululizo wa mada tatu niloziweka hapa kuhusu hawa utaelewa.

Mada ya kwanza ilikuwa ni hii : Uingereza kuwa na Mawaziri watatu wenye asili ya Afrika ambao wataongoza Wizara nyeti za nchi hiyo, Fedha, Mambo ya Nje na Mambo ya Ndani

Mada hizi zililenga kuangalia uwezo wa sisi watu ambao si wazungu na kama tunaweza kweli kupewa majukumu mazito ya kushika nafasi nyeti katika serikali za huko.

Huko Uingereza yaaminika kuwa wizara za fedha, mambo ya nje na mambo ya ndani ni wizara nyeti sana na mawaziri wake hukaimu nafasi ya waziri mkuu na naibu wake ikitokea wote hawapo.

Hivyo huwa yafikirisha kama kunakuwepo na figisufigisu tu au ni uwezo mdogo tu wa kushika nafasi hizo.

Usitumie kadi ya ubaguzi hilo si lengo langu.
 
Afrika nayo ni kubwa sana basi kama huyo naye ana asili ya Afrika basi PW Botha pia alikuwa ana asili ya Afrika!
 
Ndio Mana pound inazidi kuporomoka sema bana mwaka huu hasahasa since Ukraine war. USD imeendelea kuzigalagaza zarafu nyingi duniani. Hii Ni fursa kwa trader just short pound/USD usubirie mti ukue ule matunda na sio haraka Sasa.

For 35+yrs paundi dhidi ya dola haijawahi fika around 1.0356 Ila mwaka huu imegusa.
 
Screenshot_20221020-113449.png
already shorted since yesterday so saivi Ni mwendo wa kudondoka.
Jamani trading Ni professional Kama zingine. Kama huna muda wa kukaa darasani for not less than 5yrs uisome uijue nje ndani bado usidhubutu.
Kila kitu Ni kamari Ni wangapi wamesoma hawana kazi. Wangapi wameoa wake zao hawajazaa. Wangapi wamefungua biashara na hazijaendelea zikafungwa,wangapi wamesafiri wakapata ajali,
Wangapi wamewekeza kwa marafiki ama urafiki na mtu mwishoni wakasalitiwa.
Ila Ila chondechonde jifunze mwenyewe ukiangukq unajua why umeanguka Mana hata mtt hakuna anayemfundisha kutembea Bali ana improve with his failures of falling down.kama ukianguka down unakuwa mnyonge huku ndio hao walimu wako Sasa Mana ukianguka chini kaa tulia ujue why umeanguka down.


Kufundishwa Ni sawa na kufundishwa how to fakuu. Ni Nani aliyefundishwaa how to do this thing loved by people
 
Siasa za wenzetu raha sana,safi sana inavutia sana wanavyofanya, ukizingua unawajibika ukikaidi unawajibishwa safi kabisa. Uchaguzi huru na hata raia wake wameelimika. Safi sana.
in my opinion nadhani hata kama tungekuwa na tume huru,magufuli bado angeshinda 2020 Kwa sababu ya elimu kwa watanzania.
 
Siasa za wenzetu raha sana,safi sana inavutia sana wanavyofanya, ukizingua unawajibika ukikaidi unawajibishwa safi kabisa. Uchaguzi huru na hata raia wake wameelimika. Safi sana.
in my opinion nadhani hata kama tungekuwa na tume huru,magufuli bado angeshinda 2020 Kwa sababu ya elimu kwa watanzania.

Bila uwajibikaji na kujituma ukipewa kazi basi wafaa kukaa pembeni uwachie wengine.
 
Hivi Uafrika wake katika hii content unaongezea uzito wowote wa habari ? Au tunamuongezea msomaji maneno ya kusoma...
 
Hivi Uafrika wake katika hii content unaongezea uzito wowote wa habari ? Au tunamuongezea msomaji maneno ya kusoma...
Bila shaka, kwa wafuatiliaji pekee na hata weye ukitaka fuatilia basi wafanya tafiti na kusoma habari zaidi.
 
Back
Top Bottom